Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 4,435
- 4,151
Gwajima anasema viongozi na wataalamu wetu ni vigeugeu na hawafai kuongoza, Wanafanya mambo kwa kuangalia upepo na sio utaalamu
Anasisitiza wajiuzulu mapema kwenye suala la covid-19
Akihutubia maelfu ya waumini wake leo Gwajima amesema wataalamu wetu ndio hao walijenga pale Muhimbili jiko la kujifukiza nyungu na waliwaaminisha wananchi kuwa chanjo hazifai
Gwajima anasema Leo ghafla wataalamu hao wanahubiri chanjo, Je wanamdanganya nani?
Gwajima anahoji lile jiko sasa wanaalitumia kwa kazi gani pale Muhimbili kwani waliokataa chanjo ndio hao vinara wa kusisitiza chanjo
Gwajima anasisitiza hao wataalamu wa ndani walete Papers au Research zao wamefanya lini na wapi kuhusu chanjo za korona.
Gwajima anasema waje wataalamu hao wa ndani waeleze Madhara ya muda mrefu na mfupi wa chanjo ndio hapo atakuja na Maswali magumu ya kufanya watawanyike
Anasema viongozi makini wangejiuzulu kazi hawafai kuongoza Taifa kwa kuwa vigeugeu kwa kuangalia nani anaongoza juu yao
Enzi za Magufuli hakukuwa na Covid-19; kulikuwa na “changamoto” iliyokuwa ikimalizwa kwa maombi, nyungu, na juisi mchanganyiko wa tangawizi, malimao, pili pili kichaa, n.k.
Covid-19 imefahamika awamu ya 6 na kuagiziwa chanjo. Halafu watu ni wale wale minus JPM!
Gwajima anajifanya kama vile hajui kuwa yuko kwenye chama cha wasanii kinachoendeshwa kwa propaganda. Anajifanya hajui kuwa wenzake walikuwa wanafanya usanii ili kwenda sawa na Magufuli. Kupotea kwa ile connection aliyokuwa nayo Ikulu kumemchanganya hasa!