Askofu Pengo: Serikali iwashughulikie wahuni wachoma makanisa

Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki nchini na ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), ‘kudhibiti wahuni wanaotaka kuvuruga amani visiwani humo'.Kauli hiyo ya Pengo ni ya kwanza tangu kuibuka kwa vurugu visiwani Zanzibar mapema mwezi huu, na kusababisha uharibifu wa mali, huku makanisa yakilengwa zaidi na kikundi kinachojiita cha Jumuiya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI).

Pengo alitoa kauli hiyo wakati wa ibada maalumu iliyofanyika katika Kanisa la Msalabani Bagamoyo, mkoani Pwani, ikiwa ni maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, utakaofanyika kwa siku 30 kuanzia jana.

Kardinali Pengo alisema, ‘wahuni hawawezi kuizidi Serikali makini'."Makanisa yetu yamecomwa moto na watu wahuni. Kama Serikali ipo na haiwezi kuchukua hatua dhidi ya wahuni, usalama uko wapi?" alihoji Kardinali Pengo.

"Wahuni wanaweza kutuunguzia makanisa saba kwa mpigo, lakini mbele ya hapo kuna makanisa kadhaa ambayo yalikwishaunguzwa na kubomolewa na hao wahuni," alisema.Pengo aliendelea kuhoji, "Kama sasa wahuni wameishinda nguvu Serikali ya watu kwa hiyo tutawaliwe na wahuni na wafanye lile wanalolitaka, tunajiuliza tunakwenda wapi?

Mara baada ya vurugu za Zanzibar, jopo la maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali, walifanya mazungumzo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), huku wakiituhumu kushindwa kudhibiti vitendo vya uchomaji moto makanisa na kuihadharisha kuchukua hatua za haraka.

Jana, Pengo alilitaka shirika hilo kumsaidia Askofu Augustine Shayo wa Jimbo Katoliki Zanzibar, kuunganisha nguvu zao katika harakati za kuimarisha amani.
Pengo alisema mbali ya vurugu hizo, hivi sasa utumwa bado unandelea kukithiri nchini, hususan kwa viongozi wa Serikali kuwakandamiza wananchi wa hali ya chini.

Alisema wapo baadhi ya viongozi wanaotaka utumwa uendelee kuwapo kutokana na matendo yao dhidi ya wananchi.

"Tanzania ni huru sawa, lakini mimi sitaki kusadiki kuwa ni huru kwa kila mmoja na kila Mtanzania, wapo watu ambao wangependa wao waneemeke hata kwa madhara ya wengi bila huruma hadi siku ya leo," alisema na kuongeza:

"Tangu Shule ya St. Marian inaanzishwa, kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakitaka watoto wao wakasome pale na watoto wa maskini wasipate nafasi."

Alitoboa siri kuwa ‘kuna barua za maombi zisizo za msingi ambazo amekuwa akipelekewa Askofu Shayo na kuzikataa, na wakati mwingine amekuwa akitishiwa maisha, kwani wapo wanaotaka kuwasomesha watoto katika shule nzuri ili waendele kujineemesha. Sasa huu sio utumwa?'
Kardinali Pengo alililitaka Shirika la Roho Mtakatifu kutumia mkutano huo kuendelea kuhimiza amani hapa nchini na kutupia jicho Zanzibar, ambako amani inavurugika kwa matendo ya watu aliowaita wahuni.

Source:Mwananchi Jumatatu
 
Ni bora uwe mganga wa kienyeji kuliko mfuasi wa muhamadans

Sasa hapo ndio na ww unasema nini ? napata uchizi wamtima na upeo na weledi wa akili yako. Nyie mna dini yenu na wao dini yao, ww kuwa na imani yako na wao wawe na imani yao, shida iko wapi ?
 
serikali haiwezi kupambana na uamsho kwa sababu uamsho uko serikalini tayari...its too late..hapa tunasubiri tu kuanza kuuana mitaani..ndo tunakoelekea huko

Vipi mauaji ya Albino nayo yana mkono wa UAMSHO?

