Askofu Kakobe ataja vyama vya Kufutwa.

Status
Not open for further replies.
Askofu Kakobe ataja vyama vya Kufutwa.


Askofu Mkuu wa Kanisa la
Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe, amezitaka mamlaka zinazohusika kuvifuta vyama vyote vya siasa vinavyoendeshwa kwa misingi ya ukabila havivurugi nchi.

Askofu Kakobe, amezungumza Kanisa kwake hivi karibuni kwenye ibada ya sikukuu ya Krismas alisema miaka kadhaa iliyopita nchi haikuwa akiandamwa na vitendo vya ukabila tofauti na sasa ambapo hali imekuwa mbaya.

Alisema kuna baadhi ya vyama vya siasa nchini ambavyo kwa kipindi kirefu kimejulikana kuwa vinendeshwa kikabila tofauti na sasa ambapo hali imekuwa mbaya.

Alisema kuna baadhi ya vyama nya siasa nchini ambavyo kwa kipindi kirefu vimeendeshwa kikabila, jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi.

Askofu Kakobe, alizishauri mamlaka zinazohusika kuvifuatilia vyama hivyo kuvifuta katika orodha ya vyama vya siasa kwani ni hatari katika mustakabadhi wan chi na wananchi wake.

Akizungumza suala zima la uongozi wanachi, hususani kitendo cha mawaziri kadhaa kuondolewa katika nyadhifa zao, alisema ubovu wa viongozi unachangia na mfumo wa kuteua viongozi.

Askofu Kakobe alisema kwa kawaida uongozi ni kipaji, hivyo watu wanapoona kunakuwa na viongozi wasiowajibika kikamilifu, wajue kuwa kuna tatizo katika uteuzi wao. Moja ya tatizo kubwa linaloathiri nchi kwa sasa alisema ni kuchagua watu kwa kuangalia maenao wanayotoka.


Kama ni kweli Kakobe kayasema haya nnamkumbusha asisumbuke sana sababu ktk Tanzania yetu ipo ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ,kama upo ukiukwaji wa misingi ya kuanzisha vyama vya siasa basi ofisi hii italiona hilo na itavifungia..
 
Yeye ndiye mkabila. Yeye huyu si wa kakonko huko Kigoma. Tangu babu wa Loliondo amharibie biashara kachnganyikiwa. Pole sana self-ordained bishop.
 
Nadhani hapa pia angeongelea pia madhehebu yanayostahili kufutwa kwa kuvuruga amani ya nchi,
Nakumbuka naye aliwahi kuwaweka waumini wake barabarani kuzuia ujenzi wa nguzo za umeme kupita kwenye eneo la kanisa
madai yake yalikuwa kwamba kuna njama za kulihujumu kanisa lake.
Isije ikawa amezungumza haya kufuatia mtu wa kabila lake kuwa kwenye mgogoro wa kisiasa,huku
akitafuta kuungwa mkono na watu wa kabila lake.
 
Nadhani mleta uzi alitakiwa aweke kichwa cha uzi "KAKOBE ACHAFUA HALI YA HEWA".
 
serikali inahitajika kuheshimu na kutii sauti ya Mungu hiyo kupitia mchungaji wake Kakobe.
Kifuteni CHADEMA hiyo ndio sauti ya Mungu.

Huyu Mungu wa Kakobe alimuingiza Mrema chaka baada ya kumutabilia kuwa angepata urais.Mpaka leo hakuna cha urais wala cha baba yake na Rais.
 
Askofu Kakobe ataja vyama vya Kufutwa.


Askofu Mkuu wa Kanisa la
Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe, amezitaka mamlaka zinazohusika kuvifuta vyama vyote vya siasa vinavyoendeshwa kwa misingi ya ukabila havivurugi nchi.

Askofu Kakobe, amezungumza Kanisa kwake hivi karibuni kwenye ibada ya sikukuu ya Krismas alisema miaka kadhaa iliyopita nchi haikuwa akiandamwa na vitendo vya ukabila tofauti na sasa ambapo hali imekuwa mbaya.

Alisema kuna baadhi ya vyama vya siasa nchini ambavyo kwa kipindi kirefu kimejulikana kuwa vinendeshwa kikabila tofauti na sasa ambapo hali imekuwa mbaya.

Alisema kuna baadhi ya vyama nya siasa nchini ambavyo kwa kipindi kirefu vimeendeshwa kikabila, jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi.

Askofu Kakobe, alizishauri mamlaka zinazohusika kuvifuatilia vyama hivyo kuvifuta katika orodha ya vyama vya siasa kwani ni hatari katika mustakabadhi wan chi na wananchi wake.

Akizungumza suala zima la uongozi wanachi, hususani kitendo cha mawaziri kadhaa kuondolewa katika nyadhifa zao, alisema ubovu wa viongozi unachangia na mfumo wa kuteua viongozi.

Askofu Kakobe alisema kwa kawaida uongozi ni kipaji, hivyo watu wanapoona kunakuwa na viongozi wasiowajibika kikamilifu, wajue kuwa kuna tatizo katika uteuzi wao. Moja ya tatizo kubwa linaloathiri nchi kwa sasa alisema ni kuchagua watu kwa kuangalia maenao wanayotoka.

Hivi watu bado wanamsikiliza huyo mwensa wazimu, kwanza kedi yaje ya kutafuna hela ya kanisa imeishia wapi,
 
So Kakobe ni muha, na ana mfeva Kabwe kwa vile ni muha.
Nani mkabila hapo kati ya vyama vya siasa na Kakobe?
 
Mtumishi wa Mungu hakutaja hata jina chama lakini kuna baadhi ya watu wanaojinadhibisha na chama fulani kwa sasa wamepagawa na statement yake.

Inaonekana kama jiwe lililorushwa gizani limempata mlengwa!.

Hakuna njia nyingine ya kupambana na statement yake zaidi ya kuachana na ukabila.

Watanzania wengi hawapendi na hawataki ukabila, lakini kikubwa ni kuwa, Watanzania wanavifahamu vyama vinavyojiendesha kwenye mlengo wa ukabila.
 
Nilikuwa namheshimu sana Askofu Kakobe kama A man of God na mtu mzalendo.

Lakini leo natangaza rasmi kutomuani tena, Ninaomba arudi madhabahuni akatubu kwa hii dhambi ya kusaliti na kuhaini harakati za ukombozi.

mkuu , kakobe hana tatizo , bali huyu mleta uzi ana malengo maalum .
 
baada ya kunyolewa na serikali na kukaribia kufulia, sasa huyu askofu wa kujitangaza anaanza kuivuta serikali. hongera kakobe if u cant fight them...!
 
serikali inahitajika kuheshimu na kutii sauti ya Mungu hiyo kupitia mchungaji wake Kakobe.
Kifuteni CHADEMA hiyo ndio sauti ya Mungu.

Sauti ya Mungu!!! Ina maana mwaka 2000 alipompigia kampeni Mrema, kipindi chote kile alikuwa hatumii sauti ya Mungu? Au tufafanulie kidogo... Ni Mungu yupi unayemzungumzia???

Mimi Mungu wangu huwa habaatishi
 
Chama Chakavu na kizee ndio mwasisi wa ukabila, udini, uuzaji sembe mbovu, meremeta, ufisadi, kagoda, EPA, DIV5 ndio anachomaanisha!
By the way nimesikia kuwa kuna watu wamepigwa banned kuingia US eti ni kweli?

ni kweli , tunakusanya ushahidi taratibu , ukikamilika tutaweka majina yote humu humu .
 
Ilikujua ni chama kipi angalia jibu la kakobe anasema uongozi ni kipaji ila kwa chama tawala ccm .wanachagua viongozi kutokana na maeneo wanayotoka .inamaana kabila analotoke.badala kipaji na uwezo wa mtu bila kujali ni kabila gani au eneo analotoka .
 
No.! hakifutwi kitu hapa, kifutwe kwa lipi..?! Sasa pesa za walipa kodi apewe nani kama ruzuku.?

There is a saying ''kuchanganya dini na siasa ni sawa na kuchanganya mafuta na maji"(Impossible)
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom