Kuna best wangu mmoja, longtime kidogo!! Huyu best wangu nilikuwa nakaa nae room moja chuoni. Jamaa alikuwa na mpenzi wake, kwahiyo alikuwa na utaratibu kila weekend( mara nyingi ijumaa jioni!), anachomoka anakuja dar kukutana na demu wake na kurudi mji kasaoro bahari siku ya jumapili jioni! Nilishaizoea ratiba yake hii, na jamaa ilikuwa akisharudi hana stori zingine zadi ya zile zilizohusu yeye na demu wake!
Weekend nyingine ikawadia, mshikaji huyoo akaja zake town! Hii ilikuwa ni jumamosi, na jamaa alitoka Moro asubuhi, huku nikitarajia angerudi siku ya pili yake jioni kabisa kama sio usiku. Hata hivyo, tofauti na kawaida yake, ilipofika jioni ya siku hiyohiyo jamaa akarejea chuoni! Hakuongea wala kumsalimia mtu, badala yake moja kwa moja akapanda kitandani kwake na kujifunika shuka gubigubi!! Hakuongea na mtu hadi siku ya pili yake asubuhi! Nilipomuuliza amekutwa na masahibu gani; akanajibu amekorofishana na mpenzi wake! Namnukuu: Yule demu kanikera kishenzi, nimemwambia kama anataka kufunga ndoa na mimi basi abadili dini lakini kakataa! Mwisho wa nukuu!!
Sio siri, jamaa aliupiga shoti mwili wangu hadi nikahisi nataka kuyeyuka!! Kwavile watu tunafahamiana dini zetu kutokana na majina yetu, nilishangaa sana jamaa aliponiambia kwamba anamtaka demu wake abadili dini! Jamaa anaitwa George na demu wake ni Grace!! Mimi nilishangaa sana kwavile nilichojuwa ni kwamba wote ni Wakristo!! Na pale nilipomuuliza abadili dini gani wakati wote ni wakristo jamaa akanijibu kwamba demu wake ni Lutheran wakati yeye ni RC!! Hapo nikajiuliza, jamaa anaona demu wake si mwenzake kwavile tu yeye ni RC na demu wake ni Lutheran; je mimi kama mshikaji wake ananichukuliaje ambapo mimi ni muislamu na yeye ni mkristo!!
Hapa ninapoongea, hawapo pamoja ingawaje sina hakika ni u-RC na u-Lutheri ndio uliowatenganisha ingawaje hata kama sio basi naamini umechangia!!
Anyway, hoja yangu ya msingi si suala la udini kwenye ndoa, bali mtu kujiona bora kwavile tu yeye ana asili fulani!!
Utaoaje Mmakonde bwana?! Usishangae mtu mzima na akili zake akiuliza swali la kipuuzi kama hilo!! Nachojiuliza ni kwamba, inakuwaje mtu anajiona bora kuliko mwenzake kwavile tu yeye ni Mchaga au Mhaya wakati hajalipa hata senti moja kama ujira wa yeye kuwa Mchaga au Mhaya!!!! Inakuwaje mtu anajiona bora kuliko mwenzake kwavile tu yeye ni mwanaume na mwenzake ni mwanamke wakati hajawekeza hata chembe ya struggle ili yeye awe mwanaume na badala yake amejikuta tu akiwa na hiyo jinsia!!
Inawezekana kabisa mtu huyo akajiona yeye ni bora kwavile tu yeye ni Mchaga kutokana na mafanikio waliyonayo Wachaga!! Hata hivyo, unaweza kukuta Mchaga huyu anaejiona kazi yake ni Shoe Shiner!!! Unaweza kukuta mtu anajiona bora kuliko mwenzake kwavile tu yeye ni Mhaya na mwenzake ni Msukuma! Anajiona bora kwavile anaamini Wahaya ni watu waliopiga Book ile mbaya wakati mwenyewe kaishia Form TWO!!! Hivi utazichukuliaje akili za watu kama hawa?! Hivi utaithaminisha vipi akili ya mtu anayemdharau mwenzake kwavile tu mwenzake huyo ni Mgogo, Mmakonde au Mzaramo wakati anafahamu fika kwamba hajalipa japo punje ya mchanga ili yeye asiwe ni wa chimbuko la makabila hayo anayoyaoona si bora!!