Mapigano na mauaji wa wakulima na wafugaji huko Rufiji na kilosa yana mkono wa Uamsho.



Kuuwana mumeanza zamani sana. Msisisngizie uamsho
 
  • Thanks
Reactions: Tom
8D6U8671.JPG


Monday, 25 June 2012 07:56


ASHANGAA SMZ KUZIDIWA NGUVU, UAMSHO YAKUBALI KUSHIRIKI MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Ibrahim Yamola
ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), ‘kudhibiti wahuni wanaotaka kuvuruga amani visiwani humo’.
Kauli hiyo ya Pengo ni ya kwanza tangu kuibuka kwa vurugu visiwani Zanzibar mapema mwezi huu, na kusababisha uharibifu wa mali, huku makanisa yakilengwa zaidi na kikundi kinachojiita cha Jumuiya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI).

Pengo alitoa kauli hiyo wakati wa ibada maalumu iliyofanyika katika Kanisa la Msalabani Bagamoyo, mkoani Pwani, ikiwa ni maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, utakaofanyika kwa siku 30 kuanzia jana.

Kardinali Pengo alisema, ‘wahuni hawawezi kuizidi Serikali makini’.“Makanisa yetu yamecomwa moto na watu wahuni. Kama Serikali ipo na haiwezi kuchukua hatua dhidi ya wahuni, usalama uko wapi?” alihoji Kardinali Pengo.

“Wahuni wanaweza kutuunguzia makanisa saba kwa mpigo, lakini mbele ya hapo kuna makanisa kadhaa ambayo yalikwishaunguzwa na kubomolewa na hao wahuni,” alisema.Pengo aliendelea kuhoji, “Kama sasa wahuni wameishinda nguvu Serikali ya watu kwa hiyo tutawaliwe na wahuni na wafanye lile wanalolitaka, tunajiuliza tunakwenda wapi?

Mara baada ya vurugu za Zanzibar, jopo la maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali, walifanya mazungumzo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), huku wakiituhumu kushindwa kudhibiti vitendo vya uchomaji moto makanisa na kuihadharisha kuchukua hatua za haraka.

Jana, Pengo alilitaka shirika hilo kumsaidia Askofu Augustine Shayo wa Jimbo Katoliki Zanzibar, kuunganisha nguvu zao katika harakati za kuimarisha amani.
Pengo alisema mbali ya vurugu hizo, hivi sasa utumwa bado unandelea kukithiri nchini, hususan kwa viongozi wa Serikali kuwakandamiza wananchi wa hali ya chini.

Alisema wapo baadhi ya viongozi wanaotaka utumwa uendelee kuwapo kutokana na matendo yao dhidi ya wananchi.

“Tanzania ni huru sawa, lakini mimi sitaki kusadiki kuwa ni huru kwa kila mmoja na kila Mtanzania, wapo watu ambao wangependa wao waneemeke hata kwa madhara ya wengi bila huruma hadi siku ya leo,” alisema na kuongeza:

“Tangu Shule ya St. Marian inaanzishwa, kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakitaka watoto wao wakasome pale na watoto wa maskini wasipate nafasi.”

Alitoboa siri kuwa ‘kuna barua za maombi zisizo za msingi ambazo amekuwa akipelekewa Askofu Shayo na kuzikataa, na wakati mwingine amekuwa akitishiwa maisha, kwani wapo wanaotaka kuwasomesha watoto katika shule nzuri ili waendele kujineemesha. Sasa huu sio utumwa?’
Kardinali Pengo alililitaka Shirika la Roho Mtakatifu kutumia mkutano huo kuendelea kuhimiza amani hapa nchini na kutupia jicho Zanzibar, ambako amani inavurugika kwa matendo ya watu aliowaita wahuni.

