Askofu Bagonza nauliza upo upande upi kisiasa?

Deogratias Mutungi

Senior Member
Oct 1, 2019
137
178
ASKOFU BAGONZA NAULIZA, UPO UPANDE UPI KISIASA?

Na, Deogratias Mutungi

Nianze makala haya kwa kurejea msemo wa wahenga wa kiswahili usemao “Kuuliza si ujinga” aidha mwenye kuuliza ujengwa katika tabaka la udadisi, kwa muktadha huo udadisi si utundu wala ukorofi bali ni uungwana ulio jaa hekima na busara na misingi ya uungwana ni vitendo, kwa dhana hiyo swali la makala haya linajengwa katika wema wa mantiki ya kutaka kupata jibu la msingi na lenye ukweli ndani yake, maana ukweli umuweka mtu huru, na ndio hasa maudhui na kiini cha makala haya na si vinginevyo.

Ni imani ya makala haya kuwa mlengwa wa swali hili hawezi kununa, kufura na kuugua homa za vipindi wala kunungunika juu ya swali hili lenye mantiki pana katika mazingara ya jamii yetu ya kisiasa na mifumo yetu ya kuabudu hasa kwa karne hii ya haki na uhuru wa kuhoji na kutoa maoni, Makala haya yanahoji kizalendo na bila shaka yatajibiwa kizalendo zaidi.

Muktadha wa swali hili unaangukia kwa Dkt. Benson Bagonza Askofu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe, swali linanyumbulishwa ndani ya mfumo wetu wa siasa ambao unaegemea katika ulali wa mfumo wa vyama vingi vya siasa tangu mwaka 1992, aidha makala haya yanatambua na kuheshimu haki za kikatiba alizonazo Dkt. Bagonza hasa katika eneo la kujieleza, kutoa maoni yake na kukosoa mamlaka pale inapobidi kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi, Imani ya makala haya ni kuwa anachokifanya Dkt. Bagonza kipo sahihi kabisa isipokuwa ukosefu wa uhalali wake wa kujitambulisha anasimamia utambulisho wa itikadi ipi ndio nongwa na dukuduku ya swali hili inapoanzia dhidi ya Baba Askofu.

Wapinzani wanatambulika kupitia itikadi za vyama vyao, Mwenyekiti wa Chadema anaongoza falsafa na misimamo kupitia utambulisho wa chama chake na ukisikiliza hoja zake ni lazima utambue hilo, Zitto Kabwe anatambulika kwa itikadi na misimamo ya chama cha ACT-Wazalendo, Mwana CUF utamtambua kwa itikadi ya chama chake, aidha wanaharakati wenye mirengo ya kuipinga na kukosoa harakati za kisiasa pia utawatambua kwa desturi, mifumo na taratibu zao za kupinga utawala kwa kivuli cha demokrasia.

Aidha ieleweke kuwa mantiki kuu na dhana ya swali hili ni kutaka kujua ukweli wa mambo kutoka kwa Baba Askofu mwenyewe badala ya mitandao ya kijamii na watu binafsi kujenga hoja na kutaka kuhitimisha mjadala huu bila upande wa pili kuhojiwa au kuulizwa “natural justice”yaani kutompa nafasi Baba Askofu kujieleza ni kosa la kiufundi na pengine ni dhambi ya makusudi, hivyo basi makala hii imeona ni vyema kuhoji na kuuliza ni upande upi wa siasa Baba Askofu anasimama kati ya X au Y ikiwa na maana X Chama tawala au Y Vyama vya upinzani, bila shaka Baba Askofu ataweka mambo hadharani na taifa linamsubiri kwa hamu kubwa sana kwa maana kuwa ni muda mrefu sasa amekuwa mfuasi wa upande Fulani wa siasa lakini kwake imekuwa ngumu kujitambulisha, Sasa Baba Askofu makala haya yanakuomba kujitambulisha rasmi hasa kwa kipindi hiki tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu hapo oktoba kuwa wewe ni chama gani cha siasa.

Hata hivyo sijambo la ajabu viongozi wa dini kukosoa mamlaka zilizopo madarakani katika kujenga taifa imara na lenye demokrasia inayosimamia na kuzingatia haki na usawa wa binadamu ni sehemu ya jukumu lao kufanya hivyo na mataifa mengi duniani yamefanya hivyo, lakini inapoonekana kiongozi wa dini anapotea njia na kusahau mipaka yake katika kukosoa na kujenga hoja hasi na kuonyesha ushabiki wa kuegemea upande Fulani wa kisiasa hasa kwenye taifa linalofuata mfumo wa vyama vingi ni bora mtu huyo aulizwe na ajulikane ni wa moto au wa baridi kuliko kuwa wa uvuguvugu.

Inawezekana kabisa kukawepo na wasiwasi na sintofahamu kwa wasomaji wa makala haya juu ya swali hili kwa Baba Askofu Dkt. Benson, Makala haya yanawaondoa hofu kwa kujenga hoja yenye afya kuwa mantiki ya swali hili ni matokeo ya misimamo hasi na yenye mrengo wa kukosoa kila kitu kinachofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya JPM inayojengwa na Baba Askofu, Je Baba Askofu hajaweza kuona chochote kizuri kilichofanywa na serikali hii au yeye amechagua eneo moja la kukosoa.

Kwa sababu wapo wanaojenga hoja za kuhukumu misimamo ya Dkt. Benson nadhani si sahihi kuhukumu, isipokuwa usahihi wa mantiki tunaweza kuujenga katika nadharia ya kuhoji badala ya kuhukumu kwa kuuliza swali hili Dkt. Benson ni mwanachama wa chama gani cha siasa? CHADEMA, CUF,ACT-Wazalendo, TLP, NCCR-Mageuzi au CHAUMA.

Makala haya yanataja vyama vya upinzani tu ndani ya swali hili kwa sababu ni fimbo ya aina gani upendelea kuitumia kushambulia wenzake isipokuwa tu aina ya mti ndo haufahamiki kama ni fimbo ya mti gani kwa kuondoa hofu hii ni sharti Baba Askofu aulizwe kwa mantiki ya kutaka kujua ukweli wa aina ya mti anaoutumia kupata fimbo zake, bila shaka hoja ya nadharia ya swali langu inaeleweka kwa msomaji wa makala haya.

Dhana inayojengwa kumuhusisha Dkt. Benson na upinzani ni matokeo ya tabia na hoja, mitizamo na falsafa zake ambazo ujengwa katika nadharia ya upinzani na hivyo kumhalalisha kuwa ni mpinzani mwenye vinasaba vya falsafa za kupinga kila dhana ya chama tawala CCM na serikali yake aidha iwe nzuri au mbaya jukumu ni moja tu kupinga na hilo ndio azimio linalo utambulisha upinzani wa Afrika katika medali za kisiasa kuwa ujengwa katika mifumo ya kupinga tu, Japo dhana ya upinzani si kupinga tu bali kukosoa na kusifia mafanikio ya serikali au chama dola kwa sababu Afrika ukomavu wa kisiasa ni mdogo ni nadra kukutana na chama chenye falsafa na mitizamo ya namna hiyo.s

Kwa sababu Dkt.Benson Bagonza anaangukia kwenye kapu hilo ndo maana anaulizwa yupo upande upi wa siasa? Dkt. Benson Bagonza ni msomi na muungwa bila shaka atajibu swali hili ili kuondoa wasiwasi watanzania wenye uchu wa kujua ni mfuasi wa chama gani cha siasa miongoni mwa vyama vilivyopo hapa nchini, makala haya yanaamini Baba Askofu ni jasiri na shupavu hivyo hawezi kuogopa kutambulisha chama chake.

Ifahamike kuwa si dhambi wala kosa la jinai kwa Dkt. Benson Bagonza kujitambulisha bayana na kwa uwazi ni itikadi gani na mrengo upi anaufata kisiasa kwa kukitambulisha rasmi chama chake cha siasa anachokiamini si busara kwa Baba Askofu kuendelea kukaa na siri hii ni vyema sasa ikatolewa hadharani, aidha inaweza kuwa alama itakayo kumbukwa katika vitabu vya kihistoria kuwa kiongozi wa dini aliyethubutu kusimamia kile kilicho moyoni kwa kuonyesha ni mwanachama gani wa chama cha siasa kwake utakuwa ushujaa na heshima iliyotukuka.

Kwa sababu makala haya yanaamini kuendelea kufanya siasa kwa kutumia kofia ya uaskofu au kivuli cha kanisa bila kujitambulisha rasmi ni jambo ambalo kimantiki linaonyesha udhaifu wa mtu au kikundi cha watu wasivyokuwa na msimamo unaoeleweka katika kusimamia yale wanayoyaamini, ni kheri kabisa na bora kujitokeza hadharani na kujitambulisha kwa wanachama wenzako wakufahamu na kukutumia kimkakati pale utakapo hitajika na huu ndio ukomavu wa siasa za kidemokrasia zenye mfumo wa vyama vingi.

Ni rai ya makala haya kumuomba Baba Askofu ajitokeze na ajibu hoja, aidha ni imani ya makala haya kuwa Baba Askofu hataweza kuwa na woga wala wasiwasi wa kutambulisha chama chake cha siasa kwa watanzania, Kwa mantiki hiyo tunasubiri kwa hamu na bashasha tele kusikia neno kutoka kwa Baba Askofu.

dmutungid@yahoo.com
 
Hivi ni lazima mtu uwa upande fulani ili ndiyo ukosoe ama kusifia kitu? Yule bwana hana upande wowote, yeye ni muumini mzuri wa haki na usawa.

Ibada yake ya haki na usawa ndiyo itakuja mletea shida uko mbeleni.

Nb: Mungu Mbariki Bagonza.

Sent from my Phantom6 using JamiiForums mobile app
 
Deogratias Mutungi,

Ni muumini wa haki na usawa Wala si kada, kazi ya kiongozi wa dini ni kuonya, kukanya, kukosoa udhalimu na kuwa mnufaika wa udhalimu. Kiongozi wa dini anachunga roho ni mlinda amani so anapowakemea wahuni waliokosa maadili sababu ya malezi mabovu utotoni ambayo upelekea kuumiza Jamii isiyohusika na kushindwa kwao kupata malezi Bora utotoni.

Kiongozi wa dini atakiwi kushabikia kushirikiana na tawala yeyeto dhalimu kwa sababu anahongwa pesa na kuhofia kupoteza sadaka. Kiongozi yeyeto wa dini ya kweli katu ashirikiani na mwenye dhambi au watu dhalimu huyo ni mjumbe wa shetani. Mtu dhalimu tiba yake ni kutengwa na Jamii ili aujutie na kujua ubaya wa udhalimu. Kushirikiana na mtu dhalimu hakumponyi mtu dhalimu kukoma udhalimu wake.
 
Deogratias Mutungi,

OLE WAO ASKOFU BAGONZA NA ASKOFU MJEMA

ISSAYA 30: *“Ole wao watoto wanaoniasi, wanaotekeleza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mikataba kinyume cha matakwa yangu! Naam, wanarundika dhambi juu ya dhambi. Bila kunitaka shauri, wanafunga safari kwenda Misri, kukimbilia usalama katika ulinzi wa Farao, kupata mahali pa usalama nchini Misri. Lakini ulinzi wa Farao utakuwa aibu yenu, na usalama nchini Misri utakuwa fedheha yenu. Maana ingawa maofisa wao wamefika Soani, na wajumbe wao mpaka Hanesi, wote wataaibishwa na hao wasioweza kuwasaidia, watu ambao hawawezi kuwapa msaada au faida, ila tu kuwapa aibu na fedheha.”...........*

SISI WANA DKMS TUNAWAONYA ASKOFU DR. BAGONZA NA ASKOFU MJEMA,

BAGONZA UPO DAR UNAJIPITISHA PITISHA KUMSAIDIA HUYO MWENZIO ILI APATE KIBALI CHA KUTOROKA NCHI KWA KISINGIZIO CHA MATIBABU,

TUNAKUONYA BAGONZA, KAMA ASKOFU MSTAAFU MUNGA ALIKUDANGANYA KWAMBA WALE WAGOSI KULE NI MBUMBUMBU HAWAWEZI KUFANYA LOLOTE, NJOO TANGA NA MWENZIO MJEMA, KARIBUNI SANA DKMS, MTAVUNA MNACHOKIPANDA

WASAMBAA WANASEMA, *"TAAMIGHOJA"*

Sauti ya *reformers* kutoka msitu wa mizeituni.
 
Huyu Baba Askofu mwanzo nilikuwa namuelewa ila baadae kila nilivyokuwa namfuatilia nikajua kuwa anaegemea upande mmoja wa ukosoaji na hajiweki wazi kama yeye ni CHADEMA.
 
1. Makala yako iko too contradictory by itself. Haiko specific unataka nini kwa Askofu!

2. Na wewe ujibu swali hili: Kwamba, ni lazima kila mtu atoaye maoni take kinzani au yasiyo na uelekeo wa kuunga mkono utawala uliopo madarakani awe mwanachama wa chama fulani?

3. Wewe unataka ajitambulishe aidha ni ACT - WAZALENDO ama CHADEMA ama CCM ili iweje? Je, ni kwa sababu unakuwa huelewi maoni yake anayokuwa anayatoa kwa maandishi au?

4. Siasa na dini ni "inseparable theoretically & in practice". Huwezi kutenganisha haya mambo unless uwe ni mwandishi usiye na ufahamu na maarifa kuendeleza hoja hii. Viongozi wa dini wanaongoza watu. Watu hawahawa ndiyo viongozi katika jamii. Ndiyo hawahawa wanatenda yaliyo kinyume na mafundisho ya dini na imani zao. Askofu ama mchungaji anapoyakemea iwe nje ya kanisa ama msikitini ama ndani ya nyumba ya ibada, huyo anakuwa anatenda wajibu wa wito wake.

5. Kama wewe ni mkristo, nategemea uwe unajua historia ya serikali na utawala wa kidini. Hili ni somo lefu sana. Lakini kwa steji hii itoshe tu kusema, huwezi kutenganisha SIASA/UTAWALA na DINI. Hivi viwili vinategemeana. Kuna CHECKS & BALANCE miongoni mwa hivi. Serikali(siasa) ipo ili itende haki. Asili ya HAKI ni DINI (Mungu). Mungu (dini) haiwezi kunyamaza kimya wakati wanasiasa (watawala/serikali) hawatendi wajibu wao wa kutenda na kuilinda HAKI. Yesu Kristo aliteswa na kusulubiwa msalabani kwa sababu hii. Watawala (wanasiasa) hawakupenda kukosolewa. Wakadhani jibu la kukomesha ukosolewaji wao ni kumuua. Lakini walishindwa. Kwa sababu Mungu hauwawi. Haki haifi milele.

Na ili mtu asimame kwenye HAKI hahitaji kuwa kwenye chama cha siasa chochote. Ni lazima awe mtu huru kabisa. Askofu Bagonza amesimama kwenye nafasi yake, katika wakati wake. Anatekeleza wajibu wake. Hahitaji ruhusa yako. Hahitaji kujibu maswali yako ambayo mimi naomba nithubutu kusema hayana mantiki. Ni propaganda za kiovu na uharibifu tu.

Kama wewe ni mchambuzi huru na wa haki wa masuala, mimi na kila mtu angetegemea ujibu hoja zake. Muwatetee kwa hoja watawala hawa ambao kwa vipimo vyote imethibitika hawatendi HAKI.
 
OLE WAO ASKOFU BAGONZA NA ASKOFU MJEMA

ISSAYA 30: *“Ole wao watoto wanaoniasi, wanaotekeleza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mikataba kinyume cha matakwa yangu! Naam, wanarundika dhambi juu ya dhambi. Bila kunitaka shauri, wanafunga safari kwenda Misri, kukimbilia usalama katika ulinzi wa Farao, kupata mahali pa usalama nchini Misri. Lakini ulinzi wa Farao utakuwa aibu yenu, na usalama nchini Misri utakuwa fedheha yenu. Maana ingawa maofisa wao wamefika Soani, na wajumbe wao mpaka Hanesi, wote wataaibishwa na hao wasioweza kuwasaidia, watu ambao hawawezi kuwapa msaada au faida, ila tu kuwapa aibu na fedheha.”...........*

SISI WANA DKMS TUNAWAONYA ASKOFU DR. BAGONZA NA ASKOFU MJEMA,

BAGONZA UPO DAR UNAJIPITISHA PITISHA KUMSAIDIA HUYO MWENZIO ILI APATE KIBALI CHA KUTOROKA NCHI KWA KISINGIZIO CHA MATIBABU,

TUNAKUONYA BAGONZA, KAMA ASKOFU MSTAAFU MUNGA ALIKUDANGANYA KWAMBA WALE WAGOSI KULE NI MBUMBUMBU HAWAWEZI KUFANYA LOLOTE, NJOO TANGA NA MWENZIO MJEMA, KARIBUNI SANA DKMS, MTAVUNA MNACHOKIPANDA,

WASAMBAA WANASEMA, *"TAAMIGHOJA"*

Sauti ya *reformers* kutoka msitu wa mizeituni.

Unapachika maandiko ya Biblia lakini ukweli ukiwa hata hujui maudhui yake.

Askofu Bagonza anatoa hoja badala mujibu hoja mnaleta vitisho na kushambulia mtu.

Unamjua Yesu Kristo wewe? Haya maneno na vitisho ndivyo alivyopitia kwa sababu tu alikuwa mkosoaji wa watawala wa wakati ule.

Walidhani salama yao ni kumuua. Walifanikiwa kujaribu kumuua. Hakufa yuko hai. Wakafa wao. Yeye you hai hata sasa.
 
Hivi ni lazima mtu uwa upande fulani ili ndiyo ukosoe ama kusifia kitu? Yule bwana hana upande wowote , yeye ni muumini mzuri wa haki na usawa. Ibada yake ya haki na usawa ndiyo itakuja mletea shida uko mbeleni.

Nb: Mungu Mbaliki Bagonza.

Sent from my Phantom6 using JamiiForums mobile app

Angekuwa muumini mzuri wa haki asingeshindwa kumuonya mbowe kusingizia watu wasiojulikana ili hali kaanguka mwenyewe,

Na akijua kukaa kimya kwa tendo hilo ni kuleta taharuki kwa taifa, na pengine kuleta machafuko.
Huko kwenye vyama pinzani sio maraika kwaba siku zote wanatoa matamko sahihi,
Je alishawaonya hadhalani kama anavyoandika hapa JF?
Mtu wa namna hii ana chuki moyoni kwa hiyo hawezi kuwa na haki mbele ya mungu.
 
Kwani Askofu Gwajima na Pengo wapo upande gani enyi kizazi laaniwa cha Lumumba ?
Kwani gwajima unamuona kwenye mitandao kila siku?
Kwani hukumbuki.gwajima amewahi kuwatetea chadema?
Je hujui gwajima huwa anapambana na makonda ambae yupo kwenye serikari,
Je pengo unamuona kwenye media au humu JF kila mara kwa aajiri ya kusifu?
 
Deogratias Mutungi,

Unahitaji tume huru au huhitaji? Tuanzie hapo. Makala ndefuuuu,unazungukaaaa weeeee hivi mnataka kila mtu msomi awe na akili kama za Bashiru au Palamagamba? Ambao kwa Sasa huwezi kuwatofautisha na Bashite wala yule Msukuma wala Lusinde.
 
Unapachika maandiko ya Biblia lakini ukweli ukiwa hata hujui maudhui yake.

Askofu Bagonza anatoa hoja badala mujibu hoja mnaleta vitisho na kushambulia mtu.

Unamjua Yesu Kristo wewe? Haya maneno na vitisho ndivyo alivyopitia kwa sababu tu alikuwa mkosoaji wa watawala wa wakati ule.

Walidhani salama yao ni kumuua. Walifanikiwa kujaribu kumuua. Hakufa yuko hai. Wakafa wao. Yeye you hai hata sasa.

Yesu hakwenda kupambana na akina lazaro wala wafalme, yeye alienda kueneza mambo ya Mungu.

Na ilipokuwa shida yesu na wafalme kutoelewana ni pale wafalme waliikataa mahubili ya yesu kwa kuwa walikuwa na miungu wao. Sasa bagonza yeye anapambana na serikari kwa kuzuia mahubili gani kwenye dini yake?
 
Unahitaji tume huru au huhitaji? Tuanzie hapo. Makala ndefuuuu,unazungukaaaa weeeee hivi mnataka kila mtu msomi awe na akili kama za Bashiru au Palamagamba? Ambao kwa Sasa huwezi kuwatofautisha na Bashite wala yule Msukuma wala Lusinde.

Hizo tume huru mbona bado sio suruhisho kama USA Wana mashaka na ushindi wa Trump,
We unafikili ilisaidia?
2 hiyo tume huru ni Computer ambayo haiwezi kurubuniwa kwa vipande vya pesa?
 
1. Makala yako iko too contradictory by itself. Haiko specific unataka nini kwa Askofu!

2. Na wewe ujibu swali hili: Kwamba, ni lazima kila mtu atoaye maoni take kinzani au yasiyo na uelekeo wa kuunga mkono utawala uliopo madarakani awe mwanachama wa chama fulani?

3. Wewe unataka ajitambulishe aidha ni ACT - WAZALENDO ama CHADEMA ama CCM ili iweje? Je, ni kwa sababu unakuwa huelewi maoni yake anayokuwa anayatoa kwa maandishi au?

4. Siasa na dini ni "inseparable theoretically & in practice". Huwezi kutenganisha haya mambo unless uwe ni mwandishi usiye na ufahamu na maarifa kuendeleza hoja hii. Viongozi wa dini wanaongoza watu. Watu hawahawa ndiyo viongozi katika jamii. Ndiyo hawahawa wanatenda yaliyo kinyume na mafundisho ya dini na imani zao. Askofu ama mchungaji anapoyakemea iwe nje ya kanisa ama msikitini ama ndani ya nyumba ya ibada, huyo anakuwa anatenda wajibu wa wito wake...!

5. Kama wewe ni mkristo, nategemea uwe unajua historia ya serikali na utawala wa kidini. Hili ni somo lefu sana. Lakini kwa steji hii itoshe tu kusema, huwezi kutenganisha SIASA/UTAWALA na DINI. Hivi viwili vinategemeana. Kuna CHECKS & BALANCE miongoni mwa hivi. Serikali(siasa) ipo ili itende haki. Asili ya HAKI ni DINI (Mungu). Mungu (dini) haiwezi kunyamaza kimya wakati wanasiasa (watawala/serikali) hawatendi wajibu wao wa kutenda na kuilinda HAKI. Yesu Kristo aliteswa na kusulubiwa msalabani kwa sababu hii. Watawala (wanasiasa) hawakupenda kukosolewa. Wakadhani jibu la kukomesha ukosolewaji wao ni kumuua. Lakini walishindwa. Kwa sababu Mungu hauwawi. Haki haifi milele....

Na ili mtu asimame kwenye HAKI hahitaji kuwa kwenye chama cha siasa chochote. Ni lazima awe mtu huru kabisa. Askofu Bagonza amesimama kwenye nafasi yake, katika wakati wake. Anatekeleza wajibu wake. Hahitaji ruhusa yako. Hahitaji kujibu maswali yako ambayo mimi naomba nithubutu kusema hayana mantiki. Ni propaganda za kiovu na uharibifu tu...

Kama wewe ni mchambuzi huru na wa haki wa masuala, mimi na kila mtu angetegemea ujibu hoja zake. Muwatetee kwa hoja watawala hawa ambao kwa vipimo vyote imethibitika hawatendi HAKI...
Hongera kwa reply iliyotukuka
 
Back
Top Bottom