Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 34,632
- 40,790
Aliyewahi kuwa Katibu mkuu wa CHADEMA bwana. Slaa wakati akipinga ujio wa Lowassa Chamani aliwauliza wenzake kama wamepima faida na hasara za ujio huo kabla ya kufanya usajili.
Lakini bila kujali swali hilo nyeti CHADEMA walimpuuza na kuendelea na mapokezi ambayo yamewaingiza shimoni mpaka tunavyozungumza sasa.
Swali hilo la Slaa bado linauhai na linaendelea kuitafuna Chadema kwani ipo wazi kabisa kuwa mpaka sasa hawajajifunza kutokana na makosa waliyoyafanya awali na ushahidi wa hilo ni mapokezi ya hivi karibuni ya kiongozi mwingine toka ccm bila kujali hasara ambayo inatokana na ujio huo.
Inatosha kusema tu, kuwa CHADEMA bado haijafanikiwa kabisa kufumbua fumbo la Asset au libility katika mapokezi ya wanachama wapya toka vyama vingine, na hiyo ni moja wapo ya madhaifu ambayo yataendelea kukigharimu chama hiki kwa muda mrefu sana ujao.
Lakini bila kujali swali hilo nyeti CHADEMA walimpuuza na kuendelea na mapokezi ambayo yamewaingiza shimoni mpaka tunavyozungumza sasa.
Swali hilo la Slaa bado linauhai na linaendelea kuitafuna Chadema kwani ipo wazi kabisa kuwa mpaka sasa hawajajifunza kutokana na makosa waliyoyafanya awali na ushahidi wa hilo ni mapokezi ya hivi karibuni ya kiongozi mwingine toka ccm bila kujali hasara ambayo inatokana na ujio huo.
Inatosha kusema tu, kuwa CHADEMA bado haijafanikiwa kabisa kufumbua fumbo la Asset au libility katika mapokezi ya wanachama wapya toka vyama vingine, na hiyo ni moja wapo ya madhaifu ambayo yataendelea kukigharimu chama hiki kwa muda mrefu sana ujao.