Ng'wanamalundi
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,165
- 1,361
Hivi mtu kuwa mbunge wako tayari kunakufanya uwe karibu na mbunge huyo kiasi kwamba ufahamu hata uwezekano wa mtu kuwa gaidi?Askofu mkuu wa KKKT Dr Shoo amesema anamfahamu vizuri Freeman Mbowe ambaye amewahi pia kuwa mbunge wake na hakuwahi kuiona tabia ya ugaidi moyoni kwake, hivyo atashangaa sana kama Freeman ni gaidi...
Naona Askofu ameparamia mambo na kuanza kutetea vitu ambavyo ni wale tu waliokuwa wakishirikiana katika mipango hiyo ndiyo wanaweza kufahamu ukweli.
Wengine tukae kimya mpaka mambo yatakapothibitishwa au yatakaposhindikana kuthibitishwa ndiyo tushangae kwamba mambo yalikuwa hivo.