ATC Taabani! yaomba serikali Bilioni 7!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,447
39,857
Shirika la ndege la ATC ambalo liko katika hali mbaya ya kifedha linakabiliwa na ukata mkubwa kiasi cha kukimbilia serikalini na kuomba wabebwe tena kwa kupewa ruzuku ya Shilingi bilioni 7! Hii inafuatia deni kubwa walilonalo kwa kampuni ya Wallis Trading ya Liberia ambayo kutoka huko walikodisha lile dege bovu ambalo linaruka kwa masharti magumu la Airbus 320.

Hadi hivi sasa haijajulikana ni lini na kama serikali iko tayari kutoa kiasi hicho cha fedha kuinusuru tena kampuni hiyo ambayo mwishoni mwa mwaka jana chini ya uongozi wa kizembe wa David Mattaka na bodi ya kina Mustaffa Nyang'anyi ilijikuta inalazimia kuingiliwa kati na serikali ili kuwasafarisha mahujaji kwenda na kurudi toka hija takatifu.

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu ndani ya shirika hilo, hali ni mbaya sana kiasi kwamba "tunasubiri bajeti ipite kwa haraka vinginevyo siri za huku zikigundulika tumekwisha". Afisa huyo ambaye amepata nafasi ya kuona barua za kuomba ruzuku hiyo ameiambia KLHN kuwa bila kuletwa kwa wakaguzu huru wa mahesabu ya shirika hilo basi Watanzania kamwe hawatajua kilele cha uzembe na ubadhirifu ndani ya shirika hilo.

Hadi hivi sasa kwa mujibu wa chanzo hicho "ni Rais tu ndiye mwenye uwezo wa kubadilisha kwani alimuweka mshikaji wake hapo na sasa kumuondoa imekuwa mbinde, ndiyo matatizo ya ushkaji hayo".

Chanzo muhimu toka shirika la Wallis Trading lililosajiliwa huko Liberia kimesema kuwa "tumeanza kuchoka kweli na hii ATC tungejua tusingewakodisha Airbus wamekuwa wakituzungumza mno" Jitihada za kumpata kiongozi wa ATC kuzungumzia suala hili zinaendelea.

Kwa habari zaidi tembelea KLH News...
 
Hongera Mzee Mwanakijiji kwa kutimiza post 10,000! Naona hukuamua kununia zile mbili za mwisho!!!!!! Ni dalili ya ukomavu hiyo.

Kuhusu hili shirika. Wote tunajua solution. Liachiwe life.
 
HONGERA SANA MZEE MWANAKIJIJI KUTIMIZA POSTS 10,000 (makumi elfu). KUHUSU ATC, MAONYO YALISHATOLEWA MAPEMA HAPA JF KWAMBA HILI SHIRIKA LINAELEKEA KABURINI KUTOKANA NA INEFFICIENT AND POOR MANAGEMENT. SHILLING BILIONI 7 AMBAZO ATC INAOMBA NASHAURI WANYIMWE KWANI WANAVUNA WALICHOPANDA, WANAKODI NDEGE BILA KUTAFAKARI, WANAKOPA MAFUTA HAWALIPI, WANAKUWA WAJEURI HAWASILIKLIZI USHAURI WA KITAALAM NA WANADEKA KUSUBIRI KUBEBWA BEBWA, KUDADEKI!!!
 
Jamani Ushahiba unaiua nchi hii huyu Bwana hana jipya. JK anasubiri nini asiwatimue wote na bodi yake? Huyu ni fisadi mwingine. Ameshasahau msoto wa kijiweni aliokuwa anakula! Ama kweli kwa muda mfupi jamaa amekwisha jisahau ametokea kijiweni.!!!!!!!
 
Mzee Mkijiji! Hats off for the 10,000posts. Hii ya ATC ni ubadhirifu na ufisadi mtupu. Inatia kichefuchefu kwa Tanzania kukodisha ndege mbovu. Kwani hawawezi kujifunga kibwebwe wakanunua dege jipya moja hata Boeing 747 au 767 ambalo litarudisha hela kwa muda mfupi?
 
Tatizo la serikali ni kuamini kuwa kila kinachosemwa na JF ni uongo ndo matokea yake hayo, tulisema mapema wakati wanajiandaa kukodisha dege bovu kuwa litaua shirika lakini kwa kuwa walikuwa na iterest waliziba masikio na serikali ikatuona waongo na kumtuma kamanda wake makongoro kukoroma bila kuwa na data za ukweli, natamani arudi hapa atwambie kilitokea nini tulichokisema mbona ndo kinachotokea.
 
Mbona naambiwa karibia wanaanza kuruka kwenda Duniani jamani hawa watu ? Hivi JK kweli anaitakia mema Tanzania ?
 
Mzee Mwanakijiji, hongera kwa hiyo mitundiko 10,000!!! Keep up the good work!!!

Kuhusu ATCL nadhani FM hapo juu ameongea kitu kizito na chenye ujumbe mzito sana, "Shirika liachwe life"..... Sensibly, nadhani nami nimefikia wakati nikubali kama walivyosema Wakuu wengine kwenye threads zinazohusu shirika letu la ndege kuwa hatuwezi fanya kitu!!! Yaani na yote yaliyosemwa kutokea mwanzo (Nove/Dec 2007) ambayo yote yalifumbiwa macho whay should we keep on having that ka small hope??

Wawape hizo 7Bil, wasiwape sidhani kama inaweza saidia chochote zaidi ya kutajirisha wachache!!!

Mungu Ibariki Tanzania na Watu wake!!!!
 
Shirika la ndege la ATC ambalo liko katika hali mbaya ya kifedha linakabiliwa na ukata mkubwa kiasi cha kukimbilia serikalini na kuomba wabebwe tena kwa kupewa ruzuku ya Shilingi bilioni 7! Hii inafuatia deni kubwa walilonalo kwa kampuni ya Wallis Trading ya Liberia ambayo kutoka huko walikodisha lile dege bovu ambalo linaruka kwa masharti magumu la Airbus 320.

Mkuu Mwanakijiji, wameshalipa zile Bilioni 7 walizopewa kutoka TCRA kupeleka na kurudisha mahujaji?
 
Shirika la ndege la ATC ambalo liko katika hali mbaya ya kifedha linakabiliwa na ukata mkubwa kiasi cha kukimbilia serikalini na kuomba wabebwe tena kwa kupewa ruzuku ya Shilingi bilioni 7! Hii inafuatia deni kubwa walilonalo kwa kampuni ya Wallis Trading ya Liberia ambayo kutoka huko walikodisha lile dege bovu ambalo linaruka kwa masharti magumu la Airbus 320.

Hadi hivi sasa haijajulikana ni lini na kama serikali iko tayari kutoa kiasi hicho cha fedha kuinusuru tena kampuni hiyo ambayo mwishoni mwa mwaka jana chini ya uongozi wa kizembe wa David Mattaka na bodi ya kina Mustaffa Nyang'anyi ilijikuta inalazimia kuingiliwa kati na serikali ili kuwasafarisha mahujaji kwenda na kurudi toka hija takatifu.

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu ndani ya shirika hilo, hali ni mbaya sana kiasi kwamba "tunasubiri bajeti ipite kwa haraka vinginevyo siri za huku zikigundulika tumekwisha". Afisa huyo ambaye amepata nafasi ya kuona barua za kuomba ruzuku hiyo ameiambia KLHN kuwa bila kuletwa kwa wakaguzu huru wa mahesabu ya shirika hilo basi Watanzania kamwe hawatajua kilele cha uzembe na ubadhirifu ndani ya shirika hilo.

Hadi hivi sasa kwa mujibu wa chanzo hicho "ni Rais tu ndiye mwenye uwezo wa kubadilisha kwani alimuweka mshikaji wake hapo na sasa kumuondoa imekuwa mbinde, ndiyo matatizo ya ushkaji hayo".

Chanzo muhimu toka shirika la Wallis Trading lililosajiliwa huko Liberia kimesema kuwa "tumeanza kuchoka kweli na hii ATC tungejua tusingewakodisha Airbus wamekuwa wakituzungumza mno" Jitihada za kumpata kiongozi wa ATC kuzungumzia suala hili zinaendelea.
Kwa habari zaidi tembelea KLH News...


Siwezi kuamini kwamba mwaandishi makini kama Mzee Mwanakijiji ameshindwa kukaa na habari yake mpaka asikilize upande wa pili alafu ndio atuletee habari kamili...? Sio habari nusu ijaziliwe na wananchi...

Hahaha... sijui uandishi lakini kwa speed hii!!! Taifa linazama...
 
Nimeshazungumzia serikali yetu kutumia watu wenye uzoefu kuendesha mashirika ya umma na ubadhirifu wa pesa za umma.
Tanzania hakuna kuwajibishwa, na pia hakuna kuaibika kwa anayeharibu. Ukiharibu hapa unapewa hongera kwa kupewa kijiwe kingine ili uharibu zaidi. Nadhani bodi nzima ya ATCL ijiuzulu la sivyo mimi najitoa kutumia shirika hilo kwa safari zangu.

Hodi hodi PrecisionAir!!!
 
