ATCL: Another Richmond!

Hizi ni laana au kitu gani? Mambo gani haya nchi imoza kabisa au ndio watu wameamu kuwa vyote vyote itakavyokuwa kila mtu kwa anafasi yake ni kupiga bao tu hakuna kuangalia sura ya mtu... ....JK si ulisema urais wako sio wa ubia na mtu yeyote mi nina mashaka lazima utakuwa na ubia may be wa 70-30% kama sio 50-50% hii ni noma.
 
Mheshimiwa Zitto madamu ndo mwenyekiti, hebu jaribu kuangalia hii mikataba ili nayo ifikishwe bungeni ikiwezekana watu wawajibishwe kama kawaida...kazi yako inatambulika...hawa watu sio wa kuwavumilia HATA KIDOGO!

Asalale....... NakuliliaT....., haya taratibu ndugu yangu!!!!
 
tumepiga kelele hapa tangu disemba wasituambie kuwa ndege hairuki bado! tumeweka na mkataba mbovu hapa, tumeweka gharama za matengenezo ya ubovu, tumeweka mkataba na mauritius lakini hatusikiki...

Mimi nimesema huko nyuma hili dege likija kupata kisanga chochote mtu asitolee maoni!!! kwani mengine ni ya kujitakia.
 
Ndugu,

Zitto ki protocol hatakiwi ku comment hapa, hasa kwenye hili linalohusu mamlaka aliyo nayo.

Anachotaka ni sie kumwaga data ili azifanyie kazi.

Mh Zitto, ile mikataba bado ipo, tembeleeni ATC mkajionee wenyewe.
 
Kilichonichosha Mimi Ni Pale Matakka Aliporudishwa Kundini Na Muungwana,baada Ya Kuwekwa Benchi Kwa Muda Mrefu.
Hivi Mh Haoni Uozo Wanaofanya Machek'bob Wenzake?pamoja Na Ufisadi Wote Mataka Alioufanya Ppf,akaona Ampe Tuu Mshkaji Wake Ulaji?
Hapo Ndo Swali Linapokuja,hivi Kweli Ataacha Kufumbia Macho Maovu Yanayofanywa Na Wenzie?kingine Kilichonishangaza Ni Uteuzi Wa Rashid Idrissa Pale Tanesco??is This Man Serious?
Kazi Imemshinda Jamanii..
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma nipo, ninawasikiliza!......

Mhe. Mwenyekiti na Mbunge.

Nauliza hivi. Ukiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma, una mpango gani wa kushawishi utenguzi wa wakurugenzi/waendeshaji wote wa mashirika ya umma ambao hayaendeshwi kwa tija kwa sasa?

ATCL (kwa mfano tu) limekuwa inalalamikiwa kila kukicha, lakini pia fedha nyingi zinapotea aidha kwa kuwa-direct injected au kwa kukosa fursa za kibiashara (business opportunities).

Je, ukiwa M/Kiti wa Kamati hii, hauoni ni muda sasa kutangaza nafasi hizi za wakurugenzi/waendeshaji waandamizi kwa watanzania wengine wenye uwezo.

Kuna pool ya watanzania wengi tu wenye taaluma za biashara na uendeshaji (business and management) ambao wapo nchini na nje ya nchi.

Je, hili nalo linahitaji utashi wa kisiasa au ni nini hasa ?

Unisamehe kama hili si lako kwa sababu uteuzi ni wa Mhe.Rais, lakini ukiwa kama M/Kiti na Mbunge, najua una UWEZO wa kushinikiza watu wapya wapewe uwezo wa uendeshaji wa haya mashirika.
 
hawa watu siku zote wamekuwa wakilelewa na bado RAISI anakaa kimya....sasa ikulu amemwita wa nini???????\
DAVID najua uko ama on line ama unaona na kusoma mawazo ya wana JF ambayo kwa wakati mmoja yanaweza kukuonyesha nini cha kufanya kukwamika na laana hizi za kila siku......./
1)))Kwa macho yangu nimeona hii airbus sokoi kwa kukodisha ni doller 260,000 na wengine wakiweka offer nyingi tu...ninao mfano ambao utakuonyesha wapi umekosea kuna ndugu yetu mtanzania alikuja na mada yake wakaikimbiza kwa maslah binafsi..kuhusu airbus.....kuna mtanzania kama si huyu basi ninaemjua mimi anaitwa l .AZIZI ALIWEZA KUHANGAIKA SANA KATIKA HILI NA ALIFWATA PROCEDURE ZOTE AKAPEWA GO AHEAD NAPRESID +MR NYANGANYI ,,,BAADA YA KUWALETEA DETAILS ZOTE MKAMDHARAU ...ALIDIIRIKI KUNIONYESHA EMAIL ALIYOWATUMIA NA MAJIBU YENU......HATA NYANGANGANYI ALIKUWA AKIMTAMBUA HUYU....MOJA YA OFFER ZAKE MLIPEWA KWA DOLLER 260,000 NKWA MWEZI,,NA MKIEN=DELEA KULIPA KWA MUDA WA MIAKA SABA JAMAA MWENYE HIZI AIRBUS KWA RAHA ZAKE AKAWAANDIKA IKIFIKA MWAKA WA SABA INAKUWA YENU NA SI KUENDELEA KULIPA TENA KWA MWEZI...JE HILI UKULIONA ??????NA KWA BAHATI NZURI EMAIL EMEONYESHA IMEKUFIKIA SASA BASI WAWEZA KUTUELEKEZA HATA KWA MAJINA YOYOTE KWANINI ULIKIMBILIA NDEGE KWA DOLLER 360,000 NA KUSHINDWA KULIPA KUDAIWA 60,000USD EXTRA......NINI LENGO LAKO

2))KUNA WATANZANIA WENYE NIA NJEMA WALILIONA NA KATIKA KUFWATILIA WAKAKUJULISHA MAPEMA UBOVU WA HII NDEGE NA MATATIZO YAKE MKAA KIMYA NINI LENGO LENU????

3))WAKATI UKIINGIA WATU WALIKUPONGEZA SANA NA WENGINE KUFURAHIA MAISHA BORA BILA KUJUA ATCL NA PPF VITU VIWILI TOFAUTI KULE UNAPOKEA BILA KUTAFUTA NA ATCL UNATAFUTA ILI UPOKEE....SASA BASI TUNAOMBA TUELEZEE MADHUMUNI NA SAFARI AMBAZO WATANZANIA WANGEPENDA KUJUA BAADA YA UFIKA HIYO NDEGE HAPO TANZANIA ...

3)))KUNA HIZI NDEGE NDOGO MLIZODANGANYWA KWAMBA NI MPYA BAADA YA KFIKA TUNASIKIA ZIMEANZA KUFYAATA MKIA NA KUAMUA KUZIPAKLI KWENYE HOLI LENU JE UNAWEZA KUTUELEZA SABABU ZA NDEGE HIZI KUJA NA KUSHINDWA KUPAKI NINI LENGO LENU??????

4)))KUNA MKATABA TUMEUPATA MUDA SI MREFU KUTOKA KWA WAPENDA NCHI...KUNA NDEGE MMLIIOKODISHA HIVI KARIBUNI KUTOKA SOUTHAFRICA NA AIKUCHUKUA MUDA INASEMEKANA WAKAAMUA KUTOENDELEA SABABU YA KUTOLIPWA HELA...KUNA USHAHIDI WAKIWA WANAONDOKA MKAWARUDIA NA KUTUMA BAADHI YA HELA WAKAAMUA KURUDI ..SAFARI HII NASIKIIA WALIKUJA WAKINUKA..WAKARUDI KWAO MLIPOWAAMBIA HILO....KATIKA MKATABA HUU KUAN KIPENGELE KINAONNYESHA KAMA MTASHINDWA KULIPA WAKATI WOWOWOTE MWENYE NDEGE ANAUEWEZO WA KUICHUKUA NA MNATAKIWA KUENDELE KULIPA KWA KUTUMIA MIN HRS YAANI MASAA MACHACHE..NA UHAKIKA ULIOPO ILE NDEGE IKO SOUTH IMERUDI KULE NA BADO MNAENDELEA KULIPA DOLLER 185,000????JE MLIKUWA HAMJUI IMPACT YAKE ???AU AMMKUSOMA KABLA YA KUTIA SAINI,,,PILI NAUMIA KICHWA MKATABA UNAONYESHA AMESAINI ANAITWA BWANA AJAY???MIKATABA TUNAVYOJUA ANASINI MKURUGENZI JE HAPA UNAWEZA KUTOA UFAFANUZI???

5))LINGINE LIMENSHTUA KUSOMA LEO KUMBE UKIACHA HIYO DOLLER 360,000 KWA MWEZI KUNA DOLLER 200,000 KW AMWEZI JUMLA DOLLER 560,000..WAPI TUNAENDA KAKAYENGU???
 
Zitto,

Kama upo, basi shauri jamaa wasiwe recycled. Kwanini mashirika ya nje yanayoongozwa na waTanzania tena wengine vijana tu yanafanya vizuri? halafu kwanini uozo ukianikwa hadharani mawaziri wanakuja juu (Mahanga)? kama ni uzushi si wapuuzie? kama ni kweli kwanini wasifanyie kazi?

Pia checking hiyo mikataba. Kwanini ndege inakuja ndio watu wanapelekwa mafunzoni?, kwani hawakujua ndege inakuja lini?

Ni hayo tu kwa sasa.

Mkubwa Shkamoo

Hii hoja yako nimeikubali sana..Bwana Zitto shukrani sana kwa uwepo wako hapo at your capacity kama Mwenyekiti wa tume ya Mashirika ya Umma. Hili suala la hawa watendaji wakuu wa mashirika ya umma kuwepo madarakani kwa muda mrefu licha ya kuboronga katika maeneo mbali mbali ndio mojawapo ya chanzo kikubwa sana cha kudorora na hata kufikia kufilisika kwa mashirika husika. Jamani Airline ya taifa inaishiwa mpaka kiasi cha kushindwa ku-compete na shirika binafsi, for instance Precision Air.. Well hii inauma sana ingawaje ndio tumeishacheelewa basi tafadhalini tuokoe hata hicho kidogo kilichopo. Sitaki kuamini kwamba bwana David Mattaka huyu ambaye wakati wa uongozi wake NSSF alichangia sana kudorora kwa huduma zilizotolewa na shirika hilo.. huku akitumia kiburi na nguvu ya pesa za uma kufanya ubaradhuli kwa wanaume wenzie...leo ndio anaetumiwa kama mtendaji atatoa muongozo wa uokozi wa taasisi hii ya ATCL ambayo ndio kama ivo..inaelekea kudondoka...Pili kuna maeneo mengine ya mashirika ama taasisi za umma kwa mfano hili la maji safi na maji taka..kwa kweli huduma zake ni hovyo mno, hii ikielezewa kwamba inatokana na mtaji mdogo wa shirika katika kuweza kuestablish a competitive infrastructure that can cater for the expansion of the respective services and therefore kukidhi mahitaji ya ongezeko la watu wa mji huo..sasa huyo mkubwa ambaye yupo hapo, nadhani ana zaidi ya miaka 15 akiwa kama mkurugenzi mkuu, tangu enzi zile inaitwa NUWA mpaka leo..akisifika kwa ku-promote ukabila kiasi cha lugha ya kabila lake kuwa kama sehemu ya official language ya ofisi za taasisi hiyo..Ina maana hapo katikati hamna watu waliosoma na wenye uwezo wa kuongoza mashirika kama haya, kwa kuleta mawazo mapya ya maendeleo na pia kuweza kuboresha uendeshwaji wa mashirika haya..? Haya ni mawazo yangu tu..
 
Jamani Tanzania kuna makubwaaa. Halafu inashangaza sana kuona watu wanaoihujumu hii nchi ni watu na elimu zao, hapa wataka kuprove nini? Yaani kila kona imeoza! Naona hili taifa lilikumbwa na ugonjwa wa kujilimbikizia mali mtu mmoja mmoja na kupoteza uzalendo kabisa.

Jamani tunaelekea wapi? Mkipewa hivyo vyeo na mkahisi hamtaweza kudeliver ni bora mkatae kabisa kwani bora nusu shari kuliko shari kamili. Ni kutaka ujiko au ni maslahi? mie hata sielewi jamani, duh.
 
Kwa ufupi huyu bwana kwa kuangalia job experience hakustahili kukabidhiwa hii kazi.

Tatizo la Muungwana ni mtu wa watu sometimes anasahau kuwa profit making ni muhimu kwa taifa.

Na ni vizuri kutanguliza maslahi ya taifa mbele kuliko URAFIKI NA KUJUANA.

Sorry Bwana Mataka mimi wala sikujui lakini ndio hisia zangu na sina anything personal against you!
 
Jamani Tanzania kuna makubwaaa. Halafu inashangaza sana kuona watu wanaoihujumu hii nchi ni watu na elimu zao, hapa wataka kuprove nini? Yaani kila kona imeoza! Naona hili taifa lilikumbwa na ugonjwa wa kujilimbikizia mali mtu mmoja mmoja na kupoteza uzalendo kabisa.

Jamani tunaelekea wapi? Mkipewa hivyo vyeo na mkahisi hamtaweza kudeliver ni bora mkatae kabisa kwani bora nusu shari kuliko shari kamili. Ni kutaka ujiko au ni maslahi? mie hata sielewi jamani, duh.

Mkuu Mama

Tanzania siyo suala la Elimu Tanzania ni nani amtawale nani. Hili kuweza kumtawala mwenzako una mzidi kifedha. Hawa watu wanachotafuta ni nguvu ya pesa ndicho kinawafanya KUFANYA ufisadi mKUBWA KIASI hiki.

Ambacho mpaka sasa nashangaa hivi kweli viongozi wetu hawasikii/au hawajui haya? Au ndio tuseme hatuna viongozi?
 
Basi ngoja nimbane Kitila...(Kitila...wewe ungekuwa fisadi ningekuita LiKitila...Lol)

Sasa kama ufisadi wa leo ndio ule ule kama wa siku za nyuma, swali ambalo sijapata jibu lake ni nini kinachosababisha ufisadi? Na kama ufisadi upo hata Marekani, kwa nini wao ufisadi wao haukwamishi maendeleo ya jamii yao na wa kwetu unaonekana unakwamisha maendeleo yetu?

Mwafrika kagusia kidogo na akajikuta anarudi kule kule kwenye ndivyo tulivyo.....na alivyo mjanja akajistukia mapema....Lol

Mkuu ningependa kukujibu wenzetu waliwekeza kwanza na wote wapo satisfied sisi mdomo tuu
we angalia mpaka sasa nchi nzima inategemea daraja la ruvu likivunjika tuu daa inakuwa kisiwa, hata hizo pesa wanzochukua yaani ni muhimu kweli kwa uchumi wa nchi ila basi tu si unajua sera za choyo
 
Ninasikitika kuona kuwa hatua thabiti za kuzuia aibu nyingine isitokee bado hazijachukuliwa.

Katika threads zangu zilizopita juu ATCL nilishauri kuwa ATCL ilipotolewa katika mikono ya South Africans, wazalendo wapewe nafasi ya kuliongoza shirika hilo. Niliendelea kushauri kuwa wazalendo watakaopewa ni vema wakawekewa menejimenti ya kukodi kutoka kwa makampuni yaliyobobea katika kutoa huduma za 'Aviation Management' kwa walau miaka miwili ili kuwapa wazalendo wetu wakati wa kujifunza na kujenga timu ya uongozi. Kama ambavyo nilieleza hapo nyuma kuwa, biashara ya ndege ni moja kati ya biashara ngumu na sophiscated. Unahitaji kuwa na information nyingi na za kutosha wakati wote juu ya kila jambo linalohusu airline industry.

Sasa uendeshaji wa Shirika la ndege unaofanywa sasa hivi ninadiriki kusema ni wa kienyeji sana ukilinganisha na mahitaji halisi ya kimenejimenti yaliyopo ATCL kwa sasa. Hata hivyo bado nina uhakika kuwa uteuzi wa David Mattaka ulikuwa na mapungufu katika mapendekezo yake, ushauri mbaya ulifanyika, na hili litakuja kuigharimu nchi very soon. Nina hakika pia kuwa tangu shirika hilo likabidhiwe rasmi kutoka kwa South Africans linaendelea kuwepo kwa kutumia kodi za wananchi ilhali hakuna faida inayopatikana kwa maana ya bright future

Kwa waandishi wa habari:

(1)Tafadhalini tunaomba mtuletee taarifa kamili za pesa kiasi gani hadi sasa serikali imekwisha toa kuipatia ATCL tangu South Africans walipoondoka.

(2) Ni kiasi gani cha pesa ambacho tayari serikali imeshakilipa kwa South African Airways tangu mkataba uvunjwe hadi leo?

Ninajua ni waandishi wachache ambao wako serious ndiyo wataweza kuandika juu ya hayo hapo juu kwani siyo burning topic na isistoshe baadhi yao wakishakusanya data wanakwenda kuziuza kwa Mattaka.
 
Mkuu Pundam...., hii ilishakuwa bao kwetu wananchi na kwa kweli ukiangalia katika threads zote zilizopita tumehakikisha (kinadharia) kwamba tayari ni bao la kisigino tumepigwa kwa hili!!!

Nakumbuka defensive technique walikuwa wanatumia eti kwa wanaovujisha siri za shirika/kampuni (alikuwa Makongoro huyu....), sasa yako wapi yote yale??
 
Kuna ripoti ya kamati ya Bunge ya miundo mbinu ambayo hadi leo haijawahi kuwaqsilishwa Bungeni juu ya ATCL ni kamati iliyoundwa mwaka 2006,niliwahi kuipata naitafuta niwawekee hapa ili muweze kusoma walitoa mapendekezo mazuri sana .
 
Tuwekee maana naona JF ndo inawaamusha perhaps tukiijadili wataamka na kuchukua hatua za kufaa.
 
Hii ni kwa wale wenye mapenzi mema

Inasemekana wamekuwa wakitumia ndege moja kisa ukosefu wa hela ya matairi ya ndege ,...jamani hawa mabwana wanafanya nini ofisini?

Hii ni kwa taarifa yako kuna mkenya Heho na muhindi Ajay hawa ndio wanaotafuna hela ya kampuni wakishirikiana na mkubwa na wenzake...sasa kwa taarifa tu...wakati hawa mabwana wanateseka na kutokuwa na hela za kulipia matairi...hawa mabwana wako south africa wameidhinisha dollar 17,000
kwa ajili ya kuonyesha product za Airtanzania kwenye maonyesho yanaitwa -----sijui indiaba huko South Africa natumaini wewe mgonja unaetoa hizo hela unajua hili...je haki kuidhinisha pesa kwa ajili ya product Airtanzania .....wana product gani?? Wamekuwa tianshi...mimi nalisikitikia sana natamani ningekuwa nafanya kazi huko nafikiri ningewaumbua kabla hawajanifukuza..

Nimejaribu kuulizia kwa jamaa wa eng tairi ni dollar 4000 moja..kwa 17,000dollar unapata matairi 4 na chenji dollar 1000...jamani hii kampuni watakula mpaka lini? Ndugu yangu mattaka mbona unapoelekea siko na walipokufikiria haya tumwache Jakaya ayaone haya yetu macho??

Hela za matairi hazipo ila za kwenda South Africa kwamaonyesho zipo oooohhh ma GOD..JK WHY?? KWANININI KAKA..............UNAANGAMIZA TAIFA ZIMA SI KAMPUNI PEKEE...................

MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom