Askofu Mwamakula Atangaza siku saba mfululizo za maombi kumshitakia Mungu juu ya uonevu aliofanyiwa Freeman Mbowe

haya maombi ayatofautiani na ya sheikh Kishki kumuomba Yarabi amtoe roho afande Sele lakini mpka leo jamaa anadunda tu.
Hayo maombi hayakuvuka hata dari la nyumba yake.

Kosa la afande Sele lilikuwa lipi?
 
Watumishi wajinga hawa.
Kuna miaka mmoja naye maeneo ya Mwenge aliwahi kutoa unabii, ambao haukutimia.
Hivi askofu anakuwa na chama je washiriki wake wakiwa tofauti na chama chake si atakuwa kazi kuwaombea laana
 
haya maombi ayatofautiani na ya sheikh Kishki kumuomba Yarabi amtoe roho afande Sele lakini mpka leo jamaa anadunda tu.
Kumbukumbu:
Mchungaji mmoja alionya kuhusu kangi kukufuru kwani ni kwamba anamwombea mabaya rais,, hakuna aliyejali. Tunapoongea leo Kangi alishindwa ubunge na huyo rais akafariki dunia.
Gwajima alimtamkia adhabu makonda ,,hakuna aliyejali ,,makonda si mkuu wa mkoa tena.

KUMBUKUMBU,, You will never see it coming.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
kwanini asiseme aombewe kwa mwaka mzima?!!!! si hana kazi, atangaze mwaka kabisa tujue kuwa yuko serious
 
wanasiasa wa kiafrika wanajiona wanaharakati na kutafuta huruma kwa kupambana na vyombo vya dola. Huyu Abubakari Shekau Hata akiachiwa atatafuta namna nyingine awekwe tena korokoroni.
 
Freeman Mbowe hajafanyiwa uonevu wowote.

Yeye alitangaza mapambano na rais Samia , je alitegemea rais wa nchi atapambana naye face to face au atapambana na vyombo vilivyo chini yake?

Aliposema hatupo tayar kumpa muda rais kuhusu katiba maana yake ni kuwa watapambana nae.
 
Huyu askofu naye ni mpuuzi na kilaza.kwanza ashugulike na corona.kumuombea gaidi ni sawa na kumpalia makaa ya Moto kichani,maombi yatageuka kuwa pigo kwa gaidi.atasababisha majanga makubwa bule kwa gaidi ,bola akaushe tu!
 
View attachment 1870225

Niwakumbushe wenye madaraka nchi hii

1. Askofu Mwamakula na Sheikh Ponda waliomba dua ya Maangamizi kwa ambao wangeshiriki kuvuruga uchaguzi wa mwaka 2020, Nyote mnaona leo yule mvurugaji mkuu katwaliwa mapema kabisa hata miezi 6 ya kipindi cha pili hakuifaidi

7. Leo Askofu anatangaza dua kuhusu suala la Mbowe.

Hizi dua zichukulieni poa tu, lakini Siyo za kufanyia mchezo.
Zikianza kuwatafuna, msitafute mchawi!

ZABURI 20:7

"...Wengine hujigamba kwa magari ya vita; wengine kwa farasi wao. Lakini sisi tunajivunia Mwenyezi Mungu, Mungu wetu..."


AMINA, na iwe hivi...!!

Mimi nitashiriki maombi haya kuanzia leo...

Kama watazuia kukasanyika, msipate tabu wala mtu asisikitike...

Na kamwe msilazimishe kukusanyika kimwili kwa sababu watawaumiza kweli kama waseamavyo mara kwa mara...

Ni kwa sababu Neno la Mungu linampa uwezo kila mtu kupigana vita yoyote ya kiroho ikiwemo hii ya kumwokoa ndugu yetu Freeman Mbowe toka midomoni mwa simba efficiently hata ukiwa ndani ya chumba chako..

Kumbukeni hili: "...Mungu ni Roho (siyo mwili) na wote wamuabuduo imewapasa kumwabudu katika roho na kweli..."

Maombi yoyote katika Mungu aliye hai ni IBADA takatifu...

Hivyo, hii vita tunayoindea ni ya kiroho si ya kimwili...

Hebu soma hapa chini mamlaka na nguvu iliyo katika Neno la Mungu juu ya vita yoyote:

2 WAKORINTO 10: 3 - 5

"....Kweli tunaishi duniani, lakini hatupigani vita kidunia. Maana silaha tunazotumia katika vita vyetu si silaha za kidunia, ila ni nguvu ya Mungu yenye kuharibu ngome zote za adui. Tunaharibu hoja zote za uongo na kubomoa kila kizuizi cha majivuno kilichowekwa kuipinga elimu (haki) ya Mungu; tunaziteka fikra zote na kuzifanya zimtii Kristo Yesu... "


Sikilizeni ndugu zangu, Hii vita kwelikweli. Ukiingia ktk vita hii kichwa kichwa tu bila kuwa tayari, utaumizwa na tutashindwa vibaya sana...

Neno la Mungu lina sema "kuweni na hekima na busara"...

Lakini pia kila mwombaji NI MUHIMU akumbuke NA LAZIMA avae/abebe silaha zote muhimu ktk vita hii....

Silaha hizo ni soma Biblia katika ;

[ WAEFESO 6: 12 - 19]

In summary, silaha hizo ni:

1. UTAYARI - Kila mtu aamue kweli
2. UKWELI - Kama mkanda kiuononi mwako
3. UADILIFU - Vazi la kivita kujikinga na mashambulizi yote ya adui dhidi yako
4. HAMU YA KUTANGAZA UADILIFU NA HAKI (HABARI NJEMA) - Viatu vya kivita vya miguu yako
5. IMANI - Ngao ya mikononi mwako ya kuzuia/kuzimia mishale ya adui , yule mwovu akitumia mawakala wake.
6. WOKOVU - Ni kama kofia ya chuma (helmet) ya kuzuia majeraha ya mashambulizi ya adui

7. NENO LA MUNGU - Huu ndiyo upanga mkali sana unaomkata kata adui au kwa lugha rahisi ni bunduki yako yenye risasi kumpigia adui popote alipo..

Ndugu zangu, hatuko pamoja kimwili. Lakini katika ulimwengu w roho tuko pamoja bila kujali utakuwa unaomba ukiwa sehemu gani...

Sikilizeni tena hili:

Yesu Kristo anatuambia hivi katika hili;

MATHAYO 18: 20

"...Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika [wamepatana au wamenia pamoja] kwa jina langu, nami nipo hapo hapo katikati yao..."


Sisi hatuko wawili au watatu bali tuko maelfu kwa maelfu Tanzania yote na duniani, na kwa kuwa tumepatana na kunia pamoja, Mungu Yehova katika YESU KRISTO yupo pamoja nasi...!!

MSIOGOPE, AMININI TU...

NB: Nukuu ya maandiko ni kutoka BIBLIA HABARI NJEMA - BHN, toleo la Kiswahili cha kisasa/rahisi..
 
Mwaka huu kuna majibu ya maombi yaliletwa mwezi wa 3 hapo,ngoja tusubiri tena maombi ya askofu.
 
askofu wa kanisa linaloruhusu ndoa za jinsia moja. anamwomba mungu gani, baali au Mungu anayekataza usodoma? hako kajamaa hakajui nini maana ya askofu. ameweka pembeni Biblia amekuwa chadema, si akagombee tu ubunge kama mwenzie gwajiboy? ni kavurugaji na serikali ifike mahali ichoke. wasimuogope, ni wakristo wachache sana wanamsapotu huyo kimbaumbau.
Kwani Alisha kushikisha ukuta?
 
askofu wa kanisa linaloruhusu ndoa za jinsia moja. anamwomba mungu gani, baali au Mungu anayekataza usodoma? hako kajamaa hakajui nini maana ya askofu. ameweka pembeni Biblia amekuwa chadema, si akagombee tu ubunge kama mwenzie gwajiboy? ni kavurugaji na serikali ifike mahali ichoke. wasimuogope, ni wakristo wachache sana wanamsapotu huyo kimbaumbau.

Ww mwenyewe unaishi mjini kwa kutegemea wanaume, unawezaje kumnyooshea kidole askofu? Kwani serikali ya majizi ya kura inawaogopa hao wananchi, achia mbali hao wakristo unaosema ni wachache wanaomsupport? Kama serikali hii ingekuwa inakubalika tusingeona ule ushenzi na uhayawani kwenye uchaguzi mkuu na wa SM.
 
Watumishi wajinga hawa.
Kuna miaka mmoja naye maeneo ya Mwenge aliwahi kutoa unabii, ambao haukutimia.
Hivi askofu anakuwa na chama je washiriki wake wakiwa tofauti na chama chake si atakuwa kazi kuwaombea laana
Huyu mtumishi tumfananishe na Gwajiboy
 
Back
Top Bottom