MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,974
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limeipongeza Serikali ya Awamu ya Tano, kwa kuboresha miundombinu ya barabara na hatua ya kufufua njia ya reli ya Dar es Salaam hadi Moshi mkoani Kilimanjaro.
Kanisa hilo limesema siri ya kwanza ya maendeleo katika nchi ni uwepo wa miundombinu bora na miongoni mwake miundombinu ya kwanza ni ya njia ya reli.
Mkuu wa KKKT, Askofu Dk Fredrick Shoo alitoa pongezi hizo kwa Serikali ya Awamu ya Tano Rais Dk John Magufuli juzi kwenye mahubiri ya Ibada ya Misa ya Jumapili, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Bungo KKKT Dayosisi ya Morogoro.
Ibada hiyo maalumu ya Jubilee ya miaka 25 ya Ndoa na Utumishi wa Kichungaji wa Baba Askofu Jacob Mameo Ole Paulo na mkewe Rose Suleiman Kim’hanga, ilihudhuriwa pia na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa, mkewe Regina, na wakuu wa mikoa ya Njombe, Christopher Ole Sendeka, wa Kigoma, Emmanuel Maganga na mwenyeji wao wa Morogoro, Loata Ole Sanare.
Askofu Shoo amesema siri ya kwanza ya maendeleo katika nchi ni uwepo wa miundombinu bora na miongoni mwake miundombinu ya kwanza ni ya njia ya reli.
Dk Shoo alisema kama Taifa linataka maendeleo, siri ya kwanza ni kuwa na miundombinu bora na zaidi ni ya reli, hivyo alimshukuru Rais John Magufuli kwa kuanzisha tena treni kutoka Dar es Salaam hadi Moshi. “Miundombinu bora ni jambo la msingi sana kwa maendeleo ya nchi, sisi hapa sote tumesafiri kutoka mbali kuja Morogoro kwenye sherehe hii.
“Na watu wa Kaskazini wakati huu ni kurudi nyumbani, nasikia wanatumia usafiri wa treni na imejaa kweli kweli kutoka Dar es Salaam kwenda mikoa ya Kaskazini mbali na usafiri wa mabasi,” alisema Askofu Mkuu huyo wa KKKT.
Alisema treni hiyo ilikuwa imefungwa muda mrefu, ambayo wakati huo ilikuwa ikitoka Dar es Salaam, Kilimanjaro kwenda hadi Taveta nchini Kenya. Hata hivyo, baada ya usafiri huo kusimama kwa miaka mingi, baadhi ya watu walidiriki kung’oa vyuma vya reli na kwenda kuviuza kama chuma chakavu kwani jambo hilo lilimchukiza kuona hakuna reli.
“Jambo la kung’oa miundombinu ya reli lilinisikitisha kweli na kama vitu vilivyonichukiza ni kuona hatuna reli kweli nilijuliza tuna kwenda wapi kama nchi? Kwa hali ya sasa namshukuru Rais Magufuli, treni iliyoanza kusafiri siku chache zilizopitia kwenda Moshi na mikoa ya Kaskazini mabehewa yote yanajaa licha ya uwepo wa mabasi,” alisema Askofu Mkuu Shoo.
Kutokana na mahitaji makubwa ya usafiri huo, aliambiwa kuwa hata baadhi ya mabehewa ya treni ya Deluxe ya kwenda Kigoma, yamehamishiwa njia ya Moshi kutokana na mahitaji makubwa ya usafiri huo.
“Kwa sasa nilikuwa natamani nisafiri na treni, lakini kwa vile upo ujenzi wa reli ya mwendokasi (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi hapa Morogoro itakuwa ni kiunganishi cha usafiri wa haraka kwa treni,” aliongeza.
Treni ya abiria inayofanya safari zake Dar es Salaam kupitia mikoa ya Pwani, Tanga na Kilimanjaro ilianza rasmi Desemba 6, mwaka huu baada ya huduma hiyo kusimama kwa takribani miaka 25 iliyopita. Pia safari za treni ya mizigo kutoka Tanga hadi Moshi zilishaanza.
Chanzo: Habari Leo
VIDEO: MAONI YA WANANCHI WAKIWA NDANI YA TRENI