Silent Mafia
Member
- Dec 6, 2017
- 45
- 19
Naomba nimjibu Bishop Gwajima lile swali aliloulizaga kitambo. .MAHARAGE YALE YALIKUA YA TANDAHIMBA.
Hamna popote wanapohatarisha amani ya nchi..Ningekuona una hekima ungeanisha ni sehemu ipi ktk ule waraka unaonyesha maaskofu wanavunja amani ya nchi?
Nimesikiliza kauli ya Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo. Nimesikitika. Na nimegundua mambo mawili:
1. Hajui tena wajibu wake kwa jamii anayoongoza.
2. Amefanya siasa kwa mgongo wa dini. Kwa wanaojua kwamba yeye ni mwanachama wa CCM na rafiki binafsi wa JPM, kauli yake ni sawa na utetezi wa mambo maovu yanayofanywa na serikali anayoipenda. Kwake, bora serikali kuliko kanisa!
Hii ni mara vya pili katika miaka mitatu, anatetea serikali, anapuuza msimamo wa kanisa.
Mwaka 2014 alipingana na kanisa kuhusu katiba inayopendekezwa; akasimama na CCM na serikali.
Kwa kauli na msimamo wake, Kardinali Pengo anafanya siasa chafu dhidi ya kanisa na jamii. Yeye anadhani kuchanganya dini na siasa maana yake ni kukosoa serikali. Haoni kwamba yeye anayeunga mkono serikali anachanganya dini na siasa.
Sasa naona hekima ya kanisa kuweka umri wa maaskofu kustaafu. Kardinali Pengo, ambaye anafikisha umri huo mwakani (2019), angeshauriwa apumzike mapema kuliko kuendelea kukwaza waamini.
Kiukweli, katika hili la kupingana na maaskofu wake, sioni aibu kusema: “he is not my bishop."
Kwanini mnataka Maaskofu wote wawe Chadema.. Askofu anasema hakuna uhuru, wakati wanaongea kila sikuPengo amekuwa akionyesha mapenzi yake waziwazi Kwa Chama cha Mapinduzi kiasi kwamba amekuwa akikingia kifua
Sasa unamwambia nani? Kama wewe hutaki kwenda kanisani kwa sababu ya kauli ya Pengo hiyo ni juu yako.Kesho yangu isingekucha vema bila kutoa ya moyoni, japo najua hakuna wasomaji usiku but potelea mbali.
Nimekuwa nikitafakari sana kauli ya Pengo ambaye inasemekana amesema kwamba "Maaskofu wenzake wanajaribu kuchanganya dini na siasa kwenye waraka wao walioutoa"...