Askofu Benson Bagonza: Madaraka hayaondoi udhaifu. Madaraka si chanjo ya kuzuia kufanya makosa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Ujumbe wa baba Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD), mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
____________________

Mwaka 2015 hatukuchagua malaika kuwa serikali. Tulichagua watu wenye ubinadamu. Watu hao na udhaifu wao wakaunda serikali. Serikali iliyoundwa na binadamu dhaifu, haiwezi kuwa takatifu kama malaika.

Kwa hiyo serikali ni dhaifu, kwa sababu imeundwa na watu dhaifu, na ilichaguliwa na watu dhaifu. Udhaifu maana yake ni "si kamilifu", "si takatifu" na ina uwezekano wa kufanya makosa.

Madaraka hayaondoi udhaifu. Madaraka si chanjo ya kuzuia kufanya makosa.

Kwa hiyo, nafasi au madaraka hayakingi uchoyo, ubabe, ulafi, uwongo, fitna, ukatili, upendeleo, ukabila, udini, ujinga, maradhi, na hila. Kisingizio cha "kufanya siasa" si kinga ya kuzuia madhara ya udhaifu huo.

Hali kadhalika, kutambua udhaifu si tiketi ya kuendelea kufanya makosa.

Kukubali kuwa unaweza kufanya makosa, ni ibada inayokubalika mbele za Mungu kwa sababu ni ukiri (admission) kuwa wewe si Mungu bali mwanadamu.

Kukiri udhaifu ni kupata nguvu, si kupoteza nguvu. Kunyenyekea ni kuhifadhi nguvu si kuogopa. Hapa ndipo tunakutana na tofauti kati ya ukatili na ujasiri, uungwana na unyonge.

Kama ningechagua, ningemheshimu anayenipa chakula kuliko anayeninyima chakula ili nimjue ana madaraka juu yangu.

Haki huanzia pale tunapokubaliana kuwa sisi ni binadamu wenye udhaifu katika kufikiri, kunena, kutenda. Waliopewa mengi, wadaiwa mengi. Yatosha siku kwa uovu wake.

Hasira ya Mwanadamu haitendi haki ya Mungu. Kisasi ni kwa Bwana wa visasi vyote, anayependa rehema kuliko sadaka!

Baba Askofu Bagonza
 
Huyu Askofu ni hazina kwa Taifa kwasasa,hamumunyi maneno,anatoa ukweli wa serikali isiyotaka kuambiwa ukwel,vyombo vya habari vimekuwa vya hovyo kabsa,masaa 24/7 ni kumsifu Bwana mkubwa,mihimili miwili nayo imegeuka kuwa wabeba makabrasha ya bwna mkubwa,hata kwenye uzinduzi wa darasa moja, wanakuepo mbele kumsifia bwana mkubwa,huo UTOPOLO haukuwepo tawala za nyuma
 
Ujumbe wa baba Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD), mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
____________________
Mwaka 2015 hatukuchagua malaika kuwa serikali. Tulichagua watu wenye ubinadamu. Watu hao na udhaifu wao wakaunda serikali. Serikali iliyoundwa na binadamu dhaifu, haiwezi kuwa takatifu kama malaika...
Huyu Mtumishi angekuwa Askofu Mkuu ingependeza
 
Ujumbe wa baba Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD), mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
____________________

Mwaka 2015 hatukuchagua malaika kuwa serikali. Tulichagua watu wenye ubinadamu. Watu hao na udhaifu wao wakaunda serikali. Serikali iliyoundwa na binadamu dhaifu, haiwezi kuwa takatifu kama malaika....
Huyu wakuchunga naye atulize mshono, yaaani baada ya Tanzania kukataaa kufungisha ndoa za ushoga kanisanii, aligeuka kuwa adui. Hata afanyeje tz hatuko tayari kwa hilo, kama anataka ahamie huko wapokubaliana

Na misaada hapati kabisaaa.
 
Hivi Madokta kama hawa walisomea wapi? Kumbe nchi hii kuna Udoctorate na Udoctoless?
Huyu Askofu siyo Msomi ni Muelimika.
Asante Mungu kwa zawadi hii ya Askofu Bagonza.
Naona mmeitana mmekuja sasa
 
Haleluyaa. Amina.
Ujumbe wa baba Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD), mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
____________________

Mwaka 2015 hatukuchagua malaika kuwa serikali. Tulichagua watu wenye ubinadamu. Watu hao na udhaifu wao wakaunda serikali. Serikali iliyoundwa na binadamu dhaifu, haiwezi kuwa takatifu kama malaika...
 
Ujumbe wa baba Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD), mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
____________________

Mwaka 2015 hatukuchagua malaika kuwa serikali. Tulichagua watu wenye ubinadamu. Watu hao na udhaifu wao wakaunda serikali. Serikali iliyoundwa na binadamu dhaifu, haiwezi kuwa takatifu kama malaika...
Amen kubwa!!
 
Hii ndiyo Injili ya kweli.

Nami nimewahi kulinena hili mara kadhaa, japo siyo kwa ufasaha kama wa Baba Askofu.

Rais Magufuli atambue kuwa yeye ni mwanadamu. Urais haukumwongezea ubinadamu, haukumwongezea akili na wala haukumwongezea maarifa. Kama kweli yeye ni muumini na anayependa kumtii Mwenyezi Mungu, anatakiwa kutambua yeye hana mamlaka ya kuamua nani aishi na nani afe, apotezwe au auawe.

Kwa ujumla mpaka sasa Rais wetu na wasaidizi wake wamejawa na kiburi cha ajabu ya kupindukia, kiburi cha madaraka. Ametunga sheria za ajabu, sheria za kuwagandamiza watu, sheria za kuwatesa watu, sheria za kuwaonea watu. Ajue haya yote anayatenda kwa sababu amemwondoa Roho wa Mungu nafsini mwake.

Ana machaguo mawili, kujutia, kutubu na kumgeukia Mungu. Afute sheria zote zile zilizotungwa kwa nguvu ya shetani. Ama la kama hataki hilo, aendelee kumtumikia shetani lakini ajue ufalme wa shetani una mwisho, ufalme wa Mungu ni wa milele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom