BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI ISITISHE ZOEZI LA UTEUZI WA WAGOMBEA KATIKA MAJIMBO YALIYO NA KASORO.
Kanuni ya Dhahabu (golden principle) inasema: "Siyo tu kuwa Haki itendeke, bali Haki ionekane kuwa imetendeka"! Katika mchakato wa Urudishaji fomu kuna vituko na shida mbalimbali ikiwemo baadhi ya Wagombea kutekwa, kuvamiwa, kukamatwa na Jeshi la Polisi, kuporwa Fomu nk. Tume inao wajibu katika kutunza amani na utulivu wa nchi kwa kuhakikisha kuwa haki inatendeka.
Tume haiwezi kuendelea na Uchaguzi katika Majimbo ambayo baadhi ya Wagombea wameenguliwa kimabavu na hila nje ya Mfumo wa Sheria. Tunatoa wito kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kusitisha mchakato wa Urudishaji Fomu katika Majimbo yaliyokumbwa na matatizo. Tunapenda kuona Haki inatendeka na ionekane kuwa imetendeka (Zaburi 101).
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
Kanuni ya Dhahabu (golden principle) inasema: "Siyo tu kuwa Haki itendeke, bali Haki ionekane kuwa imetendeka"! Katika mchakato wa Urudishaji fomu kuna vituko na shida mbalimbali ikiwemo baadhi ya Wagombea kutekwa, kuvamiwa, kukamatwa na Jeshi la Polisi, kuporwa Fomu nk. Tume inao wajibu katika kutunza amani na utulivu wa nchi kwa kuhakikisha kuwa haki inatendeka.
Tume haiwezi kuendelea na Uchaguzi katika Majimbo ambayo baadhi ya Wagombea wameenguliwa kimabavu na hila nje ya Mfumo wa Sheria. Tunatoa wito kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kusitisha mchakato wa Urudishaji Fomu katika Majimbo yaliyokumbwa na matatizo. Tunapenda kuona Haki inatendeka na ionekane kuwa imetendeka (Zaburi 101).
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani