Askofu Kulola: Kuna mtandao wa kisiasa makanisani

Namheshimu sana mtumishi huyu wa Mungu, lakini napingana na hoja yake ya kutoangalia sifa za wagombea U Rais,
Kwanza yeye ndiye aliyeingiza siasa makanisani baada ya mwaka 2005 kutudanganya kwamba Kikwete ni chaguo la Mungu. TUKADANGANYIKA.
Basi kwake kama ni chaguo la Mungu, tunamwomba anyamaze maana wanadamu hawawezi kubadili uamuzi wa Mungu.Mbona mtumishi wa Mungu anaacha kumshukuru Mungu kwa chaguo lake hilo na ananza kulalama?
Kwako yeye aliyeonyesha na Mungu Kikwete kesha shinda ana hofu gani,maana kesha shinda!

Akiendelea kulalama tutafahamu huyo siye yule Mungu JEHOVAH tunayemjua.Aache wenzake watoe elimu ya uraia.
 
kuutetea Ukristo unaodaiwa uko mbioni kutokomezwa na Uislamu kwa kumkataa Rais Jakaya Kikwete na kuona Rais mkristo ndiye atakayenusuru ukristo hapa nchini.

Mzee Kulola namuheshimu sana kwa vile ni kiongozi wa kanisa na ameanza kazi ya kumtumikia Mungu tangu akiwa kijana mdogo.Na kwa hivyo nampongeza kwa maoni yake maana naye ni sehemu ya raia wa Tanzania.Lakini namshauri azingatie yafuatayo.Kwanza hakuna kiongozi yeyote wa dini ambaye ametamka kwamba watu wasichague uislamu bali kiongozi mkiristo.Muamko unaojitokeza kwa hivi sasa kwa watanzania ni kwamba wanataka kiongozi atakayewatetea wananchi wa kawaida kwa vile miaka ya hivi karibuni hasa toka kifo cha baba wa taifa hayati mwalimu Julius Nyerere nchi imekumbwa na wimbi zito la uongozi usioridhisha, kwa mfano rushwa imeshamiri wazi wazi, na tumeona hata hata baadhi ya watu wenye sifa za uongozi na uadilifu wa kuongoza taifa letu wanahujumiwa wazi wazi.Kwa ujumla maisha ya watu wa hali ya chini yanazidi kuwa magumu kwa walio wengi, huku wachache wakitumia dhamana tulizo wakabidhi kujinufaisha wao na familia zao.Hali hiyo ndiyo inaendelea kuwakera watu wengi , wasomi, raia wa kawaida na hata viongozi wa dini wale tu wanaosimamia kwenye ukweli na siyo wale waoga na wanaopenda kujipendekeza kwa watawala.Hilo la kwanza ningependa mzee wetu Moses Kulola alielewe vizuri.
Tukirudi kwenye madai kwamba udini unatumika kwenye kampeni.Kama wapo watu hao, naamini wapo, basi ni wale ninaowaita ni opportunists ambao lengo lao ni kuficha ukweli na kuchomeka mambo (hoja dhaifu ya udini) ili kuleta mkanganyiko kwa watanzania.Ukifuatilia hali ya kisiasa ilivyo kwa hivi sasa ni kwamba kuna wimbi kubwa la watanzania ambao wanahisi mambo hayaendi jinsi inavyotakikana, na hivyo basi wana kiu ya kufanya mabadiliko kubadili uongozi.Na hii inajidhihirisha jinsi watu wanavyohamasika kujitokeza (Reference angalia jinsi watu wa Mwanza juzi jumatano walivyomiminika kumsikiliza Dr Slaa pale uwanja wa magomeni) kuwasikiliza jinsi wagombea mbali mbali.Mimi naamini ule umati mkubwa wa watu haukuwa wa dini fulani baili ni watanzania wa kila dini na pengine hata wasio na dini wakijitokeza kumsikiliza Dr Slaa.

Hivi sasa inaonekana watu wamekomaa kisiasa na wanaangalia zaidi sifa na uwezo wa mgombea husika na siyo dini dini, chama, kabila au mkoa anaotoka.
Mwanafalsafa maalufu Karl Max aliwahi kusema, haiingii akilini kwa mtu akajitenga asijihusishe na siasa za nchi yake ili hali siasa hizo zinaathiri maisha ya kila siku ya kila raia.Na kwa hivyo basi ikumbukwe kwamba viongozi wa dini ni raia nao wana haki ya kutoa maoni yao , na kubwa zaidi viongozi hao nao wanapaswa kutoa mchango wao ili nchi ipate viongozi bora na siyo bora viongozi, ili mradi hawavunji sheria ya nchi yetu. Na mfano mzuri ni askofu mkuu wa KKT Dr Alex Malasusa alitamka hivi karibuni watu wachague kiongozi makini na siyo chama.Hiyo kauli kwa mtu mwenye kufikiri vizuri haina chembe hata moja la udini, ubaguzi na wala uchochezi.Kwa hali inavyoonekana endapo mtu au kiongozi wa dini akitoa maoni yasiyounga mkono chama fulani basi watu wenye fikra za ajabu wanadai eti ni huo ni uchochezi au wanajihusisha na kazi isiyowahusu.Haiwahusu vipi wakati waumini wao ni sehemu ya watu ambao wanaweza kuathirika na uongozi mbaya wa nchi? Endapo kiongozi wa dini atakaa kimya huku baadhi ya watu kwa mfano wakitoa rushwa ili warudi au waingie madarakani, basi kiongozi huyo atakuwa hatimizi wajibu wake si tu kwa waumini wake bali hata kwa taifa lake kwa ujumla.

Nahitimisha kwa kusema kwamba watu wawashawishi watanzania (wapiga kura) kwa kutoa hoja za msingi zinazolenga kuisaidia nchi yetu, na waachane na kutaka kuleta confusion miongoni mwa watu wetu kwa kisingizio eti watu hawataki kiongozi wa dini fulani.Mwalimu Nyerere aliwahi kuonya kwa kusema, "Hivi sasa watu wameanza kuzumgumzia udini katika masuala ya uongozi, kinachohitajika ni mtu mwenye sifa za kuwaongoza watanzania dini ni yake yeye binafsi, sisi inatuhusu nini?

Tijadili hoja za msingi zitakazojenga mustakabari wa nchi yetu
 
Naheshimu sana watumishi wa Mungu,ila naweza kumkumbusha askofu kuwa huu sio wakati wa kuelezwa mambo yasiyoeleweka.Kama alivyo mtumishi wa Mungu amtaje kwa jina anayefanya siasa kanisani.Kinachofanywa na hao anaowaita kuwa wanafanya siasa kanisani ni kuwaelewesha waumuni wao umuhimu wa kuchagua kiongozi bora.Kama hapatakuwa na elimu hiyo akisema kuwa kazi ya kanisa ni kuomba tu,kwa nini yeye mwenyewe asingeomba tu akabaki kwenye dhehebu lake la awali mpaka akaanzisha la kwake EAGT kwa nini asiombe tu akatulia huko huko???.Askofu naomba uwaelimishe waumini wako vizuri juu ya uchaguzi na wachague kiongozi atakayewapeleka kaanani.
Mtu kujenga kanisa kilimanjaro hata kama hana sifa za kuongoza tumkubali tu??eti kwa sababu kajenga kanisa??Hata angejenga makanisa kila kijiji kama hana sifa za uongozi hawezi kuongoza.Askofu sikia sauti ya Mungu kama wengine walivyosikia.Kila jambo na nyakati zake.Hizi ni nyakati za mageuzi usishindane na wakati.Wakati ni ukuta.
2010 HATUDANGANYIKI
 
Mjukuu wake Mbasha si yuko kwenye kampeni za JK , hilo linafahamika. wale wale!

hajajua kuwa naye kaongea kisiasa hapo, anatakiwa kujua kuwa siasa ni watu, na makanisani kuna watu,
tofauti ya kanisa na siasa ni muongozo unaotumiwa, siasa moja kwa moja iko chini kanisa, hasa tukizingatia
kuwa siasa ni mpango wa wanadamu kutawalana si kwa mabavu bali kwa haki, bali kanisa ni habari za Mungu na
wanadamu, hapa panahitaji hekima sana kuweza kutambua,

vipi kanisa likae kimya ikiwa linajua kwamba anayegombe kwa chama fulani firauni harafu uniambie lijitenge bila ya kuwajuklisha waumini
hatari za kutawaliwa na mtu firauni? Mi naona kuna baadhi ya viongozi wa dini wanatumiwa kuwatisha wananchi ambao ni waumini wao
kutosimama kutetea haki yao ya kutawaliwa/kuongozwa.

Kanisa kama kanisa lina haki ya kuwakumbusha watu ambao ni waumini wake umuhimu wa kuchagua kiongozi ambae linaona kuwa
anatalifaa taifa kwa ujumla, Mimi kama kiongozi wa kanisa siwezi kamwe kuwashauri waumini wangu kumchagua
mtu anayejihususha na mambo ya kishirikina kwa kukubari kupokea nguvu za kiganga kumlinda
na huku amemuacha Mungu ambae yu juu ya yote,
 
Kulola ni obsolete,amenasa kwenye mtego na hawezi kujinasua. Tumuombee roho wa bwana amuangazie maana sasa haoni.
 
Mimi nilishtuka kidogo niliposikia askofu,nilipo gundua ni wa TAG haaa! hawa si wale wale wanao waibia maskini kwa kusema wanaponyesha magonjwa, hawana tofauti na waganga wa kienyeji hata ukiangalia matangazo yao mengi, na ponya hili nalile hawana jipya, hawa watu si wasafi

Irrelevant.
 
Primitive society utaijua tu..lol..

Sometimes naanza kuelewa kwanini tutaendelea kufa maskini a thousands of generations to come.
 
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Askofu Kulola huipigia debe CCM[/FONT][FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]
[/FONT]
kulolazaro.jpg

[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Nani anamdanganya nani?[/FONT][FONT=Arial, Helvetica, sans-serif] Askofu Moses Kulola na mkewe wakikumbatiana na aliyekuwa askofu wa TAG Tanzania, Emanuel Lazaro na mkewe. Wanaoangalia ni Askofu Kitonga (wa pili kulia) Pia alikuwepo mlinzi maalum wa Askofu Kulola anayejulikana kwa jina moja tu ALEX. Bila hata kuambiwa, sura yake tu inaonyesha yuko kazini. Wenzake wanacheka, lakini yeye hacheki na watu. Ana sura ya mawe. (Ni wa kwanza kulia.) CCM tangu wakati wa Nyerere, ilimpatia Kulola walinzi wanaolipwa na serikali, ili akipigie debe chama hicho. Kulola alikaidi uongozi wa TAG ikazuka vita kati yake na Askofu Emanuel Lazaro. Serikali ilimpendelea kulola kwani alidai misaada mingi kutoka Marekani ilikuwa na lengo la kupenyeza CIA Tanzania kwa kutumia TAG. Nyerere aliinunua hiyo jumla kwani sera zake za ujamaa zilizoshindwa zilikuwa zikihofu sana Marekani wasijeleta ubepari Tanzania. Kulola alionekana malaika wakati Lazaro serikali ilimuona shetani. Lazaro alikwamishwa mpaka alipoachia ngazi ya uaskofu. Kulola mpaka leo anafaidi uongo wake wa kuidanganya serikali kwamba CIA walimtumia Lazaro. Ukiyasikiliza mahubiri ya kulola kwa makini, utakuta anawalisha waumini siasa za CCM bila wao kujua. Kulola ndiye mhubiri wa DOLA Tanzania. Mikutano yake inalindwa na kikosi maalum, Yeye mwenyewe analindwa kila aendako, Ni kipenzi cha CCM. Tuombe iwe hata mbinguni Mungu atampa heshima anayopewa na CCM. Vinginevyo atakuwa ameshavuna duniani. Nchini Kenya Kitonga aliipamba sana KANU na alikuwa mhubiri wa dola Kenya. Tangu KANU waachie ngazi Kitonga yuko nje ya duara la madaraka.[/FONT]
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg

Mkewe Kulola anasadikiwa kuwa na pea elfu tatu za vitenge na khanga. Kila mkutano washirika hulazimishwa kununua vitenge na zawadi nyingine kwa mama askofu. Inasemekana kwamba kina Mwasota walikosana na Kulola pale na wao walipopewa zawadi za vitenge na ikaonekana mke wa Mwasota anashindana na mama askofu kimavazi na ndipo Mwasota alipotimuliwa. Inasemekana kwamba mke wa kulola hupenda kuonekana amewazidi wote kimavazi. Nchini Kenya Kitonga aliipamba sana KANU na alikuwa mhubiri wa dola Kenya. Tangu KANU waachie ngazi Kitonga yuko nje ya duara la madaraka
source: Munishi blog KulolaOnline
 
Kulola alikwishasema roho yake ni ya Yesu, mwili ni mali ya Yanga na damu yake yote ni CCM
 
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Askofu Kulola huipigia debe CCM[/FONT]​


kulolazaro.jpg

[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Nani anamdanganya nani?[/FONT][FONT=Arial, Helvetica, sans-serif] Askofu Moses Kulola na mkewe wakikumbatiana na aliyekuwa askofu wa TAG Tanzania, Emanuel Lazaro na mkewe. Wanaoangalia ni Askofu Kitonga (wa pili kulia) Pia alikuwepo mlinzi maalum wa Askofu Kulola anayejulikana kwa jina moja tu ALEX. Bila hata kuambiwa, sura yake tu inaonyesha yuko kazini. Wenzake wanacheka, lakini yeye hacheki na watu. Ana sura ya mawe. (Ni wa kwanza kulia.) CCM tangu wakati wa Nyerere, ilimpatia Kulola walinzi wanaolipwa na serikali, ili akipigie debe chama hicho. Kulola alikaidi uongozi wa TAG ikazuka vita kati yake na Askofu Emanuel Lazaro. Serikali ilimpendelea kulola kwani alidai misaada mingi kutoka Marekani ilikuwa na lengo la kupenyeza CIA Tanzania kwa kutumia TAG. Nyerere aliinunua hiyo jumla kwani sera zake za ujamaa zilizoshindwa zilikuwa zikihofu sana Marekani wasijeleta ubepari Tanzania. Kulola alionekana malaika wakati Lazaro serikali ilimuona shetani. Lazaro alikwamishwa mpaka alipoachia ngazi ya uaskofu. Kulola mpaka leo anafaidi uongo wake wa kuidanganya serikali kwamba CIA walimtumia Lazaro. Ukiyasikiliza mahubiri ya kulola kwa makini, utakuta anawalisha waumini siasa za CCM bila wao kujua. Kulola ndiye mhubiri wa DOLA Tanzania. Mikutano yake inalindwa na kikosi maalum, Yeye mwenyewe analindwa kila aendako, Ni kipenzi cha CCM. Tuombe iwe hata mbinguni Mungu atampa heshima anayopewa na CCM. Vinginevyo atakuwa ameshavuna duniani. Nchini Kenya Kitonga aliipamba sana KANU na alikuwa mhubiri wa dola Kenya. Tangu KANU waachie ngazi Kitonga yuko nje ya duara la madaraka.[/FONT]
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg
kulolamrsndogo.jpg

Mkewe Kulola anasadikiwa kuwa na pea elfu tatu za vitenge na khanga. Kila mkutano washirika hulazimishwa kununua vitenge na zawadi nyingine kwa mama askofu. Inasemekana kwamba kina Mwasota walikosana na Kulola pale na wao walipopewa zawadi za vitenge na ikaonekana mke wa Mwasota anashindana na mama askofu kimavazi na ndipo Mwasota alipotimuliwa. Inasemekana kwamba mke wa kulola hupenda kuonekana amewazidi wote kimavazi. Nchini Kenya Kitonga aliipamba sana KANU na alikuwa mhubiri wa dola Kenya. Tangu KANU waachie ngazi Kitonga yuko nje ya duara la madaraka​

source: Munishi blog KulolaOnline


Nasikia Kulola na wafuasi wake walipigana na Lazaro na wafuasi wake wakigombea uaskofu. Huyu Kulola inaoneka ni mtu wa mwili si wa roho. Halafu inakuwaje kampeni za JK ni za vituko vituko tu vya kuiangamiza nchi yetu. Sasa hivi kampeni za JK ni udini tu, ni mtu wa namna gani huyu?
 
Mimi nilishtuka kidogo niliposikia askofu,nilipo gundua ni wa TAG haaa! hawa si wale wale wanao waibia maskini kwa kusema wanaponyesha magonjwa, hawana tofauti na waganga wa kienyeji hata ukiangalia matangazo yao mengi, na ponya hili nalile hawana jipya, hawa watu si wasafi
Have you recognize how stupid you are?
1. Kulola is NOT TAG he is EAGT
2. TAG don't do what you say they do
3. Hakuna Mkristo aliye msafi kwa haki yake. tu wasafi kwa kuwa tumeoshwa kwa damu ya Yesu
 
Have you recognize how stupid you are?
1. Kulola is NOT TAG he is EAGT
2. TAG don't do what you say they do
3. Hakuna Mkristo aliye msafi kwa haki yake. tu wasafi kwa kuwa tumeoshwa kwa damu ya Yesu

Lakini TAG na EAGT mwanzoni ilikuwa moja. Baada ya Kulola kutwangana na Lazao wakigombea uaskofu ndiyo wakatengana kila mmoja akaanzisha kanisa lake.
 
Nasikia Kulola na wafuasi wake walipigana na Lazaro na wafuasi wake wakigombea uaskofu. Huyu Kulola inaoneka ni mtu wa mwili si wa roho. Halafu inakuwaje kampeni za JK ni za vituko vituko tu vya kuiangamiza nchi yetu. Sasa hivi kampeni za JK ni udini tu, ni mtu wa namna gani huyu?
Watanzania!
Unajua huyu jamaa yetu bila fitna mambo hayaendi. Sasa ukisoma hiyo stori ya gazeti la uhuru kuhusu Kulola utaona kabisa ni story iliyojaa udini! Kwa sababu wanataka watu wa-conclude kuwa Kikwete anapingwa kwa ajili ya uislam wake na Dr Slaa amependwa kwa sababu ya Ukristio wake. Hizi zote ni technics za Kikwete baada ya kuona mambo si mazuri!
 
Watanzania!
Unajua huyu jamaa yetu bila fitna mambo hayaendi. Sasa ukisoma hiyo stori ya gazeti la uhuru kuhusu Kulola utaona kabisa ni story iliyojaa udini! Kwa sababu wanataka watu wa-conclude kuwa Kikwete anapingwa kwa ajili ya uislam wake na Dr Slaa amependwa kwa sababu ya Ukristio wake. Hizi zote ni technics za Kikwete baada ya kuona mambo si mazuri!

Lakini Nyerere aliwakataza CCM wasifanye siasa za udini, inakuwaje huyu JK? ana uchu sana wa madaraka Kikwete au ni vipi?
 
Back
Top Bottom