The wave
JF-Expert Member
- Feb 27, 2021
- 278
- 308
Amani ya nchi hii iko mikononi mwa Mwenyezi Mungu na Mungu ni Mungu wa haki. Anachotendewa Mbowe siyo haki, hata Kama unakula na kuamkia kwa hao wanaosigina haki na Uhuru wa Mbowe, jirudi hujachelewa. Na Kama unafanya makusudi sababu ya tumbo au ushabiki Mungu ndiye anajua, utajibu siku ya hukumu.AMANI ya NCHI ni ya MUHIMU zaidi kuliko Mbowe au mwanasiasa yeyote yule.
Funzo kwa wanasiasa kwa hiki anacho pitia Mbowe kwa sasa ni;
Mtu yeyote yule au mwanasiasa yeyote atakaye jaribu kuchezea/kucheza na Amani ya Nchi atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria bila kujali wadhifa wake, awe CCM, NCCR, CDM, CUF, n.k atashughulikiwa kikamilifu.
Amani yetu ni kitu muhimu zaidi kuliko mtu yeyote au chama chochote kile.