#COVID19 Askofu Gwajima awataka watu wasiingilie imani ya kanisa lake, hawachanjwi, watakaojaribu kuiingilia wataingia kwenye "crusher" watasagwa

Huyu siku zake zinahesabika.. Wako kimya wananuacha kwanza amalize kupayuka... Anawachokonoa kwa namna zote lakini wako kimya kabisa.... Inatia hasira sana kwake WAMEMPUUZA...NA INAMUUMIZA SANA HII


Kwa vipi?

Mnachochea kuni wapate kumdhuru?

Ikumbukwe kuwa ; penye wengi hapakosi kuwa na mengi !

Uongozi unataka kuwa na kifua cha kustahamili mengi na siyo kukimbilia visasi.

Nilizani wewe ni muumini wa demokrasia kumbe unaungamkono maswala ya komoakomoa? Au ?
 
Angehubiri kwamba chanjo ni hiyari, kisha aendelee na mambo yake ya ufufuko na uzima. Ila mtu akilazimishwa ana wajibu wa kuongea kwa kutumia busara. Kumbuka ni swala la kitaifa na linamhusu raisi.
 
Leo katika kanisa la ufufuo na uzima Askofu Gwajima asema watu wasiingilie imani ya kanisa lake, amesema kuwa kiimani wakristo na hata waislamu wanaamini pombe ni dhambi na mahubiri hutolewa kupinga matumizi ya pombe, Je hao wanaohubiri wanatakiwa wakamatwe kwa sababu wanaikosesha serikali mapato ?

Amesema wale wanaojaribu kuingilia imani ya kanisa lake wanaingia kwenye "crusher" watasagwa sagwa. Askofu Gwajima amesisitiza imani ya kanisa lake ni hawachanjwi na hivyo wasitishwe na yoyote.

Askofu Gwajima anaenedelea kumwashia moto Waziri Afya, more updates to follow

===

Askofu Gwajima awataka Waziri wa Afya na Naibu Waziri wa Afya wajiuzulu kwa sababu walizunguka nchi nzima kuelezea athari za chanjo kisayansi miezi michache iliyopita, lakini hivi sasa wameanza kuzunguka tena kuwaambia watu wachanjwe bila kutoa elimu ya kisayansi.

Amesisitiza Waziri wa Afya Dr. Dorothy and Naibu Waiziri wa Afya Dr. Mollel wajiuzulu kwa sababu wamemsaliti Rais, wanalazimisha watu kuchanjwa japokuwa chanjo ni hiari.

Amemshutumu Dr. Dorothy kwa kuwaita watanzania waliokataa chanjo ambao ni takribani 70% wajinga.
Usipojikinga kwa chanjo ukiupata ugonjwa huenda utaambukiza wengine.
Hata serikali inakosea kusisitiza "uhiari" wa chanjo.
Mixed messages za government zinawachanganya watu. Zinaweza kugharimu maisha ya baadhi ya watakaokataa chanjo.

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
Asiishie ya Corona tu na za watoto zote wakatae, na ikiwezekana madawa ya wazungu yote wakatae
Anachosema zile nyingine zimefanyiwa tafiti za kutosha. Na zimefuata hatua zote kabla ya kutumika kwa binadamu.
 
Usipojikinga kwa chanjo ukiupata ugonjwa huenda utaambukiza wengine.
Hata serikali inakosea kusisitiza "uhiari" wa chanjo.
Mixed messages za government zinawachanganya watu. Zinaweza kugharimu maisha ya baadhi ya watakaokataa chanjo.

Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
Unaambiwa hata aliyechanjwa bado ana uwezo wa kuwaambukiza wengine. Hapo unasemaje?
 
Kweli Kaka Mshana selikali isipo chukua hatua mapema taasisi yote ya ikulu inachafuka.Mh Rais Samia Hassan achukie hatua mapema kabla Mambo hayajaharibika.
Proven beyond doubt.... Gwajima hana hekima, mropokaji na anayechanganya family matters na siasa
Bro your accusation is wrong ulitaka anyamaze? Mbona yule waziri alizungumza vitu ambavyo sio sensible kwa askofu? Yale matashi aliyoyasema je ilitakiwa kiongozi wa serikali kusema muheshimia mshana tubalance story basi hata Kama mtu humkubali haitoshi kumpa nafasi ya kumsikiliza na kumuelewa
 
Proven beyond doubt.... Gwajima hana hekima, mropokaji na anayechanganya family matters na siasa
Aliyeanza kuleta mambo ya familia ni Dorothy, yeye ndio alianzisha huo mtanange alipoanza kusema askofu ni shemeji yake ila hajali msimamo na kuongelea "mkono wa baunsa", kumfufua Amina Chifupa....alitakiwa ajibu hoja kwa hoja akaingiza mambo ya kuoakana matope kumbe nido kakutana na nguruwe kwenye himaya yake !
 
Nilikua muumini wake mtiifu,,Ila anachosha na anafanya mambo ya aibu.. Ibada nzima anagombana na mipasho, watu tunataka kula neno. Tunaondoka kapa,,na mbaya zaidi waumini wanamshangilia ,,anachamba ukifika muda wa sadka wanatoa anaendelea kuchamba, tunatoa sadaka baada ya kusikiliza misutano, SAD
 
Huyu siku zake zinahesabika.. Wako kimya wananuacha kwanza amalize kupayuka... Anawachokonoa kwa namna zote lakini wako kimya kabisa.... Inatia hasira sana kwake WAMEMPUUZA...NA INAMUUMIZA SANA HII
Wewe una akili japo huipendi ccm, wengine ni fuata upepo.

Gwaji anajifanya anajua kila kitu duniani, yeye mwenyewe alisemaga eti corona ni 5G leo waumini wake wamesahau kuwa aliwapotosha.
Anahubiri kwa kutegemea habari za kuokota mitandaoni.
Tanzania hakuna watafiti waliotafiti madhara ya chanjo.
Ni kumuacha ajifurahishe tu anatafuta umaarufu.
 
Nilikua muumini wake mtiifu,,Ila anachosha na anafanya mambo ya aibu.. Ibada nzima anagombana na mipasho, watu tunataka kula neno. Tunaondoka kapa,,na mbaya zaidi waumini wanamshangilia ,,anachamba ukifika muda wa sadka wanatoa anaendelea kuchamba, tunatoa sadaka baada ya kusikiliza misutano, SAD
Waumini niliowaona pale wengi ni wa kike.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom