MovingForward
JF-Expert Member
- Nov 10, 2009
- 489
- 49
Atakayechakachua matokeo na kuharibu uchaguzi wa wananchi atakumbana na kichapo cha Yehova. kwa taarifa tu ni kwamba tangu mwaka wa jana Watanzania tumeendelea kuomba mbele za Mungu, tena kwa kujinyima kwa ajili ya uchaguzi huu. Mkusanyiko wa maombi hayo yote, upo mbele za Mungu na matokeo yake ndiyo uchaguzi wenye utulivu tulioushuhudia. Sasa, atakayebeba mikoba ya shetani, hata kama anayo heshima kiasi gani, ndani ya nchi, akaharibu na kuvuruga matakwa ya wananchi, atakuwa amejipalia mkaa juu ya kichwa na miguu yake.
Hakika, atapigwa na Mungu kipigo cha mbwa mwizi. Awe ni wa chama cha upinzani au chama tawala, yeyote atakayesababisha kupindisha haki ya watanzania atapigwa.
Hakika, atapigwa na Mungu kipigo cha mbwa mwizi. Awe ni wa chama cha upinzani au chama tawala, yeyote atakayesababisha kupindisha haki ya watanzania atapigwa.