Askofu Shoo akemea utekaji na utesaji wa raia, uvunjifu wa haki na kiburi kilichopo kwa viongozi wa nchi

5ef20c6e6fd4bb1d8047d2c97fd1b11f
Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Frederick Shoo
TABIA ya utekaji, utesaji, unyongaji haki, dhuluma na kiburi inayolalamikiwa nchini, imekemewa vikali na Dk. Frederick Shoo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Anaripoti Mwandishi Wetu, Moshi … (endelea).

Kiongozi huyo wa dini amesema, watu waliompokea Yesu mioyo yao haina kiburi wala majivuno. Amesema, kuna watu wanaotesa wenzao wasiokuwa na hatia jambo ambalo halimfurahishi Mungu.

“Yesu Kristo akatuguse mioyo yetu, tubadilike, tuache kiburi, tuache kuwatesa binadamu wenzetu na tuache kufurahia kuwatesa wenzetu wasio na hatia,” amesema Dk. Shoo.

Licha wateswaji kukumbana na matuio ya kikatili kutoka kwa wenye mamlaka, Dk. Shoo amewatia moyo kwamba, mateso yao hayapotei na kwamba ipo siku mateso ya watesaji yatafika ukomo wake.

“Katika kuteseka kwenu, kwa namna yoyote ile, hata tunapoteswa bila hatia, tujue kwamba Mungu yupo pamoja nasi, hivyo usiogope na usikate tamaa wala kuondoa tumaini lako kwa Mungu, kwani mateso unayokutana nayo kwenye maisha, jua hakika yana mwisho wake,” amesema Dk. Shoo.
Mbona hakukemea wakati wa mauaji ya kibiti. Aidha, sijasikia akikemea wanaotukana na kukejeli viongozi wa nchi kupitia mitandao ya kijamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo dogo na fikirishi.
Maaskofu, mapadri, wachungaji na viongozi mbalimbali wa kiimani, je wao taasisi zao ziko sahihi?
Toa kwanza boriti kwenye jicho lako, utaona kibanzi kwenye jicho la mwenzako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom