Astashahada zazidi kupotea sasa mwendo mdundo ni stashahada 2020

Masiya

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
7,578
7,281
Katika kuangalia NACTE Admission Guide 2020/2021 ya June 15, 2020 nimegundua vyuo vingi vimefuta utunukiwaji wa Technicians Certificate na badala yake wanadahili waombaji kwa program za Ordinary Diploma miaka 3.

Sifa zinazotakiwa kwa ujumla ni zile zile kama za kusoma Technician Certificate. Nafikiri hii ina ashiria wameona Certificate haitoi ujuzi wa kutosha hivyo kuhitaji mtu apige miaka 3 moja kwa moja.

Kwa vyuo vikuu vilivyokuwa viatoa certificate na diploma naona kuna shift ya kuzipunguza wabaki na diploma chache sana.
Ni muhimu waombaji kupitia Guidebook hiyo wanapo chagua nini wakafanye.
 
Dah....hizi si ndio mheshimiwa mkubwa alizikataa hizi? Na mama nae alisema lazima mtu apige advance ndio aende shahada?sielewi
 
Dah....hizi si ndio mheshimiwa mkubwa alizikataa hizi? Na mama nae alisema lazima mtu apige advance ndio aende shahada?sielewi
Diploma za D4 ukiacha masomo ya dini kwa sasa zinakubalika, lakini ukitaka kwenda chuo shahada ni vizuri ukawa makini. Jiridhishe kwa kupitia TCU guide ili ujue nini kinatakiwa kama una diploma.
 
Basi kunauwezekano na TCU nao qualification zao wamezishusha hasa kwenye course za afya
 
Back
Top Bottom