Askofu Bagonza: Utandawazi ni UHURU, siyo vitu wala fedha. Tanzania ya viwanda inawezekana bila matumizi ya "kufuta" na "kutaifisha

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Kumjua adui ni nusu ya ushindi. Tanzania ya viwanda kwa sasa ina maadui wakubwa wawili: wa kwanza ni neno "kufuta" na wa pili ni neno "kutaifisha". Tukiwajua maadui zetu hawa wawili, ndoto ya viwanda itawezekana.

Maneno haya mawili yakikaa midomoni mwa watawala, yanafukuza uwekezaji, yanatishia usalama wa mitaji na kuyeyusha uthubutu katika kukopa na kudhoofisha kujiamini katika kutumia (consumer confidence).

Uchumi wa soko huria hutawaliwa na usalama wa mitaji na kuheshimu sekta binafsi na mali zake. Soko huria hushamiri mahali palipo na uhuru wa kujumuika, kuungana, kutengana na kushiriki. Maneno "kufuta" na "kutaifisha" ni sumu ya uhuru huo.

Maendeleo katika uchumi wa utandawazi ni UHURU, siyo vitu wala fedha. Tanzania ya viwanda inawezekana bila matumizi ya "kufuta" na "kutaifisha".
 
Kumjua adui ni nusu ya ushindi. Tanzania ya viwanda kwa sasa ina maadui wakubwa wawili: wa kwanza ni neno "kufuta" na wa pili ni neno "kutaifisha". Tukiwajua maadui zetu hawa wawili, ndoto ya viwanda itawezekana.

Maneno haya mawili yakikaa midomoni mwa watawala, yanafukuza uwekezaji, yanatishia usalama wa mitaji na kuyeyusha uthubutu katika kukopa na kudhoofisha kujiamini katika kutumia (consumer confidence).

Uchumi wa soko huria hutawaliwa na usalama wa mitaji na kuheshimu sekta binafsi na mali zake. Soko huria hushamiri mahali palipo na uhuru wa kujumuika, kuungana, kutengana na kushiriki. Maneno "kufuta" na "kutaifisha" ni sumu ya uhuru huo.

Maendeleo katika uchumi wa utandawazi ni UHURU, siyo vitu wala fedha. Tanzania ya viwanda inawezekana bila matumizi ya "kufuta" na "kutaifisha".
Ni Watanzania wachache sana wenye uwezo kuelewa unachosema hapa!
 
Tuna watumishi wachache sana wa Mungu Tanzania. Walio wengi ni Viongozi wa dini.
 
Watukufu wetu watamwelewa? Ama wataishia kusema tunyamaze kwa vile wao ndio madereva na wanajua wanakotupeleka?
 
Back
Top Bottom