Askofu Fredrick Shoo ameongea kama kiongozi au mfuasi wa Lowassa?

TataMadiba

JF-Expert Member
Feb 7, 2014
9,866
5,742
Jana 31/01/2016 ilikuwa ni siku ya kumuingiza kazini Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT, Fredrick Shoo. Shughuli iliyofanyika katika Kanisa Kuu la KKKT, mjini moshi. Mgeni rasmi katika ibada hiyo muhimu alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kassim Majaliwa.

Ibada hiyo pia ilihudhuriwa na Waziri Mkuu aliyeshinikizwa kujiuzulu kutokana na kashfa ya mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya RICHMOND.

Leo takribani magazeti yote yameandika kauli ya Askofu Fredrick Shoo kuhusiana na Serikali ya Magufuli, Vyombo vya dola na mihimili ya yake.

Kwenye kurasa za mbele kabisa za magazeti zimepambwa na vichwa vya habari kama: "ASKOFU AMPASULIA JIPU MAJALIWA LA POLISI KUINGIA BUNGENI", "ASKOFU MPYA KKKT AONYA UTUMBUAJI MAJIPU", "ASKOFU MPYA KKKT AWASHUKIA POLISI", "MAGUFULI AONYWA".

Kazi ya utumbuaji majipu inafanywa na viongozi wenye akili timamu na makini tena kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi. Aidha Bunge ni muhimili ambao watu wenye taaluma mbalimbali wakiwemo wanasheria. Ni muhimili unaofanya kazi kwa kufuata kanuni, sheria na Katiba ya nchi.

Iweje leo Kiongozi wa kanisa aone kama yote hayo ni kinyume na kanuni, utaratibu, sheria na Katiba ya nchi?
 
Ameongea kama mpakwa mafuta wa Mungu, kazi yao hawa ni kuongoza watu wa Mungu kutenda yaliyo mema. Sasa wanapo ona kuna shida mahali ni lazima waseme kama mtumishi wa Mungu.
Akikaa kimya basi damu itabaki mikononi mwake lakini akisema na kukemea lililo baya na msimsikilize kwa kiburi chenu wanadamu, damu haiko mikononi mwake teeena.
Ni kweli mhimili wa dola unaingilia bunge. Mbona hatuoni vurugu mahakamani, mbona hatuoni vurugu ikulu. Kwanini polisi wawaingilie wabunge ambao ndio wanao tunga sheria za nchi.
Asante baba askofu, Mungu aendelee kukujaza hekima.
Pia asante Mh Waziri mkuu, katende kama ulivyo jibu mbele ya madhabahu ya bwana.
 
Ameongea kama mpakwa mafuta wa Mungu, kazi yao hawa ni kuongoza watu wa Mungu kutenda yaliyo mema. Sasa wanapo ona kuna shida mahali ni lazima waseme kama mtumishi wa Mungu.
Akikaa kimya basi damu itabaki mikononi mwake lakini akisema na kukemea lililo baya na msimsikilize kwa kiburi chenu wanadamu, damu haiko mikononi mwake teeena.
Ni kweli mhimili wa dola unaingilia bunge. Mbona hatuoni vurugu mahakamani, mbona hatuoni vurugu ikulu. Kwanini polisi wawaingilie wabunge ambao ndio wanao tunga sheria za nchi.
Asante baba askofu, Mungu aendelee kukujaza hekima.
Pia asante Mh Waziri mkuu, katende kama ulivyo jibu mbele ya madhabahu ya bwana.
Hivi na Gwajima naye unamuweka kwenye kundi la waliopakwa mafuta na Mungu? Tehetehetehetehe. Mnamdhalilisha bure Mungu
 
TataMadiba
Kaka kila mtu ana haki ya kutoa maoni na ndio maana Kanisa lilimualika Waziri Mkuu na akahudhuria na pia hiyo miimili yote uliyoitaja inaongozwa na binadamu na kwa binadamu kukosea ni kitu cha kawaida, na ndio maana hata tukisoma tunajikumbusha. Hao hao wanasheria na wasomi ndio walisababishwa ile hoja ya Serikali ikaondolewa Bungeni juzi.Ni vizuri tukajifunza kusikiliza na kufanyia kazi maoni ya wengine, sio kila anaekukosoa ana wivu na wewe, ili tuendeleee we need positive critisim
 
Heshima ya nini!? Kwani uongo fisadaisi hakuomba kura kanisani na kusema ni zamu yao walutheli?
 
Back
Top Bottom