madindigwa
JF-Expert Member
- Aug 30, 2017
- 2,453
- 2,849
Gombea ubunge tujue kama ni mwanasiasaAmeandika Asikofu Dr Kalikawe Lwakalinda Bagonza PHD
TUAZIME TENA HEKIMA YA WANYAMBO
"Nyani asiyekomaa bado (mchanga), huangua kicheko aonapo msitu ukiteketea". Kwa uchanga wake huwa hajiulizi usiku atalala wapi?
"Mtoto mtundu aliyezoea kutukana watu wazima, huwa haishii kwa mmoja".
Tumesikia mengi ya sirini. Hatukupaswa kuyasikia. Nini kinafuata?
1. Wakimaliza ya kwenye simu, watahamia hospitali. Majipu yetu, damu zetu, mikojo yetu, mate yetu, na vinyesi vitaanikwa!
2. Mikopo yetu na bill za baa zisizolipwa zitajukikana. Usisahau mkopo wa nyama wa mwaka jana wakati sasa unakula kisamvu!
3. Toba zetu na vitubio havitakuwa siri tena maana vitaanikwa. Bajameni, acheni kuwasumbua kwa simu watubishaji wenu. Hawana uhakika tena wa kutunza mambo yenu.
4. Kama wana siri hizo, hata "password" za ATM hazina haja tena. Akiba zetu ni akiba zao. Kukwapua mikoba hakufai tena, watu wanachukua wanachopenda kwa kuwa wanamiliki siri zetu.
Bi Kidude hata kama hakuwa Mnyambo, aliwahi kusema "Kunambia siri kisha ukasema nisimwambie mtu, mie siwezi kwa sababu hata wewe umeshindwa kutunza ukaniambia mimi".
Tumejiruhusu kuona "uchi wa mama zetu", acha tupatwe na upofu!!