Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,409
NI NANI WA KUIONYA TBC KUACHA UPENDELEO?!
TBC inaongozwa na AYUBU RYOBA,huyu ni mhafidhina aliyegeuka kuwa mwimba kwaya.
ameharibu sana TBC na kimekuwa chombo cha chama badala ya UMMA.
Kumbuka amekuwa akimdanganya mkuu kwamba TBC hakuna matatizo na pia amekuwa akifanya ujanja ujanja ili JPM asifanye ziara pale TBC, na pia hasikilizi ushauri wa kitaalam hasa kwa watu wa procurement ,na wengineo.
SAFARI CHANNEL imepata vyombo vya kisasa kabisa kwa maagizo cha JPM lakini hii TBC ! hakuna kitu kabisa.
Watu wanalipa kodi! Kodi zao zinatumika kulipa gharama za uendeshaji wa TBC ikiwemo kuwalipa mishahara waandishi wa habari, wapiga picha na watangazaji wake! Sehemu ya hao walipa kodi wanasikika wakilalamika kuwa TBC wanapendelea CCM! Wanahoji kwa nini TBC inatangaza mubashara mikutano ya CCM lakini haiwezi kutangaza mubashara mikutano ya vyama vikuu vya Upinzani kikiwemo CHADEMA na ACT Wazalendo!
Ni wajibu wa Askofu kuwatuliza watu hawa wasikasirike na waendelee kuwa watulivu, lakini pia ni wajibu wa Askofu kuwakemea wenye mamlaka ya kuendesha, kusimamia na kuiagiza TBC kuwa vitendo hivyo vya upendeleo visipokoma vitaichafua nchi! Kwa sababu hiyo basi, tunawaonya Uongozi wa TBC na wale wote wenye mamlaka ya kuisimamia na kuiagiza TBC watambue kuwa hasira dhidi ya TBC huku uraiani kutoka sehemu ya Watanzania wasio wana CCM inazidi kujaa katika kikombe cha ghadhabu! Ni wajibu ya wenye mamlaka kulirekebisha hili mapema iwezekanavyo!
Mimi nimetimiza wajibu wangu kama Askofu (Ezekieli 33:1-20)
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
From Askofu Mwamakula