Askofu Severine Niwemugizi: Kukosekana kwa taarifa na takwimu za kuaminika kuhusu hali ya Korona kuna hasara zaidi kuliko faida

Usidhani kila mtu ni mbumbumbu kama MATAGA wenzako. Muda wa miaka sita wa NiweMugizi uliisha.

Halafu upumbavu wako unadhani ukardinali unarithiwa.
Naelewa haurithiw lakini angekuwa consistent angeupata sababu nchi zenye wakatoliki wengi Papa huteua Kardinali

Niwemugizi kapwaya hadi Papa kamgwaya kumteua kardinali!!

Sababu sifa ya kardinali hatakiwi kuwa na misuguano na watawala kwenye nchi zenye majority na watawala high office catholics

Niwemugizi anambeza Raisi mkatoliki Magufuli as if he is nobody!!!

Anaenda kinyume na vision ya kanisa Katoliki worldwide ya kutawala dunia!!

Niwemugizi hajapikwa vizuri hata kuwa Askofu!!
 
Watakatifu mashahidi wa Uganda walipewa utakatifu kwa kusuguana na watawala.

Kigezo cha ujasiri katika kanisa katoliki ni kukemea viongozi wanaojidhani wameshindikana kama akina Hitler, Napoleon, Gorbechov.

Naelewa haurithiw lakini angekuwa consistent angeupata sababu nci zenye wakatoliki wengi Papa huteua Kardinali

Niwemugizi kapwaya hadi Papa kamgwaya kumteua kardinali!!

Sababu sifa ya kardinali hatakiwi kuwa na misuguano na watawala kwenye nchi zenye majority na watawala high office catholics

Niwemugizi anambeza Raisi mkatoliki Magufuli as if he is nobody!!!

Anaenda kinyume na vision ya kanisa Katoliki worldwide ya kutawala dunia!!

Niwemugizi hajapikwa vizuri hata kuwa Askofu!!
 
Duh! Hii noma. Taharuki kwa sasa iko juu! Viongozi wa dini wameamua kujilipua.

Mimi binafsi sikuhizi nikiona mitandaoni jina TANZANIA nashtuka nikidhani ni TANZIA.
 
Watakatifu mashahidi wa Uganda walipewa utakatifu kwa kusuguana na watawala.
Sio kweli hawakusuguana na watawala kisiasa waliuawa sababu ya kusali sala ya baba yetu uliye mbinguni ufalme wako uje

Mfalme kabaka alikuwa mpagani walipokuwa wakisali hiyo sala watu wakaenda kuwachongea kwa Mfalme Kabaka kuwa hawa kila siku wanasali wanamuomba mtu asiyeeleweka kuwa ufalme wake uje wewe inaonyesha hawakutaki!!! Wanataka mfalme mwingine aje!!! ndipo akaamuru wauawe kama waasi wanaotaka mfalme mwingine aje kwenye utawala wa mfalme Kabaka.Wale walikuwa wafia dini sio siasa acha kupotosha
 
Hawa maaskofu sasa naona bora wawe wanakutana na kutoa tamko moja, hii biashara inayoendelea sasa kila mmoja kusema lake naona itakuwa ngumu kuwatofautisha na wanasiasa, ni kama vile wanaelekea kuwa wanasiasa wa makanisani.
Unasema Maaskofu hawa 2 wamegeuka kuwa wanasiasa makanisani! Vipi yule mwanasiasa aliuegeuka kuwa Askofu nr 1 kwenye jukwaa la siasa?
 
Ndiyo hivyohivyo. Niwemugizi ksongea kiroho. Halafu mapunguwani wanakimbilia kidunia.

Pia usidhani utaratibu wa kumteua kardinali ni sawa na rais kumteua waziri.

Sio kweli hawakusuguana na watawala kisiasa waliuawa sababu ya kusali sala ya baba yetu uliye mbinguni ufalme wako uje

Mfalme kabaka alikuwa mpagani walipokuwa wakisali hiyo sala watu wakaenda kuwachongea kwa Mfalme Kabaka kuwa hawa kila siku wanasali wanamuomba mtu asiyeeleweka kuwa ufalme wake uje wewe inaonyesha hawakutaki!!! Wanataka mfalme mwingine aje!!! ndipo akaamuru wauawe kama waasi wanaotaka mfalme mwingine aje kwenye utawala wa mfalme Kabaka.Wale walikuwa wafia dini sio siasa acha kupotosha
 
Sasa kelele za nini.? Wewe funga kanisa lako huko ,lock down waumini wako we don't care.we know you don't believe in God.In many countries the church has contributed in starting the war ,plan to kill leaders sometimes was made in the church.


MTAZAMO WA MHASHAMU BABA ASKOFU SEVERINE NIWEMIGIZI WA KANISA KATOLIKI JIMBO LA RULENGE-NGARA

Nawaza kivyangu kwa sauti. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 katika ibara ya 19 (2) inasema hivi: “Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi”.

Kwa kuwa ni hivyo, kwa maoni yangu:

1)Kiongozi wa dini akisubiri aambiwe na mamlaka ya nchi aendeshe ibada au asiendeshe ibada, kufungua au kufunga kanisa hajui haki na wajibu wake.

2) Katika mazingira ya sasa ya janga la COVID 19 kila kona ya dunia ambapo mikusanyiko ya watu wengi inasemekana kuwa hatari kwa maambukizi ya virusi, mtu kusema mikusanyiko ya makanisani au misikitini siyo hatari kwa maambukizi anaudanganya umma na kuuweka hatarini. Sidhani kama Korona inakuogopa huko.

3) Kiongozi wa dini akifikiri kwamba itakuwa halali tu kwa mamlaka ya nchi kusema mikusanyiko hiyo isitishwe na siyo halali kwa kiongozi wa dini kusitisha kwa muda anaepa wajibu wake.

4) Nyuki wakali wakiingia kwenye nyumba ya ibada, kiongozi wa dini ukawaambia waamini wako ingieni tu kwa ibada hamtaumwa kwa kuwa Mungu yuko humo, utakuwa unawatakia mema waamini? Wakiumwa na hata akafa mtu lawama imwendee nani? Mimi najua hata mshumaa ukiobarikiwa unaungua ukiuwasha!

5) Kuna msemo “don’t copy and paste” (usinakili na kuchapisha), kwa ufupi usiige. Ninamfahamu aliyenakili tamko langu kuhusu mali kwa mapadre wa jimbo na kulichapisha kwenye kitabu chake, tena bila kuomba ruhusa kwangu, nami sijamlaumu. Sijamlaumu kwa sababu siyo kosa kuiga jambo zuri. Wataalamu wanatuambia kuna nadharia ya “the best practices”. Kwamba ukiwa na lako jambo si vibaya kujifunza na kutenda ukifuata njia, miongozo au taratibu nzuri zilizowekwa na mamlaka fulani kadiri ya mazingira. Kutotaka kujifunza kwa wengine ni alama ya kiburi, na unaweza kuangamia kwa kung’ang’ania ujinga wako. Bila shaka mjinga naye huwa anaamini yeye ndiye anajua zaidi ya wote.

6) Naamini taarifa na takwimu sahihi ni muhimu kwa kupanga mipango ya maendeleo ya mtu na taifa. Bila hayo ni vigumu kufanya tathmini na kupanga. Naamini kukosekana kwa taarifa na takwimu za kuaminika kuhusu hali ya Korona kuna hasara zaidi kuliko faida.

7) Viongozi wa dini tutende tulivyojifunza namna ya kufanya kazi zetu badala ya kuambiwa cha kufanya na watu ambao hawajui tulifundishwaje huko chuoni.

Niko tayari kupigwa kwa mawe. Bwana awabariki watakaofanya hivyo, maana alisema: “Naam, saa yaja atakapodhania kila awauaye anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi” (Yn 16:2).
 
Wananchi wanaweza kuchanganyikiwa miluzi ni mingi sana!
Hawa wachungaji ni hatari sana uwezo wao wanguvu za kimungu umepotea kaabisa.
Kwa sasa makanisa ni sehemu ya jukusanyia sadaka ili watu wape ujira na sio sehemu ya kupata tumaini la mwenyezi mungu.
Sas kama maaskofubna wachungaji wameanza kuwa na hofu na uwezo wa mungu kwao sasa kanisani wanatupeleka kufanya nini?

Kumbe mungu wa siku hizi anapenda watu wenye afya na raha sio wenye shida, na hao wenye shida hawezi kuwasaidia.
Hii ndio imani haba.

Yule bwana aliyetupwa kwenye shimo la simba kume alikuwa na urafiki na simba ndo maana hawakumla ila tunadanganywa tu kuwa kulikuwa na nguvu ya mungu.
 
