tucker carlson
Senior Member
- Oct 5, 2025
- 103
- 420
Baraza la Viongozi wa Dini nchini limeiomba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufanya mapitio ya mahusiano ya kidiplomasia na nchi ya Marekani ili kulinda umoja na amani ya taifa.
Akisoma tamko hilo mbele ya waandishi wa habari leo Mei 26, 2026, mmoja wa viongozi hao Askofu Israel Maasa, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania Mei 26 ameeleza kuwa kuna haja ya kuangalia upya ushirikiano huo ili kuhakikisha nchi za nje haziwi chanzo cha uchochezi wa kidini au migogoro ya ndani.
"Tunaomba Serikali ya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ifanye mapitio ya mahusiano ya kidiplomasia na ya kinchi baina ya Tanzania na Marekani, ili pamoja na mambo mengine, iweke msimamo wa kukataa kutokuvumilia uchochezi wa kidini unaoweza kuliingiza taifa kwenye matatizo makubwa," alisema kiongozi huyo.
Akisoma tamko hilo mbele ya waandishi wa habari leo Mei 26, 2026, mmoja wa viongozi hao Askofu Israel Maasa, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania Mei 26 ameeleza kuwa kuna haja ya kuangalia upya ushirikiano huo ili kuhakikisha nchi za nje haziwi chanzo cha uchochezi wa kidini au migogoro ya ndani.
"Tunaomba Serikali ya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ifanye mapitio ya mahusiano ya kidiplomasia na ya kinchi baina ya Tanzania na Marekani, ili pamoja na mambo mengine, iweke msimamo wa kukataa kutokuvumilia uchochezi wa kidini unaoweza kuliingiza taifa kwenye matatizo makubwa," alisema kiongozi huyo.