Rafiki yangu George alikuwa hafahamu kwamba yeye ni Mkristo kwavile tu ni mwenyeji wa Iringa, na bila shaka si ajabu angekuwa ni Abdulrahman endapo mungu angeamua chimbuko lake liwe Pangani!! Hafahamu kwamba si ajabu huyu Askofu Pengo tuliyenaye sasa angekuwa ndie Sheikh Yahya Hussein endapo Mungu angeamua huyu Polycarp awe ni mwenye chimbuko la Zanzibar! Si ajabu Wanyakyusa hivi sasa wangekuwa ndo akina Sunni, Shiha, Shafii (Madhehebu ya Kiislamu) endapo hali ya hewa ya Mbeya ingekuwa inalandana na ile ya Arabuni kiasi cha kuwafanya Wakoloni wa Kiarabu kuamishia makazi yao Mbeya badala ya ukanda wa pwani!! Si ajabu waislamu wa leo wangekuwa ndiwo wakristo endapo wazungu wangeamua kupiga kambi zao ukanda wa pwani badala ya bara!! Sasa ya nini mtu kujiona bora kutokana na dini au kabila lake?!
Mentality hii ni mbaya kwavile inafifisha ustawi wa jamii, kuanzia at individual, national to regioanl level! Hata mimi siwezi kushirikiana na mtu anayejiona bora kuliko mwenzie. Leo hii wapo Watanzania wasiopenda ushirikiano wa Afrika Mashariki kutokana tu na tabia ya baadhi ya Wakenya ya wao kujiona bora kuliko wenzao wa TZ au UG, wakati ubora wanaojivunia wala hautokani na mafanikio yao binafsi!! Mkenya huyu atamdharau mwenzake Mtanzania sio kwavile yeye (Mkenya) ana kitu chake binafsi cha kujivunia kuliko huyu mwenzake, bali ni kwavile tu yeye ni Mkenya wakati Ukenya wake ni gift from Nature!!Waswahili wengi hawapendi kushirikiana na ndugu zetu Wa-Tz wenye asili ya asia, hususani bara hindi kwavile tu ndugu zetu hawa wana tabia kujiona bora kuliko wenzao weusi! Usishangae kukuta Mhindi akimdharau mweusi wakati yeye kazi yake ni kuuza duka la Mhind mwenzake pale Kitumbini!!
Hii ni changamoto kwa wale wote wanaozani wao ni bora kuliko wenzao kwa tafsiri yoyote ile. Jamii yenye watu ambao baadhi wanajiona bora kuliko wenzao ni jamii inayotishia ustawi wake wenyewe!! Kusingekuwa na ubaguzi wa rangi SA endapo Makaburu wasingejiona wao ni bora kuliko weusi!
Weekend nyingine ikawadia, mshikaji huyoo akaja zake town! Hii ilikuwa ni jumamosi, na jamaa alitoka Moro asubuhi, huku nikitarajia angerudi siku ya pili yake jioni kabisa kama sio usiku. Hata hivyo, tofauti na kawaida yake, ilipofika jioni ya siku hiyohiyo jamaa akarejea chuoni! Hakuongea wala kumsalimia mtu, badala yake moja kwa moja akapanda kitandani kwake na kujifunika shuka gubigubi!! Hakuongea na mtu hadi siku ya pili yake asubuhi! Nilipomuuliza amekutwa na masahibu gani; akanajibu amekorofishana na mpenzi wake! Namnukuu: Yule demu kanikera kishenzi, nimemwambia kama anataka kufunga ndoa na mimi basi abadili dini lakini kakataa! Mwisho wa nukuu!!
Sio siri, jamaa aliupiga shoti mwili wangu hadi nikahisi nataka kuyeyuka!! Kwavile watu tunafahamiana dini zetu kutokana na majina yetu, nilishangaa sana jamaa aliponiambia kwamba anamtaka demu wake abadili dini! Jamaa anaitwa George na demu wake ni Grace!! Mimi nilishangaa sana kwavile nilichojuwa ni kwamba wote ni Wakristo!! Na pale nilipomuuliza abadili dini gani wakati wote ni wakristo jamaa akanijibu kwamba demu wake ni Lutheran wakati yeye ni RC!! Hapo nikajiuliza, jamaa anaona demu wake si mwenzake kwavile tu yeye ni RC na demu wake ni Lutheran; je mimi kama mshikaji wake ananichukuliaje ambapo mimi ni muislamu na yeye ni mkristo!!
Hapa ninapoongea, hawapo pamoja ingawaje sina hakika ni u-RC na u-Lutheri ndio uliowatenganisha ingawaje hata kama sio basi naamini umechangia!!
Anyway, hoja yangu ya msingi si suala la udini kwenye ndoa, bali mtu kujiona bora kwavile tu yeye ana asili fulani!!
Utaoaje Mmakonde bwana?! Usishangae mtu mzima na akili zake akiuliza swali la kipuuzi kama hilo!! Nachojiuliza ni kwamba, inakuwaje mtu anajiona bora kuliko mwenzake kwavile tu yeye ni Mchaga au Mhaya wakati hajalipa hata senti moja kama ujira wa yeye kuwa Mchaga au Mhaya!!!! Inakuwaje mtu anajiona bora kuliko mwenzake kwavile tu yeye ni mwanaume na mwenzake ni mwanamke wakati hajawekeza hata chembe ya struggle ili yeye awe mwanaume na badala yake amejikuta tu akiwa na hiyo jinsia!!
Inawezekana kabisa mtu huyo akajiona yeye ni bora kwavile tu yeye ni Mchaga kutokana na mafanikio waliyonayo Wachaga!! Hata hivyo, unaweza kukuta Mchaga huyu anaejiona kazi yake ni Shoe Shiner!!! Unaweza kukuta mtu anajiona bora kuliko mwenzake kwavile tu yeye ni Mhaya na mwenzake ni Msukuma! Anajiona bora kwavile anaamini Wahaya ni watu waliopiga Book ile mbaya wakati mwenyewe kaishia Form TWO!!! Hivi utazichukuliaje akili za watu kama hawa?! Hivi utaithaminisha vipi akili ya mtu anayemdharau mwenzake kwavile tu mwenzake huyo ni Mgogo, Mmakonde au Mzaramo wakati anafahamu fika kwamba hajalipa japo punje ya mchanga ili yeye asiwe ni wa chimbuko la makabila hayo anayoyaoona si bora!!
Rafiki yangu George alikuwa hafahamu kwamba yeye ni Mkristo kwavile tu ni mwenyeji wa Iringa, na bila shaka si ajabu angekuwa ni Abdulrahman endapo mungu angeamua chimbuko lake liwe Pangani!! Hafahamu kwamba si ajabu huyu Askofu Pengo tuliyenaye sasa angekuwa ndie Sheikh Yahya Hussein endapo Mungu angeamua huyu Polycarp awe ni mwenye chimbuko la Zanzibar! Si ajabu Wanyakyusa hivi sasa wangekuwa ndo akina Sunni, Shiha, Shafii (Madhehebu ya Kiislamu) endapo hali ya hewa ya Mbeya ingekuwa inalandana na ile ya Arabuni kiasi cha kuwafanya Wakoloni wa Kiarabu kuamishia makazi yao Mbeya badala ya ukanda wa pwani!! Si ajabu waislamu wa leo wangekuwa ndiwo wakristo endapo wazungu wangeamua kupiga kambi zao ukanda wa pwani badala ya bara!! Sasa ya nini mtu kujiona bora kutokana na dini au kabila lake?!
Mentality hii ni mbaya kwavile inafifisha ustawi wa jamii, kuanzia at individual, national to regioanl level! Hata mimi siwezi kushirikiana na mtu anayejiona bora kuliko mwenzie. Leo hii wapo Watanzania wasiopenda ushirikiano wa Afrika Mashariki kutokana tu na tabia ya baadhi ya Wakenya ya wao kujiona bora kuliko wenzao wa TZ au UG, wakati ubora wanaojivunia wala hautokani na mafanikio yao binafsi!! Mkenya huyu atamdharau mwenzake Mtanzania sio kwavile yeye (Mkenya) ana kitu chake binafsi cha kujivunia kuliko huyu mwenzake, bali ni kwavile tu yeye ni Mkenya wakati Ukenya wake ni gift from Nature!!Waswahili wengi hawapendi kushirikiana na ndugu zetu Wa-Tz wenye asili ya asia, hususani bara hindi kwavile tu ndugu zetu hawa wana tabia kujiona bora kuliko wenzao weusi! Usishangae kukuta Mhindi akimdharau mweusi wakati yeye kazi yake ni kuuza duka la Mhind mwenzake pale Kitumbini!!
Hii ni changamoto kwa wale wote wanaozani wao ni bora kuliko wenzao kwa tafsiri yoyote ile. Jamii yenye watu ambao baadhi wanajiona bora kuliko wenzao ni jamii inayotishia ustawi wake wenyewe!! Kusingekuwa na ubaguzi wa rangi SA endapo Makaburu wasingejiona wao ni bora kuliko weusi!