BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,009
Mamlaka zote duniani zinazofinya haki, uhuru wa kujieleza, uhuru wa kujumuika, demokrasia, nk hufanya mambo yanayofana kama vile: kutumia Majeshi na Idara za Usalama kuwadhibiti, kuwatisha na hata kuwatesa wapinzani, wakosoaji na watetezi wa haki; kutumia Idara za Usalama na pesa katika kudhoofisha upinzani kwa kuugawa na hata kuwanunua baadhi ya viongozi wenye ushawishi na ikishindikana, basi kuwaua baadhi kwa njia mbalimbali; kutumia Vyombo vya Habari katika kujisafisha mbele ya umma kwa kupamba Sera za Serikali, na kuwasifia viongozi, nk;
Pia, hulitumia Bunge katika kutunga sheria za kukandamiza upinzani na kuwalinda watawala; hutumia Mahakama kuwahukumu wapinzani, wakosoaji na wanaharakati kupitia kesi za 'uchochezi', 'uhaini', nk; huondoa uhuru wa taasisi muhimu kama vile Tume za Uchaguzi, Mahakama, Bunge, Vyombo vya Habari, nk na kuviweka chini ya udhibiti wa Serikali; hudhibiti taasisi za dini kwa kuhakikisha kuwa viongozi wa taasisi hizo wanakuwa ni wale wanaounga mkono watawala; hufanya chaguzi bandia ili kuudanganya ulimwengu kuwa kuna demokrasia; huunda vyama bandia vya upinzani ili kuudanganya ulimwengu ambapo viongozi wa vyama hivyo huwa sehemu ya mfumo; hutumia nguvu kubwa katika kuvidhibiti vyama vya upinzani vinavyoonyesha upinzani wa dhati kwa kuhakikisha kuwa havipati fursa ya kutumia vyombo vya habari, kueneza sera, kufanya mikutano na maandamano, nk.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
Pia, hulitumia Bunge katika kutunga sheria za kukandamiza upinzani na kuwalinda watawala; hutumia Mahakama kuwahukumu wapinzani, wakosoaji na wanaharakati kupitia kesi za 'uchochezi', 'uhaini', nk; huondoa uhuru wa taasisi muhimu kama vile Tume za Uchaguzi, Mahakama, Bunge, Vyombo vya Habari, nk na kuviweka chini ya udhibiti wa Serikali; hudhibiti taasisi za dini kwa kuhakikisha kuwa viongozi wa taasisi hizo wanakuwa ni wale wanaounga mkono watawala; hufanya chaguzi bandia ili kuudanganya ulimwengu kuwa kuna demokrasia; huunda vyama bandia vya upinzani ili kuudanganya ulimwengu ambapo viongozi wa vyama hivyo huwa sehemu ya mfumo; hutumia nguvu kubwa katika kuvidhibiti vyama vya upinzani vinavyoonyesha upinzani wa dhati kwa kuhakikisha kuwa havipati fursa ya kutumia vyombo vya habari, kueneza sera, kufanya mikutano na maandamano, nk.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki