Askofu Kakobe: Tulipomchagua Magufuli kuwa Rais; tulimchagua Rais mtarajiwa mhe.Samia kwa mujibu wa Katiba !

Elisha Sarikiel

JF-Expert Member
Aug 29, 2020
889
1,515
YALIYOJIRI KONGAMANO LA WATUMISHI WA MUNGU KUMWOMBA NA KUMSHUKURU MUNGU KWA SIKU 100 ZA MHESHIMIWA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KUWA MADARAKANI KUONGOZA NCHI YA TANZANIA
Kongamano lilianzia kwa maneno ya salamu za viongozi mbalimbali wa dini sawa na kusudi la kongamanona sambamba na mada kuu maalum zilizotolewa katika kutafakari siku 100 za Rais wetu, mhe.Samia Suluhu Hassan. Kongamano lilifanyika mubashara kupitia vyombo vya habari na mitandao ya jamii kama YouTube ! Unaweza kutazama video zenye ujumbe kamili kwa ufunguo huu >>> Kongamano la viongozi wa dini leo ! Kongamano hili lilifanyika ukumbi wa Kisenga,Millenium Tower;Dar Es Salaam tarehe 26/Juni/2021 siku ya Jumamosi asubuhi.
Miongoni mwa waliotoa mada kwa walihudhuria na watanzania kwa ujumla, ni askofu mkuu Zachary Kakobe; ambaye alijibu minong'ono iliyojitokeza katika jamii yetu baada ya kuapishwa mhe.Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kufariki kwa mpendwa wetu Rais mhe.Dkt.John J.P.Magufuli ! Askofu Kakobe alisema kwamba 'tulipomchagua Rais Magufuli, kimsingi tulimchagua Samia vilevile.' Kama mtu anafikiri alimchagua Magufuli kuwa Rais lakini hakumchagua mhe.Samia Suluhu Hassan ni upungufu wa elimu ya Uraia !
Katika uchaguzi wetu mkuu wa Rais haiwezekani kufanyika bila mgombea mwenza (Makamu wa Rais). Kwa wale wanaokumbuka mwaka 2005,ulikuwa ufanyike uchaguzi mkuu tarehe 30/Oktoba/2005; lakini ulihairishwa kwa sababu ya kufariki kwa mgombea mwenza wa kutoka Chadema, aliyeitwa Jumbe Rajabu Jumbe aliyefariki tarehe 26/Oktoba/2005 siku nne tu kabla ya kupiga ya kura uliofanyika tarehe 18/Desemba/2005. Mgombea wa urais wa Chadema wakati huo alikuwa ni Freeman Aikaeli Mbowe ambaye aliyesonga mbele na ANNA KOMU baada kuchaguliwa kuwa mgombea mwenza wake.

Aliendelea kusema askofu mkuu Kakobe "Mgombea mwenza si tu anashika madaraka ya makamu wa Rais, lakini ilivyo katika KATIBA katika ibara ya 37, ibara ndogo 35 inaelekeza wazi kwamba Rais atakapofariki, anayechukua nafasi yake ni makamu wa Rais." Hivyo, kimsingi tunapokwenda katika uchaguzi mkuu wa Rais; tunamchagua Rais wa nchi na tunamchagua Rais mtarajiwa ! Kwa hiyo, tulipomchagua Rais Magufuli mpendwa wetu; tumemchagua na makamu wa Rais, yaani Mgombea mwenza. Ni kweli wananchi tulipomchagua Rais Magufuli tulimchagua Mama Samia vilevile kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu.

Pia, askofu Kakobe aligusia tofauti ya mtindo wa kufanya kazi kwa aliyekuwa Rais Magufuli na Rais Samia katika siku 100 madarakani. Alisema kuna watu wanauliza mbona hafanyi kama mpendwa wetu Magufuli ? Hii ni shida ! Aliendelea kufafanua kwa kusema:
  1. Alama za kipekee katika kila kidole (finger print) cha mkono wa mwanadamu ni tofauti.​
  2. Alama za kipekee katika ulimi (Tongue Print) mwanadamu ni tofauti na ulimi wa mwenzake.
  3. Alama ya kipekee katika mboni ya jicho ni tofauti mwanadamu mwingine.
  4. Lips print
  5. Alama ya kipekee katika vidole vya miguu kati mwanadamu
  6. Kuna alama ya kipekee Retina kwenye jicho
  7. Seti za meno maumbo na namna yalivyo tofauti kati mwanadamu na mwanadamu.
  8. Kuna tofauti iliyopo ya sauti kisayansi.
  9. Alama nyingine ya tofauti ni "harufu" kati ya mwanadamu na mwanadamu.
Mungu katika uumbaji wake hajamuumba mwanadamu mmoja afanane na mwingine; bali kila mwanadamu yuko tofauti na mwanzake. Kwa sababu hii Mungu katika Neno lake anasema kuna tofauti za kutenda kazi; zinazotokana na uumbaji wake ( 1WAKORINTHO 12:6 ). Hivyo, Rais Samia Suluhu Hassan tukitarajia atende kazi kama magufuli; hatuelewe utofauti uliwekwa na Mungu kwa utukufu wake ! Kwa hiyo Rais Samia akitaka kufanya kazi kwa style ya mpendwa wetu Magufuli atakuwa ni mwigizaji na msanii. Tumemchagua wenyewe Rais Samia, na hivyo tumpe nafasi ya kutuongoza kwa style yake.

Askofu Kakobe alisema "Samia wewe ni Rais si msanii au mwigizaji na kwa sababu hii; tuongoze kwa style yako mwenyewe. Nikuombe Rais utuongoze vile ulivyo kwa asili yako katika mpango wa Mungu; maana hataki kumwona Magufuli mwingine; bali Rais Samia kwa kuwa kila jambo lina kusudi la Mungu." Nasi tukubali atuongoze kwa style yake; kwa kuwa hakuna Magufuli mwingine atakayekuwepo; na atakayejaribu kuwa kama Magufuli atakuwa mwingizaji. Nia ni moja ya kazi iendelee kwa kuwa ilani ya uchaguzi mkuu ni ileile bali mtindo wa kuongoza ni tofauti kati yao.

Askofu Kakobe, alisema Tumpe ushirikiano mia kwa mia Rais Samia Suluhu Hassan. Na watu wote walisimama ukumbini na kuadhimiwa leo katika kongamano na kusema kwamba '"MHESHIMIWA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN TUONGOZE KWA STYLE YAKO USIWE MWIGIZAJI WALA MSANII. TUONGOZE VILEVILE ULIVYOUMBWA. TULIVYOKUCHAGUA MGOMBEA MWENZA, TULIKUCHAGUA KAMA RAIS MTARAJIWA. TUNAMSHUKURU KWA SIKU 100, TUNAMTUKUZA KUKUUMBA VILE ULIVYO. "


Mwisho wa Kongamano alipata nafasi Askofu mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship naye kuongoza maombi maalum kwa Rais Samia Suluhu Hassan; na taifa letu kulibariki sawa sawa na mapenzi ya Mungu aliyeumba mbingu na nchi. Kauli ya askofu mkuu Zachary Kakobe alipopewa nafasi alisema "TUMESHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA "Tazama video clip hapa chini kwa ufupi.

picha kongamano dini.jpg
 

Attachments

  • MAOMBI MALUM KWA RAIS SAMIA YALIONGOZWA NA ASK.KAKOBE.mp4
    81.2 MB
Mmh mmeanza
Kusifu na kuabudu nyakati zake ziliisha
Mkulu anawalegeza mnaingia kiulani
sisiem ni ile ile as long as wastaafu wanaongoza hakuna Jipya
Katiba Mpya uwe ni chorus humo makanisani sio kuja na ngonjera zilizokosa ubeti
Mmeambiwa msizungumze swala la Katiba ndio mmeanza kujitutumua
Makanisa yatabaki magofu au nyumba za popo siku moja
 
Sina cha kuongeza Best. Ukaribu wa huyu Maza na yule Kikwete hasa ukitilia maanani kufufuliwa kwa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, kauli yake kwamba Katiba mpya tutasubiri sana imeondoa imani niliyokuwa nayo kwake huyu. Maza anataka kuirebrand Tanzania kwa kuwa ina Rais mwanamke
😂😂😂😂😂😂😂
Mmh mmeanza

Kusifu na kuabudu nyakati zake ziliisha
Mkulu anawalegeza mnaingia kiulani
sisiem ni ile ile as long as wastaafu wanaongoza hakuna Jipya
Katiba Mpya uwe ni chorus humo makanisani sio kuja na ngonjera zilizokosa ubeti
Mmeambiwa msizungumze swala la Katiba ndio mmeanza kujitutumua
Makanisa yatabaki magofu au nyumba za popo siku moja
 
Mmh mmeanza
Kusifu na kuabudu nyakati zake ziliisha
Mkulu anawalegeza mnaingia kiulani
sisiem ni ile ile as long as wastaafu wanaongoza hakuna Jipya
Katiba Mpya uwe ni chorus humo makanisani sio kuja na ngonjera zilizokosa ubeti
Mmeambiwa msizungumze swala la Katiba ndio mmeanza kujitutumua
Makanisa yatabaki magofu au nyumba za popo siku moja
Una hela kwa ajili ya katiba mpya
 
Sina cha kuongeza Best. Ukaribu wa huyu Maza na yule Kikwete hasa ukitilia maanani kufufuliwa kwa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, kauli yake kwamba Katiba mpya tutasubiri sana imeondoa imani niliyokuwa nayo kwake huyu. Maza anataka kuirebrand Tanzania kwa kuwa ina Rais mwanamke
😂😂😂😂😂😂😂


Mkuu BAK heshima kwako.

Heche kaandika vyema sana. Ila nadhani hiyo ni kwa tafsiri yake ya neno rebranding inayotofautiana na ya mama kama alivyolitumia hapa.

Tafsiri za maneno anayotumia mtu kwenye hotuba hayawezi kuwa na maana anayoitaka msikilizaji.

Kwanini isiwe hivi:

1. Yote aliyosema Heche tunayataka, wala si ombi. Ila si kwa maana ya neno rebranding kama aliyoongelea Mama?
2. Mikataba ya uwekezaji ya nchi iwekwe wazi kwa wananchi kuelewa yote yaliyomo kuepusha kulishana matango pori.

Katiba mpya yaja, hii ni kwa Mama kuwahi kwa yeye kuridhia kabla na kuongoza jitihada au kwa kushinikizwa.


Kwa hali hiyo mkuu hadi hapo, na Mama tuko vizuri.

Ni kwa sababu kuu hii ndiyo maana Elitwege na kundi lake wanafanya jitihada zote kumchonganisha mama kwa lolote na kwa yeyote.

Maneno "jitihada zote, kwa lolote na kwa yeyote" yanabeba maana zake kamili!
 
Na bahati mbaya kwa Magu na nzuri kwa SSH ni kwamba kampeni ya 2020 SSH ndio kazunguka nchi nzima,Mzee alikuwa kwenye siku zake za mwisho kukata moto.

Mda mwingi alikata pumzi hadi washindani wake wakamfananisha na gari ya mkaa
 
Back
Top Bottom