Mkutano wa Shirika

Kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, Padre John Kuff kutoka Ghana, mkutano huo unafanyika Afrika kwa mara ya kwanza, tangu kuanzishwa kwa shirika hilo mwaka 1868.

Tanzania ni mwenyeji wa mkutano huo wa 20 ambao umekuwa ukifanyika kila baada ya miaka sita, na mkutano wa mwisho ulifanyika Ureno mwaka 2004.
Baadhi ya nchi zitakazoshiriki mkutano huo ni Canada, Nageria, Ureno, Ufaransa, Ghana, Uingereza, Irand na mwenyeji Tanzania.”

Akizungumzia shirika hilo, Pengo alisema wakati linaanza kazi nchini walikuta amani imevurugika, lakini walifanya kazi kubwa amani ikarejea, hivyo alilitaka kusimamia ukweli hata kama watu wengine watawabeza.

Kipozi aahidi amani
Akitoa salamu za Serikali kanisani hapo, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi alisema washiriki wa mkutano huo wawe na amani kwani ulinzi utaimarishwa wakati wote.

“Kwa siku zote 30 za mkutano huu ulinzi na usalama utaimarishwa ili kuhakikisha mnafikia malengo yenu,” alisema Kipozi.

 
Mimi naona Pengo hapa wenzake wamemwingiza choo cha Kike naye pasi aibu yoypte amekubali kuingia pasi na kufanya utafiti.

Mimi ningemshauri kuwa KWANZA ONDOA KIBANZI JICHONI KWAKO KABLA KUTOA KWA MWENZAKO.

Nini tamko lake dhidi ma fujo na mauaji ya vurugu baina ya wakulima na wafugaji huko RUFIJI. Mabona amelikalia kimya hilo na kuamua kuvuka maji.


Ni vizuri ajuwe nguvu zake Pengo mwisho Chumbe. Znz hana bao. Znz ni nchi kamili na ina mipaka yake. Soma katiba ya Znz ibara ya kwanza imebainisha hayo.

Pengo hajateuliwa wala kuchaguliwa na Wazanzibari wala Watanganyika! Mamlaka yake kapewa na Papa. Hata Zanzibar kuna Askofu kateuliwa na Papa. Askofu wa Zanzibar yuko chini ya Pengo kwa hiyo Pengo ana mamlaka juu ya Zanzibar katika maswala ya ukristo katoliki.

Bwana Baru kuwa mwelewa!
 
Source -TBC 1
Askofu mkuu wa katoliki( PENGO), ameiagiza serikali kupamba na watu wanao onekana kuleta uvunjifu wa amani nchini.

Askofu ame yasema hayo katika semi ya mapadri iliyokuwa inafanyika bagamoyo na kusisitiza amani na utulivu nchini.

Akionekana kukerwa na vitendo vya uchomaji wa makanisa vilivyo tokea huko zanziba ,Askofu ameiomba serikali kuwa shughulikia walio husika na vitendo hivyo kwa kutumia myamvuri ya dini kwa kuwa ni wa huuni tu na wachochezi.

PENGO amesema uchomaji wa makanisa haukuanza leo, serikali inapaswa kuwashughulikia wa husika.

Naungana na pengo kuwasihi wapenda amani na waelewa kutotumia dini kwa maslai yao,dini itumike kuleta amani na upendo baini yetu.

Hivyo serikali inapaswa kuchukua hatua stahiki kwa kikundi,vyombo vya habari au mtu ambaye anaonekana kuwa chachu ya uvunjifu wa amani na uchochezi.

Kabisaa..ni uhuni tu bila hata maelezo. Dunia hii haitakuja kuwa na dini moja sababu maana kila mtu ana hiari ya kufuata kile anachotaka kufuata. Kisa nini kulazimishana kuamini kitu bila ridhaa ya muhusika?
 
jamaa baada ya kumaliza kula pesa za LOWASA kaibuka? EPA vs richomond ikiingia makanisani. madatkari hugoma
 
ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), ‘kudhibiti wahuni wanaotaka kuvuruga amani visiwani humo’.Kauli hiyo ya Pengo ni ya kwanza tangu kuibuka kwa vurugu visiwani Zanzibar mapema mwezi huu, na kusababisha uharibifu wa mali, huku makanisa yakilengwa zaidi na kikundi kinachojiita cha Jumuiya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI).

Pengo alitoa kauli hiyo wakati wa ibada maalumu iliyofanyika katika Kanisa la Msalabani Bagamoyo, mkoani Pwani, ikiwa ni maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, utakaofanyika kwa siku 30 kuanzia jana.

Kardinali Pengo alisema, ‘wahuni hawawezi kuizidi Serikali makini’.“Makanisa yetu yamecomwa moto na watu wahuni. Kama Serikali ipo na haiwezi kuchukua hatua dhidi ya wahuni, usalama uko wapi?” alihoji Kardinali Pengo.

“Wahuni wanaweza kutuunguzia makanisa saba kwa mpigo, lakini mbele ya hapo kuna makanisa kadhaa ambayo yalikwishaunguzwa na kubomolewa na hao wahuni,” alisema.Pengo aliendelea kuhoji, “Kama sasa wahuni wameishinda nguvu Serikali ya watu kwa hiyo tutawaliwe na wahuni na wafanye lile wanalolitaka, tunajiuliza tunakwenda wapi?

Mara baada ya vurugu za Zanzibar, jopo la maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali, walifanya mazungumzo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), huku wakiituhumu kushindwa kudhibiti vitendo vya uchomaji moto makanisa na kuihadharisha kuchukua hatua za haraka.

Jana, Pengo alilitaka shirika hilo kumsaidia Askofu Augustine Shayo wa Jimbo Katoliki Zanzibar, kuunganisha nguvu zao katika harakati za kuimarisha amani.
Pengo alisema mbali ya vurugu hizo, hivi sasa utumwa bado unandelea kukithiri nchini, hususan kwa viongozi wa Serikali kuwakandamiza wananchi wa hali ya chini.

Alisema wapo baadhi ya viongozi wanaotaka utumwa uendelee kuwapo kutokana na matendo yao dhidi ya wananchi.

“Tanzania ni huru sawa, lakini mimi sitaki kusadiki kuwa ni huru kwa kila mmoja na kila Mtanzania, wapo watu ambao wangependa wao waneemeke hata kwa madhara ya wengi bila huruma hadi siku ya leo,” alisema na kuongeza:

“Tangu Shule ya St. Marian inaanzishwa, kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakitaka watoto wao wakasome pale na watoto wa maskini wasipate nafasi.”

Alitoboa siri kuwa ‘kuna barua za maombi zisizo za msingi ambazo amekuwa akipelekewa Askofu Shayo na kuzikataa, na wakati mwingine amekuwa akitishiwa maisha, kwani wapo wanaotaka kuwasomesha watoto katika shule nzuri ili waendele kujineemesha. Sasa huu sio utumwa?’
Kardinali Pengo alililitaka Shirika la Roho Mtakatifu kutumia mkutano huo kuendelea kuhimiza amani hapa nchini na kutupia jicho Zanzibar, ambako amani inavurugika kwa matendo ya watu aliowaita wahuni.

Mkutano wa Shirika

Kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, Padre John Kuff kutoka Ghana, mkutano huo unafanyika Afrika kwa mara ya kwanza, tangu kuanzishwa kwa shirika hilo mwaka 1868.

Tanzania ni mwenyeji wa mkutano huo wa 20 ambao umekuwa ukifanyika kila baada ya miaka sita, na mkutano wa mwisho ulifanyika Ureno mwaka 2004.
Baadhi ya nchi zitakazoshiriki mkutano huo ni Canada, Nageria, Ureno, Ufaransa, Ghana, Uingereza, Irand na mwenyeji Tanzania.”

Akizungumzia shirika hilo, Pengo alisema wakati linaanza kazi nchini walikuta amani imevurugika, lakini walifanya kazi kubwa amani ikarejea, hivyo alilitaka kusimamia ukweli hata kama watu wengine watawabeza.

Kipozi aahidi amani
Akitoa salamu za Serikali kanisani hapo, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi alisema washiriki wa mkutano huo wawe na amani kwani ulinzi utaimarishwa wakati wote.

“Kwa siku zote 30 za mkutano huu ulinzi na usalama utaimarishwa ili kuhakikisha mnafikia malengo yenu,” alisema Kipozi.
Sourrce Gazeti Mwananchi ya Leo.
 
Naunga mkono hoja ila pia nina swali kwa Pengo. Kwani makanisa yamechomwa jana? Kwa nini msimamo wake umekawia sana? Tukisema ni mtu wa kupima upepo kwanza katika issue muhimu za kitaifa kuangalia bendera inakoelekea tumekosea?
My take: serikali ya sisiem inapenda sana viongozi wenye kusubiri kwanza upepo upite ndipo watoe maamuzi ima ni magumu au mepesi kwa namna ya kadinali Pengo. Na kwa njia hii sii hata kidogo serikali inaweza kubadilika ama kuchukua maamuzi magumu.
.

Huwa kanisa halipo kwajili ya kulipiza kisasi na kanisa halikurupuki na Kwakiongozi mkubwa kama Pengo hawezi kukurupuka ni lazima atume watu wake wafanye utafiti wa kutosha ili akiongea aongee kitu chenye uhakina.

Serekali ndiyo ilitakiwa kuchukua hatua mapema maana wana dola na kazi ya serekali ni kulinda usalama wa raia na mali zake,Pengo hata angeongea siku ile ile natumaini isengekuwa na maana sana sana kwa wale wanauamsho ndiyo wangeona tunajibizana nao na ingeongezeka machafuko
 
kitendo cha uchomaji kanisa ni cha kulaaniwa na kila mpenda amani. lazima tuvumiliane kidini. tusipovumiliana, tunaweza kuelekea ktk fitna za kidini kama za nigeria. Mungu atujalie tusifike huko! amen!

pengo anaposema wahuni sidhani kama anamaanisha uamsho. hapa siasa ipo. aliechoma makanisa alifanya hivyo kwa msingi wa siasa. watanzania kuzuiwa kujadili muungano wautakao kwa kina, kumewaudhi wengi na khasa wazanzibari.

Wao wanaona kuwa wameonewa! hasira zao wakazipeleka kwenye kuchoma makanisa! nimewahi kufanya kazi znz kwa muda wa miaka 2. wao wanahisi kuwa bara inawakandamiza. hivi ili watulize hasira zao, huushambulia ukristo na mali za wakristo. hili siyo sahihi. serikali iwape uhuru. kama wanataka kuvunja muungano, waruhusiwe kufanya hivyo.

Wakilazimishwa, wataendelea kuchoma makanisa na huku bara wakristo wakichoma miskiti na waislamu wa bara wakajibu mapingo, nchi haitotawalika. wakristo na waislamu tunaishi kama ndugu kwa kuvumiliana.tuendelee kuishi hivyo!
 
Pengo hajateuliwa wala kuchaguliwa na Wazanzibari wala Watanganyika! Mamlaka yake kapewa na Papa. Hata Zanzibar kuna Askofu kateuliwa na Papa. Askofu wa Zanzibar yuko chini ya Pengo kwa hiyo Pengo ana mamlaka juu ya Zanzibar katika maswala ya ukristo katoliki.

Bwana Baru kuwa mwelewa!

Kwani Pengo anaweza kuwa na mamlaka Kenya au Uganda?

Je umesoma Katiba ya Znz ibara a kwanza?
 
Kama ni rahisi njoo wakamate wewe tumechoka na sera za kujaza makinisa z'bar bila kuwa na waumini hilo ni onyo na yatazidi kuchomwa ikiwa mtaendelea na upuuzi wenu huo hatupendi makanisa na dini yenu ya kuekti
Hebu tueleze hapa tawi lako ni lipi na unalipwa na nani? Alquaeda? Alshaabab? Boko haram? mna lengo gani mnapoyachoma makanisa? mpango wa muda mrefu ni upi? Kuwachinja wakristo? Unataka muishi peke yenu? Huu uharamia mlifundishwa na nani? Your days are numbered just wait a bit!
 
Kwani Pengo anaweza kuwa na mamlaka Kenya au Uganda?

Je umesoma Katiba ya Znz ibara a kwanza?
Pengo hana mamlaka Kenya wala Uganda kwa kuwa hizo ni dola. Zanzibar siyo DOLA, bali ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya amiri jeshi mkuu Kikwete na mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ni Mwamunyange.

Au nalo hili hujui?
 
Mimi naona Pengo hapa wenzake wamemwingiza choo cha Kike naye pasi aibu yoypte amekubali kuingia pasi na kufanya utafiti.

Mimi ningemshauri kuwa KWANZA ONDOA KIBANZI JICHONI KWAKO KABLA KUTOA KWA MWENZAKO.

Nini tamko lake dhidi ma fujo na mauaji ya vurugu baina ya wakulima na wafugaji huko RUFIJI. Mabona amelikalia kimya hilo na kuamua kuvuka maji.


Ni vizuri ajuwe nguvu zake Pengo mwisho Chumbe. Znz hana bao. Znz ni nchi kamili na ina mipaka yake. Soma katiba ya Znz ibara ya kwanza imebainisha hayo.
Wewe mbona umevuka mipaka na kuja huku kumzungumzia pengo,acha uzandiki wewe.Pengo amesema wahuni wanaochoma makanisa,je wewe ni wakili wa wahuni?muungano wa znz na bara haukuasisiwa na kanisa. wawakilishi wa waasisi wapo,mbona hamchomi nyumba na maofisi yao,au kwa sababu kanisa na bar havina jeshi.Na kama mnasema kuwa waumini wa kikristo ni wachache znz,hayo ma-bar yanayoongezeka mnamaanisha yanajiendesha kwa hasara,kama jibu ni hapana wateja wa bar hizo wanatoka wapi? Unatakiwa kujua kuwa moja ya majukumu ya viongozi wa dini ni kukemea vitendo viovu bila kuwa na mipaka,sasa unata kuniambia kuwa zanzibar ni wapi huko ambako pengo hawezi kuona na kukemea vitendo hivyo vya uamsho a.k.a alshabab a.k.a boko haram a.k.a alcaeda.Binafsi siwapingi viongozi wa uamsho kwa sababu ya rangi yao,nawapinga kwa sababu ya maneno na vitendo vyao,kwani kama zanzibar mnataka uhuru wa kweli,nini basi kikwazo ktk kufikia malengo yenu,ni makanisa,ni bar, ni ukristo au ni nini?tuwekeni wazi basi tumjue adui yenu namba moja ktk kufikia malengo ya kuwa na znz ya maziwa, asali na mafuta.Na kama hujui unakokwenda,njia yoyote ile itakufikisha. nawasilisha
 
Pengo hajateuliwa wala kuchaguliwa na Wazanzibari wala Watanganyika! Mamlaka yake kapewa na Papa. Hata Zanzibar kuna Askofu kateuliwa na Papa. Askofu wa Zanzibar yuko chini ya Pengo kwa hiyo Pengo ana mamlaka juu ya Zanzibar katika maswala ya ukristo katoliki.

Bwana Baru kuwa mwelewa!

Kama si kwa mujibu wa mawazo yako, ni kifungu gani cha utaratibu wa Kanisa katoliki kinachompa Polycarp Pengo mamlaka juu ya Askofu wa Zanzibar.
 
Back
Top Bottom