Askofu Gwajima: Kamati ya Bunge imenifanya nionekane kama Jitu baya na Korofi, sasa hili ndio lililojiri kikaoni


Kila mtu aliona na kusikiliza namna bunge lilivyomjadili Mch. Gwajima (MB) na mwenzake na kumhukumu kutohudhuria vikao vya mikutano miwili vya bunge...

Kwa waliofuatilia mjadala ule siku ya J'nne tarehe 31/8/2021 bunge likiwajadili hawa wabunge wawili, bila shaka atakubali kuwa lilikuwa ni tukio la kupangwa, lenye hila kwa lengo la kuwadhalilisha na kuwavunjia heshima na utu wao tu ili kuwatisha na kuwaogopesha wasiendeleze ajenda zao hizo huko nje kwa umma...

Tuliona na kusikiliza hoja za upande mmoja yaani za KAMATI YA BUNGE YA KUHOJI WENZAO chini ya M/kiti wake mbunge wa Tabora mjini ndg. Mwakasaka na kisha bunge zima kuzitumia kama "base" ya kuwahukumu wenzao...

Kwa kudhalilishwa kule na kunenewa UONGO, ni ngumu sana mbunge (hata kama ungekuwa wewe usomaye sasa) asiye na hatia, anayejiamini kunyamaza kimya asiseme lolote kwa umma baada ya hapo kwa lengo la kuweka rekodi ya mambo haya sawa...

Bahati mbaya kwa Job Ndugai (Spika wa Bunge) na wabunge wenzake, kuwa, kwa Askofu Gwajima wameshafeli tayari, YOU CAN BELIEVE THAT..!

Leo tarehe 5/9/2021 Bishop Rwv. Dr. Josephat Gwajima wa makanisa ya GCTC - UFUFUO NA UZIMA Tanzania na duniani ametujuza upande wake ambayo tulikuwa hatuyajui...

Ni ajabu kuwa, kuna upotoshaji mwingi unaendelea kupitia mitandao ya kijamii alichokisema Mch. Gwajima leo.

Kuna wengine wanasema alipaswa kunyamaza kimya kwa sababu mambo ya kamati ya bunge ni SIRI ambayo haipaswi kutolewa nje....

Hawa ni wajinga kwa sababu, taarifa ya KAMATI YA KUHOJI ilisomwa hadharani mbele ya kamera za TV zote duniani bungeni na wabunge wote wakaijadili taarifa hiyo kwa uwazi na bunge kuamua lilivyoamua...

Rev. Josephat Gwajima hajafanya kosa lolote kukanusha baadhi ya hoja za uongo za kamati huku baadhi ya wabunge wakizitumia kumdhalilisha na kumtukana kumuonesha kama ni mtu mbaya sana...

Nategemea na Jerry Silaa atatoka na kusema kwa wazi ya upande wake ili umma ujue...
 
Siasa za KILIBERALI na dini wapi na wapi ?!!!

Hivi angekuwa ni sheikh anayafanya haya MSIKITINI angechukuliwa kawaida tu kama anavyochukuliwa yeye?!!! 😲😲😲


CCM IMFUKUZE GWAJIMA

HASHTAG GWAJIMA AFUKUZWE CCM

#SiempreJMT
#NchiKwanza
#ChanjoNiBoraKulikoTiba
 
Huwezi tenganisha dini na siasa. Angalia like Babeli Daniel na wenzake walipoambiwa kusujudia sanamu ya mfalme Nebukadineza walikataa wakasimama kumtetea Mungu wa kweli. Yanayotokea sass ulimwenguni hayajaanza Leo na yataendelea kuwepo lakinu watu was Mungu watasimama katika kweli.
 
View attachment 1925317
Kila mtu aliona na kusikiliza namna bunge lilivyomjadili Mch. Gwajima (MB) na mwenzake na kumhukumu kutohudhuria vikao vya mikutano miwili vya bunge...

Kwa waliofuatilia mjadala ule siku ya J'nne tarehe 31/8/2021 bunge likiwajadili hawa wabunge wawili, bila shaka atakubali kuwa lilikuwa ni tukio la kupangwa, lenye hila kwa lengo la kuwadhalilisha na kuwavunjia heshima na utu wao tu ili kuwatisha na kuwaogopesha wasiendeleze ajenda zao hizo huko nje kwa umma...

Tuliona na kusikiliza hoja za upande mmoja yaani za KAMATI YA BUNGE YA KUHOJI WENZAO chini ya M/kiti wake mbunge wa Tabora mjini ndg. Mwakasaka na kisha bunge zima kuzitumia kama "base" ya kuwahukumu wenzao...

Kwa kudhalilishwa kule na kunenewa UONGO, ni ngumu sana mbunge (hata kama ungekuwa wewe usomaye sasa) asiye na hatia, anayejiamini kunyamaza kimya asiseme lolote kwa umma baada ya hapo kwa lengo la kuweka rekodi ya mambo haya sawa...

Bahati mbaya kwa Job Ndugai (Spika wa Bunge) na wabunge wenzake, kuwa, kwa Askofu Gwajima wameshafeli tayari, YOU CAN BELIEVE THAT..!

Leo tarehe 5/9/2021 Bishop Rwv. Dr. Josephat Gwajima wa makanisa ya GCTC - UFUFUO NA UZIMA Tanzania na duniani ametujuza upande wake ambayo tulikuwa hatuyajui...

Ni ajabu kuwa, kuna upotoshaji mwingi unaendelea kupitia mitandao ya kijamii alichokisema Mch. Gwajima leo.

Kuna wengine wanasema alipaswa kunyamaza kimya kwa sababu mambo ya kamati ya bunge ni SIRI ambayo haipaswi kutolewa nje....

Hawa ni wajinga kwa sababu, taarifa ya KAMATI YA KUHOJI ilisomwa hadharani mbele ya kamera za TV zote duniani bungeni na wabunge wote wakaijadili taarifa hiyo kwa uwazi na bunge kuamua lilivyoamua...

Rev. Josephat Gwajima hajafanya kosa lolote kukanusha baadhi ya hoja za uongo za kamati huku baadhi ya wabunge wakizitumia kumdhalilisha na kumtukana kumuonesha kama ni mtu mbaya sana...

Nategemea na Jerry Silaa atatoka na kusema kwa wazi ya upande wake ili umma ujue...
Nawaonea huruma waumini ambao kila wanapoenda kusali kanisani na kusikiliza neno la Mungu wanaishia tu kusikiliza mawazo au maoni ya kiongozi wao kuhusu kuhojiwa na kamati ya maadili au kuhusu kupata chanjo au la. Katika muktadha huu tunaweza kusema kama Karl Marx alivyosema: 'Religion is the opium of the people'.
 
Hakuna wa kuingilia dini za watu
Gwajima Yuko sawa.
Uzuri alishasema Yuko tayari kwa uamuzi wowote isipokuwa kufa.

CHADEMA wanataka afukuzwe wapate wa kuokoa jahazi.
CCM si rahisi wakawa wanakubaliana na yote...

Vivyo hivyo, si rahisi CHADEMA wote wakawa wanakubaliana kwa yote...

Mfano, mimi ni shabiki na mpenzi wa CHADEMA lakini kushabikia Mch. Gwajima afukuzwe CCM kwa sababu ya hili, sikubaliani nao...

Ni kwa sababu sioni kosa la Mch. Gwajima. Amechukua uamuzi wa kutochanjwa na anashawishi na awapendao kufuatana nae ktk msimamo huo...

Mimi ni miongoni mwa wanaomuunga mkono Mch Gwajima. HAKUNA WA KUTUFUNGA MDOMO KWA HAJAZALIWA NA HAWEZI KUZALIWA KABISA....!
 
Mimi ni muumini wake...

Kwa kuniona na kunitazama, unadhani mimi ni mjinga wa kuburuzwa tu kama zuzu bila kuchuja jambo na kujiridhisha...?

Ndugu tunajua tunakokwenda na tutokako. Sisi siyo wajinga wala wapumbavu..

Na kwako wewe nakuambia hivi, hujui usemalo na kumbuka;

JAMBO USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA GIZA TOTORO...!!

Subiri kuche labda unaweza kuona mwanga wa kukufanya uelewe mambo....!!
Nawaonea huruma waumini ambao kila wanapoenda kusali kanisani na kusikiliza neno la Mungu wanaishia tu kusikiliza mawazo au maoni ya kiongozi wao kuhusu kuhojiwa na kamati ya maadili au kuhusu kupata chanjo au la. Katika muktadha huu tunaweza kusema kama Karl Marx alivyosema: 'Religion is the opium of the people'.
 
Nawaonea huruma waumini ambao kila wanapoenda kusali kanisani na kusikiliza neno la Mungu wanaishia tu kusikiliza mawazo au maoni ya kiongozi wao kuhusu kuhojiwa na kamati ya maadili au kuhusu kupata chanjo au la. Katika muktadha huu tunaweza kusema kama Karl Marx alivyosema: 'Religion is the opium of the people'.
"....opium...."
 
Mimi ni muumini wake...

Kwa kuniona na kunitazama, unadhani mimi ni mjinga wa kuburuzwa tu kama zuzu bila kuchuja jambo na kujiridhisha...?

Ndugu tunajua tunakokwenda na tutokako. Sisi siyo wajinga wala wapumbavu..

Na kwako wewe nakuambia hivi, hujui usemalo na kumbuka;

JAMBO USILOLIJUA NI SAWA NA USIKU WA GIZA TOTORO...!!

Subiri kuche labda unaweza kuona mwanga wa kukufanya uelewe mambo....!!
Elewa hili: 'What is said generally does not apply to you particularly'.
 
Back
Top Bottom