Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, amevitaka vyama vya siasa na serikali kwa ujumla kuacha mara moja kuwazuia watu wanaodaiwa kuwa mafisadi kwenda kupata huduma za kiroho.
Kauli ya Kardinari Pengo imekuja siku chache baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, kusema mafisadi walioenguliwa na chama hicho wanataka kuwatumia viongozi wa dini ili kujisafisha.
Pengo alitoa rai hiyo jana baada ya kuhitimisha ibada ya misa takatifu ya sikukuu ya Pasaka katika Kanisa la Mt Vinsent wa Paulo, wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani.
Kanisa Katoliki halitamfukuza mtu yeyote yule anayedaiwa na serikali au chama kuwa ni fisadi eti asipate huduma zinazomstahili! Kanisa litampokea iwapo ni muumini mzuri na amekwenda kwa ajili ya kupata huduma za kiroho, alisema.
Kumtenga mtu ni kosa. Mbona Yesu hakumkataa Maria Madgalena na Zakayo mtoza ushuru sasa iweje leo kanisa liwatenge watu wanaodaiwa kuwa ni mafisadi huku wakiwa ni waumini wa kanisa?
Aidha, alisema iwapo mtu hakubaliki katika chama si kweli kuwa na katika kanisa hakubaliki kwa kuwa chama na kanisa ni vitu viwili tofauti. Alisema vyama vinahitaji watu wasafi, lakini kanisa linahitaji wenye dhambi (watu wachafu) ili wapate kutubu na kumrudia Mungu ndio maana Yesu alikuja kwa ajili ya watu wagonjwa na si wazima.
Source: Tanzania Daima
Kauli ya Kardinari Pengo imekuja siku chache baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, kusema mafisadi walioenguliwa na chama hicho wanataka kuwatumia viongozi wa dini ili kujisafisha.
Pengo alitoa rai hiyo jana baada ya kuhitimisha ibada ya misa takatifu ya sikukuu ya Pasaka katika Kanisa la Mt Vinsent wa Paulo, wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani.
Kanisa Katoliki halitamfukuza mtu yeyote yule anayedaiwa na serikali au chama kuwa ni fisadi eti asipate huduma zinazomstahili! Kanisa litampokea iwapo ni muumini mzuri na amekwenda kwa ajili ya kupata huduma za kiroho, alisema.
Kumtenga mtu ni kosa. Mbona Yesu hakumkataa Maria Madgalena na Zakayo mtoza ushuru sasa iweje leo kanisa liwatenge watu wanaodaiwa kuwa ni mafisadi huku wakiwa ni waumini wa kanisa?
Aidha, alisema iwapo mtu hakubaliki katika chama si kweli kuwa na katika kanisa hakubaliki kwa kuwa chama na kanisa ni vitu viwili tofauti. Alisema vyama vinahitaji watu wasafi, lakini kanisa linahitaji wenye dhambi (watu wachafu) ili wapate kutubu na kumrudia Mungu ndio maana Yesu alikuja kwa ajili ya watu wagonjwa na si wazima.
Source: Tanzania Daima