Money Stunna
JF-Expert Member
- Aug 9, 2011
- 13,054
- 6,281
MSANII wa muziki wa kizazi kipya ambaye amejikita kwenye muziki wa mduara zaidi Ally Ramadhani AT, sasa anaitwa baba, kwani mke wake ambaye alifunga naye pingu za maisha amejifungua mtoto wa kike wiki moja iliyopita.
Mtoto wa mkali AT
Wakati mkewe akijifungua AT alikuwa tayari ameshasafiri kwenye nchini Uingereza ambapo ameenda kwa ajili ya show na ameondoka nchini tangu Novemba 4 mwaka huu.
Akiongea na DT, Nipo nje kikazi lakini taarifa ninazo na nashukuru mungu kwani mke wangu ameweza kujifungua bila matatizo na kama unavyojua siku hizi wanawake wajawazito wamekuwa wakipata matatizo sana wakati wa kujfungua, alisema.