Askofu Gwajima: Vita ya kwanza ya dunia iliizaa UN, vita ya pili ikazaa taifa la Israel, Je Corona itazaa nini? Watu wenye akili tunajiuliza

Itamfufua dhalimu mwendazake ili arudi Ikulu.
Askofu Gwajima amesema dunia ina mambo yake na utaratibu wake wa kufikia malengo na usipokuwa na akili basi utapata tabu sana.

Askofu Gwajima amesema vita ya kwanza ya dunia iliyoua watu zaidi ya milioni 20 ilipomalizika ukazaliwa Umoja wa Mataifa ( League of Nations)

Vita ya pili nayo iliuwa watu wengi na ilipomalizika likazaliwa taifa la Israel, Mrengo wa Magharibi na Mrengo wa Mashariki.
Kwa sababu Nyerere alikuwa na akili yeye na wenzake wakajianzishia Umoja wa nchi zisizofungamana na upande wowote.
Hata hivyo Umoja huu ulikuwa na faida 50% na hasara 50% kwa sababu nchi zake zilionekana hazina msimamo.

Askofu Gwajima anasema Watu wenye akili wamejichimbia kwenye maktaba zao wanatafakari hii Corona itazaa nini, na nini itakuwa impact yake kwenye uchumi na siasa

Gwajima amesema anamshauri Rais Samia atafute vijana " wenye akili " wajikite katika hili na kutupa mrejesho ili tuwexe kuvuka.

Chanzo: Ibadani Kanisa la Ufufuo na Uzima

Mungu ni mwema wakati wote!
 
Yes sina akili ndio maana nalinganisha Covid na vita za dunia??? Utadhani ndio pandemic iliyotesa kuliko Dubonic Plague au Spanish Influenza!!
Katika jicho la kiroho vita kuu ya pili ya dunia na covid19 pandemic vyote ni sawa tu kwa sababu vyote vimetumika kufungua lango kwa dunia kuingia katika msimu mpya, ndio maana unasikia msemo "new normal"
 
Black plague au Spanish Flu ziliua kuliko Corona na World war 1 ila zilizaa nini??

Msipende kuwa watu wa speculation na conspirancy.... Maisha ni process na dunia inapitia mabadiliko sio kila kitu kimepangwa.

Nakumbuka hata Tsunami ya 2004/05 kuna watu walidai ilisababishwa na bomu la nuclear iliyolipuliwa baharini na mabeberu!!!
Ndui iliua zaidi ya watu milioni 300, ilizaa nini? Gwajima ni kwaajili ya wajinga.
 
Askofu Gwajima amesema dunia ina mambo yake na utaratibu wake wa kufikia malengo na usipokuwa na akili basi utapata tabu sana.

Askofu Gwajima amesema vita ya kwanza ya dunia iliyoua watu zaidi ya milioni 20 ilipomalizika ukazaliwa Umoja wa Mataifa ( League of Nations)

Vita ya pili nayo iliuwa watu wengi na ilipomalizika likazaliwa taifa la Israel, Mrengo wa Magharibi na Mrengo wa Mashariki.
Kwa sababu Nyerere alikuwa na akili yeye na wenzake wakajianzishia Umoja wa nchi zisizofungamana na upande wowote.
Hata hivyo Umoja huu ulikuwa na faida 50% na hasara 50% kwa sababu nchi zake zilionekana hazina msimamo.

Askofu Gwajima anasema Watu wenye akili wamejichimbia kwenye maktaba zao wanatafakari hii Corona itazaa nini, na nini itakuwa impact yake kwenye uchumi na siasa

Gwajima amesema anamshauri Rais Samia atafute vijana " wenye akili " wajikite katika hili na kutupa mrejesho ili tuwexe kuvuka.

Chanzo: Ibadani Kanisa la Ufufuo na Uzima

Mungu ni mwema wakati wote!
Hivi mtu na akili zake unamfuatilaje mzinzi huyu!
 
Mwambieni Gwajima kuwa Covud 19 itawaondoa wahubiri matapeli kama yeye wanaotumia neno ka Mungu kuwahadaa wanadamu wajinga.
 
''GWAJIMA KUKAA KIMYA NI HEKIMA ILIYO KUU''walishe wana kondoo kili kilicho chema kitokacho ndani ya biblia takatifu. wengine huku sisi ni wanasayansi nguli tunajua nini kinatafutwa ulimwenguni isipokuwa tunakaa kimywa tu
 
Ndui iliua zaidi ya watu milioni 300, ilizaa nini? Gwajima ni kwaajili ya wajinga.
Ye anajulia wapi mkuu, na bahati yake hicho kipindi pandemic heavy kama ndui zinatokea dunia ilikuwa bado haijawa kijiji, hii Corona Leo inatutesa Kwa ajili ya muingiliano wa watu katika mabara yote lasivyo ingeishia huko huko ingekuwa ni miaka Ile, na hii ni dalili kuwa Kwa sasa tunaenda kusafa kwenye kila pandemic ambayo itakuwa kubwa
 
Huyu jamaa kweli kiazi.
Elimu za magumashi ndio taabu yake, Ugonjwa wa corona ndio vita kuu ya 3 ya dunia!
Pathetic!
 
Black plague au Spanish Flu ziliua kuliko Corona na World war 1 ila zilizaa nini??

Msipende kuwa watu wa speculation na conspirancy.... Maisha ni process na dunia inapitia mabadiliko sio kila kitu kimepangwa.

Nakumbuka hata Tsunami ya 2004/05 kuna watu walidai ilisababishwa na bomu la nuclear iliyolipuliwa baharini na mabeberu!!!
umeambiwa wenye akili, kwa comment yako unadhani mada inakuhusu?
 
Back
Top Bottom