rosemarie
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 6,887
- 3,412
Mtumishi wa Bwana
Nataka ujuwe sipingani na wewe wala sipo kinyume na wewe, nataka nieleze mawazo yangu kuhusu somo lako la leo kuhusu kuchanjwa.
Leo umehubiri kuhusu chanjo kwamba waumini wako wasikubali kuchanjwa, napenda nikufungue macho kidogo uweze kuona,
Nilipozaliwa nikiwa mtoto mchanga kutoka tumboni mwa mama yangu nilichanjwa chanjo tano siku ile ile nazaliwa,na kwa taarifa yako hao wazungu unaowapinga kwa nguvu zote wangependa kuniangamiza wangenimalizia kwenye zile chanjo tano nilizopokea wakati nazaliwa.
Napenda nikusaidie upate kuelewa,dunia hii tunayoishi inaongozwa na watu wachache sana wala hawafiki kumi
Napenda nikufahamishe kabla corona haijaingia kuna watu walikuwa na taarifa,nimekueleza hilo ili ujue nini kinaendelea duniani
chanjo ya corona inatoka kwa wazungu na wao wameonyesha mfano kuanza kuchanjwa wao.
Nataka ujue kama wazungu wana nia mbaya na sisi wangeweza kutumia njia yoyote ile kutumaliza,
Kwa taarifa tupo mikononi mwao na sisi kama waafrica hatuna chance ya kusimama mbele yao kwa kuwa hatuna jambo lolote tulilofanya katika kuchangia maendeleao ya dunia tangu tunajitawala mpaka muda huu
Mtumishi naomba ujuwe kuna dunia,mwili na roho,haya ni mambo matatu yanayotofautiana sana na sijakusikia ukigusia,huu mwili ukipata chanjo hauwezi kuathiri roho kwa sababu kila kitu kinajitegema,kumbuka ukifa roho inatoka ndani ya mwili na huo mwili unabaki kurudishwa mavumbini
Shirika la Afya Duniani linasimami chanjo dunia nzima unaingilia kati na kuanza kuwanyima washarika wako wasichanjwe naona kuna hatari inakujia hapo mbele
Corona inabadilika kila siku vipi kikija kirusi ambacho waliochanjwa wanapona na ambao wamechanjwa wanakufa??
Utaficha wapi uso wako Mtumishi wa Bwana
Nikiwa kama mkristo aliyeokoka nakushauri ubiri ujumbe wa aina nyingine kwa sababu haya mambo ni magumu kidogo,kumbuka ni watumishi wangapi wa Mungu wamekufa kwa corona?
Nataka ujuwe sipingani na wewe wala sipo kinyume na wewe, nataka nieleze mawazo yangu kuhusu somo lako la leo kuhusu kuchanjwa.
Leo umehubiri kuhusu chanjo kwamba waumini wako wasikubali kuchanjwa, napenda nikufungue macho kidogo uweze kuona,
Nilipozaliwa nikiwa mtoto mchanga kutoka tumboni mwa mama yangu nilichanjwa chanjo tano siku ile ile nazaliwa,na kwa taarifa yako hao wazungu unaowapinga kwa nguvu zote wangependa kuniangamiza wangenimalizia kwenye zile chanjo tano nilizopokea wakati nazaliwa.
Napenda nikusaidie upate kuelewa,dunia hii tunayoishi inaongozwa na watu wachache sana wala hawafiki kumi
Napenda nikufahamishe kabla corona haijaingia kuna watu walikuwa na taarifa,nimekueleza hilo ili ujue nini kinaendelea duniani
chanjo ya corona inatoka kwa wazungu na wao wameonyesha mfano kuanza kuchanjwa wao.
Nataka ujue kama wazungu wana nia mbaya na sisi wangeweza kutumia njia yoyote ile kutumaliza,
Kwa taarifa tupo mikononi mwao na sisi kama waafrica hatuna chance ya kusimama mbele yao kwa kuwa hatuna jambo lolote tulilofanya katika kuchangia maendeleao ya dunia tangu tunajitawala mpaka muda huu
Mtumishi naomba ujuwe kuna dunia,mwili na roho,haya ni mambo matatu yanayotofautiana sana na sijakusikia ukigusia,huu mwili ukipata chanjo hauwezi kuathiri roho kwa sababu kila kitu kinajitegema,kumbuka ukifa roho inatoka ndani ya mwili na huo mwili unabaki kurudishwa mavumbini
Shirika la Afya Duniani linasimami chanjo dunia nzima unaingilia kati na kuanza kuwanyima washarika wako wasichanjwe naona kuna hatari inakujia hapo mbele
Corona inabadilika kila siku vipi kikija kirusi ambacho waliochanjwa wanapona na ambao wamechanjwa wanakufa??
Utaficha wapi uso wako Mtumishi wa Bwana
Nikiwa kama mkristo aliyeokoka nakushauri ubiri ujumbe wa aina nyingine kwa sababu haya mambo ni magumu kidogo,kumbuka ni watumishi wangapi wa Mungu wamekufa kwa corona?