TEC haihusiki alitumia madaraka vibaya kisa tu ohhh Askofu ana mamlaka jimboi kwake kujiamlia chochote!!

Niwemugizi kichwa maji ndio maana alinyimwa kuwa Askofu jimbo kuu la Dar es salaam sababu haivi na wenzie too much know!!!

Angeweza hata kuwa mwenyekiti wa baraza la maaskofu Tanzania au kardinali lakini kaachwa akae na ujuaji wake wanapewa vijana anaachwa na u senior wake wa kijeuri
Wewe ni mjinga
Askofu Niwe Mugizi amewahi kuwa mwenyekiti wa TEC huko nyuma,inaonyesha hujui lolote kuhusu kanisa katoliki.
 


MTAZAMO WA MHASHAMU BABA ASKOFU SEVERINE NIWEMIGIZI WA KANISA KATOLIKI JIMBO LA RULENGE-NGARA

Nawaza kivyangu kwa sauti. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 katika ibara ya 19 (2) inasema hivi: “Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi”.

Kwa kuwa ni hivyo, kwa maoni yangu:

1)Kiongozi wa dini akisubiri aambiwe na mamlaka ya nchi aendeshe ibada au asiendeshe ibada, kufungua au kufunga kanisa hajui haki na wajibu wake.

2) Katika mazingira ya sasa ya janga la COVID 19 kila kona ya dunia ambapo mikusanyiko ya watu wengi inasemekana kuwa hatari kwa maambukizi ya virusi, mtu kusema mikusanyiko ya makanisani au misikitini siyo hatari kwa maambukizi anaudanganya umma na kuuweka hatarini. Sidhani kama Korona inakuogopa huko.

3) Kiongozi wa dini akifikiri kwamba itakuwa halali tu kwa mamlaka ya nchi kusema mikusanyiko hiyo isitishwe na siyo halali kwa kiongozi wa dini kusitisha kwa muda anaepa wajibu wake.

4) Nyuki wakali wakiingia kwenye nyumba ya ibada, kiongozi wa dini ukawaambia waamini wako ingieni tu kwa ibada hamtaumwa kwa kuwa Mungu yuko humo, utakuwa unawatakia mema waamini? Wakiumwa na hata akafa mtu lawama imwendee nani? Mimi najua hata mshumaa ukiobarikiwa unaungua ukiuwasha!

5) Kuna msemo “don’t copy and paste” (usinakili na kuchapisha), kwa ufupi usiige. Ninamfahamu aliyenakili tamko langu kuhusu mali kwa mapadre wa jimbo na kulichapisha kwenye kitabu chake, tena bila kuomba ruhusa kwangu, nami sijamlaumu. Sijamlaumu kwa sababu siyo kosa kuiga jambo zuri. Wataalamu wanatuambia kuna nadharia ya “the best practices”. Kwamba ukiwa na lako jambo si vibaya kujifunza na kutenda ukifuata njia, miongozo au taratibu nzuri zilizowekwa na mamlaka fulani kadiri ya mazingira. Kutotaka kujifunza kwa wengine ni alama ya kiburi, na unaweza kuangamia kwa kung’ang’ania ujinga wako. Bila shaka mjinga naye huwa anaamini yeye ndiye anajua zaidi ya wote.

6) Naamini taarifa na takwimu sahihi ni muhimu kwa kupanga mipango ya maendeleo ya mtu na taifa. Bila hayo ni vigumu kufanya tathmini na kupanga. Naamini kukosekana kwa taarifa na takwimu za kuaminika kuhusu hali ya Korona kuna hasara zaidi kuliko faida.

7) Viongozi wa dini tutende tulivyojifunza namna ya kufanya kazi zetu badala ya kuambiwa cha kufanya na watu ambao hawajui tulifundishwaje huko chuoni.

Niko tayari kupigwa kwa mawe. Bwana awabariki watakaofanya hivyo, maana alisema: “Naam, saa yaja atakapodhania kila awauaye anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi” (Yn 16:2).
watu wanaolipwa au kuahidiwa mazuri na mzungu ili kututia hofu serikali yetu ituingize kwenye mkenge wao tumesha wastukia pakubwa.

Mtu kama askofu anaweza andaliwa makao ughaibuni na hana hata watoto yamkini..hivyo hana uchungu wowote wa yeye kua ajenti wa beberu na kusaliti nchi yake.

MUNGU atasimama na dalili za kushinda ni za %90 maana huku mtaani hakuna kitu inaitwa Corona
 
Back
Top Bottom