Siwezi kuamini kwamba mwaandishi makini kama Mzee Mwanakijiji ameshindwa kukaa na habari yake mpaka asikilize upande wa pili alafu ndio atuletee habari kamili...? Sio habari nusu ijaziliwe na wananchi...

Hahaha... sijui uandishi lakini kwa speed hii!!! Taifa linazama...

Upande wa pili gani huo?
 
Siwezi kuamini kwamba mwaandishi makini kama Mzee Mwanakijiji ameshindwa kukaa na habari yake mpaka asikilize upande wa pili alafu ndio atuletee habari kamili...? Sio habari nusu ijaziliwe na wananchi...

Hahaha... sijui uandishi lakini kwa speed hii!!! Taifa linazama...

na kweli taifa linazama kuwa na watu kama Kasheshe ambao hawataki kusema upande wao wa pili bali wanasema tu "uandishi.... kwa speed hii!!!"
 
Mwanakijiji nikupe kwanza hongera kwa posts 10,000 wakati naendelea kutafakari upumbavu unaoendelea hapa nchini.
 
Mattaka cio mshikaji wa JK..ila ni mtu ambaye alikuwa recomended na AC akiwa miundombinu kushika wadhifa huo..huyu jamaa actually ni rafiki ya Maria kejo amabaye ana uhusiano wa karibu na AC..baada ya kumuona jamaa kachoka sana ndo akamwambia jamaa am-hook hiyo nafasi..AC alimwita jamaa na kuongea nae..ktk mazungumzo yao alimwambia ana taarifa zake zote ila anampa 2nd chance lkn kama kawaida ya jambazi/fisi.....
 
Waheshimiwa hivi lile dege limeshaanza safari?

Ndiyo ndege imeanza kuruka kwenda Afrika Kusini.. lakini inaruka kwa hasara! miye yangu macho siku everything is said and done tutajua huyo aliyependekeza tukodishe jidege hilo na kununua mpya toka Hamburg angetiwa pingu siku nyingi tu.
 
Matatizo makubwa ya ATC ni mawili;
  1. Uongozi mbovu. Maelezo yatolewe na aliyemteua Bw. Mattaka ilihali ikijulikana wazi kuwa aliboronga PPF na kuiba. Kama alishindwa PPF ambako operating costs ni ndogo kabisa, inakuwaje akapewa kuendesha shirika linalotegemea uzoefu wa hali ya juu katika kuimprove operating efficiency? Sio kila fundi ni mjuzi wa kutengeneza Mercedes, kama hatuna mbongo mwenye sifa, kwa nini asiajiriwe Mkenya, Mganda, Mzambia, Mhindi, Mmarekani n.k., as long as analipwa within our means, kuliko huyu Mkullo tunayemlipa officially say $3,000 halafu anatuibia $10,000, hiyo ni ukiondoa uzembe wake mwingine na kutojua kazi?
  2. Liquidity. Inajulikana kabisa kuwa ATC wanahitaji mtaji mkubwa ili kufufuka. Kwa nini isiwekwe wazi kiasi wanachohitaji na kwa kipindi kipi, halafu kijadiliwe na kupitishwa bungeni, ili ijulikane wazi kama wana improve au wanadidimia wanapokuja kuomba pesa?
Kasheshe; By the way, Sidhani kama MJJ au mtu mwingine yeyote, anahitajika kubalance habari zake kabla ya kuzileta JF, maana hii sio official news media. Ila akibalance itapendeza zaidi na kuonyesha some professionalism. Good observation anyway.
 
Mattaka cio mshikaji wa JK..ila ni mtu ambaye alikuwa recomended na AC akiwa miundombinu kushika wadhifa huo..huyu jamaa actually ni rafiki ya Maria kejo amabaye ana uhusiano wa karibu na AC..baada ya kumuona jamaa kachoka sana ndo akamwambia jamaa am-hook hiyo nafasi..AC alimwita jamaa na kuongea nae..ktk mazungumzo yao alimwambia ana taarifa zake zote ila anampa 2nd chance lkn kama kawaida ya jambazi/fisi.....

It is hard to believe kuwa JK ni mbumbumbu kuliko mimi kwa jinsi tunavyowajua vigogo wa TZ na viroja vyao. But for the sake of consuming what you have, will take your word kuwa ubavu wa Chenge ndio uliomuweka Mattaka ATC. Lakini itabidi utueleze zaidi ili isije ikawa tunamsafisha JK. Hii ni muhimu ili tusije tukamrundikia AC madudu yote kwa vile tu ashang'atuka. Next itaambiwa kuwa marehemu Ballal ndiye aliyemrecommend kwa AC.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom