Askofu Bagonza ajiepushe na upindifu wa kimantiki unaoweza kuzaa taharuki ya kijamii bila uhalali

Mama Amon

JF-Expert Member
Mar 30, 2018
2,019
2,473
1676280650053.png

Bagonza akiwa amemkumbatia Lissu Kwenye Uwanja wa Kayanga, Karagwe, 2020. Kuhusu sababu mojawapo ya uzushi angalia tofauti kati ya urefu wa kidole cha pili na kidole cha nne, ambapo duara A ni vidole vya Mlinzi wa Lissu vikionyesha kidole cha pili kikiwa kifupi kuliko kidole cha nne na duara B ni vidole vya Lissu vikionyeshs kidole cha pili kikiwa kirefu kuliko kidole cha nne. (Picha kwa hisani ya: Chadema in blood)


I. Usuli

Wanazuoni tunalo jukumu endelevu la kuibua, kujadili, kuchuja na kutetea tunu za binadamu, kwa kupendekeza haki za binadamu kama mbinu ya kufanikisha lengo hilo. Haki hizi ziko katika makundi makuu kumi. Kuna haki za kiuchumi, kisiasa, kielimu, kiafya, kimazingira, kijamii, kiutamaduni, kijinsia, kidini, na kisaikolojia.

Kwa kuzingatia wigo huu, baada ya utangulizi unaojadili kauli za Askofu Benson Bagonza na wenzake, kauli ambazo ni chimbuko la andiko hili, najadili mambo yafuatayo:

(1) Sayansi ya ushoga inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga? (2) Falsafa ya ushoga inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga? (3) Teolojia ya dhambi ya ulawiti inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga? (4) Tunaweza kutumia mbinu gani ili kufanya uchunguzi wa kuwatofautisha watu ambao ni mashoga na watu wasio mashoga? (5) Takwimu zinasemaje kuhusu ukubwa wa tatizo la ushoga hapa nchini Tanzania? (6) Chanzo cha dira ya ashiki kama vile uheterofilia na uhomofilia ni nini hasa? (7) Je, kuhusu suala la ushoga tuwasikilize wanateolojia, wanafalsafa, au wanasayansi? (8) Na je, tunasongaje mbele baada ya hapa?

Mwisho, kwa kuwa yeye ni "Askofu mwenye uthubutu", nitamwalika Askofu Bagonza awakusanye na kushauriana na kina Askofu Nkwande, Paul Makonda na timu yake iliyomjumuisha Afande Suleiman Kova, kina Kigwangala, na wanasiasa baki, kuhusu madhara ya "teolojia ya dhambi ya ulawiti" na sayansi ya uhandisi wa marifa ya kijamii kwa usalama wa nchi.

Kwa msaada wa falsafa ya udhati wa mambo (realism), na sio falsafa ya uhandisi wa kijamii (social constructionism), nitawaalika wakae pamoja na kutafuta mwafaka wa kisayansi, kiteolojia na kifalsafa kuhusu changamoto ya uhomofilia.

Sipendi kuona teolojia ya dhambi ya ulawiti inavuruga nchi kila kukicha, tena pasipo sababu zenye mashiko, kwa kuwafanya baadhi ya watuhumiwa wa ushoga kupigwa risasi 17 mara mbili, kwa kisingizio cha kutekeleza maagizo ya Misahafu katika KItabu cha Mambo ya Walawi, kwenye Agano la Kale.

II. Utangulizi kuhusu chimbuko la andiko hili

Mwaka 2020, wakati wa uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, Askofu Benson Kalikawe Rwalinda Bagonza, wa Dayosisi ya KKKT Karagwe, mkoani Kagera, alizushiwa tuhuma kwamba ni rafiki na mtetezi wa mashoga kwa sababu mbili.

Kwanza ni kutokana na kujitokeza hadharani kwenye uwanja wa Kayanga, Karagwe, na kumsalimia Tundu Lissu, kwa kumkumbatia kama wafanyavyo wanyarwanda. Lissu alikuwa mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha Chadema.

Na pili, ni kutokana na tofauti za urefu wa vidole katika kiganja cha Lissu. Kwenye picha iliyobandikwa hapo juu, tofauti hizo zinaonekana vema kama ukifananisha kiganja kilicho katika duara A (kiganja cha “mlinzi” wa Lissu) na kiganja kilicho katika duara B (kiganja cha Lissu).

Vidole vya “mlinzi” wa Lissu (duara A) vinaonyesha kuwa kidole cha pili ni kifupi kuliko kidole cha nne. Yaani, ukitafuta uwiano wa urefu wa kidole cha pili dhidi ya urefu wa kidole cha nne (2D:4D ratio) utapata namba ya desimali iliyo ndogo kuliko moja.

Lakini, vidole vya Lissu (duara B) vinaonyesha kuwa kidole cha pili ni kirefu kuliko kidole cha nne. Yaani, ukitafuta uwiano wa urefu wa kidole cha pili dhidi ya urefu wa kidole cha nne (2D:4D ratio) utapata namba ya desimali iliyo kubwa kuliko moja.

Kwa mujibu wa maoni ya viongozi kadhaa wa vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja na viongozi kadhaa wa seminari kuu za Kikristo hapa nchini Tanzania, kama mtu anakuwa na kidole cha pili ambacho ni kirefu kuliko kidole cha nne anakuwa na "ulemavu wa vidole" unaomfanya mhusika kuwa na “vidole vya kishoga”, na hali hiyo inachukuliwa kama ishara inayomaanisha kwamba mtu huyo ni shoga.

Ni kwa sababu hii, waseminari wenye “vidole vya kishoga” huwa wananyimwa daraja la upadre; vijana wenye “vidole vya kishoga” wanaoomba ajira kwenye jeshi la polisi na JWTZ hunyimwa ajira; na wagombea wa nafasi za kisiasa wenye wenye “vidole vya kishoga” hupata kejeli sana wakati wa kampeni, kama msukosuko wa Tundu Lissu mwaka 2020 ulivyoonyesha.

Tazama picha ifuatazo Kwa ajili ya kuelewa vema msingi wa tuhuma zinazohusiana na kitu kinachoitwa “vidole vya kishoga” hebu angalia picha zifuatazo:

1676449035898.png


Kwa mujibu wa uchunguzi wangu, Picha hii ikifananishwa na picha ya kiganja cha vidole vya Tundu Lissu, utaona kuwa viganja vyake vinamweka, sio katika kundi la mchoro A, bali katika kundi la mchoro B au mchoro C. Angalia picha zake zifuatazo kwa ajili ya uelewa:

1.jpg

Picha kwa hisani ya: Maswayetu Blogspot.com na gazeti la The Citizen

NAI110-319_2021_082724.jpg

Kwa hisani ya: Niagrafallsreview

thumb_vqv8kf32u2idc5a4fab15da42c.jpg

Kwa hisani ya: Standard Media Kenya

lissu-pic.jpg

Picha kwa hisani ya: The Citizen

Ni kwa sababu hii, wakati wa kampeni za mwaka 2020, “watu wasiojulikana” walitumia mitandao ya kijamii kumvisha Lissu joho la ushoga.

Baadhi ya hawa “watu wasiojulikana” ni zao la propaganda ya hayati Magufuli aliyekuwa anasumbuliwa sana na tatizo la uhomofobia.

Ukirejea hotuba yake kule Kibaha, mkoani Pwani, mwaka 2017, siku alipopiga marufuku wanafunzi waliopata mimba kurejea shuleni baada ya kujifungua, utaona vizuri ukubwa wa hofu aliyokuwa nayo dhidi ya mashoga.

Alimwambukiza hofu hiyo Paul Makonda, RC wa Dar es Salaam wakati huo, hadi akaunda kikosi kazi cha kuwasaka na “kuwashugulikia” mashoga.

Kigezo kikubwa kilichokuwa kinatumiwa na kikosi kazi hicho ili kuwatambua mashoga ni “vidole vya kishoga,” kama picha hapo juu zinavyoonyesha.

Kikosi kazi hiki kilipata msukumo mpya mwaka 2021, wakati wa mazishi ya hayati John Pombe Magufuli, pale Askofu Renatus Nkwande, wa Jimbo Katoliki la Mwanza, alipotumia sehemu ya mahubiri yake kwenye mazishi ya kitaifa kujadili ajenda ya “ushoga,” kana kwamba ni tatizo la kitaifa, japo hakuongelea “vidole vya kishoga.”

Kwa sababu ya propaganda hizi kuhusu “ushoga” na “vidole vya kishoga” sasa jamii yetu, kwa kiasi fulani, imefika hatua ya kuaminishwa kwamba “ushoga ni tatizo la kijamii” ambalo ni “changamoto namba moja” dhidi ya ustawi wa taasisi ya familia kama inavyofahamika, kwa mujibu wa mtazamo wa kimapokeo.

Bila kuweka takwimu bayana, jamii inaaminishwa kwamba, tayari mashoga ni wengi kuliko idadi ya watoto wanaozaliwa nje ya ndoa, kuliko idadi ya wazinzi, kuliko idadi ya waasherati, kuliko idadi ya watalikiwa, kuliko idadi ya michepuko, kuliko idadi ya nyumba ndogo, kuliko idadi ya vimada.

Na watu wanaoeneza propaganda hizi ni wanzuoni, baadhi wakiwa na tasnifu za uzamivu—yaani watafiti waliothibitishwa.

Mfano mzuri ni Askofu Bagonza ambaye, labda bila kujua, anaendesha vita dhidi ya watuhumiwa wa ushoga, akiwemo Tundu Lissu, lakini wakati huo huo yeye akiwa ni mpambe wa Tundu Lissu yule yule anayetuhumiwa kwa ushoga.

Na mwezi Desemba 2022, Askofu Bagonza ameripotiwa katika mitandao ya kijamii kuungana na kina Magufuli na Makonda kwa kutoa kauli ifuatayo:

"Sikubaliani na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya. Hapa kwetu [Tanzania] tayari hali inatisha. Imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, na serikali itaufyata. Wataunda chama chao na kuwania uongozi ... Tuamke."

Hapana! Bila utafiti hakuna haki ya kutuhumu, maana mleta tuhuma ndiye anapaswa kuzithibitisha. Bagonza amevunja kanuni hii.

Lakini, ni kosa kuipotosha jamii kwa kuanzisha tuhuma zisizo na uthibitisho wa kitakwimu. Lazima kuweka sawa mizania ya maarifa ya jamii katika suala hili. Nafahamu kuwa ni jukumu lake Tundu Lissu kujibu tuhuma zinazomkabili.

Alipomaliza kampeni za mwaka 2020 Lissu aliondoka nchini bila kujibu tuhuma dhidi yake. Na mpambe wake Askofu Bagonza amekuwepo nchini muda wote bila kujibu tuhuma hizi pia.

Yaani, mpaka naandika uzi huu, hakuna majibu ya kukanusha ama kuthibitisha tuhuma zifuatazo yalikuwa yemetolewa:

(1) Kwamba, kidole cha pili cha Lissu ni kirefu kuliko kidole chake cha nne; na
(2) kwamba, kwa kuwa kidole cha pili cha Lissu ni kirefu kuliko kidole chake cha nne, basi, taarifa hiyo inamaanishwa kwamba Lissu ni shoga.


Bado analo jukumu la kujibu tuhuma hizi. Hivyo, sitajihusisha na mambo haya mawili.

Badala yake nataka kujielekeza kwenye masuala mtambuka, kuhusu ujenzi wa imani ya jamii pana, yaani “overlapping social doctrine,” kwa faida ya Taifa. Nataka kujibu maswali yafuatayo:

(1) Sayansi ya ushoga inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga? (2) Falsafa ya ushoga inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga? (3) Teolojia ya dhambi ya ulawiti inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga? (4) Tunaweza kufanya uchunguzi wa namna gani ili kuwatofautisha watu ambao ni mashoga na watu wasio mashoga? (5) Takwimu zinasemaje kuhusu ukubwa wa tatizo la ushoga hapa nchini Tanzania? (6) Chanzo cha dira ya ashiki kama vile uheterofilia na uhomofilia ni nini hasa? (7) Je, kuhusu suala la ushoga tuwasikilize wanateolojia, wanafalsafa, au wanasayansi? (8) Na je, tunasongaje mbele baada ya hapa?

III. Sayansi ya ushoga inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga?

Kina Bagonza ni wanateolojia wanaotumia neno "ushoga" bila kutaja fasili yake. Lakini, kisayansi, hili ni neno lenye maana kuu mbili.

Kwa msaada wa mtandao wa Wikipedia, hapa nataka kueleza maana hizi mbili kama sehemu ya mfumo mpana wa misamiati inayotumiwa na wansayansi kueleza aina tofauti za dira ya ashiki (sexual orientation) kati ya watu wawili.

Kwa ajili hii, nitajadili tofauti kati ya mwanamume na mwanamke, tofauti kati ya mlawiti na mlawitiwa, tofauti kati ya msagaji na msagwaji, ulawiti wa kishoga na ulawiti usio wa kishoga, na hatimaye, nitajadili ukiukwaji wa kanuni ya “5W’s na 1H” na madhara yake dhidi ya kanuni za kimantiki.

Tofauti kati ya mwanamume na mwanamke: Ujinsia wa binadamu ni kama sumaku ambayo huweza kuwalazimisha watu wawili kuwasiliana, kujadiliana, kufanya tendo la ngono ya kuunganisha jenitalia ya kiume kwa jenitali ya kike, kuzaa watoto, na hata kuishi pamoja kama mke na mume, ambao ni baba na mama.

Mambo haya hutokea kwa sababu ya kuwepo kwa jozi ya wapenzi wanaounda jozi ya kijinsia yenye vitovu viwili vya ashiki (two erotic centers).

Katika kituo kimoja cha ashiki, kuna mtu mwenye hali ya kuvutiwa kimapenzi na mwanamume, inayoitwa "uandrofilia," (androphilia). Huyu anao dira ya ashiki ya kiandrofilia (androphilic sexual orientation).

Na katika ncha ya pili cha ashiki, kuna mtu mwenye hali ya kuvutiwa kimapenzi na mwanamke, inayoitwa "ugainofilia," (gynophilia). Huyu anao dira ya ashiki ya kigainofilia (gynophilic sexual orientation)

Kwa mujibu wa kawaida ya kitakwimu, karibu asilimia 99 ya watu, huwa wana dira ya ashiki kati ya mwanamke na mwanamume, yaani “androphilia-gynophilia attraction.”

Mkamilishano wa kiashiki wa namna hii, kati ya mwanamke na mwanamume, huitwa "uheterofilia" (heterophilia). Yaani, hali ya mtu mmoja kuvutiwa kimapenzi na mtu mwingine, ambapo watu hawa wawili wanazo jinsia tofauti.

Yaani, uheterofilia hutokea pale ambapo mtu mwenye hali ya uandrofilia anapovutana kimapenzi na mtu mwenye ugainofilia, yaani “androphilia-gynophilia attraction.”

Kuna maheterofilia wa aina tofauti kulingana na tabia zao. Baadhi ya maheterofilia ni wazinzi na wengine sio wazinzi; baadhi ni wabakaji na wengine sio wabakaji; baadhi ni waasherati na wengine sio waasherati; baadhi ni walawiti na wengine sio walawiti.

Tofauti kati ya mlawiti na mlawitiwa: Kwa nadra hutokea uandrofilia kati ya wanaume wawili ambao huzaa sumaku ya kimapenzi kati yao, yaani “androphilia-androphilia attraction.” Hii ni hali ya uhomofilia (homophilia) wa kiume.

Homofilia wa kiume anayelawiti wenzake anaitwa basha, yaani "pedicon" kwa Kiingereza. Sio kila homofilia wa kiume ni basha.

Na homofilia wa kiume anayelawitiwa na wenzake anaitwa chicha, yaani "effeminate" kwa kimombo. Sio kila homofilia wa kiume ni chicha.

Tofauti kati ya msagaji na msagwaji: Kwa nadra hutokea ugainefilia kati ya wanawake wawili ambao huzaa sumaku ya kimapenzi kati yao, yaani “gynephilia-gynephilia attraction.” Hii ni hali ya uhomofilia wa kike (female homophilia).

Homofilia wa kike anayetumia jenitalia yake kuchua jenitalia ya mwanamke mwenzake anaitwa msagaji. Sio kila homofilia wa kike ni msagaji.

Na homofilia wa kike ambaye jenitalia yake ya kike inafanyiwa uchuaji kwa kutumia jenitalia ya mwanamke mwenzake anaitwa msagwaji. Sio kila homofilia wa kike ni msagwaji.

Kitendo cha wanawake wawili kusagana kinaitwa "tribadism" au "tribbing" au "grinding," kwa Kiingereza. Msagaji anaitwa "tribber" na msagwaji anaitwa "tribbee"

Tofauti kati ya ulawiti wa kishoga na ulawiti usio wa kishoga: Hadi hapa, sasa tunaweza kuelewa kirahisi hoja kwamba, neno “ushoga” lina maana mbili.

Maana ya kwanza ya neno “ushoga” ni tabia ya "ulawiti." Na maana ya pili ni hali ya "uhomofilia."

Lakini, tumeona kwamba, sio kila homofilia ni mlawiti (basha), na kwamba, sio kila homofilia ni mlawitiwa (chicha).

Kwa hiyo, neno shoga lina maana tatu. Ama “shoga” ni mtu ambaye ni homofilia na mwenye tabia ya kufanya ulawiti (basha); au ama “shoga” ni mtu ambaye ni homofilia na mwenye tabia ya kufanyiwa ulawiti (chicha); au “shoga” ni mtu ambaye ni homofilia na asiye basha wala chicha. Yaani, tuna shoga mlawiti, shoga mlawitiwa, na shoga asiye mlawiti wala mlawitiwa.

Lakini pia, mlawitiwa anaweza kuwa mwanamke. Kwa kuwa shoga havutiwi na mwanamke, ulawiti wa aina hii utafanywa na mtu ambaye sio shoga, yaani mtu ambaye ni hetrerofilia au mtu ambaye ni heterofilia na homofilia kwa mpigo. Mtu ambaye ni heterofilia na homofilia kwa mpigo huitwa mtu mweney sumaku ya ambifilia.

Hivyo, kwa kuwa kuna ulawiti wa kiheterofilia, ulawiti wa kihomofilia na ulawiti wa kiambifilia, tendo la ulawiti sio “tabia ya kishoga” kwa asilimia mia moja.

Aina tofauti za dira ya ashiki (sexual orientation): Kutokana na yaliyojadiliwa hapo juu, na kwa msaada wa mtandao wa Wikipedia, sasa tunaweza kusema vizuri kwamba, kwa mujibu wa tafiti za kisayansi, kuna aina zifuatazo za dira ya ashiki: uandrofilia, againofilia, uhomofilia, uheterofilia, uhomofilia wa kiandrofilia, na uhomofilia wa kiheterofilia. Michoro ifuatayo inaweka bayana mchanganuo huu:

Mchoro Na. 01: Jedwali la kuonyesha aina tofauti za dira ya ashiki kwa kutofautisha kati ya uhomofilia dhidi ya uheterofilia
1676644450466.png

Chanzo: Wikipedia.com

Mchoro Na. 02: Mchoro wa Venn, wenye duara nne, kwa ajili ya kuonyesha uhusiano uliopo kayi ya uhomofilia, uheterofilia, uandrofilia na ugainofilia
1676644858973.png

Chanzo: Wikipedia.com


Ukiukwaji wa kanuni ya “5W’s and 1H”: Mpaka hapo, ni wazi kwamba, kina Bagonza wanatumia neno “ushoga” bila kuzitofautisha maana zake tofauti, na hivyo kufanya ulaghai kwa njia ya misamiati tata, ama kwa makusudi au kwa bahati mbaya.

Ninachotaka kusisitiza ni ukweli huu: kauli kwamba "mtu fulani ni shoga" ni "question begging."

Yaani inazalisha maswali kadhaa, yakiwemo yafuatayo: mtu huyo ni basha au chicha? Kama sio basha wala chicha tumejuaje kuwa ni shoga? Kama ni chicha, basha wake nani, huwa wanakutana linin a wapi? Kama ni basha chicha wake nani, huwa wanakutana linin a wapi?

Ni vivyo hivyo kwa tuhuma kwamba, "mtu fulani ni mwizi, mwongo, mzinzi, au mbakaji." Mwizi huiba kitu cha mtu baki, hivyo kitu na mmiliki wake lazima watajwe; mwongo hutoa tamko la uwongo dhidi ya mtu baki, hivyo tamko la uwongo na mtu aliyedanganywa lazima vitajwe; mzinzi hujamiiana na mke wa mtu baki, hivyo mke na mume wake lazima watajwe; na orodha inaendelea.

Bila kufanya hivyo, tunakuwa tunaongelea majungu, jambo ambalo ni kosa kubwa kufanywa na mwanazuoni.

Kila mwanazuoni anapaswa kuheshimu kanuni ya "5W's and 1H". Yaani, "what was done, where was it done, when was it done, who was the subject and who are the objects of the action, why was it done, and how was it done?"

Haya ni mswali kuhusu "Usita wa Herufi ya 'U' katika Taarifa Kamilifu", yaani "6U's." Naongelea herufi zifuatazo: "Unani, Ulini, Unini, Uwapi, Uvipi, Usababu na Utaratibu wa tukio au kitendo." Kina Bagonza wanakiuka kanuni hii ya "Usita wa Herufi ya 'U' katika Taarifa Kamilifu."

Upotoshaji wa kanuni za kimantiki: Ukiukwaji wa kanuni ya "Usita wa Herufi ya 'U' katika Taarifa Kamilifu," kama unavyofanywa na kina Bagonza unaambatana na upotofu wa kimantiki. Upotofu wa kimantiki ni upindifu wa kimantiki, yaani “logical fallacy.”

Hili ni kosa la kimantiki ambapo mwongeaji hutunga hoja inayokiuka misingi ya usanifu wa hoja bora na uendeshaji wa mijadala.

Kwa lugha nyingine, upotofu wa kimantiki ni upotoshaji wa maadili ya kimatiki.

Mfano mzuri wa upotofu wa kimantiki ni tabia ya kutumia neno lenye maana nyingi bila mwongeaji kueleza maana anayoikusudia (equivocation).

Mfano ni "Juma amekalia mbuzi". Neno mbuzi linamaanisha mnyama au kifaa cha kukunia nazi. Katika maneno ya Bagonza, neno "shoga" linamaanisha ama "mlawiti" au "homofilia."

Na neno "shoga" lina maana tatu. Linamaanisha ama homofilia basha, au homofilia chicha, au homofilia asiye chichi wala basha.

Kwa hiyo, mwongeaji akitumia neno "shoga" bila kufafanua maana anayokusudia hawezi kueleweka kwa watu wanaoueleea ukweli huu wote. Kina Bagonza hawaeleweki kwa sababu hii.

Mfano mwingine wa upindifu wa kimantiki katika kauli za Bagonza ni tabia ya kuongelea kitu kilicho kwenye tabaka moja, kwa kukibebesha, kimakosa, sifa za kitu baki kilicho kwenye tabaka jingine (category mistake).

Mfano, “sauti” iko katika tabaka la vitu vinavyosikika, wakati “harufu” iko katika tabaka la vitu vinavyonusika. Lakini, mara nyingi watu husema, "nasikia harufu ya chakula."

Maneno haya yanaiweka dhana ya "harufu" katika kundi moja na dhana ya "sauti." Hili ni kosa la kuchanganya pamoja kada za vitu visivyopaswa kuwekwa pamoja.

Yaani, “we say that one has committed a category mistake when she ascribes, to a certain entity, a property or properties which that entity could not have... [meaning that] one locates some entity in a category it does not belong.” (Bernard Matolino, 2014:142)

Kina Bagonza, bila kufafanua, wanatumia neno "ushoga" ama kumaanisha ama homofilia chicha, homofilia basha, homofilia asiye chicha wala basha, ambazo ni kada tatu tofauti za watu, kila kada ikiwa na sifa zake za kitabia.

Lakini, tofauti hizi zinayo maana kubwa katika ulimwengu wa maadili ambapo uadilifu wa mtu unapimwa kwa kuangalia dhamira yake, kitendo chake na mazingira ya kitendo chake.

Kwa hiyo, pendekezo langu ni kuhusu "the law of licit logical inference." Linahusu mbinu za "usanifu wa hoja bora." Na maneno "usanifu wa hoja bora" yana sehemu mbili. Kwanza ni "usanifu" na pili ni "hoja bora".

Kusanifu kitu ni kuunda kitu kwa kukipa umbo fulani, yaani "designing a thing." Hivyo, "usanifu wa hoja bora" ni uundaji wa hoja bora.

Na "hoja bora" ni hoja yenye muundo bora, yaani muundo unaokubaliana na anatomia ya hoja, kama tukiongozwa na nadharia mamboleo za kimawazo kuhusu usanifu wa hoja.

Ziko nadharia kuu mbili. Kuna nadharia ya Aristotle wa Ugriki na nadharia ya Stephen Toulmin wa Uingereza.

Nadharia ya Aristotle wa Ugriki ya Kale inasema kuwa hoja bora inapaswa kuwa na muundo wenye sehemu tatu: dokezo kuu, dokezo dogo, na hitimisho. Mfano:

(1) Cheti cha kuzaliwa cha Bagonza kinasema alizaliwa Tanzania, (2) Wazazi wa Bagonza wanasema kuwa alizaliwa Tanzania, (3) Hivyo, Bagonza ni Raia wa Tanzania.

Na nadharia ya Stephen Toulmin wa Uingereza, iliyobuniwa miaka ya 1960, inaboresha nadharia ya Aristotle.

Toulmin anasema kuwa hoja bora inapaswa kuwa, sio na sehemu tatu pekee, kama alivyofundisha Aristotle, bali inapaswa kuwa na sehemu angalau sita zifuatazo:

(1) Tamko (claim), (2) Uthibitisho wa kuunga mkoni tamko (ground), (3) Utetezi wa kuunga mkoni uthibitisho (warrant), (4) Msingi wa kuimarisha utetezi (backing), (5) Pingamizi dhidi ya tamko (objection), (6) Majibu ya pingamizi (rebuttal), na (7) Mipaka ya tamko linalopendekezwa (qualifier/concession). Mfano:

(1) Bagonza ni Raia wa Tanzania. (2) Wazazi wa Bagonza wanasema kuwa alizaliwa Tanzania. (3) Cheti cha kuzaliwa cha Bagonza kinasema alizaliwa Tanzania. (4) Sheria ya uraia inasema kuwa kila mtu aliyezaliwa nchini Tanzania anakuwa na sifa ya uraia wa kuzaliwa. (5) Huenda Bagonza ameshakana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa nchi nyingine au ameshakufa. (6) Hakuna ushahidi wowote wa kuthibitisho pingamizi hilo. Na (7) Kama Bagonza hajakana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa nchi nyingine na hajafa, basi tamko kuu hapo juu linasimama. Lakini, litaanguka kama ameshakana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa nchi nyingine au ameshakufa.

Katika uwasilishaji wa mawazo kupitia maongezi ya kawaida pointi hizi saba zitaunganishwa na kuonekana hivi:

Kuna uwezekano mkubwa kwamba, (1) Bagonza ni Raia wa Tanzania, kwa sababu (2) Wazazi wa Bagonza wanasema kuwa alizaliwa Tanzania; na kwa kuzingatia kwamba, (3) Cheti cha kuzaliwa cha Bagonza kinasema alizaliwa Tanzania; na kutokana na ukweli kuwa, (4) Sheria ya uraia inasema kuwa kila mtu aliyezaliwa nchini Tanzania anakuwa na sifa ya uraia wa kuzaliwa; isipokuwa kama itathibitika kwamba, Bagonza ameshakana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa nchi nyingine au ameshakufa, mapingamizi ambayo hayana ushahidi wa kuyaunga mkono kwa sasa.

Hivyo ndivyo wanazuoni tunavyopaswa kufikiri. Kanuni hizi zikiheshimiwa, halafu tukaunganisha nguvu kufundishana juu ya sheria asilia za maadili, tutakuwa tumeutakatifuza ulimwengu vizuri zaidi.

IV. Falsafa ya ushoga inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga?

Nataka kuongelea falsafa ya ushoga kwa kutumia mawazo yaliyo katika mapokeo ya kimetafizikia kutoka kwa Aristotle na Aquinas kuhusu udhati wa vitu. Yaani, "Aristotelian-Thomistic metaphysics."

Kwa mujibu wa maandiko ya David Oderberg(2011), Aristotle alifundisha na Aquinas akaunga mkono hoja kwamba: mtu atakuwa anafahamu hulka ya kitu kwa ukamilifu kama anajua mambo manne.

Mambo hayo ni muundo wa kitu husika (formal cause); maudhui ya kitu husika katika ngazi ya kifizikia, kikemia na kibayolojia (material cause); sababu ya kihistoria kuhusu uwepo wa kitu husika (efficienct cause); na sababu ya kimatarajio kuhusu uwepo wa kitu husika (teleological cause).

Ufafanuzi wa misingi ya metafizikia ya Aristotle na Aquinas: Kusudi tuweze kuelewa mambo haya twende kwa njia ya mifano. Tuchukue tofali kwanza.

Muundo wake ni mche mstatili unaotokana na umbo la kifyatulio cha matofali. Maudhui yake ni simenti, mchanga na udongo.

Sababu ya kihistoria kuhusu uwepo wake ni maamuzi na matendo ya mfyatua matofali aliyechanganya simenti, mchanga na udongo. Na sababu ya kimatarajio kuhusu uwepo wa tofauli ni kufanikisha ujenzi wa nyumba.

Mara nyingi, wanafunzi wangu wa somo la falsafa hushindwa kutofautisha kati ya sababu ya kihistoria kuhusu uwepo wa kitu husika (efficienct cause) na sababu ya kimatarajio kuhusu uwepo wa kitu husika (teleological cause).

Lakini, huwa natumia mfano ufuatao kuwapa mwangaza. Fikiria kwamba, unatembea kwa mguu kupitia kichochoro fulani katika bonde na unaibukia kwenye kilima na kukuta hoteli kwa ajili ya kuhudumia wasafiri, yaani moteli.

Ukiulizwa, "kwa nini hoteli hiyo iko hapo?" kuna majibu mawili yanawezekana. Jawabu la kwanza linahusu sababu ya kihistoria kuhusu uwepo wa hoteli (efficienct cause).

Yaani, hoteli hiyo iko hapo kwa sababu kuna wahandisi walisomba mawe, matofali, maji, nondo na kokoto, na kisha kuijenga.

Na jawabu la pili linahusu sababu ya kimatarajio kuhusu uwepo wa kitu husika (teleological cause).

Yaani, lengo walilokuwa nalo wajenzi hawa, wakati wanachora ramani ya hoteli na kuijenga hadi kukamiliki. Lengo lao lilikuwa ni kutoa huduma ya chakula, vinywaji na malazi kwa wasafiri.

Katika falsafa za Aristotle na Aquinas, hiyo ndiyo tofauti kati ya sababu za kihistoria na sababu za kimatarajio.

Kama tukitumia nyenzo hizi za kifikra kutoka kwenye mapokeo ya falsafa za Aristotle na Aquinas, napendekeza kwamba, tutakuwa na majibu yafuatayo kuhusu hulka ya binadamu ambaye ni shoga:

(a) Muundo wa shoga (formal cause of a male homophilic person): Akili, utashi, jenitalia za kiume, mwonekano wa binadamu mwanamume.

(b) Maudhui ya shoga (material cause of a male homophilic person): Viungo vya mwili wa binadamu, homoni za kike zilizo juu kidogo ya homoni za kiume, kromozomu 46 zenye fomati ya XY, ana dira ya ashiki inayomfanya kutamani wanaume badala ya kutamani wanawake.

(c) Sababu ya kihistoria kuhusu uwepo wa shoga (efficient cause of a male homophilic person): Baba na mama yake waliomzaa na kumlea.

(d) Sababu ya kimatarajio kuhusu uwepo wa shoga (teleological cause of a male homophilic person): Kuwa mtu mzima anayetekeleza majukumu mbalimbali katika jamii kulingana na vipaji alivyozaliwa navyo.

Kama tukitumia mfumo huu wa kifikra kujadili hulka ya binadamu mwanamume asiye shoga, tofauti itajitokeza kwenye kipengele cha (b), ambapo tutaandika kwamba: ana dira ya ashiki inayomfanya kutamani wanawake badala ya kutamani wanaume.

Kwa hiyo, ni maoni yangu kwamba, maneno “hulka ya ubinadamu”, yaani “human nature,” yanazo maana zaidi ya moja. Kwa hapa, tunazo seti tofauti kwa ajili ya kutaja sifa za mtu mwenye "hulka ya binadamu mwenye uheterofilia", na "hulka ya binadamu mwenye uhomofilia."

Seti hizi zina mlaliano (intersection) katika ngazi ya urazini, lakini pia kutakuwepo na tofauti kadhaa za kimwili na kihisia.

Vivyo hivyo, tunazo seti tofauti kwa ajili ya kutaja sifa za mtu mwenye “hulka ya binadamu mwanamke mwenye uhomofilia”, na “hulka ya binadamu mwanamke mwenye uheterofilia.” Seti hizi zina mlaliano (intersection) katika ngazi ya urazini, lakini pia kutakuwepo na tofauti kadhaa za kimwili na kihisia.

Kadjalika, tunazo seti tofauti kwa ajili ya kutaja sifa za mtu mwenye “hulka ya binadamu mwanamke”, na “hulka ya binadamu mwanamume.” Seti hizi zina mlaliano (intersection) katika ngazi ya urazini, lakini pia kutakuwepo na tofauti kadhaa za kimwili na kihisia.

Hii maana yake ni kwamba, tunapoongelea “hulka ya ubinadamu” kama msingi wa sheria asilia za ustawi wa binadamu, kuna sheria asilia hazitamhusu mwanamume mwenye uhomofilia, japo zinamhusu mwanamume mwenye uheterofilia; na kuna sheria asilia hazitamhusu mwanamke mwenye uhomofilia, japo zinamhusu mwanamke mwenye uheterofilia.

Tofauti kati ya umiliki, upotevu na udumavu: Katika misamiati ya Metafizikia ya Aristotle na Aquinas, tofauti kati ya mtu mwenye uhomofilia na mtu mwenue uheterofilia, inaelekezeka kwa kutofautisha dhana tatu.

Oderberg(2011) anasema kuwa, dhana hizo ni, "umiliki, upotevu na udumavu." Yaani, "possession, privation and deprivation."

Kwa mfano, mtu mzima aliyepata ajali ya gari na kupoteza meno aliyokuwa anayamiliki anakuwa na tatizo la "upotevu" (privation). Lakini, mtu mzima anbaye kwa sababu zisizofahamika hakuwahi kuota meno na tatizo la "udumavu" (deprivation).

Lakini, nyoka asiye na miguu, ndivyo hulka yake ilivyo. Na hivyo, hatusema kwamba nyoka ana tatizo la "uptevu" wa miguu wala udumavu" wa miguu.

Kwa kuzingatia mantiki hii, binadamu mwenye dira ya ashiki ya kihomofilia hana tatizo la kupoteza dira ya ashiki ya kiheterofilia, kana kwamba ni sifa alikuwa nayo hapo kabla (“privation”).

Bali ana tatizo la kutopata kabisa dira ya ashiki ya kiheterofilia, ambayo ni sifa aliyopaswa kuwa nayo (“deprivation”).

Hii maana yake ni kwamba, kuongelea ustawi wa binadamu mwenye hulka ya uheterofilia kwa kutumia vigezo vya ustawi wa binadamu mwenye hulka ya uhomofilia, ni kuchanganya maembe na machungwa, Yaani, ni kushindwa kuelewa na kutumia ipasavyo mawazo ya Aristotle na Aquinas kuhusu hulka ya kitu.

Ufanano na utofauti kati ya ulawiti, utianaji , uzinzi na uasherati: Mpaka sasa tumeona kwamba, uhomofilia ni hali ya mwanamume kuwa na dira ya ashiki inayomsukuma kufanya ulawiti (pedication), au hali ya mwanamke kuwa na dira ya ashiki inayomsukuma kufanya usagaji (tribbing).

Pia, tumeona kwamba, uheterofilia ni hali ya mwanamume au mwanamke kuwa na dira ya ashiki inayomsukuma kufanya utianaji (copulation), ama ndani au nje ya ndoa, ama kabla ya ndoa au baada ya ndoa.

Ngono kati ya mwanandoa na mtu asiye mwanandoa mwenza ni uzinzi (adultery). Ngono kati ya watu wawili wasio na ndoa popote ni uasherati (fornication).

Maneno ya msingi hapa ni "ulawiti, usagaji, utianaji, uzinzi na uasherati." Hivyo, katika hatua hii, napenda kutumia metafizikia ya Aristotle na Aquinas kuelezea ufanano na utofauti wa kifalsafa uliopo kati ya matendo haya.

Kwa ajili hii, naanza kwa kueleza tofauti kati ya lengo la mtendaji na lengo la kitendo. Chukulia mfano wa fundi anayefanya kazi ya kuunda na kuuza saa, yaani kifaa cha kuhesabu majira.

Fundi saa ni mtu anayetengeneza saa kwa lengo la kupata mkate wake wa kila siku--kipato.

Lakini, atafanikisha lengo lake kama saa anayoitengeneza inafanya kazi yake vizuri, yaani kazi ya kuhesabu majira.

Kwa hiyo, hapa kuna malengo mawili tofauti. Kwanza, kuna lengo la mtendaji (finality of the operator) anayeunda saa. Na pili, kuna lengo la kitendo cha kuunda saa (finality of the operation).

Katika Metafizikia ya Aristotle na Aquinas, lengo la mtendaji tunaweza kuliita finali ya mtendaji; na lengo la kitendo tunaweza kuliita fainali ya kitendo.

Katika sentensi hii, nafasi ya neno "fainali" inaweza kuchukuliwa na neno "telosia." Hivyo, tukaongelea telosia ya mtendaji na telosia ya kitendo.

Sasa naweza kusema pointi yangu kama ifuatavyo: Tofauti iliyopo kati ya telosia ya kitendo na telosia ya mtendaji kwenye kitendo cha kuunda na kuuza saa, pia inapatikana kwenye kila kitendo cha kufanya ngono.

Mahusiano ya kimapenzi, yanaweza kuanzishwa kwa ajili ya ki=ufanikisha malengo kadhaa ya watendaji, kama vile kutafuta kipato, kutoa shukrani, kuonyesha upendo, kutuliza mawazo, na kadhalika.

Lakini, mbali na telosia za watendaji, kama mahusiano ya kimapenzi yakitamzamwa katika barabara ya kihistoria na kieskatolojia (chronological timeline), yanahusisha tendo la ngono lenye telosia kadhaa.

Mosi, kila tendo la ngono linalofahamika, kama vile ngono ya jenitalia kwa jenitalia, jenitalia kwa vidole, jenitalia kwa matiti, jenitalia kwa kwapa, jenitalia kwa mapaja, jenitalia kwa mdomo, au jenitalia kwa rektamu, huzalisha telosia ya "umoja wa kimwili na kiakili," yaani "body-self unity" au "personal unity", angalu kwa mshiriki mmoja.

Hapa kuna tunu ya "utulivu wa kiakili na kimwili," yaani "psycho-somatic reintegration." Hapa, umoja wa vitu viwili, mwili na akili, hutokana na kitu cha tatu, yaani, "utulivu wa kiakili na kimwili."

Kuhusu telosia hii, wakati wa kujamiiana, Salzman na Lawler (2008:127-28) wanasema kuwa, mwitiko wa kiakili na kimwili wakati wa kufanya mapenzi hupitia kwenye hatua nne.

Kuna "kusisimka, kutafuta mshindo, kupata mshindo, kushusha pumzi." Yaani, "excitement, plateau, climax and resolution." Kila hatua inaambatana na mabadiliko mahsusi ya kimwili na kiakili.

Katika hatua ya kwanza jenitalia ya kiume husimama, jenitalia ya kike kulainika, mapigo ya moyo na kasi ya kupumua huongeza, misuli ya mwili yakiwemo matiti ya mwanamke hutuna na kukakamaa.

Katika hatua ya pili, jenitalia ya kiume huingizwa katika jenitalia ya kike; mapigo ya moyo, kasi ya kupumua, na ukakamavu wa misuli ya mwili huendelea kuongezeka; na kichwa cha jenitalia ya kiume husuguliwa dhidi ya ukuta wa jenitalia ya kike hadi jenitalia ya kiume inapolegea.

Katika hatua ya tatu, jenitalia ya kiume hutema manii ndani ya jenitalia ya kike, misuli ya sphinkta yenye kuzunguka jenitali za kike na kiume hubana na kuachia ikisindikza manii, na kuhitimisha hatua ya mshindo, inayoambatana na hali inayoonekana kama "kifafa cha mapenzi."

Na hatua ya nne ni hitimisho linaloambatana na kushuka kwa mapigo ya moyo, kushuka kwa kasi ya kupumua, na kushuka kwaukakamavu wa misuli ya mwili.

Hatua zote nne husindikizwa na anasa ya kierotiki, ambayo ukomo wake huonekana kumaanisha kukarabatika kwa mwili na akili, yaani "psycho-somatic re-creation."

Mara nyingi, lengo wa watendaji huwa ni "kuvuna" anasa ya mwili, lakini lengo la kitendo, yaani kuibuka kwa "utulivu wa kimwili na kiakili," linabaki pale pale, bila kujali kama ni tendo la ndoa, tendo la uzinzi, tendo la uasherati, au tendo la punyeto.

Pili, kila tendo la ngono linalofahamika, huzalisha telosia ya umoja wa kijiografia (spatial unity). Hapa, umoja wa watu wawili hutokana na kitu cha tatu, yaani, eneo la kufanyia tendo la ngono.

Yaani, kusudi watu wawili waweze kufanya tendo la ngono, lazima wakutane mahali fulani, mfano chumbani, kitandani, hotelini, au garini.

Tatu, kila tendo la ngono linalofahamika, huzalisha telosia ya umoja wa kimajira (temporal unity). Hapa, umoja wa watu wawili hutokana na kitu cha tatu, yaani, muda wa kufanya tendo la ngono. Mfano, tendo la ngono huchukua muda angalau wa dakika tano.

Tatu, kila tendo la ngono linalofahamika, huzalisha telosia ya umoja wa kijamii, yaani, jamii ya watianaji, au jozi ya watianaji (interpersonal unity).

Hapa, umoja wa watu wawili hutokana na kitu cha tatu, yaani, mapatano ya watu wawili kukutana katika eneo moja la kijiografia wanalolikalia kwa mpigo wakati wa tendo la ngono.

Nne, kila tendo la ngono linalofahamika, huweza kuzalisha telosia ya umoja wa kikemia katika jozi ya watianaji (chemical unity).

Hapa, umoja wa watu wawili hutokana na kitu cha tatu, yaani, homoni ya pingu za kimahaba, yaani "oxytocin," ambayo huzalishwa mwilini kutokana na matukio ya kutomasana, kukumbatiana, na kujamiiana.

Homini ya "oxytocin" huzalisha kumbukumbu za kimahaba hata baada ya wapenzi kuachana (sex afterglow), na hivyo kuwafanya watafutane tena na tena.

Na kadiri wanavyokutana tena homoni zaidi huzalishwa miilini mwao, na hivyo kuzidi kuzimiana katika hisia zao(emotional unity).

Tano, kila tendo la ngono ya jenitalia kwa jenitalia, inayofanyika bila kutumia kingamimba, huweza kuzalisha telosia ya ndoa (marital unity).

Hapa, umoja wa watu wawili hutokana na kitu cha tatu, yaani, maisha ya mwanamke na mwanamume, wakiishi chini ya paa moja, kama mke na mume, wenye fursa ya kukutana mara kwa mara kimpenzi, bila haja ya kutafutana kwa masafa.

Na sita, kila tendo la ngono ya jenitalia kwa jenitalia, inayofanyika bila kutumia kingamimba, huweza kuzalisha telosia ya uzazi (procreative unity).

Hapa, umoja wa watu wawili hutokana na kitu cha tatu, yaani, mchakato wa uzazi unaojumuisha utianaji, urutubisho, upandikizaji, kulea mimba, kuzaa na kulea mtoto.

Yaani, kadiri homoni zaidi inavyozalishwa frikwensi ya mahusiano ya kimpenzi huongezeka, hadi fursa ya kubeba mimba kujitokeza, kama ngono ya jenitalia kwa jenitalia inayofanyika bila kutumia kingamimba inahusika.

Kwa ujumla, kutokana na tendo la ngono ya jenitalia kwa jenitalia, inayofanyika bila kutumia kingamimba, familia ya baba, mama na watoto huzaliwa, na hivyo, umoja wa kifamilia kuwepo (familia unity).

Ujio wa mtoto mpya humaanisha kuanza kwa umoja kati ya baba na mama kwa sababu ya mtoto, umoja kati ya babu na bibi kwa sababu ya wajukuu, na hivyo umoja wa watoto, wazazi na mababu kwa sababu ya ukoo mmoja (intergenerational unity).

Kwa maneno mengine, tendo la ngono ya jenitalia kwa jenitalia, inayofanyika bila kutumia kingamimba, linaweza kuwa na telosia kuu tatu: telosia ya umoja wa kisaikolojia na kimwili, telosia ya umoja wa jozi ya watianaji, telosia ya umoja wa wanandoa, telosia ya umoja wa wanafamilia, na telosia ya umoja wa wanaukoo.

Kwa Kiingereza tunaweza kufupisha maneno haya kwa kusema kwamba, "uncontracepted copulation is personally unitive in type, interpersonally unitive in type, and intergenerationally unitive in type."

Au tunaweza kusema kwamba, "uncontracepted copulation is personally reintegrative in type, interpersonally relative in type, and intergenerationally reproductive in type." Maneno "reintegratove, relative, na reproductive" yanaturuhusu kuongelea "the three R's of sex," yaani "utatu wa herufi ya R katika mapenzi."

Ukisoma waraka wa Papa Paul VI (1968), "Humanae Vitae," yaani "Maisha ya Binadamu ", utakutana na mawazo haya matatu katika tamko lake kwamba, "each and every marital act [of sexual intercourse entails] ... unitive significance and procreative significance both of which are inherent to it" (HV, 11-12).

Anachosema Papa Paul VI kupitia maneno kwamba "each and every marital act [of sexual intercourse entails] ... unitive significance," ni kwamba, "each and every marital act is personally and interpersonally unitive in type."

Na anachosema kupitia maneno kwamba "each and every marital act [of sexual intercourse entails] ... procreative significance," ni kwamba, "each and every marital act is intergenerationally unitive in type."

Neno "significance" linamaanisha "maana" inayobebwa na "alama." Kutokana na taaluma ya semiolojia (semiotics) tunafahamu kwamba, alama elekezi (indexical sign) ni alama asilia kwa kuwa inatokana na uhusiano asilia kati ya sababu na matokeo.

Kwa mfano, moshi husababishwa na moto, na hivyo moshi huchukuliwa kama alama ya moto. Hapa matokeo ni alama ya sababu.

Lakini pia, mawingu husababisha mvua, na hivyo mawingu huchukuliwa kama alama ya mvua. Hapa, sababu ni alama ya matokeo.

Hivyo, kusema kwamba, tendo la ngono linabeba maana ya uzazi, ni kifupi cha maneno kwamba, tendo la ngono, ni sababu na hivyo alama ya, matokeo yanayoitwa uzazi.

Vivyo hivyo, kusema kwamba, tendo la ngono linabeba maana ya umoja, ni kifupi cha maneno kwamba, tendo la ngono, ni sababu na hivyo alama ya, matokeo yanayoitwa umoja. Maneno ya msingi katika ufafanuzi huu ni "alama," "maana," "sababu" na "matokeo."

Hivyo, maneno "unitive significance" yanakumbatia "utata wa kimismaiati", yaani "equivocation," unaopaswa kuondolewa ili kuboresha mafundisho ya Kanisa kuhusu maadili asilia kuhusu ujinsia wa binadamu.

Utata huo unaweza kuondoka hivi: "each and every marital act [of sexual intercourse entails] ... [personally and interpersonally] unitive significance."

Viongozi wengi wa dini huongea sana kuhusu " [interpersonally]unitive significance," kila wanapojadili telosia ya ndoa

Lakini, hawasemi sana kuhusu " [personally] unitive significance," inayohusu telosia ya "umoja wa mwili na roho," yaani "utulivu wa mwili na roho," kama "tunu ya msingi" (basic good) ambayo ni zao la tendo la ngono.

Kwa maoni yangu, wanakwepa kuongelea telosia hii kwa sababu ya hofu kwamba inaweza kuwapa wazinzi, waasherati na mashoga sababu nzuri ya kuendelea kufanya matendo ya ngono yaliyo haramu kimaadili.

Lakini, ni muhimu kuongelea telosia hii kusudi tupate kuelewa vema sababu ya kuongezeka kwa wazinzi, waasherati na walawiti, na hivyo kutafuta dawa mwafaka ya matatizo haya matatu kwa pamoja, badala ya kuelekeza nguvu kwenye ulawiti, wakati takwimu za walawiti ni kidogo kuliko takwimu za uzinzi na uasherati.

Kubwa tukumbuke mambo mawili. Mosi, uzinzi, uasherati, ulawiti/usagaji/punyeto na utianaji unaofanyika kama tendo la ndoa ni matendo ya ngono yanayofanana kwa sababu yote huleta telosia ya umoja wa kisaikolojia na kimwili (personal unity) na telosia ya umoja wa kijamii (interpersonal unity).

Na pili, tofauti kati ulawiti/usagaji na matendo haya baki ni kwamba, ulawiti/usagaji/punyeto ni tendo la ngono lisilo na telosia ya uzazi, japo linayo telosia ya umoja wa kijamii na telosia ya umoja wa kisaikolojia na kimwili.

Katika kuhitimisha sehemu hii, napenda kurejea maneno ya Papa Paul VI, katika andiko lake "Maisha ya Binadamu (1968)," kama "mstari mnyoofu" unaotenganisha "ndoa za jinsia tofauti" na kile ambacho huko ughaibuni kinaitwa "ndoa za jinsia moja". Ni haya:

"... each and every [heterosexual] marriage act ...[entails an] inseparable connection ... between the [personally unitive significance, interpersonally] unitive significance and the procreative significance which are [triply] inherent to the [heterosexual] marriage act." (HV, 11-12).

Ni maoni yangu kwamba, maneno haya, ni mwongozo mzuri kila tunapojadili "utatu wa herudi ya R katika mapenzi ya wanandoa," yaani, "reintegration, relationality, and reproduction." Kwa Kiingereza hapa tunaongelea "the 3R's of marital sex."

Kwa njia hii ule utata wa neno "unitive" uliomo katika waraka wa "HUmanae Vitae (1968) unakuwa umeondoka, lakini bila kufungua milango kwa ajili ya kukaribisha "ndoa za jinsia moja."

V. Teolojia ya dhambi ya ulawiti inasema kuwa ushoga ni kitu gani na watu gani wanahesabika kuwa ni mashoga?

Kwa mujibu wa Biblia, ninachokitaja hapa kama "teolojia ya dhambi ya ulawiti" ni sehemu ndogo ya "teolojia ya dhambi za kijinsia", yaani "hamatiolojia ya ujinsia", yaani "sexual harmatiology" kwa Kiingereza. Upande wa pili wa shilingi ya teolojia ya dhambi za kijinsia ni "teolojia ya wokovu wa kijinsia, yaani "sexual soteriology." unahusiana moja kwa moja na "teolojia ya ndoa."

Mwanateolojia John Yates (1995), amenisaidia kuelewa mengi kuhusu mijadala ya wanateolojia kuhusu swali hilo hapo juu. Ni mijadala inayojenga hoja ifuatayo:

Kwamba, kwa kuwa kila dhambi ni kitendo cha kuukataa mpango wa Mungu; na kwa kuwa, pasipokutubu, kuukataa mpango wa Mungu katika eneo Mungu ni sawa na kuukataa Mpango wa Mungu katika maeneo yote; basi, mtenda dhambi yeyote ni mtu aliyemktaa Mungu, na hivyo asiye na nafasi katika jumuiya ya watu wanaomwamini Mungu. Ni wazi kwamba huu ni udini mkali.

Ni mijadala inayochagua ulawiti kama dhambi kubwa kuliko dhambi zote baki, ikiwemo dhambi ya kuua mutu. Lakini, kama nitakavyoonyesha, hadi leo teolojia ya dhambi ya ulawiti haina jawabu kwa swali "shoga ni mtu wa aina gani na sio mtu wa aina gani?"

Nataka nifupishe baadhi ya masuala madhubuti ya kiteolojia yanayohusika katika mijadala hii, yakiwa ni madai yanayoanzia kwenye teolojia ya ubinadamu (theological anthropology), yaani matamko haya:

Kwamba, wanadamu wote, bila kujali dira ya ashiki, wana heshima ya asili waliyopewa kutokana na kuumbwa kwao na Mungu; kwamba, ujinsia sio sifa ya bahati mbaya katika mwili wa mtu bali ni sehemu muhimu ya utu wake; na kwamba, wanadamu wote wanagawanyika kwenye kambi mbili pekee, yaani kambi ya wanamume na kambi ya wanawake, na kambi hizi zimeumbwa kwa madhumuni ya kufanikisha upendo na uzazi kati ya jinsia tofauti;

Matamko mengine ni kwamba, hali ya mgawanyiko wa wanadamu katika tabaka la kiume na tabaka la kike, inaonyesha mkamilishano wa kijinsia ambao unahusisha sifa tofauti za jinsia walizonazo wanaume na wanawake, mkamilishano unaorutubisha uhusiano wa ndoa kati ya wanaume na wanawake; kwamba, taasisi ya ndoa kati ya mwanamke na mwanamume inaakisi uhusiano uliopo kati ya Mungu na wanadamu.

Kadhalika, kuna matamko kwamba, Mungu ndiye mwanzilishi na mtekelezaji wa sheria ambayo huongoza mahusiano ya kimapenzi kati ya mwanamume na mwanamke; kwamba, mahusiano ya kimapenzi kati ya mwanamume na mwanamke yana kazi kuu mbili, yaani kazi ya kujenga umoja na kazi ya kufanikisha uzazi; na kwamba, uhalisi wa vitu vyote vilivyoumbwa, wakimwemo mwanamke na mwanamume, unaakisi wema wa Mungu, ambapo, mwanamume na mwanamke, wameumbwa kwa sura na sura ya Mungu.

Pia, kuna matamko kwamba, Mungu huwatakia usafi wa moyo na maisha marefu watu wa jinsia tofauti waliooana; na kwamba, utofauti wa kijinsia wa binadamu unafanikisha tendo la ngono lenye mkamilishano wa kijinsia unaozalisha “mwili mmoja”; na kwamba, “mwili mmoja” unaotokana na tendo la kujamiiana kati ya mwanamke na mwanamume ni "umoja wa kimwili" usioweza kupatikana kati ya wanawake wawili wanaosagana au kati ya wanaume wawili wanaolawitiana.

Hivyo, katika teolojia ya dhambi ya ulawiti ninayoijadili hapa, dhana ya “mwili mmoja” (Mwanzo 2:24) ndio kigezo cha kiteolojia kwa ajili ya kutofautisha kati ya tendo la ngono linalofanyika bila kutumia kingamimba na kwa kuunganisha jenitalia ya kiume na jenitalia ya kike (copulation), dhidi ya matendo baki ya ngono.

Matendo baki ni kama vile, tendo la ngono linalofanyika kwa kuunganisha jenitalia ya kiume na rekitamu (pedication), au jenitalia ya kiume na mdomo (felatio), au jenitalia ya kike na mdomo (cunnilingus), au jenitalia na vidole (masturbation), au jenitalia ya kiume na mapaja (intercrural sex), au au jenitalia ya kuume na kwapa (armpit sex), au au jenitalia ya kiume na matiti (inter-breast sex).

Kuhusu tofauti hii, Profesa Melissa Moschella (2019:254), wa Chuo Kikuu Katoliki huko Amerika, anasema kuwa, “only in coitus can two human organisms truly become one organism (in a certain respect), by jointly coordinating for the single biological end of procreation (whether or not procreation actually results).”

Anachosema Profesa Moschella ni kwamba, kwa sababu ya uwezekano wa kusababisha mimba, jozi ya mke na mume huuanzisha "umoja wa kimwili" wakati wa tendo la ngono ya kuunganisha jenitalia ya kiume na jenitalia ya kike. Kwa maneno mengine, hii ndio kusema kwamba, "a copulating pair is one biological organism."

Fundisho hili ni zao la mradi wa kifalsafa ulioanza mwaka 1968, kupitia waraka wa "Humanae Vitae". Siku hizi linaungwa mkono na wanasayansi kama vile Queller na Strassmann (2016).

Queller na Strassmann (2016) wanafafanua kwamba, neno "organism" linamaanisha vitu kama vile binadamu, kondoo, wanandoa, familia na timu ya mpira.

MIfano miwili ya kwanza ni "biological organisms" wakati mifani mitatu inayofuata ni "social organisms."

Ufanano wa mifano hii ni kwamba, mifano yote ni mifumo yenye sehemu nyingi zinazofanya kazi kwa kushirikiana, bila kupingana, kwa ajili ya kufanikisha lengo la pamoja.

Sifa hii inaitwa "organismality", yaani "uoganizimalia" kwa Kiswahili, kama tukitohoa neno la Kiingereza.

Tofauti moja kati ya "biological organism" na "social organism" ni kwamba, wakati "kanuni ya uratibu" iko ndani ya mfumo uitwao "biological organism," kanuni hiyo iko nje ya mfumo uitwao "social organism."

Tofauti nyingine kati ya "biological organism" na "social organism" ni kwamba, kiungo cha mwili wa "biological organism" kikikatwa kinakufa, lakini kiungo cha mwili wa "social organism" kikikatwa kinabaki hai, na kinaweza kuunganishwa tena na kuwa sehemu ya "social organism".

Mfano, mchezaji wa mpira wa miguu akipewa kadi nyekundi anaondoka uwanjani na anabaki hai. Akisamehewa anarejea kwenye timu.

Lakini, mkono wako ukikatawa kwa panga hadi kutenganishwa na mwili wako utaoza na baada ya hapo hauwezi kurejeshwa kuwa sehemu ya mwili wako.

Kwa upande mwingine uhai wa "social organism" unaanzia na kukomea kwenye mapatano ya wanajamii husika, kwa maana kwamba, sehemu za kitu kizima zinaanza kuwepo kabla ya kitu hicho kizima kuwepo.

Lakini uhai wa "biological organism" hautokani na mapatano ya viungo vya mwili, maana viungo hivyo huota baada ya kitu kizima kuwepo.

Kwa ujumla, wanachosema ni kwamba , kila mtianaji ni "biological organism," ambaye "uoganizimalia" wake unatokana na ushirikiano kati ya viungo vya mwili kwa ajili ya kulinda uhai wa mwili wa mhusika;

Kwamba, "jozi ya watianaji" inaunda "social organism," ambaye "uoganizimalia" wake unatokana na ushirikiano kati ya mtiaji na mtiwaji kwa ajili ya kurutubisha yai la kike kwa kutumia mbegu za kiume;

Na kwamba, hakuna "lengo la pamoja" linaloweza kutufanya tuseme kwamba, kuna "uoganizimalia" kama huu katika tendo la ngono linalofanyika kwa kuunganisha jenitalia ya kiume na rekitamu (pedication), au jenitalia ya kiume na mdomo (felatio), au jenitalia ya kike na mdomo (cunnilingus), au jenitalia na vidole (masturbation).

Ni maoni yangu kwamba, hoja hii iko sawa kimantiki, hata kama tutaendelea kubishana kuhusu madai kwamba "jozi ya watianaji" hugeuka "mwili mmoja" au hapana.

Ni kwa sababu hizi, Yates (1995) anasema kuwa, mwitikio mkubwa wa Kikristo kwa changamoto ya uwepo wa mashoga hapa duniani unahusisha misimamo ifuatayo: kwamba, tendo la ulawiti haliwezi kuzlisha "uoganizimalia" wa aina yoyote;

Kwamba, Mungu huwaacha wale wanavunja maadili ya kijinsia, ikiwa ni pamoja na vitendo vya ulawiti wa kishoga, kwa sababu ya tabia hizo hizo; kwamba, Mungu anawatakia usafi wa moyo wapenzi wote, wakiwemo wapenzi wa jinsia tofauti na wapenzi wa jinsia moja, ambao wanaweza kushinda vishawishi kwa kumfuata Kristo;

Na kwamba, Mungu huwaita watu wa jinsia tofauti na mashoga kuwa washiriki kamili katika jumuiya ya Kikristo.

Hata hivyo, Wakristo wachache hujibu kwa ukamilifu swali: ushoga ni nini na kina nani wanaohesabiwa kuwa ni mashoga?

Tangu miaka ya 1950 wametumia nguvu kubwa na muda mwingi kutafiti na kusanifu hoja inayohusu "uoganizimalia wa jozi ya watu wanaofanya tendo la kujamiiana" (the organismality of a copulating pair) wakasahau kudadisi swali la shoga ni nani na sio nani.

Kama wangewekeza muda kidogo katika eneo hili la pili, wangegundua kwamba, kuna "uoganizimalia wa jozi ya watu wanaofanya tendo la kulawitiana" (the organismality of a pedicating pair). Na ugunduzi huu ungewapunguzia kiwango cha uhomofilia unaowakabili.

Nadhani sababu ni kwamba, Biblia iliyo msingi wa udadavuzi wao wa kiteolojia, haina jawabu kwa swali hili la shoga ni nani na sio nani. Kwa sababu hii, hata wanapojaribu kujibu swali hili, hutoa jawabu lenye mkanganyiko.

Mfano mzuri wa mkanganyiko huu upo katika ibara za 2357 na 2358 katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki ya mwaka 1992. Ibara hizi zinatoa fasili ya ushoga (homosexuality) ifuatayo:

2357 Homosexuality refers to (sexual) relations between men or between women who experience an exclusive or predominant sexual attraction toward persons of the same sex...
…..Basing itself on Sacred Scripture, which presents homosexual acts (of pedication, felatio, irrumation, frottage and tribbing) as acts of grave depravity, tradition has always declared that "homosexual acts (of pedication, felatio, irrumation, frottage and tribbing) are intrinsically disordered"...
2358 The number of men and women who have deep-seated homosexual tendencies is not negligible. This (is an ) inclination....

Katika nukuu hii, kuna makundi manne ya maneno yafuatayo yenye kuzalisha utata wa kimantiki: "Homosexuality refers to (sexual) relations," "homosexual acts ," "homosexual tendencies," na "this (is an) inclination."

Katika vishazi hivi vinne, vishazi viwili vya mwisho vinazalisha hitimisho kwamba, "Homosexuality refers to ... an exclusive or predominant sexual attraction toward persons of the same sex." Maneno ya msingi hapa ni "sexual attraction."

Lakini, Katekisimu hiyo hiyo inasema kuwa "homosexuality refers to (sexual) relations between men or between women." Maneno ya msingi hapa sasa ni "sexual relations."

Maana hizi mbili za neno "homosexuality" kama "sexual attraction" na "homosexuality" kama "sexual relations" zinaashiria mkanganyiko wa kimantiki ndani ya Katekisimu ile ile moja.

Hapa kuna matumizi ya neno moja lenye maana mbili, bila kuweka bayana maana gani inatumika lini (equivocation). Hatuwezi kutakatifuza ulimwengu wa ujinsia wa binadamu kwa njia ya utata huu.

Lakini pia, Katekisimu inasema uwongo kwamba: "Sacred Scripture ... presents homosexual acts (of pedication) as acts of grave depravity."

Hakuna mahali Biblia inaongelea "homosexual acts of pedication." Kinachoongelewa katika Biblia ni "acts of pedication," yaani ulawiti, na sio kila ulawiti hufanywa na mashoga. Yaani, Biblia haisemu kama kinachojadiliwa ni ulawiti wa kihomofilia au ulawiti wa kiheterofilia.

Kwa sababu hizi, napendekeza kwamba Kamati ya Kipapa iliyoandika Katekisimu hii, chini ya Kiranja Mkuu wa Imani wa wakati huo, Kardinali Joseph Ratzinger, hawakuwa na weledi kamilifu juu ya mada ya uhomofilia, uheterofilia, ulawiti na usagaji.

Ni kama hawakujua tofauti kati ya "hali ya ushoga" yaani "homosexual condition," "tabia ya ulawiti wa kishoga" yaani "homosexual pedication," na "tabia ya ulawiti usio wa kishoga" yaani "non-homosexual pedication."

Nimejaribu kupitia Biblia na nimebaini kwamba kuna makatazo dhidi ya “ulawiti” katika kitabu cha Mwanzo 2:24, 2:28; na 19:1-11; Waalawi 18:22 na Walawi 20:13; na Warumi 1:26-27.

Walawi 18:22 inasema kuwa, “Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke, ni machukizo.”

Na Walawi 20:13, inasema kwamba, “Mtu mume akilala pamoja na mtu mume kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauwawa; damu yao itakuwa juu yao.”

Kuhusu aya hizi, Helminiak (1994:33) anapendekeza kwamba, katika Agano la Kale, walichokuwa wanaongelea Walawi ni homogenitality (uhomojenitalia)” na sio homosexuality (ushoga).”

Kisha, anahitimisha kuwa, kwa sababu hizi, Biblia haina majibu kwa maswali yanayohusiana na “dira ya ashiki ya kishoga (homosexual orientation)” kama tatizo la maumbile.

Na Rogers (2006:65) anakubaliana naye. Katika muktadha wa historia ya neno "ushoga" yaani "homosexuality." Nami naona kuwa mawazo yao ni sahihi.

Hivyo, ni sahihi kuhitimisha kuwa, kuna wanateolojia walikaa mahali na kukubaliana kwamba, "tuseme kuwa Biblia inaongelea ushoga," na wakasonga mbele bila kukumbuka kuwa, Biblia wanayoiongelea iko mitaani kwetu, nasi tumesomea mbinu za kutafsiri fasihi andishi kama wao. Huu ni uhandisi wa maarifa ya kijamii kwa njia ya kura (social construction of knowledge).

na kwa kweli, suala la uhandisi wa maarifa ya kijamii kwa njia ya kura halijaishia kwenye teolojia. Hata kwenye siasa limo. Yaani, suala la “ushoga” limekuwa likichukuliwa kisiasa zaidi, hata pale ambapo wanasiasa hawana mamlaka ya kiweledi kulijadili.

Taarifa ya September 2016 kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya wa wakati huo, Dk. Hamisi Kigwangala, akiandika kwenda kwa Dk. Pierre Somse, Mkurugenzi Msaidizi wa UNAIDS katika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Dk. Kigwangala ilisema haya:

“Pamoja na kwamba watu walio katika kundi la LGBTI wapo nchini mwetu, [sisi kama serikali] hatuungi mkono kauli kwamba ‘kuna jinsia zaidi ya mbili.’ Bado tunatambua jinsia mbili kwa mujibu wa mapokeo [na sheria], yaani mwanaume na mwanamke. Na hakuna kitu chochote katikati au nje ya jinsi hizi mbili! Hivyo, jitihada zozote za kudai vinginevyo ni jambo lisiloruhusiwa [kisheria na kimapokeo] nchini Tanzania (facebook).”

Kwa kauli hii, alichokifanya Dk. Kigwangala ni kuitangazia dunia kwamba, ukweli kuhusu “hali ya ushoga” unapaswa kuamuliwa kwa kutumia kura za kisiasa na sio vinginevyo, pamoja na kwamba yeye ni mwanasayansi kitaaluma.

Nadhani kilichomchanganya ni kifupi cha meneno "LGBTI" kinachobeba maembe na machungwa kimakosa.

Sheria yetu ya vizazi na vifo, inawatambua "Lesbians," "Gays," "Bisexuals," na "Trangenders," ama kama wanaume au kama wanawake, kila mmoja kulingana na jenitalia yake aliyozaliwa nayo.

Na hakuna mtu anayedai watambuliwe kama kada mpya ya kijinsi. Makundi haya manne yana tatizo la utata katika "dira ya ashiki" aliyo nayo kila mmoja wao.

Wana dira ambayo inapindua kichwa chini miguu juu kanuni za mahusiano ya kila siku yanayofahamika kwa watu wengi. Ni tatizo linalohitaji majibu ya kisayansi.

Sala na maombezi haviwezi kuleta mabadiliko. Na haiwezekani kulifumbia macho tatizo hili milele, kwa kujidanganya kwamba watu hawa hawapo. Vinginevyo, tutakuwa tunasaliti taaluma zetu za kisayansi na kifalsafa tulizo nazo.

Lakini, kuhusu herufi ya "I" katika kifupi cha meneno "LGBTI," hoja sio utata katika "dira ya ashiki." Tatizo ni utata wa jenitalia za nje na ndano ya mwili wa mhusika.

Hawa ni mahunta (hermaphrodites), wapo na wanaendelea kuzaliwa. Manesi, wasajili wa vizazi na vifo na wazazi hawana elimu juu ya kuwahudumia watoto wa aina hii.

Naona kuwa ni wajibu wa serikali kubeba jukumu la kutoa elimu hii. Ni kazi ya maafisa wa ustawi wa jamii. Haiwezekani kulikwepa milele, eti kwa sababu tu kwaba Misahafu inasema kuwa kuna jinsi mbili pekee. Katika jambo hili misahafu imepitwa na wakati.

VI. Mbinu za uchunguzi wa kuwatambua mashoga

Je, tunaweza kufanya uchunguzi wa namna gani ili kuwatofautisha watu ambao ni mashoga na watu wasio mashiga?

Kisayansi, tuhuma za ushoga huanzia kwenye maumbile ya “vidole vya kishoga.” Jambo hili linaungwa mkono na tafiti mbalimbali za kisayansi.

Mfano, utafiti uliofanywa mwaka 2016 na Caixia Li akishirikiana na wenzake kadhaa, ulikusanya uwiano wa urefu wa vidole vya makundi ya matatu: “mahomofilia, maambifilia na maheterofilia,” yaani "homosexuals, bisexuals and heterosexuals," na kurekodi taarifa zifuatazo :

Table. 01: The mean digit ratio values amongst the homosexual, bisexual and heterosexual groups
1676460749550.png

Source: Caixia Li et al, "The relationship between digit ratio and sexual orientation in a Chinese Yunnan Han population," Personality and Individual Differences, 101 (2016):26-29, at p.27

Katika safu wima yenye jina "2D:4D," yaani uwiano wa urefu wa kidole cha pili na urefu wa kidole cha nne, jedwali hili linaonyesha kwamba mahomofilia (mashoga) wana uwiano mkubwa kuliko uwiano wa mahaterofilia (wasio mashoga).

Kwa ujumla, tafiti zote za kisayansi zinaonyesha kwamba, miongoni mwa wanaume, “hisa ya urefu wa kidole cha pili dhidi ya urefu wa kidole cha nne” inaanzia 0.918 hadi 0.976, yaani wastani wa 0.947. Watu wenye uwiano wa urefu wa vidole vilivyo nje ya mipaka hii, hutuhumiwa kwa ushoga.

Ni kwa sababu hii, hapa Tanzania, vijana wenye vidole kama vya Lissu hufukuzwa jeshi la polisi kwa tuhuma kwamba ni mashoga.

Na miongoni mwa wanawake, tafiti hizo zinaonyesha kwamba, “hisa ya urefu wa kidole cha pili dhidi ya urefu wa kidole cha nne” inaanzia 0.939 hadi 0.991, yaani wastani wa 0.965. Watu wenye uwiano wa urefu wa vidole vilivyo nje ya mipaka hii, hutuhumiwa kwa usagaji.

Hata hivyo, takwimu za uwiano wa urefu wa vidole ni ushahidi wa awali katika mchakato wa kuthibitisha tuhuma za ushoga. Kuna ushahidi mwingie wa kisayansi unahitajika ili kukamilisha uthibitisho au kukanusha tuhuma.

Kuna njia kadhaa za kuthibitisha ushoga wa mtu. Njia ya kwanza ni yeye kutamka kwamba anapata sumaku ya kimapenzi kwa sababu ya kuwaona wanaume wenzake. Yaani ushuhuda wake.

Njia ya pili ni kutumia kanuni kwamba, tunautambua mti kwa kuangalia matunda yake. Yaani, tabia za mtu ndizo zinatwambia anao mwelekeo gani wa kimapenzi. Kama mtu anapenda kuwalawiti wanaume wenzake, basi hiyo ni dalili kwamba ni shoga.

Na njia ya tatu ni kupima kiwango cha homoni alicho nacho mtu mwilini mwake. Kwa kawaida, kila mtu anazo homoni za kiume na kike mwilini mwake.

Wanawake wanazo homoni nyingi za kike kuliko homoni za kiume. Lakini, kama vipimo vikionyesha homoni nyingi za kiume wakati mtu anaonekana mwanamke hiyo ni dalili ya usagaji.

Na Wanaume wanazo homoni nyingi za kiume kuliko homoni za kike. Lakini, kama vipimo vikionyesha homoni nyingi za kike wakati mtu anaonekana mwanamume hiyo ni dalili ya shoga msagwaji.

VII. Takwimu zinasemaje kuhusu ukubwa wa tatizo la ushoga hapa nchini Tanzania?

Kina Bagonza wanasema kuwa "imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi..."

Kwa maoni haya, kina Bagonza, wanajaribu kutuaminisha kwamba, sasa mashoga ni kundi kubwa linaloweza kuanzisha chama cha siasa. Lakini, hakuna takwimu wanazozitaja kuthibitisha taharuki wanayoichochea.

Bila kujali kama kina Bagonza wanatumia neno "ushoga" kumaanisha mashoga walawiti, mashoga walawitiwa, au mashoga wasio walawiti wala walawitiwa, kuna maswali ya kitafiti wanapaswa kutusaidia kuyajibu.

Tangu tupate uhuru tumefanya sensa mara tano. Hakuna takwimu za serikali zinaonyesha idadi ya mashoga nchini.

Kila mwaka serikali kupitia jeshi la Polisi na Idara ya takwimu (NBS) wanatoa takwimu za uhalifu kupitia kitabu kiitwacho “Tanzania in Figures.”

Idadi ya “mashoga” haitajwi katika ripoti hii pia. Badala yake, ripoti hii hutaja takwimu za matukio ya ulawiti.

Mfano, takwimu za mwaka 2021 zinaonyesha kuwa yalikuwepo matukio ya ulawiti 1,296.

Taarifa hiyo haisemi kama ulawiti huu ulifanywa dhidi ya wanaume au dhidi ya wanawake au kama ulifanywa na mabasha au kama ulifanywa na walawiti wasio mahomofilia.

Lakini bado kina Bagonza wanasema hawakubaliani na “wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya" kwa sababu tayari "hapa kwetu ... hali inatisha."

Kina Bagonza wanasema kuwa "imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi...."

Wanasema “tuamke” na kuwashughulikia mashoga wote, kama alivyokuwa anafanya Paul Makonda na kikosi kazi chake.

Kwa maoni ya kina Bagonza, mashoga hawana haki za msingi za kibinasamu zilizotajwa kwenye kayiba ya nchi kwa sababu tu wao wanafanya jinai zinazoitwa “ulawiti” na “usagaji.”

Lakini, swali linaloshangaza ni hili: Sheria yetu ya kuzuia makosa ya jinai imetamka bayana makosa haya na adhabu yake. Polisi wapo, na wanapokea taarifa zote zinazopelekwa pale na raia wema, wakiwemo kina Bagonza.

Naongelea, Sheria ya Makosa ya Jinai, Sura ya 16, Toleo la 2002, (Tanzania Penal Code—TPC). Ibara za 154 (1)(a) na 155 katika TPC zinasema kwamba:

“Any person who has carnal knowledge of any person against the order of nature, commits an offence.”

Ndio kusema kwamba, “mtu yeyote atakayefanya ngono iliyo kinyume cha maumbile na mtu mwingine yeyote atakuwa ametenda kosa la jinai.” Kifungu hiki kinawahusu wanaume wanaolawitiana na wanawake wanaosagana pia.

Lakini, kina Bagonza wanalifanyia “propaganda” kubwa suala la ushoga, kana kwamba nchi haina sheria zinazoweza kutumika kulimaliza. Kwa nini wanaenenda hivi?

Nadhani kuna tatizo mahali. Litafutwe. Sioni mantiki ya kushikia bango “maadili ya chupi” na kusahau maadili ya uchumi, maadili ya elimu, na maadili mengine yaliyo na nafasi kubwa zaidi katika maisha ya watu.

Lakini pia, kwa nini msimamo wa kina Bagonza dhidi ya tuhuma za “uhalifu” unaishia kwa watuhumiwa wa “ulawiti” pekee?

Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya kila mwaka, iitwayo “Tanzania in Figures,” kuna makundi mengi ya uhalifu na yote yanapaswa kumulikwa kisheria (tazama picha).

1670523888039.png


Kwa maoni yangu, kauli za kina Bagonza zingeeleweka sana kama wangesema hivi: "imebaki kidogo [wahalifu] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi... Tuamke."

Wahalifu ni pamoja na wezi, wala rushwa, watu wanaotelekeza watoto mitaani, wafanya biashara ya binadamu, wateka watu, na orodha inaendelea.

Na takwimu halisi za kiserikali kupitia taarifa ya “Tanzania in Figures” ya kila mwaka, zinaonyesha kuwa baadhi ya watu hawa tayari wana makanisa, wengine ni wamiliki wa vyombo vya habari, wengine ni maaskofu, wengine ni wachungaji.

Kwa upande wa Kanisa Katoliki, sijawahi kuona "Askofu jambazi" kama alivyokuwa hayati Askofu Balina. Huyu ndiye aliyemfanya Dakta Slaa kuacha upadre!

Kina Bagonza wanaujua ukweli huu fika. Lakini bado wanaamua kuibuka na habari ya "ushoga" isiyo na takwimu za kitafiti. Hapana.

Kuna tatizo mahali katika mtazamo wao wa kifikra. Nadhani "teolojia ya dhambi ya ulawiti" wanayoisoma wakiwa huko seminari kuu ni chimbuko la uhomofobia huu uliopitiliza.

Mawazo yao yangeleweka na kukubalika zaidi kama wangesema kuna "mashoga" wangapi kwenye kaya zao, koo zao, vijiji/mitaa yao, kata zao, wilaya zao, mikoa yao, na Tanzania kwa ujumla. Hawatoi takwimu zozote katika ngazi yoyote.

Hivyo, napenda kuwakumbusha mawili. Kwanza, kauli bila takwimu ni sawa na kelele. Na pili, wakumbuke kuwa, sifa tata za kimaumbile hazifuti haki za msingi za mahomofilia waadilifu, maalibino waadilifu, mashoto waadilifu, watu wenye makengeza waadilifu, nk.

Sifa hizo ni kama vile haki ya kuishi, kujumuika, kugombea nafasi za kisiasa, kupiga kura, kuabudu, kulindwa na serikali, na haki baki za kibinadamu.

VIII. Chanzo cha dira ya ashiki kama vile uheterofilia na uhomofilia ni nini hasa?

Swali hili linaweza kusomeka hivi: Katika hali ya kawaida, kwa nini mwanamume avutiwe kimapenzi na mwanamke na sio mwanamume mwenzake?

Au, katika hali ya kawaida, kwa nini mwanamke avutiwe kimapenzi na mwanamume na sio mwanamke mwenzake?

Vivyo hivyo, tunaweza kuuliza: Katika hali isiyokuwa ya kawaida, kwa nini mwanamume avutiwe kimapenzi na mwanamume mwenzake na sio kuvutiwa na mwanamke?

Na Katika hali isiyokuwa ya kawaida, kwa nini mwanamke avutiwe kimapenzi na mwanamke mwenzake na sio kuvutiwa na mwanamume?

Sayansi inayoeleza namna ambavyo jinsi ya mtoto wa kawaida hupatikana, kama ikichunguzwa pamoja na sayansi inayoeleza jinsi mahunta wanavyopatikana inapaswa kutupa majawabu ya maswali haya.

Kuhusu, kupatikana kwa jinsi ya kawaida ya mtoto, kulingana na Leon Speroff pamoja na Marc A. Fritz (2005), mchakato wa kusimikwa kwa jinsi ya mtoto aliye tumboni hufanywa na vinasaba kadhaa ndani ya wiki saba za kwanza za mimba. Kwa mujibu wa utafiti wao, mchakato huu unapitia katika hatua kuu tano.

Hatua ya kwanza ni kusimika jinsi ya mtoto katika ngazi ya seli (chromosome sex) wakati wa urutubisho.

Kupitia tendo la ngono, mbegu ya kiume yenye kromozomu 23, zikiwemo kromozomu 22 ziitwazo “X” na moja iitwayo “Y,” huungana na yai la kike lenye kromozomu 23 ziitwazo “X”, na kuunda mimba yenye kromozomu 46.

Hivyo, mimba hii huweza kuwa na ama kromozomu 46 zenye fomati ya kike, yaani ‘XX’ (46XX KE), au kromozomu 46 zenye fomati ya kiume, yaani XY (46XY ME).

Katika hatua hii ya kwanza, mimba inakuwa na mfumo wa uzazi usiofungamana na upande wowote. Badala yake kunakuwa na “kinyama” chenye sehemu tatu: gonadi huria, yaani mbili zisiofungamana na jinsi yoyote (bipotential ginads); mifereji miwili ya muleria (Mellerian ducts) na mifereji miwili ya wolfi (Wolfian ducts).

Kulingana na mazingira ya wakati husika, gonadi huria na mifereji yake huweza kugeuka jenitalia za kiume au jenitalia za kike, kama tutakavyoona punde.

Hatua ya pili, hujitokeza katika wiki ya saba ya mimba, na inahusu kusimikwa kwa jinsi ya mtoto katika ngazi ya gonadi (gonadal sex).

Katika hatua hii, gonadi huria mbili (bipotential gonads), ama hugeuka ovari au hugeuka korodani .

Gonadi huria zikigeuka ovari, inapatikana mimba ya mtoto mwanamke. Na zikigeuka korodani, inapatikana mimba ya mtoto mwanamume. Mabadiliko haya hutokea katika mimba yenye umri wa siku hamsini.

Hatua hii husimamiwa na vinasaba kadhaa, lakini, kinasaba muhimu ni “kinasaba kinachotengeneza jinsia ya mtoto,” yaani “sex determining region Y gene—SRY gene.”

Kwa ufupi, “kinasaba kinachotengeneza jinsia ya mtoto” ni pingili inayopatikana katika ncha mojawapo ya kromozomu ya “Y,” ambayo ni kromozomu ya kiume.

Kazi ya “kinasaba kinachotengeneza jinsia ya mtoto” ni kuzalisha kemikali inayobadilisha gonadi huria kuwa korodani. Kemikali hiyo, ni “protini inayootesha korodani,” yaani “testicle determining factor—TDF.”

Kupatikana kwa SRY na TDF huzilazimisha gonadi huria mbili kugeuka korodani, na hivyo, kupatikana kwa mimba ya kiume. Hili ni tukio katika wiki ya saba ya uhai wa mimba.

Kwa upande mwingine, kukosekana kwa kwa SRY na TDF huziruhusu gonadi huria zilizo katika mimba iliyo na mfumo wa jenetiki wenye fomati ya ‘XX’ kugeuka ovari, na hivyo, kupatikana kwa mimba ya kike. Hili ni tukio katika wiki ya saba ya uhai wa mimba.

Hivyo, mtoto akizaliwa ni mwanaume kamili anakuwa na mfumo wa jenetiki wenye fomati ya “XY” ulioambatana na “uwepo” wa “kinasaba kinachotofautisha jinsia ya mtoto.” Yaani, anakuwa na jinsi ya kijenetiki yenye fomati ya “46XY ME, SRY+.

Kwa upande mwingine, mtoto akizaliwa ni mwanamke kamili anakuwa na mfumo wa jenetiki wenye fomati ya “XX” ulioambatana na “ukosefu” wa “kinasaba kinachotofautisha jinsi ya mtoto.” Yaani, anakuwa na jinsi ya kijenetiki yenye fomati ya “46XX KE, SRY-.

Hatua ya tatu ni kudhihirisha jinsi ya mimba katika ngazi ya jenitalia na viungo kadhaa vya mwili, na hivyo kumpa mofolojia/mwonekano maalum (genital sex).

Hatua hii husimamiwa na homoni za kiume, kama vile testosterone, zinazozalishwa kwenye korodani ya mimba, na homoni za kike, kama vile estrojeni, zinazozalishwa kwenye ovari ya mimba.

Katika hatua hii, mimba ya kike hupata jenitalia za nje zifuatazo: uke wa nje (vulva), kisimi, mlango wa uzazi na mlango wa mkojo. Aidha, mwanamke hupata jenitalia za ndani zifuatazo: njia ya uzazi, yuterasi, mifereji miwili ya falopia na ovari.

Na mimba ya kiume, hupata jenitalia za nje zifuatazo: uume na korodani mbili zilizoshuka kwenye mifuko yake. Aidha, mwanaume hupata jenitalia za ndani zifuatazo: tezi dume, epididimisi, seminovesko, na vasidiferensi.

Na kuhusu chimbuko la mahunta, kama ambavyo kuna walemavu wa viungo mbalimbali mwilini, pia kuna walemavu wa viungoi vya mwili vinavyoitwa “jenitali” yaa “uume” na “uke,” mfano ukiwa ni mtu mwenye jemitalia mbili, yaani “uume” na “uke.”

Friedrich Vogel na Arno G. Motulsky (1996) wameeleza jinsi ulemavu huu unavyotikea. Wanaongelea ulemavu wa jinsi tata, yaani “Disorders of Sexual Development (DSD).”

Hapo awali tuliona kwamba, mtoto akizaliwa ni mwanaume kamili anakuwa na jinsi ya kijenetiki yenye fomati ya “46XY ME, SRY+.” Kwa upande mwingine, tulisema kuwa, kama mtoto akizaliwa ni mwanamke kamili anakuwa na na jinsi ya kijenetiki yenye fomati ya “46XX KE, SRY-.

Lakini kwa bahati mbaya, ikitokea kwamba, mimba yenye mfumo wa jenetiki wenye fomati ya “XY” ikaambatana na kromozomu ya “Y” iliyomeguka na kupoteza kipande cha “kinasaba kinachotofautisha jinsi ya mtoto,” madhara makubwa ya kijenetiki hutokea kwa mimba.

Kwanza, mimba hii haitapata “protini inayootesha korodani,” yaani TDF, ili mtoto aweze kuzaliwa wa kiume. Badala yake, pamoja na kwamba mimba inao mfumo wa jenetiki wenye fomati ya ‘XY,’ ambayo ni fomati ya kiume katika ngazi ya kromozomu, mimba hii itaotesha ovari kana kwamba mimba hiyo inao mfumo wa jenetiki wenye fomati ya ‘XX,’ ambayo ni fomati ya kike.

Hatimaye, atazaliwa mtoto mwenye jinsi ya kiume katika ngazi ya seli, wakati anayo jinsi ya kike katika ngazi ya gonadi. Atakuwa ni mlemavu wa kijinsia mwenye mfumo wa jenetiki ulio na fomati ya “46XY KE, SRY-.

Ovari zake zitazalisha homoni za kike, na atakuwa na mofolojia ya kike, wakati ndani anazo seli zenye fomati ya kiume (genotypitical male, phenotypical female).

Mabadiliko haya yanaitwa mapinduzi ya kijinsi kutoka uanaume kwenda uanauke (male-to-female sex reversal).

Hivi ndivyo, mwanamume mwenye sura ya kike, kama vile Caster Semenya, mwanariadha wa Afrika Kusini, anavyokuja duniani. Huyu ni binadamu kamili kwa kuwa anazo kromozomu 46 za viumbe walio katika ukoo wa “homo sapiens,” anayo akili na utashi pia.

Kwa bahati mbaya tena, ikitokea kwamba, mimba yenye mfumo wa jenetiki wenye fomati ya ‘XX’ ikaambatana na kromozomu ya X iliyookota kipande cha “kinasaba kinachotofautisha jinsia ya mtoto,” baada ya kuwa kimemeguka na kudondoka kutoka katika kromozomu ya Y, madhara makubwa ya kijenetiki hutokea kwa mimba pia.

Kwanza, mimba hii hupata “protini inayootesha korodani,” yaani TDF, na kusababisha mtoto kuzaliwa na jenitalia za kiume.

Kwa sababu hii, pamoja na kwamba mimba inao mfumo wa jenetiki wenye fomati ya ‘XX,’ ambayo ni fomati ya kike, bado mimba hii itaotesha korodani kana kwamba mimba hiyo inao mfumo wa jenetiki wenye fomati ya ‘XY,’ ambayo ni fomati ya kiume.

Hatimaye, atazaliwa mtoto mwenye jinsi ya kike katika ngazi ya seli, wakati anayo jinsi ya kiume katika ngazi ya gonadi (genotypitical female, phenotypical male). Atakuwa ni mlemavu wa kijinsia mwenye mfumo wa jenetiki ulio na fomati ya “46XX ME, SRY+.

Korodani zake zitazalisha homoni za kiume, na atakuwa na mofolojia ya kiume, wakati ndani anazo seli zenye fomati ya kike.

Mabadiliko haya yanaitwa mapinduzi ya kijinsi kutoka uanauke kwenda uanaume (female-to-male sex reversal). Hivi ndivyo mwanamke mwenye sura ya kiume, anavyoweza kuja duniani.

Endapo kipande cha “kinasaba kinachotofautisha jinsia ya mtoto,” yaani SRY, hakitameguka chote kutoka kwenye kromozomu ya “Y,” basi, mapinduzi ya kijinsi kutoka uanauke kwenda uanaume au mapinduzi ya kijinsi kutoka uanaume kwenda uanauke, yatafanyika nusu-nusu kiasi kwamba, mimba inapata jenitalia ya kiume na jenitalia ya kike.

Uchambuzi huu unaweza kuhitimishwa kirahisi kwa kutumia maarifa ya misukumano iliyopo kati ya sababu na matokeo, yaani "causality."

Kietiolojia tunasema kuwa, kama tukio X ni sababu ya tukio Y, basi tukio X likitokea na tukio Y litafuata. Vivyo hivyo, tukio X lisipotokea na tukio Y halitafuata.

Katika mjadala wetu hapo juu, kwa sehemu kubwa, mtoto mwenye jinsi ya kiume hupata dira ya ashiki ya kigaonofilia.

Na mtoto mwenye jinsi ya kike hupata dira ya ashiki za kiandrofilia. Kwa hiyo, jinsi ya mtoto wa kawaida ni sababu ya mwelekeo wa ashiki yake. Na kwa kuwa homoni na vinasaba ni sababu ya jinsi ya mtoto, basi, inafuata kimantiki kwamba, homoni na vinasaba ni sababu ya dira ya shiki aliyo nayo mtu.

Vivyo hivyo, inafuata kimantiki kwamba, jinsi tata ya mtoto aliyekumbwa na mapinduzi ya kijenetiki ni sababu ya utata katika dira ya ashiki yake. Yaani, mahomofilia ni walemavu kama ambavyo mahunta ni walemavu.

Mazingira ya malezi yanaweza kuchangia kukuza tatizo, lakini nadharia iliyojadiliwa hapa inaaminika zaidi kuliko "nadharia ya upiga ramli" inayoazia kwenye dhana ya "dhambi ya asili," ambayo huwa tunaambiwa inafutwa kwa njia ya ubatizo, lakini bado mtu aliyebatizwa anazaa mtoto mwenye dhambi hiyo.

IX. Tuwafuate wanateolojia, wanasiasa, wanasayansi au wanafalsafa?

Kutokana na yaliyojadiliwa hapo juu, tumeona yafuatayo: Mosi, sayansi na falsafa za ushoga zinasema kwamba "ushoga wa kiume" (male homophilia) ni hali ya mwanamume kuwa na "dira ya shiki" (sexual orientation) inayomsukuma kufanya ngono na mwanamume mwenzake.

Shoga wa kiume anakuwa na tatizo la uhomofilia wa kiume . Ngono inayihusika zaidi ni ulawiti, ufelasio, na punyeto (pedication, fellatio, and manual masturbation).

Na "ushoga wa kike" (female homophilia) ni hali ya mwanamke kuwa na "dira ya shiki" (sexual orientation) inayomsukuma kufanya usagaji dhidi ya mwanamke mwenzake.

Shoga wa kike anakuwa na tatizo la uhomofilia wa kike. Ngono inayohusika zaidi ni kusagana, ukanilingusi, na punyeto ya vidole (tribbing, cunnilingus, and manual masturbation).

Miongoni mwa mahomofilia, "dira ya shiki" ambayo ingemsukuma mhusika kufanya ngono na mtu wa jinsia tofauti, ama imedumaa kwa asilimia mia moja (deprivation), au umepotea baada ya kuwa imeibuka (privation). Chimbuko la udumavu au upotevu huu ni homoni na vinasaba vya kijinsia.

Na pili, tumeona kuwa "teolojia ya dhambi ya ulawiti" kwa mujibu wa Biblia, shoga ni mtu yeyote anayefanya ulawiti. Kwa hiyo, masimulizi yote yanayohusu "ulawiti" katika Biblia yanatafsiriwa kwamba ni matukio ya "ulawiti wa kishoga". Tafsiri hii inapingana na mtazamo wa kisayansi na kifalsafa uliojadiliwa hapo awali. Kuna mashoga wasio walawiti, na kuna walawiti wasio mashoga.

Hivyo, naweza kusema kwa uhakika kwamba, wakati kauli za wanasayansi zinaanzia kwenye imani kwamba, ukweli upo nje ya akili za mtu na unagunduliwa (realism), kauli za wanateolojia na wanasiasa wanaojadili ushiga zinaanzia kwenye nadharia ya uhandisi wa maarifa ya kijamii kwa njia ya kura za wengi, yaani “social constructionism.”

Lakini, wanazuoni tunasema kuwa, "plausibility does not necessarily imply validity." Yaani, "mawazo ya wengi sio kigezo turufu cha ukweli unaopatikana nje ya akili ya wahusika."

Hii ndiyo dosari kubwa ya nadharia za uhandisi wa maarifa ya kijamii (social constructionism), hutengeneza maarifa kutokana na mapatano ya kibinadamu. Profesa John Rogers Searle (1969) wa Amerika ni bingwa wa uhandisi wa kijamii.

Katika maandiko yake Searle, kuhusu maarifa yanayotengenezwa kutokana na uhandisi wa kijamii, anataja kanuni kadhaa.

Kanuni moja inahusu "collective intentionality," nyingine inahusu "the assignment of status functions," na kanuni ya tatu inahusu "constitutive rules." Ninataka kuongelea hii kanuni ya tatu, ambayo ni kanuni ya kubuni na kutumia alama.

Kwa mujibu wa Searle(1969:34) kanuni hii inasema hivi: watu wanaweza kukaa wakakubaliana kwamba katika mazingira haya (X), kitu hiki (Y) kitakuwa alama inayowakilisha kitu kile (Z), na mapatano haya yatakoma pale watakapokaa tena na kukubaliana kuyabadilisha.

Mfano wake muhimu ni jumuiya ya wanampira waliokubaliana kuwa, katika mazigira ya uwanja wa mpira wa miguu (X), mchezaji akipokea mpira wakati anaelekea kufunga kwenye goli la mpizani wake wakati mbele yake hakuna mchezaji wa timu pinzani (Y), basi hilo ni kosa linaitwa offside (Z).

Kanuni hii inafaa kwenye mpira wa miguu pekee, na sio kwenye mpira wa mikono wala kwenye mpira wa kikapu.

Kwa hiyo, ikitokea siku wachezaji wa michezo yote hii wakajikuta wako pamoja kwa ajili ya mchezo mmoja, itabidi waunde kanuni mpya zinazokubalika kwa wote na kuwafaa wote. Ni vivyo hivyo kwenye maisha ya jamii mseto.

Yaani, kanuni zenye kutokana na mchakato wa mapatano ya kijamii (social constructionism) zinaweza kutumika kwenye jamii ya watu wenye imani moja, lakini sio kwenye jamii za leo ambako kuna utitiri wa kifikra (plural society).

Kwa mfano, wakati wa Papa Yohanne Paulo II, baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki waliweka msimamo kwamba mahunta sio binadamu.

Mfano wa mwathirika ni Padre Selwyn Gross (jina la zamani la kiume) na baadaye Padre Sally Gross (jina jipya la kike), baada ya kubadilisha jinsia yake.

Hivyo, "Padre Sally Gross" aliyekuwa hunta (intersexual), alivuliwa upadre, kwa kuwa wanawake hawana haki ya kuwa mapadre.

Pia alifutiwa ubatizo kwa hoja kwamba mahunta sio binadamu, na hivyo hawana haki ya kubatizwa.

Mawazo kwamba "mahunta sio binadamu" ni zao la nadharia ya uhandisi wa kijamii (social constructionism) ndani ya Kanisa Katoliki kwa wakati ule wa Papa Yohanne Paul II.

Lakini, leo hii sayansi mamboleo inathibitisha kwamba mahunta wana kromozomu 46 kama watu baki walioko kwenye ukoo wa homosapiensia.

Yaani kumwondoa Padre Sally kwenye tabaka la binadamu ulikuwa ni uamuzi wenye sura ya "category mistake," na ulitokana na matumizi mabaya ya kanuni za uhandisi wa maarifa ya kijamii ndani ya Kanisa Katoliki.

Nionavyo mimi, basi, kwa sasa, tunakabiliana na changamoto ya sekta chache za wanazuoni kufikiri kwamba wanayo hatimiliki juu ya ukweli ambao uko nje ya wigo wao wa kimaarifa.

Wanasiasa na wataalam wa teolojia ya Kibiblia hawana weledi stahiki wa kuongelea mada ya “ushoga” na chimbuko la “vidole vya kishoga.”

Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii inayokubalika kwa watu wote katika jamii yenye mapokeo mseto sio kutumia kanuni za uhandisi wa maarifa ya kijamii kwa njia ya kura (social constructionism) zilizopigwa na sekta moja ya kijamii.

Badala yake, tunapaswa kuanzia kwenye kanuni za sheria asilia zinazoweza, na zinazopaswa, kuthibitika kwa njia ya urazini huru mbele ya kadamnasi mseto (public reason).

Bila kukubaliana na ukweli huu, kazi ya ujenzi wa imani ya jamii yenye imani mseto itakwama, maana mwafaka wa kijamii ni ajenda ya mpito tu.

Hapa, niseme tu kuwa, katika mradi huu wa kujenga imani ya jamii, wadau wote, yaani wanateolojia, wanasayansi asilia, wanasayansi ya jamii, wanafalsafa, wanasasiolojia, wanahistoria, wanasheria, walei, makasisi, na wanazuoni baki wanayo nafasi.

Lakini, mchango wa kila mmoja una mipaka inayokamilishwa na michango ya wenzake.

Mfano, kwenye Safina ya Nuhu tunaambiwa kuwa Nuhu aliagizwa kuweka kila kiumbe kwa kuzingatia kanuni ya ME na KE.

Lakini, leo hii sayansi inatwambia kuwa kuna viumbe havina mgawanyo huo wa ME na KE. Mfano ni minyoo. Kwa hiyo, mwandishi wa Agano la Kale hakuwa na habari ya ukweli huu wa viumbe wasio na mgawanyo wa jinsia ya ME na KE.

Na hii maana yeke ni kwamba, wanateolojia wanaofanya udadavuzi kwa kuanzia kwenye Biblia wanahitaji kuelimishwa na wanabayolojia katika suala ya asexual reporoduction. Biblia haina mamlaka katika jambo hili.

Vivyo hivyo, Biblia haina mamlaka juu ya fenomena ya "ushoga" katika ujumla wake. Biblia inaongelea "ulawiti," yaani "pedication," basi.

Kwa mfano, haitwambii kama umati wa watu wote wa Sodoma waliotaka kufanya kitendo cha ulawiti walikuwa ni mashoga au hapana.

Na hata kama ingesema hivyo, tusingeamini taarifa kwamba umati wa watu 50 na zaidi walikuwa ni mashoga.

Kwa hiyo, ni maoni yangu kwamba, wanateolojia wanaoongozwa na Biblia hawana mamlaka ya kutuhubiria juu ya mada ya "ushoga" kama ilivyojadiliwa katika uzi huu.

Lakini, wanayo mamlaka ya kujadili na kufundisha juu ya maadili ya ulawiti. Tugawane majukumu ili kutoa nafasi kwa kila kambi ya wanazuoni kutekeleza majukumu yale ipasavyo.

X. Majumuisho muhimu

Katika majumuisho ningependa tukumbushane kuhusu dhana muhimu zifuatazo kama msingi wa mjadala utakaendelea baada ya hapa:

Kwamba, maneno “mwelekeo wa ashiki” (sexual orientation) na “tabia ya kijinsia (sexual behaviour)” yanabeba maana mahsusi. Napenda maana zifuatazo zieleweke vkizuri.

Kwamba, tabia ya kijinsia (‘sexual behaviour’) ni hali ya kuwepo kwa mahusiano ya kimapenzi kati ya watu wa jinsia tofauti, watu wa jinsia moja au watu wa jinsia zote mbili (Bailey et al 2016:48).

Kwamba, dira ya ashiki (sexual orientation) ni hali ya kuwepo kwa sumaku ya kimapenzi kati ya watu wa jinsia tofauti, au kati ya watu wa jinsia moja, au kati ya watu wa jinsia zote mbili (Bailey et al 2016:48).

Kwamba, hali ya kuwepo kwa dira ya ashiki inayowaelekea watu wa jinsia tofauti inaitwa uheterofilia au mwelekeo wa ashikia za kiheterofilia (heterophilic sexual orientation’). Watu wengi kati ya 92%-99% wako katika kundi hili.

Kwamba, hali ya kuwepo kwa dira ya ashiki kumweleke mtu wa jinsia moja inaitwa uhomofilia au mwelekeo wa ashiki za kihomofilia (‘homophilic sexual orientation). Watu wachache kati ya 2%-11% wako katika kundi hili.

Kwamba, hali ya kuwepo kwa dira ya ashiki kumwelekea mtu wa jinsia moja ya kike unaitwa uhomofilia wa kike au usagaji (female homophilic sexual orientation).

Kwamba, hali ya kuwepo kwa dira ya ashiki kumwelekea mtu wa jinsia moja ya kiume inaitwa uhomofilia wa kiume au ushoga (male homophilic sexual orientation).

Na kwamba, hali ya kuwepo kwa dira ya ashiki kuelekea watu wa jinsia zote mbili inaitwa uambifilia (ambiphilic sexual orientation / bisexuality); na kwamba, uambifilia ni dira ya kijinsia ambayo ni mseto wa uhomofilia na uheterofiia.

XI. Hitimisho na mapendekezo: tunasongaje mbele baada ya hapa?

Katika kazi ya kujenga imani ya jamii, basi, wanasayansi, wanasheria na wanamaadili wanapaswa kushirikiana katika kujenga imani ya jamii.

Kwa ujumla, sote tunakamilishana kimaarifa, na hivyo kuna haja ya kuunganisha nguvu katika kufanikisha mradi wa kujenga imani ya jamii yenye utulivu, haki na amani kkwa kuanzia kwenye misingi ya uhalisia asilia (social realism) badala ya kukimbilia kwenye unadisi wa maarifa ya kijamii kwa njia ya kura (social constructionism).

Tujenge hoja bila mihemuko wala taharuki. Na mara zote tuongozwe na kanuni za udadavuzi wa kimantiki zifuatazo, ambazo ni kipimo cha urazini wa binadamu:

1. Law of identity: Kwa kila kitu kinachohesabika kuna sifa angalau moja inayokitofautisha na vitu baki hata kama vinafanana kwa asilimia 99.99 .

2. Law of non-contradiction: Kila kauli inayokumbatua mkanganyiko ni kauli potofu.

3. Law of excluded middle: Kila kauli ama ni ukweli au ni uwongo, na hakuna mbadala wa tatu.

4. Law of sufficient reason: Kila kauli isiyoambatana na maelezo yanayotosheleza mahitaji ya kukubalika kwa ukweli wake haipaswi kukubalika.

Hapa naongelea "kanuni ya usita wa herufi U," yaani, "unini, unani, ulini, uwapi, usababu, na utaratibu" wa tukio. Yaani, "5W's and 1H."

5. Law of licit logical inference: Hakuna hoja inayopaswa kuwa na hitimisho lenye taarifa ambayo haimo katika madokezo yanayozalisha hitimisho hilo.

Mwisho, basi, kwa kuwa yeye ni "Askofu mwenye uthubutu", ninamwalika Askofu Bagonza awakusanye na kushauriana na kina Askofu Nkwande, Paul Makonda na timu yake iliyomjumuisha Afande Suleiman Kova, kina Kigwangala, na wanasiasa baki, kuhusu madhara ya "teolojia ya dhambi ya ulawiti" na sayansi ya uhandisi wa marifa ya kijamii kwa usalama wa nchi.

Kwa msaada wa falsafa ya udhati wa mambo (realism), na sio falsafa ya uhandisi wa kijamii (social constructionism), kaeni pamoja na mfute mwafaka wa kisayansi, kiteolojia na kifalsafa kuhusu changamoto ya uhomofilia. Ukweli uwaweke huru.

Sipendi kuona teolojia ya dhambi ya ulawiti inavuruga nchi kila kukicha, tena pasipo sababu zenye mashiko. Jambo hili linatufanya tuwaone viongozi wa dini kama wataalam wa teolojia ya dhambi ya ulawiti pekee, hadi tunapoteza imani kwao!

XII. Marejeo Muhimu
  1. Bailey J.M., et al. (2016). “Sexual Orientation, Controversy, and Science,” Psychological Science for Public Interest, 17:45-101.
  2. Bernard Matolino (2014), Personhood in African Philosophy (Dorpspruit: Cluster Publications).
  3. Caixia Li (2016) et al, "The relationship between digit ratio and sexual orientation in a Chinese Yunnan Han population," Personality and Individual Differences, 101:26-29.
  4. David Oderberg(2011), “Essence and Properties.” Erkenntnis, 75(1):85-111.
  5. Friedrich Vogel and Arno G. Motulsky (1996), Human Genetics: Problems and Approaches, 3rd edition (Germany: Springer).
  6. Helminiak, D.A (1994). What the Bible Really Says About Homosexuality (San Francisco: Alamo Square Press).
  7. John Searle (1969), Speech acts: An essay in the philosophy of language (Cambridge University Press).
  8. John Yates (1995), “Towards a Theology of Homosexuality”, Evangelical Quarterly, 67.1:71-87.
  9. Leon Speroff and Marc A. Fritz (2005), Clinical Gynaecologic Endocrinology and Infertility (New York: Lippinkott William and Wilkins).
  10. Melissa Moschella (2019), “Sexual Ethics, Human Nature, and the ‘New’ and ‘Old’ Natural Law Theories,” Catholic Bioethics Quarterly 19.2: 251–278.
  11. Queller, D.C. and Strassmann, J.E. (2016). "Problems of Multi-Species Organisms: Endosymbionts to Holobionts". Biology Faculty Publications & Presentations. Paper 126:1-35.
  12. Rogers. J., (2006). Jesus, The Bible, and Homosexuality: Explode the Myths, Heal the Church. (Westminster: John Knox).
  13. Todd Salzman and Michael Lawler (2008), The Sexual Person: Toward a Renewed Catholic Anthropology, (Washington, D.C.: Georgetown University Press).
Mama Amon Desk,
"Sumbawanga Mjini"
07 Desemba 2022.
 

Attachments

  • 1676447479558.png
    1676447479558.png
    88.8 KB · Views: 21
Ushahidi gani. Kwamba akiwa ameshikishwa ukuta???
Umeandika" "Mashoga wanaongezeka kila uchao. " Leta ushahidi
Lkn pia habari ya kushikishwa ukuta inahitaji ushahidi pia.
Tabia ya kupiga ramli hapana
 
Hili bandiko lako ungelipeleka kwenye jumuia za kimagharibi, naamini lingepokewa kwa namna ambayo uliikusudia wakati unaliandika, lakini kwa kulileta kwenye jamii yetu, hapana; lazima utakumbana na upinzani.

Mfano ulioutoa kwa andiko la Bagonza, kwamba ipo siku mashoga wataunda jumuia zao ikiwemo makanisa nk, na kuonesha kuushangaa ukiamini kwamba mashoga tayari wana haki hizo, hapa nathubutu kusema unaenda kinyume na amri na mafundisho ya Mungu aliyetuumba.

Naona umejaribu kuwafanya mashoga waonekane ni jamii ya kawaida miongoni mwetu, lakini kimsingi, hali ya mambo haiko hivyo, mimi binafsi kusema kweli nawaogopa mashoga, na ninaamini haya mawazo yangu, ndio mawazo ya wengine wote wanaokwenda kwa kufuata mafundisho ya yule aliyetuumba.

Kwa hali hiyo, kitendo chochote cha kuwaacha mashoga wafikie hatua ya kuanzisha makundi yao ikiwemo makanisa, ni sawa na kuwaruhusu wafanye mambo yao kwa uwazi bila kificho, na kama hili litafanyika, basi hapo ndipo tunakwenda kuharibu watoto wetu kwa kasi zaidi ya sasa.

Kufikia hapa, binafsi ndipo naungana na Askofu Bagonza, jamii ya hawa watu haitakiwi kuachwa izidi kusambaa kwa uhuru na uwazi miongoni mwetu, kwani kwa kufanya hivyo, sio tu tutakuwa tunakwenda kinyume na mafundisho ya yule aliyetuumba, lakini pia, tutakuwa tumekaribisha janga kubwa zaidi la kuiharibu jamii yetu kwa vizazi vijavyo.
 
Mila na desturi za jamii yetu hazikubaliani na suala hili. Japo ni dhahiri kuwa wapo wengi ktk familia zetu. Acha wawepo hivyo hivyo illegally.

Hawatambuloki na wanakanwa na jamii pamoja na kubanwa na sheria. Hivyo kwa zama hizi hata haki zao wananyimwa.

Muda ukifika mtazamo dhidi yao ukipinduka tutaandika mengine hapa.
 
View attachment 2438877
Profesa John Searle, mtalaama wa social constructionism iliyo msingi wa maadili yanayobadilika kwa sababu ya mazingira na iliyo mbadala kwa social realism iliyo msingi wa maadili yasiyobadilika kwa sababu ya mazingira

Leo, kupitia mitandai ya kijamii, Benson Bagonza ameripotiwa kutamka kauli zifuatazo:

"Sikubaliani na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya. Hapa kwetu [Tanzania] tayari hali inatisha. Imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, na serikali itaufyata. Wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea. Tuamke."

Ama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" au "uhomofilia."

Mtu mmwenye tatizo la uhomofilia anaitwa homofiliki. Sio kila mlawiti ni homofiliki na sio kila homofiliki ni mlawiti.

Yaani kuna mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti. Hizi ni kada nne za watu, lakini Bagonza haonekani kuzitofautisha.

Bagonza anahimiza mapambano dhidi ya makundi yote manne, na hivyo kuhamasisha uhomofobia katika jamii. Sio sawa.

Hivyo kuna haja ya kujadili mawazo yake ili kusafisha akili za watumiaji wa mitandao ya kijamii. Naanza kwa kuonyesha makosa yake ya kimantiki.

Tatizo la Upindifu wa kimantiki

Upindifu wa kimantiki, yaani logical fallacy, ni kosa la kimantiki ambapo mwongeaji hutunga hoja inayokiuka misingi bora ya usanifu wa hoja na uendeshaji wa mijadala.

Mifano ya upindifu wa kimantiki ni tabia ya kutumia neno lenye maana nyingi bila kueleza maana inayoikusudiwa na mwongeaji (equivocation).

Mfano ni neno "ushoga" lenye maana mbili, yaani "ulawiti" au "uhomofilia."

Uhomofilia ni hali ya mtu kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsia yake. Na "ulawiti" ni tabia ya kufanya ngono kwa kuingiza jenitalia ya kiume kwenye rektamu.

Mfano mwingine wa Upindifu wa kimantiki ni kuongelea kitu kilicho kwenye tabaka moja, kwa kukibebesha kimakosa sifa za kitu baki kilicho kwenye tabaka jingine (category mistake).

Mfano, sauti iko katika tabaka la vitu vinavyosikika, wakati harufu iko katika tabaka la vitu vinavyonuka. Lakini, mara nyingi utasikia watu wanasema, "nasikia harufu ya chakula."

Maneno haya yanaiweka dhana ya "harufu" katika kundi moja na dhana ya "sauti." Hili ni kosa la kuchanganya pamoja kada za vitu visivyopaswa kuwekwa pamoja.

Yaani, “we say that one has committed a category mistake when she ascribes, to a certain entity, a property or properties which that entity could not have... [meaning that] one locates some entity in a category it does not belong.” (Bernard Matolino, Personhood in African Philosophy (Dorpspruit: Cluster Publications; 2014, p. 142)

Hivyo, mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti ni kada nne za watu, kila kada ikiwa na tabia na sifa zake zinazoitofautisha.

Kupuuzia ukweli huu ni kufanya kosa la kuchanganya kada za vitu kwa kuvivisha baadhi ya vitu sifa visivyokuwa nazo.

Maana ya kwanza ya ushoga ni uhomofilia

Kwa upande mmoja, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "uhomofilia," ambayo ni sifa ya kimaumbile, kama ulivyo ufupi na urefu, weupe na weusi, ualibino na siualibino, njia pekee ya kupambana, kama anavyopendekeza, na "ushoga" ni kuwaua "mashoga" hao.

Hivyo, Bagonza hapa anahubiri tabia hatari ya uhomofobia. Sijui kama alitafakari vema juu ya uwezekano huu.

Lakini, pia Bagonza anapswa kutoa sababu nzuri ya kupambana na mahomofilia na kuacha kupambana na mazeruzeru, watu wenye tatizo la colour blindness, na matabaka ya pembezoni kama hayo.

Wote hawa wako hivyo kwa sababu za kimaumbile. Hawakuchagua hali zao.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [mahomofiliki] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea."

Kwa maoni haya ya Bagonza, hata "mahomofilia" wasio na tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi. Kwa kiwango hiki maoni yake nayapinga.

Urefu, ufupi, sauti nene, sauti nyororo, umashoto, umakengeza, uzeruzeru, colour blindness, na ladhalika, ni sifa asilia walizo nazo watu kadhaa.

Lakini watu hawa hawapotezi haki zao za kibayolojia, kisaikosomatika, kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa sababu hiyo pekee.

Huenda Bagonza hauoni ukweli huu kwa sababu anaongea kama mwanateolojia. Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii mseto sio mradi wa wanateolojia pekee, kama nitakavyoeleza hapa chini baadaye.


Maana ya pili ya ushoga ni ulawiti

Kwa upande mwingine, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" kuna maswali ya kitafiti anapswa kutusaidia kuyajibu.

Tangu tupate uhuru tumefanya sensa mara tano. Hakuna takwimu za serikali zinaonyesha idadi ya mashoga nchini.

KIla mwaka serikali kupitia jeshi la Polisi na Idara ya takwimu (NBS) wanatoa takwimu za uhalifu kupitia kitabu kiitwacho TANZANIA IN FIGURES. Huku pia idadi ya mashoga haitajwi.

Lakini takwimu za mwaka 2021 zinaonyesha kuwa yalikuwepo matukio ya ulawiti 1,296.

Taarifa hiyo haisemi kama ulawiti huu ulifanywa dhidi ya wanaume au kama wanawake au kama ulifanywa na mashoga.

Lakini bado Bagonza anasema hakubaliani "na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya" kwa sababu tayari "hapa kwetu mbona hali inatisha," anasema.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [walawiti] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke"

Kwa maoni ya Bagonza, "mahomofilia" wenye tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi kwa sabavu ya uhalifu wao.

Sawa. Lakini msimamo huu haupaswi kuishia kwa wahalifu wa ulawiti pekee. Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya kila mwala, iitwayo Tanzania in Figures, kuna makundi mengi ya uhalifu na yote yanapaswa kumulikwa na serikali.

Bagonza angeeleweka sana kama angesema hivi: "imebaki kidogo [wahalifu] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke."

Kwa kiwango hiki ningekubaliana naye Bagonza. Hapa kuna wezi, wala rushwa, watu wanaotelekeza watoto mitaani, wafanya biashara ya binadamu, wateka watu, na orodha inaendelea.

Na takwimu halisi za kiserikali kupitia taarifa ya Tanzania in Figures ya kila mwaka, zinaonyesha kuwa baadhi ya watu hawa tayari wana makanisa, wengine ni wamiliki wa vyombo vya habari, wengine ni maaskofu kuanzia makanisa ya kipentekoste hadi Kanisa Katoliki, wengine ni wachungaji, na Bagonza anaujua ukweli huu fika.

Lakini bado Bagonza kaamua kuibuka na habari ya "ushoga" isiyo na takwimu za kitafiti.

Angeleweka na kukubalika zaidi kama angesema kuna "mashoga" wangapi kwenye kaya yake, ukoo wake, kijiji/mtaa wake wa Mwisho wa Lami, kata yake ya Kayanga, wilaya yake ya Karagwe na mkoa wake wa Kagera. Hakutoa takwimu zozote katika ngazi hizi.


Hivyo, napenda kumkumbusha kuwa, sifa tata za kimaumbile hazifuti haki za msingi za mahomofilia, maalibino, mashoto, na wenye makengeza, nk.

Sifa hizo ni kama vile haki ya kuishi, kujumuika, kugombea nafasi za kisiasa, kupiga kura, kuabudu, kulindwa na serikali, na haki baki za kibinadamu.


Changamoto ya social constructionism

Kwa maoni yangu, tamko la Bagonza linaambatana na makosa mawili ya kimantiki: equivocation and category mistake.

Bahati mbaya, kwa sehemu kubwa, hadhira inayomsikiliza Bagonza, haina weledi wa kuyabaini haya makosa.

Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii yenye utulivu na amani inapaswa kuongozwa na kanuni bora za usanifu, utetezi na ubomozi wa hoja.

Vinginevyo tutawalisha watu matango pori, na kupanda magugu katika Taifa letu. Sio haki.

Ukisoma vizuri mawazo ya Bagonza utaona kuwa yanaongozwa na kanuni za kambi ya wanazuoni makuwadi wa nadharia ya social constructionism, yaani nadharia za ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu, kama vile Profesa John Rogers Searle (Amerika).

Katika maandiko yake, John Rogers Searle’s kuhusu ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu (social ontology), anatala kanuni kadhaa kuhusiana na ujio wa ukweli wa kijamii (social reality).

Kanuni moja inahusu "collective intentionality," nyingine inahusu "the assignment of status functions," na kanuni ya tatu inahusu "constitutive rules." Ninataka kuongelea hii kanuni ya tatu, ambayo ni kanuni ya kubuni na kutumia alama.


Kanuni hii inasema hivi: watu wanaweza kukaa wakakubaliana kwamba katika mazingira haya (X), kitu hiki (Y) kitakuwa alama inayowakilisha kitu kile (Z), na mapatano haya yatakoma pale watakapokaa tena na kukubaliana kuyabadilisha. (John R. Searle, Speech acts: An essay in the philosophy of language (Cambridge University Press; 1969, p. 34))

Mfano wake muhimu ni jumuiya ya wanampira waliokubaliana kuwa, katika mazigira ya uwanja wa mpira wa miguu (X), mchezaji akipokea mpira wakati anaelekea kufunga kwenye goli la mpizani wake wakati mbele yake hakuna mchezaji wa timu pinzani (Y), basi hilo ni kosa linaitwa offside (Z).

Kanuni hii inafaa kwenye mpira wa miguu pekee, na sio kwenye mpira wa mikono wala kwenye mpira wa kikapu.

Kwa hiyo, ikitokea siku wachezaji wa michezo yote hii wakajikuta wako pamoja kwa ajili ya mchezo mmoja, itabidi waunde kanuni mpya zinazokubalika kwa wote na kuwafaa wote. Ni vivyo hivyo kwenye maisha ya jamii mseto.

Yaani, kanuni zenye kutokana na mchakato wa mapatano ya kijamii (social constructionism) zinaweza kutumika kwenye jamii ya watu wenye imani moja, lakini sio kwenye jamii za leo ambako kuna utitiri wa kifikra (plural society).

Mfano, wakati wa Papa Yohanne Paulo II, baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki waliweka msimamo kwamba mahunta sio binadamu.

Mfano wa mwathirika ni Padre Selwyn Gross (jina la zamani la kiume) na baadaye Padre Sally Gross (jina jipya la kike), baada ya kubadilisha jinsia yake.

Hivyo, "Padre Sally Gross" aliyekuwa hunta (intersexual), alivuliwa upadre, kwa kuwa wanawake hawana haki ya kuwa mapadre.

Pia alifutiwa ubatizo kwa hoja kwamba mahunta sio binadamu, na hivyo hawana haki ya kubatizwa.

Lakini, sayansi mamboleo inathibitisha mahunta wana kromozomu 46 kama watu baki walioko kwenye ukoo wa homosapiensia.

Yaani kumwondoa Padre Sally kwenye tabaka la binadamu ulikuwa ni uamuzi wenye sura ya "category mistake."

Hivyo, Kanisa Katoliki sasa limejisahihishana halibebi tena mawazo yale potofu kuhusu hulka ya mahunta. Kanuni za maumbile ziliwaleta karibu na ukweli.

Kwa sasa bado Kanisa Katoliki linapambana na fundisho lake tata kwamba "a copulating pair is a biological organism"

Fundisho hili ni zao la mradi wa social constructionism wa miaka ya 1968, na ni fundisho linalopingana na kanuni za kibayolojia na kifalsafa.

Kifalsafa, neno "organism" lina maana tatu. Yaani "biological organism" kama vile binadamu na kondoo; "social organism" kama vile familia na timu a mpira; na "mechanical organism" kama vile gari au saa ya kuhesabu majira.

Ufanano wake ni kwamba, aina zote tatu ni mifumo yenye sehemu nyingi zinazofanya kazi kwa kushirikiana bila kupingana kwa ajili ya kufanikisha lengo la pamoja.

Tofauti kati ya "biological organism" kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine, "social organism" na "mechanical organism" ni kwamba, wakati "kanuni ya uratibu" iko ndani ya "biological organism," kauni hiyo iko nje ya "social organism" na "mechanical organism"

Tofauti kati ya "biological organism" na "social organism" ni kwamba, kiungo cha mwili wa "biological organism" kikikatwa kinakufa, lakini kiungo cha mwili wa "social organism" kikikatwa hakifi.

Mfano, mchezaji wa mpira wa miguu akipewa kadi nyekundi anaondoka uwanjani na anabaki hai. Lakini, mkono wako ukikatawa unaoza haraka.

Kwa upande mwingine uhai wa "social organism" unaanzia na kukomea kwenye mapatano ya kijamii kati ya wanachama husika. Lakini uhai wa "biological organism" hauko hivyo.

Na "mechanical organism" inaendeshwa na dereva ambaye sio sehemu yake. Mfano kujaza ufunguo kwenye saa ya kamani, kuendesha gari.

Kwa sababu hizi, sasa ulimwengu wa wanasayansi unakubaliana kwamba "a copulating pair is a social organism," na sio "biological organism," kama inavyodaiwa na baadhi ya makuwadi wa "teolojia ya mwili mmoja," yaani, "theology of one bodily union"

Lakini bado mijadala inaendelea na wataalam wa falsafa ya kibayolojia (philosophical biology) hapa wamesaidia sana kuleta mapinduzi ya kifikra yanayotakiwa kuhusiana na swali hili hapa: "what is biological individuality?"

Msingi wa kimetafizikia wa kanuni za maadili asilia, sio nadharia ya ukweli uliofinyangwa na watu na utakaokufa pale watu watakapokubaliana kuukataa (social constructionism), bali nadharia ya ukweli unaogunduliwa na watu na utakaoendelea kuwepo hata kama watu wataukataa (social realism).

Hitimisho na mapendekezo

Kwa hiyo, njia pekee ya kujenga imani ya jamii inayokubalika kwa watu wote katika jamii yenye mapokeo mseto sio kutumia kanuni za social constructionism zinazoanzia kwenye "kanuni za taharuki ya kijamii isiyo na uhalali" (unwarranted moral panic)

Badala yake, tunapaswa kuanzia kwenye kanuni za maadili asilia yanayoweza, na yanayopaswa, kuthibitika kwa njia ya urazini huru miongoni mwa umma mpana (public reason).

Bila kukubaliana na ukweli huu, kazi ya ujenzi wa imani ya jamii yenye imani mseto itakwama, maana mwafaka wa kijamii ni ajenda ya mpito tu.

Mwisho, niseme tu kuwa, katika mradi huu wa kujenga imani ya jamii, kila mdau, yaani wanateolojia, wanasayansi asilia, wanasayansi ya jamii, wanafalsafa, wanasasiolojia, wanahistoria, na wanazuoni baki wanayo nafasi.

Lakini, mchango wa kila mmoja una mipaka inayokamilishwa na michango ya wenzake.

Mfano, kwenye Safina ya Nuhu tunaambiwa kuwa Nuhu aliagizwa kuweka kila kiumbe kwa kuzingatia kanuni ya ME na KE.

Lakini, leo hii sayansi inatwambia kuwa kuna viumbe havina mgawanyo huo wa ME na KE. Mfano ni minyoo. Kwa hiyo, mwandishi wa Agano la Kale hakuwa na habari ya ukweli huu wa viumbe wasio na mgawanyo wa jinsia ya ME na KE.

Na hii maana yeke ni kwamba, wanateolojia wanaofanya udadavuzi kwa kuanzia kwenye Biblia wanahitaji kuelimishwa na wanabayolojia katika suala ya asexual reporoduction. Biblia haina mamlaka katika jambo hili.

Sote tunakamilishana kimaarifa, na hivyo kuna haja ya kuunganisha nguvu katika kufanikisha mradi wa kujenga imani ya jamii yenye utulivu, haki na amani.

Tujenge hoja bila mihemuko wala taharuki.

Makala ni ndefu lakini inavutia kuisoma mpaka mwisho. Imeandikwa kitaalamu na bila shaka toka kwa mtaalam wa Saikolojia.

Jambo moja kubwa nililolipata hapa, kwa lugha rahisi ni kwamba kuna mashoga wa kuzaliwa. Wamezaliwa na kasoro za kimaumbile, hisia au vyote kwa pamoja.

Moja ya sababu za kitaalam zinazotufanya kuwa na hisia mbalimbali zikiwemo za kuvutiwa kimapenzi ni hormones. Watu wenye hormones inbalance lazima na hisia zao haziwi za kawaida. Mathalani mtu ambaye ni mwanamke kimaumbile lakini mwenye hormones nyingi za kiume, atakuwa na hisia zaidi za kiume, hisia za kupenda kumiliki kuliko kumilikiwa. Na hawa katika mahusiano yao ya ushoga huwa wanakuwa ndiyo wanaume wa wenzao japo wote, kimaumbile ni wanawake.

Kwa upande mwingine, wanaume wenye hormones nyingi za kike, hisia zao huegemea zaidi kwenye ukike, ikiwa ni pamoja na kupenda kutunzwa na kumilikiwa.

Lakini wapo wale wanaojiingiza huko, labda kwa sababu ya kupewa fedha au kuhudumiwa, watafuta mteremko. Yaani dada ni mzima kabisa, lakini kwa vile amempata dada mwenzake mwenye uwezo lakini mwenye hisia za kiume, anakubali kuwa mke wa mwanamke mwenzake kwa vile tu anahudumiwa kwa kila kitu.

Lakini wapo walawiti, ni mwanaume kamili kabisa, labda kwa kujizoesha au kushawishiwa anakuwa mlawiti au mlawitiwa. Au dada mzuri kabisa, tena timilifu, kwa vile amempata mwanaume mlawiti anakubali kulawitiwa. Na huenda hawa ndio wengi zaidi.

Wale wa kundi la kwanza ni walemavu. Walemavu wa namna hii wasaidiwe kwa namna gani?

Kundi hili la pili ni wahalifu. Kiimani, ni wahalifu sawa na majambazi, wazinzi, waabudu sanamu/mizimu, waongo, mafisadi, n.k.

Tena kwenye biblia imeandikwa:

1Wakoritho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafilaji, wala walawiti,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Wale wa kundi la pili wanatakiwa kudhibitiwa, lakini wale wa kundi la kwanza wanatakiwa kusaidiwa, na bila shaka wapo wanaosaidiwa kitabibu, japo ni dhahiri suluhusho kamili halijapatikana. Ninaamini kosa kubwa linalofanyika ni kulikataa kuwa hili ni tatizo, na tukaishia kwa vile wana hisia hizo, basi kama jamii tukubali kuwa hali hiyo ni ya kawaida, na hivyo hakuna haja ya kuihangaikia, tuwaache waendelee na mahusiano yao ya jinsia moja.
 
View attachment 2438877
Profesa John Searle, mtalaama wa social constructionism iliyo msingi wa maadili yanayobadilika kwa sababu ya mazingira na iliyo mbadala kwa social realism iliyo msingi wa maadili yasiyobadilika kwa sababu ya mazingira

Leo, kupitia mitandai ya kijamii, Benson Bagonza ameripotiwa kutamka kauli zifuatazo:

"Sikubaliani na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya. Hapa kwetu [Tanzania] tayari hali inatisha. Imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, na serikali itaufyata. Wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea. Tuamke."

Ama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" au "uhomofilia."

Mtu mmwenye tatizo la uhomofilia anaitwa homofiliki. Sio kila mlawiti ni homofiliki na sio kila homofiliki ni mlawiti.

Yaani kuna mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti. Hizi ni kada nne za watu, lakini Bagonza haonekani kuzitofautisha.

Bagonza anahimiza mapambano dhidi ya makundi yote manne, na hivyo kuhamasisha uhomofobia katika jamii. Sio sawa.

Hivyo kuna haja ya kujadili mawazo yake ili kusafisha akili za watumiaji wa mitandao ya kijamii. Naanza kwa kuonyesha makosa yake ya kimantiki.

Tatizo la Upindifu wa kimantiki

Upindifu wa kimantiki, yaani logical fallacy, ni kosa la kimantiki ambapo mwongeaji hutunga hoja inayokiuka misingi bora ya usanifu wa hoja na uendeshaji wa mijadala.

Mifano ya upindifu wa kimantiki ni tabia ya kutumia neno lenye maana nyingi bila kueleza maana inayoikusudiwa na mwongeaji (equivocation).

Mfano ni neno "ushoga" lenye maana mbili, yaani "ulawiti" au "uhomofilia."

Uhomofilia ni hali ya mtu kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsia yake. Na "ulawiti" ni tabia ya kufanya ngono kwa kuingiza jenitalia ya kiume kwenye rektamu.

Mfano mwingine wa Upindifu wa kimantiki ni kuongelea kitu kilicho kwenye tabaka moja, kwa kukibebesha kimakosa sifa za kitu baki kilicho kwenye tabaka jingine (category mistake).

Mfano, sauti iko katika tabaka la vitu vinavyosikika, wakati harufu iko katika tabaka la vitu vinavyonuka. Lakini, mara nyingi utasikia watu wanasema, "nasikia harufu ya chakula."

Maneno haya yanaiweka dhana ya "harufu" katika kundi moja na dhana ya "sauti." Hili ni kosa la kuchanganya pamoja kada za vitu visivyopaswa kuwekwa pamoja.

Yaani, “we say that one has committed a category mistake when she ascribes, to a certain entity, a property or properties which that entity could not have... [meaning that] one locates some entity in a category it does not belong.” (Bernard Matolino, Personhood in African Philosophy (Dorpspruit: Cluster Publications; 2014, p. 142)

Hivyo, mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti ni kada nne za watu, kila kada ikiwa na tabia na sifa zake zinazoitofautisha.

Kupuuzia ukweli huu ni kufanya kosa la kuchanganya kada za vitu kwa kuvivisha baadhi ya vitu sifa visivyokuwa nazo.

Maana ya kwanza ya ushoga ni uhomofilia

Kwa upande mmoja, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "uhomofilia," ambayo ni sifa ya kimaumbile, kama ulivyo ufupi na urefu, weupe na weusi, ualibino na siualibino, njia pekee ya kupambana, kama anavyopendekeza, na "ushoga" ni kuwaua "mashoga" hao.

Hivyo, Bagonza hapa anahubiri tabia hatari ya uhomofobia. Sijui kama alitafakari vema juu ya uwezekano huu.

Lakini, pia Bagonza anapswa kutoa sababu nzuri ya kupambana na mahomofilia na kuacha kupambana na mazeruzeru, watu wenye tatizo la colour blindness, na matabaka ya pembezoni kama hayo.

Wote hawa wako hivyo kwa sababu za kimaumbile. Hawakuchagua hali zao.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [mahomofiliki] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea."

Kwa maoni haya ya Bagonza, hata "mahomofilia" wasio na tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi. Kwa kiwango hiki maoni yake nayapinga.

Urefu, ufupi, sauti nene, sauti nyororo, umashoto, umakengeza, uzeruzeru, colour blindness, na ladhalika, ni sifa asilia walizo nazo watu kadhaa.

Lakini watu hawa hawapotezi haki zao za kibayolojia, kisaikosomatika, kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa sababu hiyo pekee.

Huenda Bagonza hauoni ukweli huu kwa sababu anaongea kama mwanateolojia. Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii mseto sio mradi wa wanateolojia pekee, kama nitakavyoeleza hapa chini baadaye.


Maana ya pili ya ushoga ni ulawiti

Kwa upande mwingine, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" kuna maswali ya kitafiti anapswa kutusaidia kuyajibu.

Tangu tupate uhuru tumefanya sensa mara tano. Hakuna takwimu za serikali zinaonyesha idadi ya mashoga nchini.

KIla mwaka serikali kupitia jeshi la Polisi na Idara ya takwimu (NBS) wanatoa takwimu za uhalifu kupitia kitabu kiitwacho TANZANIA IN FIGURES. Huku pia idadi ya mashoga haitajwi.

Lakini takwimu za mwaka 2021 zinaonyesha kuwa yalikuwepo matukio ya ulawiti 1,296.

Taarifa hiyo haisemi kama ulawiti huu ulifanywa dhidi ya wanaume au kama wanawake au kama ulifanywa na mashoga.

Lakini bado Bagonza anasema hakubaliani "na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya" kwa sababu tayari "hapa kwetu mbona hali inatisha," anasema.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [walawiti] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke"

Kwa maoni ya Bagonza, "mahomofilia" wenye tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi kwa sabavu ya uhalifu wao.

Sawa. Lakini msimamo huu haupaswi kuishia kwa wahalifu wa ulawiti pekee. Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya kila mwala, iitwayo Tanzania in Figures, kuna makundi mengi ya uhalifu na yote yanapaswa kumulikwa na serikali.

Bagonza angeeleweka sana kama angesema hivi: "imebaki kidogo [wahalifu] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke."

Kwa kiwango hiki ningekubaliana naye Bagonza. Hapa kuna wezi, wala rushwa, watu wanaotelekeza watoto mitaani, wafanya biashara ya binadamu, wateka watu, na orodha inaendelea.

Na takwimu halisi za kiserikali kupitia taarifa ya Tanzania in Figures ya kila mwaka, zinaonyesha kuwa baadhi ya watu hawa tayari wana makanisa, wengine ni wamiliki wa vyombo vya habari, wengine ni maaskofu kuanzia makanisa ya kipentekoste hadi Kanisa Katoliki, wengine ni wachungaji, na Bagonza anaujua ukweli huu fika.

Lakini bado Bagonza kaamua kuibuka na habari ya "ushoga" isiyo na takwimu za kitafiti.

Angeleweka na kukubalika zaidi kama angesema kuna "mashoga" wangapi kwenye kaya yake, ukoo wake, kijiji/mtaa wake wa Mwisho wa Lami, kata yake ya Kayanga, wilaya yake ya Karagwe na mkoa wake wa Kagera. Hakutoa takwimu zozote katika ngazi hizi.


Hivyo, napenda kumkumbusha kuwa, sifa tata za kimaumbile hazifuti haki za msingi za mahomofilia, maalibino, mashoto, na wenye makengeza, nk.

Sifa hizo ni kama vile haki ya kuishi, kujumuika, kugombea nafasi za kisiasa, kupiga kura, kuabudu, kulindwa na serikali, na haki baki za kibinadamu.


Changamoto ya social constructionism

Kwa maoni yangu, tamko la Bagonza linaambatana na makosa mawili ya kimantiki: equivocation and category mistake.

Bahati mbaya, kwa sehemu kubwa, hadhira inayomsikiliza Bagonza, haina weledi wa kuyabaini haya makosa.

Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii yenye utulivu na amani inapaswa kuongozwa na kanuni bora za usanifu, utetezi na ubomozi wa hoja.

Vinginevyo tutawalisha watu matango pori, na kupanda magugu katika Taifa letu. Sio haki.

Ukisoma vizuri mawazo ya Bagonza utaona kuwa yanaongozwa na kanuni za kambi ya wanazuoni makuwadi wa nadharia ya social constructionism, yaani nadharia za ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu, kama vile Profesa John Rogers Searle (Amerika).

Katika maandiko yake, John Rogers Searle’s kuhusu ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu (social ontology), anatala kanuni kadhaa kuhusiana na ujio wa ukweli wa kijamii (social reality).

Kanuni moja inahusu "collective intentionality," nyingine inahusu "the assignment of status functions," na kanuni ya tatu inahusu "constitutive rules." Ninataka kuongelea hii kanuni ya tatu, ambayo ni kanuni ya kubuni na kutumia alama.


Kanuni hii inasema hivi: watu wanaweza kukaa wakakubaliana kwamba katika mazingira haya (X), kitu hiki (Y) kitakuwa alama inayowakilisha kitu kile (Z), na mapatano haya yatakoma pale watakapokaa tena na kukubaliana kuyabadilisha. (John R. Searle, Speech acts: An essay in the philosophy of language (Cambridge University Press; 1969, p. 34))

Mfano wake muhimu ni jumuiya ya wanampira waliokubaliana kuwa, katika mazigira ya uwanja wa mpira wa miguu (X), mchezaji akipokea mpira wakati anaelekea kufunga kwenye goli la mpizani wake wakati mbele yake hakuna mchezaji wa timu pinzani (Y), basi hilo ni kosa linaitwa offside (Z).

Kanuni hii inafaa kwenye mpira wa miguu pekee, na sio kwenye mpira wa mikono wala kwenye mpira wa kikapu.

Kwa hiyo, ikitokea siku wachezaji wa michezo yote hii wakajikuta wako pamoja kwa ajili ya mchezo mmoja, itabidi waunde kanuni mpya zinazokubalika kwa wote na kuwafaa wote. Ni vivyo hivyo kwenye maisha ya jamii mseto.

Yaani, kanuni zenye kutokana na mchakato wa mapatano ya kijamii (social constructionism) zinaweza kutumika kwenye jamii ya watu wenye imani moja, lakini sio kwenye jamii za leo ambako kuna utitiri wa kifikra (plural society).

Mfano, wakati wa Papa Yohanne Paulo II, baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki waliweka msimamo kwamba mahunta sio binadamu.

Mfano wa mwathirika ni Padre Selwyn Gross (jina la zamani la kiume) na baadaye Padre Sally Gross (jina jipya la kike), baada ya kubadilisha jinsia yake.

Hivyo, "Padre Sally Gross" aliyekuwa hunta (intersexual), alivuliwa upadre, kwa kuwa wanawake hawana haki ya kuwa mapadre.

Pia alifutiwa ubatizo kwa hoja kwamba mahunta sio binadamu, na hivyo hawana haki ya kubatizwa.

Lakini, sayansi mamboleo inathibitisha mahunta wana kromozomu 46 kama watu baki walioko kwenye ukoo wa homosapiensia.

Yaani kumwondoa Padre Sally kwenye tabaka la binadamu ulikuwa ni uamuzi wenye sura ya "category mistake."

Hivyo, Kanisa Katoliki sasa limejisahihishana halibebi tena mawazo yale potofu kuhusu hulka ya mahunta. Kanuni za maumbile ziliwaleta karibu na ukweli.

Kwa sasa bado Kanisa Katoliki linapambana na fundisho lake tata kwamba "a copulating pair is a biological organism"

Fundisho hili ni zao la mradi wa social constructionism wa miaka ya 1968, na ni fundisho linalopingana na kanuni za kibayolojia na kifalsafa.

Kifalsafa, neno "organism" lina maana tatu. Yaani "biological organism" kama vile binadamu na kondoo; "social organism" kama vile familia na timu a mpira; na "mechanical organism" kama vile gari au saa ya kuhesabu majira.

Ufanano wake ni kwamba, aina zote tatu ni mifumo yenye sehemu nyingi zinazofanya kazi kwa kushirikiana bila kupingana kwa ajili ya kufanikisha lengo la pamoja.

Tofauti kati ya "biological organism" kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine, "social organism" na "mechanical organism" ni kwamba, wakati "kanuni ya uratibu" iko ndani ya "biological organism," kauni hiyo iko nje ya "social organism" na "mechanical organism"

Tofauti kati ya "biological organism" na "social organism" ni kwamba, kiungo cha mwili wa "biological organism" kikikatwa kinakufa, lakini kiungo cha mwili wa "social organism" kikikatwa hakifi.

Mfano, mchezaji wa mpira wa miguu akipewa kadi nyekundi anaondoka uwanjani na anabaki hai. Lakini, mkono wako ukikatawa unaoza haraka.

Kwa upande mwingine uhai wa "social organism" unaanzia na kukomea kwenye mapatano ya kijamii kati ya wanachama husika. Lakini uhai wa "biological organism" hauko hivyo.

Na "mechanical organism" inaendeshwa na dereva ambaye sio sehemu yake. Mfano kujaza ufunguo kwenye saa ya kamani, kuendesha gari.

Kwa sababu hizi, sasa ulimwengu wa wanasayansi unakubaliana kwamba "a copulating pair is a social organism," na sio "biological organism," kama inavyodaiwa na baadhi ya makuwadi wa "teolojia ya mwili mmoja," yaani, "theology of one bodily union"

Lakini bado mijadala inaendelea na wataalam wa falsafa ya kibayolojia (philosophical biology) hapa wamesaidia sana kuleta mapinduzi ya kifikra yanayotakiwa kuhusiana na swali hili hapa: "what is biological individuality?"

Msingi wa kimetafizikia wa kanuni za maadili asilia, sio nadharia ya ukweli uliofinyangwa na watu na utakaokufa pale watu watakapokubaliana kuukataa (social constructionism), bali nadharia ya ukweli unaogunduliwa na watu na utakaoendelea kuwepo hata kama watu wataukataa (social realism).

Hitimisho na mapendekezo

Kwa hiyo, njia pekee ya kujenga imani ya jamii inayokubalika kwa watu wote katika jamii yenye mapokeo mseto sio kutumia kanuni za social constructionism zinazoanzia kwenye "kanuni za taharuki ya kijamii isiyo na uhalali" (unwarranted moral panic)

Badala yake, tunapaswa kuanzia kwenye kanuni za maadili asilia yanayoweza, na yanayopaswa, kuthibitika kwa njia ya urazini huru miongoni mwa umma mpana (public reason).

Bila kukubaliana na ukweli huu, kazi ya ujenzi wa imani ya jamii yenye imani mseto itakwama, maana mwafaka wa kijamii ni ajenda ya mpito tu.

Mwisho, niseme tu kuwa, katika mradi huu wa kujenga imani ya jamii, kila mdau, yaani wanateolojia, wanasayansi asilia, wanasayansi ya jamii, wanafalsafa, wanasasiolojia, wanahistoria, na wanazuoni baki wanayo nafasi.

Lakini, mchango wa kila mmoja una mipaka inayokamilishwa na michango ya wenzake.

Mfano, kwenye Safina ya Nuhu tunaambiwa kuwa Nuhu aliagizwa kuweka kila kiumbe kwa kuzingatia kanuni ya ME na KE.

Lakini, leo hii sayansi inatwambia kuwa kuna viumbe havina mgawanyo huo wa ME na KE. Mfano ni minyoo. Kwa hiyo, mwandishi wa Agano la Kale hakuwa na habari ya ukweli huu wa viumbe wasio na mgawanyo wa jinsia ya ME na KE.

Na hii maana yeke ni kwamba, wanateolojia wanaofanya udadavuzi kwa kuanzia kwenye Biblia wanahitaji kuelimishwa na wanabayolojia katika suala ya asexual reporoduction. Biblia haina mamlaka katika jambo hili.

Sote tunakamilishana kimaarifa, na hivyo kuna haja ya kuunganisha nguvu katika kufanikisha mradi wa kujenga imani ya jamii yenye utulivu, haki na amani.

Tujenge hoja bila mihemuko wala taharuki.
Wewe ndiyo wale wale. Maneno meeengi kutaka kuhalalisha haramu
 
Kwa ufupi, Kanisa linatambua uwepo wa binadamu wenye disorder kama vilema vingine ikiwemo mtu kuwa na hormones za kike lakini mapungufu hayo si mlango wa kuhalalisha vitendo ambavyo ni uovu mbele ya Mungu.

Binadamu wote wana haki sawa lakini inapofikia vitendo kama ushoga kuhalalishwa kwenye jamii ni kuua jamii tutajikuta tunahalalisha ndoa zao na mambo mengine.

Kadri tunapoachana na Mungu ndivyo binadamu anavyozidi kupotea na kupoteza tunu za kibinadamu hadi tunafikia level tunataka ku introduce jinsia kwasababu ya uhuru wa kipumbavu!

Ushoga ukemewe, upingwe, ukatazwe bila kupepesa macho! Hili halihitaji upembuzi la huo ushoga ukoje. Wenye disorder za kibinadamu uwekwe utaratibu wa kuwasaidia lakini sio kuwapa uhuru utaoharibu jamii yetu.

Askofu Bagonza amesema vyema na hilo la mchangunuo ni hatua nyingine kuelekea kufanyia kazi tatizo.
 
Tatizo letu wabongo unafiki mwingi san, hoja ya bagonza ipo deep san that's why akawa ana mention utawala kuufyata. Akijua fika utawala wetu haujawahi kulipinga publicity, ushoga haukubalik by any means!! But tusiwe wanafiki nashaur mtoa hoja mama amon uiambie serikali ifanye kama OG Putin alichofanya.. itoa strong speech ya kukemea na kuweka sheria kali ya ya ushoga na mamb yanayoendana na hayo na kupinga hoja ya bagonza kinafiki wakat kama iwekwe sheria kali mnoo juu ya hilo na hapo tutaondoa unafiki!!! Nyayo za Putin ni muhim zifuatwe Kweny hili!!!
View attachment 2438877
Profesa John Searle, mtalaama wa social constructionism iliyo msingi wa maadili yanayobadilika kwa sababu ya mazingira na iliyo mbadala kwa social realism iliyo msingi wa maadili yasiyobadilika kwa sababu ya mazingira

Leo, kupitia mitandai ya kijamii, Benson Bagonza ameripotiwa kutamka kauli zifuatazo:

"Sikubaliani na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya. Hapa kwetu [Tanzania] tayari hali inatisha. Imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, na serikali itaufyata. Wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea. Tuamke."

Ama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" au "uhomofilia."

Mtu mmwenye tatizo la uhomofilia anaitwa homofiliki. Sio kila mlawiti ni homofiliki na sio kila homofiliki ni mlawiti.

Yaani kuna mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti. Hizi ni kada nne za watu, lakini Bagonza haonekani kuzitofautisha.

Bagonza anahimiza mapambano dhidi ya makundi yote manne, na hivyo kuhamasisha uhomofobia katika jamii. Sio sawa.

Hivyo kuna haja ya kujadili mawazo yake ili kusafisha akili za watumiaji wa mitandao ya kijamii. Naanza kwa kuonyesha makosa yake ya kimantiki.

Tatizo la Upindifu wa kimantiki

Upindifu wa kimantiki, yaani logical fallacy, ni kosa la kimantiki ambapo mwongeaji hutunga hoja inayokiuka misingi bora ya usanifu wa hoja na uendeshaji wa mijadala.

Mifano ya upindifu wa kimantiki ni tabia ya kutumia neno lenye maana nyingi bila kueleza maana inayoikusudiwa na mwongeaji (equivocation).

Mfano ni neno "ushoga" lenye maana mbili, yaani "ulawiti" au "uhomofilia."

Uhomofilia ni hali ya mtu kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsia yake. Na "ulawiti" ni tabia ya kufanya ngono kwa kuingiza jenitalia ya kiume kwenye rektamu.

Mfano mwingine wa Upindifu wa kimantiki ni kuongelea kitu kilicho kwenye tabaka moja, kwa kukibebesha kimakosa sifa za kitu baki kilicho kwenye tabaka jingine (category mistake).

Mfano, sauti iko katika tabaka la vitu vinavyosikika, wakati harufu iko katika tabaka la vitu vinavyonuka. Lakini, mara nyingi utasikia watu wanasema, "nasikia harufu ya chakula."

Maneno haya yanaiweka dhana ya "harufu" katika kundi moja na dhana ya "sauti." Hili ni kosa la kuchanganya pamoja kada za vitu visivyopaswa kuwekwa pamoja.

Yaani, “we say that one has committed a category mistake when she ascribes, to a certain entity, a property or properties which that entity could not have... [meaning that] one locates some entity in a category it does not belong.” (Bernard Matolino, Personhood in African Philosophy (Dorpspruit: Cluster Publications; 2014, p. 142)

Hivyo, mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti ni kada nne za watu, kila kada ikiwa na tabia na sifa zake zinazoitofautisha.

Kupuuzia ukweli huu ni kufanya kosa la kuchanganya kada za vitu kwa kuvivisha baadhi ya vitu sifa visivyokuwa nazo.

Maana ya kwanza ya ushoga ni uhomofilia

Kwa upande mmoja, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "uhomofilia," ambayo ni sifa ya kimaumbile, kama ulivyo ufupi na urefu, weupe na weusi, ualibino na siualibino, njia pekee ya kupambana, kama anavyopendekeza, na "ushoga" ni kuwaua "mashoga" hao.

Hivyo, Bagonza hapa anahubiri tabia hatari ya uhomofobia. Sijui kama alitafakari vema juu ya uwezekano huu.

Lakini, pia Bagonza anapswa kutoa sababu nzuri ya kupambana na mahomofilia na kuacha kupambana na mazeruzeru, watu wenye tatizo la colour blindness, na matabaka ya pembezoni kama hayo.

Wote hawa wako hivyo kwa sababu za kimaumbile. Hawakuchagua hali zao.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [mahomofiliki] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea."

Kwa maoni haya ya Bagonza, hata "mahomofilia" wasio na tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi. Kwa kiwango hiki maoni yake nayapinga.

Urefu, ufupi, sauti nene, sauti nyororo, umashoto, umakengeza, uzeruzeru, colour blindness, na ladhalika, ni sifa asilia walizo nazo watu kadhaa.

Lakini watu hawa hawapotezi haki zao za kibayolojia, kisaikosomatika, kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa sababu hiyo pekee.

Huenda Bagonza hauoni ukweli huu kwa sababu anaongea kama mwanateolojia. Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii mseto sio mradi wa wanateolojia pekee, kama nitakavyoeleza hapa chini baadaye.


Maana ya pili ya ushoga ni ulawiti

Kwa upande mwingine, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" kuna maswali ya kitafiti anapswa kutusaidia kuyajibu.

Tangu tupate uhuru tumefanya sensa mara tano. Hakuna takwimu za serikali zinaonyesha idadi ya mashoga nchini.

KIla mwaka serikali kupitia jeshi la Polisi na Idara ya takwimu (NBS) wanatoa takwimu za uhalifu kupitia kitabu kiitwacho TANZANIA IN FIGURES. Huku pia idadi ya mashoga haitajwi.

Lakini takwimu za mwaka 2021 zinaonyesha kuwa yalikuwepo matukio ya ulawiti 1,296.

Taarifa hiyo haisemi kama ulawiti huu ulifanywa dhidi ya wanaume au kama wanawake au kama ulifanywa na mashoga.

Lakini bado Bagonza anasema hakubaliani "na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya" kwa sababu tayari "hapa kwetu mbona hali inatisha," anasema.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [walawiti] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke"

Kwa maoni ya Bagonza, "mahomofilia" wenye tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi kwa sabavu ya uhalifu wao.

Sawa. Lakini msimamo huu haupaswi kuishia kwa wahalifu wa ulawiti pekee. Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya kila mwala, iitwayo Tanzania in Figures, kuna makundi mengi ya uhalifu na yote yanapaswa kumulikwa na serikali.

Bagonza angeeleweka sana kama angesema hivi: "imebaki kidogo [wahalifu] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke."

Kwa kiwango hiki ningekubaliana naye Bagonza. Hapa kuna wezi, wala rushwa, watu wanaotelekeza watoto mitaani, wafanya biashara ya binadamu, wateka watu, na orodha inaendelea.

Na takwimu halisi za kiserikali kupitia taarifa ya Tanzania in Figures ya kila mwaka, zinaonyesha kuwa baadhi ya watu hawa tayari wana makanisa, wengine ni wamiliki wa vyombo vya habari, wengine ni maaskofu kuanzia makanisa ya kipentekoste hadi Kanisa Katoliki, wengine ni wachungaji, na Bagonza anaujua ukweli huu fika.

Lakini bado Bagonza kaamua kuibuka na habari ya "ushoga" isiyo na takwimu za kitafiti.

Angeleweka na kukubalika zaidi kama angesema kuna "mashoga" wangapi kwenye kaya yake, ukoo wake, kijiji/mtaa wake wa Mwisho wa Lami, kata yake ya Kayanga, wilaya yake ya Karagwe na mkoa wake wa Kagera. Hakutoa takwimu zozote katika ngazi hizi.


Hivyo, napenda kumkumbusha kuwa, sifa tata za kimaumbile hazifuti haki za msingi za mahomofilia, maalibino, mashoto, na wenye makengeza, nk.

Sifa hizo ni kama vile haki ya kuishi, kujumuika, kugombea nafasi za kisiasa, kupiga kura, kuabudu, kulindwa na serikali, na haki baki za kibinadamu.


Changamoto ya social constructionism

Kwa maoni yangu, tamko la Bagonza linaambatana na makosa mawili ya kimantiki: equivocation and category mistake.

Bahati mbaya, kwa sehemu kubwa, hadhira inayomsikiliza Bagonza, haina weledi wa kuyabaini haya makosa.

Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii yenye utulivu na amani inapaswa kuongozwa na kanuni bora za usanifu, utetezi na ubomozi wa hoja.

Vinginevyo tutawalisha watu matango pori, na kupanda magugu katika Taifa letu. Sio haki.

Ukisoma vizuri mawazo ya Bagonza utaona kuwa yanaongozwa na kanuni za kambi ya wanazuoni makuwadi wa nadharia ya social constructionism, yaani nadharia za ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu, kama vile Profesa John Rogers Searle (Amerika).

Katika maandiko yake, John Rogers Searle’s kuhusu ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu (social ontology), anatala kanuni kadhaa kuhusiana na ujio wa ukweli wa kijamii (social reality).

Kanuni moja inahusu "collective intentionality," nyingine inahusu "the assignment of status functions," na kanuni ya tatu inahusu "constitutive rules." Ninataka kuongelea hii kanuni ya tatu, ambayo ni kanuni ya kubuni na kutumia alama.


Kanuni hii inasema hivi: watu wanaweza kukaa wakakubaliana kwamba katika mazingira haya (X), kitu hiki (Y) kitakuwa alama inayowakilisha kitu kile (Z), na mapatano haya yatakoma pale watakapokaa tena na kukubaliana kuyabadilisha. (John R. Searle, Speech acts: An essay in the philosophy of language (Cambridge University Press; 1969, p. 34))

Mfano wake muhimu ni jumuiya ya wanampira waliokubaliana kuwa, katika mazigira ya uwanja wa mpira wa miguu (X), mchezaji akipokea mpira wakati anaelekea kufunga kwenye goli la mpizani wake wakati mbele yake hakuna mchezaji wa timu pinzani (Y), basi hilo ni kosa linaitwa offside (Z).

Kanuni hii inafaa kwenye mpira wa miguu pekee, na sio kwenye mpira wa mikono wala kwenye mpira wa kikapu.

Kwa hiyo, ikitokea siku wachezaji wa michezo yote hii wakajikuta wako pamoja kwa ajili ya mchezo mmoja, itabidi waunde kanuni mpya zinazokubalika kwa wote na kuwafaa wote. Ni vivyo hivyo kwenye maisha ya jamii mseto.

Yaani, kanuni zenye kutokana na mchakato wa mapatano ya kijamii (social constructionism) zinaweza kutumika kwenye jamii ya watu wenye imani moja, lakini sio kwenye jamii za leo ambako kuna utitiri wa kifikra (plural society).

Mfano, wakati wa Papa Yohanne Paulo II, baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki waliweka msimamo kwamba mahunta sio binadamu.

Mfano wa mwathirika ni Padre Selwyn Gross (jina la zamani la kiume) na baadaye Padre Sally Gross (jina jipya la kike), baada ya kubadilisha jinsia yake.

Hivyo, "Padre Sally Gross" aliyekuwa hunta (intersexual), alivuliwa upadre, kwa kuwa wanawake hawana haki ya kuwa mapadre.

Pia alifutiwa ubatizo kwa hoja kwamba mahunta sio binadamu, na hivyo hawana haki ya kubatizwa.

Lakini, sayansi mamboleo inathibitisha mahunta wana kromozomu 46 kama watu baki walioko kwenye ukoo wa homosapiensia.

Yaani kumwondoa Padre Sally kwenye tabaka la binadamu ulikuwa ni uamuzi wenye sura ya "category mistake."

Hivyo, Kanisa Katoliki sasa limejisahihishana halibebi tena mawazo yale potofu kuhusu hulka ya mahunta. Kanuni za maumbile ziliwaleta karibu na ukweli.

Kwa sasa bado Kanisa Katoliki linapambana na fundisho lake tata kwamba "a copulating pair is a biological organism"

Fundisho hili ni zao la mradi wa social constructionism wa miaka ya 1968, na ni fundisho linalopingana na kanuni za kibayolojia na kifalsafa.

Kifalsafa, neno "organism" lina maana tatu. Yaani "biological organism" kama vile binadamu na kondoo; "social organism" kama vile familia na timu a mpira; na "mechanical organism" kama vile gari au saa ya kuhesabu majira.

Ufanano wake ni kwamba, aina zote tatu ni mifumo yenye sehemu nyingi zinazofanya kazi kwa kushirikiana bila kupingana kwa ajili ya kufanikisha lengo la pamoja.

Tofauti kati ya "biological organism" kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine, "social organism" na "mechanical organism" ni kwamba, wakati "kanuni ya uratibu" iko ndani ya "biological organism," kauni hiyo iko nje ya "social organism" na "mechanical organism"

Tofauti kati ya "biological organism" na "social organism" ni kwamba, kiungo cha mwili wa "biological organism" kikikatwa kinakufa, lakini kiungo cha mwili wa "social organism" kikikatwa hakifi.

Mfano, mchezaji wa mpira wa miguu akipewa kadi nyekundi anaondoka uwanjani na anabaki hai. Lakini, mkono wako ukikatawa unaoza haraka.

Kwa upande mwingine uhai wa "social organism" unaanzia na kukomea kwenye mapatano ya kijamii kati ya wanachama husika. Lakini uhai wa "biological organism" hauko hivyo.

Na "mechanical organism" inaendeshwa na dereva ambaye sio sehemu yake. Mfano kujaza ufunguo kwenye saa ya kamani, kuendesha gari.

Kwa sababu hizi, sasa ulimwengu wa wanasayansi unakubaliana kwamba "a copulating pair is a social organism," na sio "biological organism," kama inavyodaiwa na baadhi ya makuwadi wa "teolojia ya mwili mmoja," yaani, "theology of one bodily union"

Lakini bado mijadala inaendelea na wataalam wa falsafa ya kibayolojia (philosophical biology) hapa wamesaidia sana kuleta mapinduzi ya kifikra yanayotakiwa kuhusiana na swali hili hapa: "what is biological individuality?"

Msingi wa kimetafizikia wa kanuni za maadili asilia, sio nadharia ya ukweli uliofinyangwa na watu na utakaokufa pale watu watakapokubaliana kuukataa (social constructionism), bali nadharia ya ukweli unaogunduliwa na watu na utakaoendelea kuwepo hata kama watu wataukataa (social realism).

Hitimisho na mapendekezo

Kwa hiyo, njia pekee ya kujenga imani ya jamii inayokubalika kwa watu wote katika jamii yenye mapokeo mseto sio kutumia kanuni za social constructionism zinazoanzia kwenye "kanuni za taharuki ya kijamii isiyo na uhalali" (unwarranted moral panic)

Badala yake, tunapaswa kuanzia kwenye kanuni za maadili asilia yanayoweza, na yanayopaswa, kuthibitika kwa njia ya urazini huru miongoni mwa umma mpana (public reason).

Bila kukubaliana na ukweli huu, kazi ya ujenzi wa imani ya jamii yenye imani mseto itakwama, maana mwafaka wa kijamii ni ajenda ya mpito tu.

Mwisho, niseme tu kuwa, katika mradi huu wa kujenga imani ya jamii, kila mdau, yaani wanateolojia, wanasayansi asilia, wanasayansi ya jamii, wanafalsafa, wanasasiolojia, wanahistoria, na wanazuoni baki wanayo nafasi.

Lakini, mchango wa kila mmoja una mipaka inayokamilishwa na michango ya wenzake.

Mfano, kwenye Safina ya Nuhu tunaambiwa kuwa Nuhu aliagizwa kuweka kila kiumbe kwa kuzingatia kanuni ya ME na KE.

Lakini, leo hii sayansi inatwambia kuwa kuna viumbe havina mgawanyo huo wa ME na KE. Mfano ni minyoo. Kwa hiyo, mwandishi wa Agano la Kale hakuwa na habari ya ukweli huu wa viumbe wasio na mgawanyo wa jinsia ya ME na KE.

Na hii maana yeke ni kwamba, wanateolojia wanaofanya udadavuzi kwa kuanzia kwenye Biblia wanahitaji kuelimishwa na wanabayolojia katika suala ya asexual reporoduction. Biblia haina mamlaka katika jambo hili.

Sote tunakamilishana kimaarifa, na hivyo kuna haja ya kuunganisha nguvu katika kufanikisha mradi wa kujenga imani ya jamii yenye utulivu, haki na amani.

Tujenge hoja bila mihemuko wala taharuki.
 
View attachment 2438877
Profesa John Searle, mtalaama wa social constructionism iliyo msingi wa maadili yanayobadilika kwa sababu ya mazingira na iliyo mbadala kwa social realism iliyo msingi wa maadili yasiyobadilika kwa sababu ya mazingira

Leo, kupitia mitandai ya kijamii, Benson Bagonza ameripotiwa kutamka kauli zifuatazo:

"Sikubaliani na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya. Hapa kwetu [Tanzania] tayari hali inatisha. Imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, na serikali itaufyata. Wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea. Tuamke."

Ama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" au "uhomofilia."

Mtu mmwenye tatizo la uhomofilia anaitwa homofiliki. Sio kila mlawiti ni homofiliki na sio kila homofiliki ni mlawiti.

Yaani kuna mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti. Hizi ni kada nne za watu, lakini Bagonza haonekani kuzitofautisha.

Bagonza anahimiza mapambano dhidi ya makundi yote manne, na hivyo kuhamasisha uhomofobia katika jamii. Sio sawa.

Hivyo kuna haja ya kujadili mawazo yake ili kusafisha akili za watumiaji wa mitandao ya kijamii. Naanza kwa kuonyesha makosa yake ya kimantiki.

Tatizo la Upindifu wa kimantiki

Upindifu wa kimantiki, yaani logical fallacy, ni kosa la kimantiki ambapo mwongeaji hutunga hoja inayokiuka misingi bora ya usanifu wa hoja na uendeshaji wa mijadala.

Mifano ya upindifu wa kimantiki ni tabia ya kutumia neno lenye maana nyingi bila kueleza maana inayoikusudiwa na mwongeaji (equivocation).

Mfano ni neno "ushoga" lenye maana mbili, yaani "ulawiti" au "uhomofilia."

Uhomofilia ni hali ya mtu kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsia yake. Na "ulawiti" ni tabia ya kufanya ngono kwa kuingiza jenitalia ya kiume kwenye rektamu.

Mfano mwingine wa Upindifu wa kimantiki ni kuongelea kitu kilicho kwenye tabaka moja, kwa kukibebesha kimakosa sifa za kitu baki kilicho kwenye tabaka jingine (category mistake).

Mfano, sauti iko katika tabaka la vitu vinavyosikika, wakati harufu iko katika tabaka la vitu vinavyonuka. Lakini, mara nyingi utasikia watu wanasema, "nasikia harufu ya chakula."

Maneno haya yanaiweka dhana ya "harufu" katika kundi moja na dhana ya "sauti." Hili ni kosa la kuchanganya pamoja kada za vitu visivyopaswa kuwekwa pamoja.

Yaani, “we say that one has committed a category mistake when she ascribes, to a certain entity, a property or properties which that entity could not have... [meaning that] one locates some entity in a category it does not belong.” (Bernard Matolino, Personhood in African Philosophy (Dorpspruit: Cluster Publications; 2014, p. 142)

Hivyo, mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti ni kada nne za watu, kila kada ikiwa na tabia na sifa zake zinazoitofautisha.

Kupuuzia ukweli huu ni kufanya kosa la kuchanganya kada za vitu kwa kuvivisha baadhi ya vitu sifa visivyokuwa nazo.

Maana ya kwanza ya ushoga ni uhomofilia

Kwa upande mmoja, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "uhomofilia," ambayo ni sifa ya kimaumbile, kama ulivyo ufupi na urefu, weupe na weusi, ualibino na siualibino, njia pekee ya kupambana, kama anavyopendekeza, na "ushoga" ni kuwaua "mashoga" hao.

Hivyo, Bagonza hapa anahubiri tabia hatari ya uhomofobia. Sijui kama alitafakari vema juu ya uwezekano huu.

Lakini, pia Bagonza anapswa kutoa sababu nzuri ya kupambana na mahomofilia na kuacha kupambana na mazeruzeru, watu wenye tatizo la colour blindness, na matabaka ya pembezoni kama hayo.

Wote hawa wako hivyo kwa sababu za kimaumbile. Hawakuchagua hali zao.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [mahomofiliki] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea."

Kwa maoni haya ya Bagonza, hata "mahomofilia" wasio na tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi. Kwa kiwango hiki maoni yake nayapinga.

Urefu, ufupi, sauti nene, sauti nyororo, umashoto, umakengeza, uzeruzeru, colour blindness, na ladhalika, ni sifa asilia walizo nazo watu kadhaa.

Lakini watu hawa hawapotezi haki zao za kibayolojia, kisaikosomatika, kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa sababu hiyo pekee.

Huenda Bagonza hauoni ukweli huu kwa sababu anaongea kama mwanateolojia. Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii mseto sio mradi wa wanateolojia pekee, kama nitakavyoeleza hapa chini baadaye.


Maana ya pili ya ushoga ni ulawiti

Kwa upande mwingine, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" kuna maswali ya kitafiti anapswa kutusaidia kuyajibu.

Tangu tupate uhuru tumefanya sensa mara tano. Hakuna takwimu za serikali zinaonyesha idadi ya mashoga nchini.

KIla mwaka serikali kupitia jeshi la Polisi na Idara ya takwimu (NBS) wanatoa takwimu za uhalifu kupitia kitabu kiitwacho TANZANIA IN FIGURES. Huku pia idadi ya mashoga haitajwi.

Lakini takwimu za mwaka 2021 zinaonyesha kuwa yalikuwepo matukio ya ulawiti 1,296.

Taarifa hiyo haisemi kama ulawiti huu ulifanywa dhidi ya wanaume au kama wanawake au kama ulifanywa na mashoga.

Lakini bado Bagonza anasema hakubaliani "na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya" kwa sababu tayari "hapa kwetu mbona hali inatisha," anasema.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [walawiti] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke"

Kwa maoni ya Bagonza, "mahomofilia" wenye tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi kwa sabavu ya uhalifu wao.

Sawa. Lakini msimamo huu haupaswi kuishia kwa wahalifu wa ulawiti pekee. Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya kila mwala, iitwayo Tanzania in Figures, kuna makundi mengi ya uhalifu na yote yanapaswa kumulikwa na serikali.

Bagonza angeeleweka sana kama angesema hivi: "imebaki kidogo [wahalifu] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke."

Kwa kiwango hiki ningekubaliana naye Bagonza. Hapa kuna wezi, wala rushwa, watu wanaotelekeza watoto mitaani, wafanya biashara ya binadamu, wateka watu, na orodha inaendelea.

Na takwimu halisi za kiserikali kupitia taarifa ya Tanzania in Figures ya kila mwaka, zinaonyesha kuwa baadhi ya watu hawa tayari wana makanisa, wengine ni wamiliki wa vyombo vya habari, wengine ni maaskofu kuanzia makanisa ya kipentekoste hadi Kanisa Katoliki, wengine ni wachungaji, na Bagonza anaujua ukweli huu fika.

Lakini bado Bagonza kaamua kuibuka na habari ya "ushoga" isiyo na takwimu za kitafiti.

Angeleweka na kukubalika zaidi kama angesema kuna "mashoga" wangapi kwenye kaya yake, ukoo wake, kijiji/mtaa wake wa Mwisho wa Lami, kata yake ya Kayanga, wilaya yake ya Karagwe na mkoa wake wa Kagera. Hakutoa takwimu zozote katika ngazi hizi.


Hivyo, napenda kumkumbusha kuwa, sifa tata za kimaumbile hazifuti haki za msingi za mahomofilia, maalibino, mashoto, na wenye makengeza, nk.

Sifa hizo ni kama vile haki ya kuishi, kujumuika, kugombea nafasi za kisiasa, kupiga kura, kuabudu, kulindwa na serikali, na haki baki za kibinadamu.


Changamoto ya social constructionism

Kwa maoni yangu, tamko la Bagonza linaambatana na makosa mawili ya kimantiki: equivocation and category mistake.

Bahati mbaya, kwa sehemu kubwa, hadhira inayomsikiliza Bagonza, haina weledi wa kuyabaini haya makosa.

Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii yenye utulivu na amani inapaswa kuongozwa na kanuni bora za usanifu, utetezi na ubomozi wa hoja.

Vinginevyo tutawalisha watu matango pori, na kupanda magugu katika Taifa letu. Sio haki.

Ukisoma vizuri mawazo ya Bagonza utaona kuwa yanaongozwa na kanuni za kambi ya wanazuoni makuwadi wa nadharia ya social constructionism, yaani nadharia za ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu, kama vile Profesa John Rogers Searle (Amerika).

Katika maandiko yake, John Rogers Searle’s kuhusu ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu (social ontology), anatala kanuni kadhaa kuhusiana na ujio wa ukweli wa kijamii (social reality).

Kanuni moja inahusu "collective intentionality," nyingine inahusu "the assignment of status functions," na kanuni ya tatu inahusu "constitutive rules." Ninataka kuongelea hii kanuni ya tatu, ambayo ni kanuni ya kubuni na kutumia alama.


Kanuni hii inasema hivi: watu wanaweza kukaa wakakubaliana kwamba katika mazingira haya (X), kitu hiki (Y) kitakuwa alama inayowakilisha kitu kile (Z), na mapatano haya yatakoma pale watakapokaa tena na kukubaliana kuyabadilisha. (John R. Searle, Speech acts: An essay in the philosophy of language (Cambridge University Press; 1969, p. 34))

Mfano wake muhimu ni jumuiya ya wanampira waliokubaliana kuwa, katika mazigira ya uwanja wa mpira wa miguu (X), mchezaji akipokea mpira wakati anaelekea kufunga kwenye goli la mpizani wake wakati mbele yake hakuna mchezaji wa timu pinzani (Y), basi hilo ni kosa linaitwa offside (Z).

Kanuni hii inafaa kwenye mpira wa miguu pekee, na sio kwenye mpira wa mikono wala kwenye mpira wa kikapu.

Kwa hiyo, ikitokea siku wachezaji wa michezo yote hii wakajikuta wako pamoja kwa ajili ya mchezo mmoja, itabidi waunde kanuni mpya zinazokubalika kwa wote na kuwafaa wote. Ni vivyo hivyo kwenye maisha ya jamii mseto.

Yaani, kanuni zenye kutokana na mchakato wa mapatano ya kijamii (social constructionism) zinaweza kutumika kwenye jamii ya watu wenye imani moja, lakini sio kwenye jamii za leo ambako kuna utitiri wa kifikra (plural society).

Mfano, wakati wa Papa Yohanne Paulo II, baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki waliweka msimamo kwamba mahunta sio binadamu.

Mfano wa mwathirika ni Padre Selwyn Gross (jina la zamani la kiume) na baadaye Padre Sally Gross (jina jipya la kike), baada ya kubadilisha jinsia yake.

Hivyo, "Padre Sally Gross" aliyekuwa hunta (intersexual), alivuliwa upadre, kwa kuwa wanawake hawana haki ya kuwa mapadre.

Pia alifutiwa ubatizo kwa hoja kwamba mahunta sio binadamu, na hivyo hawana haki ya kubatizwa.

Lakini, sayansi mamboleo inathibitisha mahunta wana kromozomu 46 kama watu baki walioko kwenye ukoo wa homosapiensia.

Yaani kumwondoa Padre Sally kwenye tabaka la binadamu ulikuwa ni uamuzi wenye sura ya "category mistake."

Hivyo, Kanisa Katoliki sasa limejisahihishana halibebi tena mawazo yale potofu kuhusu hulka ya mahunta. Kanuni za maumbile ziliwaleta karibu na ukweli.

Kwa sasa bado Kanisa Katoliki linapambana na fundisho lake tata kwamba "a copulating pair is a biological organism"

Fundisho hili ni zao la mradi wa social constructionism wa miaka ya 1968, na ni fundisho linalopingana na kanuni za kibayolojia na kifalsafa.

Kifalsafa, neno "organism" lina maana tatu. Yaani "biological organism" kama vile binadamu na kondoo; "social organism" kama vile familia na timu a mpira; na "mechanical organism" kama vile gari au saa ya kuhesabu majira.

Ufanano wake ni kwamba, aina zote tatu ni mifumo yenye sehemu nyingi zinazofanya kazi kwa kushirikiana bila kupingana kwa ajili ya kufanikisha lengo la pamoja.

Tofauti kati ya "biological organism" kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine, "social organism" na "mechanical organism" ni kwamba, wakati "kanuni ya uratibu" iko ndani ya "biological organism," kauni hiyo iko nje ya "social organism" na "mechanical organism"

Tofauti kati ya "biological organism" na "social organism" ni kwamba, kiungo cha mwili wa "biological organism" kikikatwa kinakufa, lakini kiungo cha mwili wa "social organism" kikikatwa hakifi.

Mfano, mchezaji wa mpira wa miguu akipewa kadi nyekundi anaondoka uwanjani na anabaki hai. Lakini, mkono wako ukikatawa unaoza haraka.

Kwa upande mwingine uhai wa "social organism" unaanzia na kukomea kwenye mapatano ya kijamii kati ya wanachama husika. Lakini uhai wa "biological organism" hauko hivyo.

Na "mechanical organism" inaendeshwa na dereva ambaye sio sehemu yake. Mfano kujaza ufunguo kwenye saa ya kamani, kuendesha gari.

Kwa sababu hizi, sasa ulimwengu wa wanasayansi unakubaliana kwamba "a copulating pair is a social organism," na sio "biological organism," kama inavyodaiwa na baadhi ya makuwadi wa "teolojia ya mwili mmoja," yaani, "theology of one bodily union"

Lakini bado mijadala inaendelea na wataalam wa falsafa ya kibayolojia (philosophical biology) hapa wamesaidia sana kuleta mapinduzi ya kifikra yanayotakiwa kuhusiana na swali hili hapa: "what is biological individuality?"

Msingi wa kimetafizikia wa kanuni za maadili asilia, sio nadharia ya ukweli uliofinyangwa na watu na utakaokufa pale watu watakapokubaliana kuukataa (social constructionism), bali nadharia ya ukweli unaogunduliwa na watu na utakaoendelea kuwepo hata kama watu wataukataa (social realism).

Hitimisho na mapendekezo

Kwa hiyo, njia pekee ya kujenga imani ya jamii inayokubalika kwa watu wote katika jamii yenye mapokeo mseto sio kutumia kanuni za social constructionism zinazoanzia kwenye "kanuni za taharuki ya kijamii isiyo na uhalali" (unwarranted moral panic)

Badala yake, tunapaswa kuanzia kwenye kanuni za maadili asilia yanayoweza, na yanayopaswa, kuthibitika kwa njia ya urazini huru miongoni mwa umma mpana (public reason).

Bila kukubaliana na ukweli huu, kazi ya ujenzi wa imani ya jamii yenye imani mseto itakwama, maana mwafaka wa kijamii ni ajenda ya mpito tu.

Mwisho, niseme tu kuwa, katika mradi huu wa kujenga imani ya jamii, kila mdau, yaani wanateolojia, wanasayansi asilia, wanasayansi ya jamii, wanafalsafa, wanasasiolojia, wanahistoria, na wanazuoni baki wanayo nafasi.

Lakini, mchango wa kila mmoja una mipaka inayokamilishwa na michango ya wenzake.

Mfano, kwenye Safina ya Nuhu tunaambiwa kuwa Nuhu aliagizwa kuweka kila kiumbe kwa kuzingatia kanuni ya ME na KE.

Lakini, leo hii sayansi inatwambia kuwa kuna viumbe havina mgawanyo huo wa ME na KE. Mfano ni minyoo. Kwa hiyo, mwandishi wa Agano la Kale hakuwa na habari ya ukweli huu wa viumbe wasio na mgawanyo wa jinsia ya ME na KE.

Na hii maana yeke ni kwamba, wanateolojia wanaofanya udadavuzi kwa kuanzia kwenye Biblia wanahitaji kuelimishwa na wanabayolojia katika suala ya asexual reporoduction. Biblia haina mamlaka katika jambo hili.

Sote tunakamilishana kimaarifa, na hivyo kuna haja ya kuunganisha nguvu katika kufanikisha mradi wa kujenga imani ya jamii yenye utulivu, haki na amani.

Tujenge hoja bila mihemuko wala taharuki.
Mbona jambo lote umelihusisha na ukirisitu na kuutenga uisilamu, yeye anajielekeza kwa wasio wanasheria kama wewe, ila nawe umetumia neno la kidikiteta la kuwafunga watu midomo "taharuki".
 
Makala ni ndefu lakini inavutia kuisoma mpaka mwisho. Imeandikwa kitaalamu na bila shaka toka kwa mtaalam wa Saikolojia.

Jambo moja kubwa nililolipata hapa, kwa lugha rahisi ni kwamba kuna mashoga wa kuzaliwa. Wamezaliwa na kasoro za kimaumbile, hisia au vyote kwa pamoja.

Moja ya sababu za kitaalam zinazotufanya kuwa na hisia mbalimbali zikiwemo za kuvutiwa kimapenzi ni hormones. Watu wenye hormones inbalance lazima na hisia zao haziwi za kawaida. Mathalani mtu ambaye ni mwanamke kimaumbile lakini mwenye hormones nyingi za kiume, atakuwa na hisia zaidi za kiume, hisia za kupenda kumiliki kuliko kumilikiwa. Na hawa katika mahusiano yao ya ushoga huwa wanakuwa ndiyo wanaume wa wenzao japo wote, kimaumbile ni wanawake.

Kwa upande mwingine, wanaume wenye hormones nyingi za kike, hisia zao huegemea zaidi kwenye ukike, ikiwa ni pamoja na kupenda kutunzwa na kumilikiwa.

Lakini wapo wale wanaojiingiza huko, labda kwa sababu ya kupewa fedha au kuhudumiwa, watafuta mteremko. Yaani dada ni mzima kabisa, lakini kwa vile amempata dada mwenzake mwenye uwezo lakini mwenye hisia za kiume, anakubali kuwa mke wa mwanamke mwenzake kwa vile tu anahudumiwa kwa kila kitu.

Lakini wapo walawiti, ni mwanaume kamili kabisa, labda kwa kujizoesha au kushawishiwa anakuwa mlawiti au mlawitiwa. Au dada mzuri kabisa, tena timilifu, kwa vile amempata mwanaume mlawiti anakubali kulawitiwa. Na huenda hawa ndio wengi zaidi.

Wale wa kundi la kwanza ni walemavu. Walemavu wa namna hii wasaidiwe kwa namna gani?

Kundi hili la pili ni wahalifu. Kiimani, ni wahalifu sawa na majambazi, wazinzi, waabudu sanamu/mizimu, waongo, mafisadi, n.k.

Tena kwenye biblia imeandikwa:

1Wakoritho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafilaji, wala walawiti,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Wale wa kundi la pili wanatakiwa kudhibitiwa, lakini wale wa kundi la kwanza wanatakiwa kusaidiwa, na bila shaka wapo wanaosaidiwa kitabibu, japo ni dhahiri suluhusho kamili halijapatikana. Ninaamini kosa kubwa linalofanyika ni kulikataa kuwa hili ni tatizo, na tukaishia kwa vile wana hisia hizo, basi kama jamii tukubali kuwa hali hiyo ni ya kawaida, na hivyo hakuna haja ya kuihangaikia, tuwaache waendelee na mahusiano yao ya jinsia moja.

View attachment 2438877
Profesa John Searle, mtalaama wa social constructionism iliyo msingi wa maadili yanayobadilika kwa sababu ya mazingira na iliyo mbadala kwa social realism iliyo msingi wa maadili yasiyobadilika kwa sababu ya mazingira

Leo, kupitia mitandai ya kijamii, Benson Bagonza ameripotiwa kutamka kauli zifuatazo:

"Sikubaliani na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya. Hapa kwetu [Tanzania] tayari hali inatisha. Imebaki kidogo mashoga wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, na serikali itaufyata. Wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea. Tuamke."

Ama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" au "uhomofilia."

Mtu mmwenye tatizo la uhomofilia anaitwa homofiliki. Sio kila mlawiti ni homofiliki na sio kila homofiliki ni mlawiti.

Yaani kuna mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti. Hizi ni kada nne za watu, lakini Bagonza haonekani kuzitofautisha.

Bagonza anahimiza mapambano dhidi ya makundi yote manne, na hivyo kuhamasisha uhomofobia katika jamii. Sio sawa.

Hivyo kuna haja ya kujadili mawazo yake ili kusafisha akili za watumiaji wa mitandao ya kijamii. Naanza kwa kuonyesha makosa yake ya kimantiki.

Tatizo la Upindifu wa kimantiki

Upindifu wa kimantiki, yaani logical fallacy, ni kosa la kimantiki ambapo mwongeaji hutunga hoja inayokiuka misingi bora ya usanifu wa hoja na uendeshaji wa mijadala.

Mifano ya upindifu wa kimantiki ni tabia ya kutumia neno lenye maana nyingi bila kueleza maana inayoikusudiwa na mwongeaji (equivocation).

Mfano ni neno "ushoga" lenye maana mbili, yaani "ulawiti" au "uhomofilia."

Uhomofilia ni hali ya mtu kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsia yake. Na "ulawiti" ni tabia ya kufanya ngono kwa kuingiza jenitalia ya kiume kwenye rektamu.

Mfano mwingine wa Upindifu wa kimantiki ni kuongelea kitu kilicho kwenye tabaka moja, kwa kukibebesha kimakosa sifa za kitu baki kilicho kwenye tabaka jingine (category mistake).

Mfano, sauti iko katika tabaka la vitu vinavyosikika, wakati harufu iko katika tabaka la vitu vinavyonuka. Lakini, mara nyingi utasikia watu wanasema, "nasikia harufu ya chakula."

Maneno haya yanaiweka dhana ya "harufu" katika kundi moja na dhana ya "sauti." Hili ni kosa la kuchanganya pamoja kada za vitu visivyopaswa kuwekwa pamoja.

Yaani, “we say that one has committed a category mistake when she ascribes, to a certain entity, a property or properties which that entity could not have... [meaning that] one locates some entity in a category it does not belong.” (Bernard Matolino, Personhood in African Philosophy (Dorpspruit: Cluster Publications; 2014, p. 142)

Hivyo, mlawiti homofiliki, mlawiti asiye homofiliki, homofiliki mlawiti, na homofiliki asiye mlawiti ni kada nne za watu, kila kada ikiwa na tabia na sifa zake zinazoitofautisha.

Kupuuzia ukweli huu ni kufanya kosa la kuchanganya kada za vitu kwa kuvivisha baadhi ya vitu sifa visivyokuwa nazo.

Maana ya kwanza ya ushoga ni uhomofilia

Kwa upande mmoja, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "uhomofilia," ambayo ni sifa ya kimaumbile, kama ulivyo ufupi na urefu, weupe na weusi, ualibino na siualibino, njia pekee ya kupambana, kama anavyopendekeza, na "ushoga" ni kuwaua "mashoga" hao.

Hivyo, Bagonza hapa anahubiri tabia hatari ya uhomofobia. Sijui kama alitafakari vema juu ya uwezekano huu.

Lakini, pia Bagonza anapswa kutoa sababu nzuri ya kupambana na mahomofilia na kuacha kupambana na mazeruzeru, watu wenye tatizo la colour blindness, na matabaka ya pembezoni kama hayo.

Wote hawa wako hivyo kwa sababu za kimaumbile. Hawakuchagua hali zao.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [mahomofiliki] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itanywea."

Kwa maoni haya ya Bagonza, hata "mahomofilia" wasio na tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi. Kwa kiwango hiki maoni yake nayapinga.

Urefu, ufupi, sauti nene, sauti nyororo, umashoto, umakengeza, uzeruzeru, colour blindness, na ladhalika, ni sifa asilia walizo nazo watu kadhaa.

Lakini watu hawa hawapotezi haki zao za kibayolojia, kisaikosomatika, kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa sababu hiyo pekee.

Huenda Bagonza hauoni ukweli huu kwa sababu anaongea kama mwanateolojia. Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii mseto sio mradi wa wanateolojia pekee, kama nitakavyoeleza hapa chini baadaye.


Maana ya pili ya ushoga ni ulawiti

Kwa upande mwingine, kama Bagonza anatumia neno "ushoga" kumaanisha "ulawiti" kuna maswali ya kitafiti anapswa kutusaidia kuyajibu.

Tangu tupate uhuru tumefanya sensa mara tano. Hakuna takwimu za serikali zinaonyesha idadi ya mashoga nchini.

KIla mwaka serikali kupitia jeshi la Polisi na Idara ya takwimu (NBS) wanatoa takwimu za uhalifu kupitia kitabu kiitwacho TANZANIA IN FIGURES. Huku pia idadi ya mashoga haitajwi.

Lakini takwimu za mwaka 2021 zinaonyesha kuwa yalikuwepo matukio ya ulawiti 1,296.

Taarifa hiyo haisemi kama ulawiti huu ulifanywa dhidi ya wanaume au kama wanawake au kama ulifanywa na mashoga.

Lakini bado Bagonza anasema hakubaliani "na wanaodhani ushoga ni tatizo la Ulaya" kwa sababu tayari "hapa kwetu mbona hali inatisha," anasema.

Bagonza anasema kuwa "imebaki kidogo [walawiti] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke"

Kwa maoni ya Bagonza, "mahomofilia" wenye tabia ya kufanya "ulawiti" hawana haki hizi kwa sabavu ya uhalifu wao.

Sawa. Lakini msimamo huu haupaswi kuishia kwa wahalifu wa ulawiti pekee. Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya kila mwala, iitwayo Tanzania in Figures, kuna makundi mengi ya uhalifu na yote yanapaswa kumulikwa na serikali.

Bagonza angeeleweka sana kama angesema hivi: "imebaki kidogo [wahalifu] wataunda umoja, watajenga nyumba zao za ibada, ... wataunda chama chao na kuwania uongozi, na serikali itaufyata. Tuamke."

Kwa kiwango hiki ningekubaliana naye Bagonza. Hapa kuna wezi, wala rushwa, watu wanaotelekeza watoto mitaani, wafanya biashara ya binadamu, wateka watu, na orodha inaendelea.

Na takwimu halisi za kiserikali kupitia taarifa ya Tanzania in Figures ya kila mwaka, zinaonyesha kuwa baadhi ya watu hawa tayari wana makanisa, wengine ni wamiliki wa vyombo vya habari, wengine ni maaskofu kuanzia makanisa ya kipentekoste hadi Kanisa Katoliki, wengine ni wachungaji, na Bagonza anaujua ukweli huu fika.

Lakini bado Bagonza kaamua kuibuka na habari ya "ushoga" isiyo na takwimu za kitafiti.

Angeleweka na kukubalika zaidi kama angesema kuna "mashoga" wangapi kwenye kaya yake, ukoo wake, kijiji/mtaa wake wa Mwisho wa Lami, kata yake ya Kayanga, wilaya yake ya Karagwe na mkoa wake wa Kagera. Hakutoa takwimu zozote katika ngazi hizi.


Hivyo, napenda kumkumbusha kuwa, sifa tata za kimaumbile hazifuti haki za msingi za mahomofilia, maalibino, mashoto, na wenye makengeza, nk.

Sifa hizo ni kama vile haki ya kuishi, kujumuika, kugombea nafasi za kisiasa, kupiga kura, kuabudu, kulindwa na serikali, na haki baki za kibinadamu.


Changamoto ya social constructionism

Kwa maoni yangu, tamko la Bagonza linaambatana na makosa mawili ya kimantiki: equivocation and category mistake.

Bahati mbaya, kwa sehemu kubwa, hadhira inayomsikiliza Bagonza, haina weledi wa kuyabaini haya makosa.

Lakini, kazi ya kujenga imani ya jamii yenye utulivu na amani inapaswa kuongozwa na kanuni bora za usanifu, utetezi na ubomozi wa hoja.

Vinginevyo tutawalisha watu matango pori, na kupanda magugu katika Taifa letu. Sio haki.

Ukisoma vizuri mawazo ya Bagonza utaona kuwa yanaongozwa na kanuni za kambi ya wanazuoni makuwadi wa nadharia ya social constructionism, yaani nadharia za ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu, kama vile Profesa John Rogers Searle (Amerika).

Katika maandiko yake, John Rogers Searle’s kuhusu ukweli wa kiontolojia unaotengenezwa na binadamu (social ontology), anatala kanuni kadhaa kuhusiana na ujio wa ukweli wa kijamii (social reality).

Kanuni moja inahusu "collective intentionality," nyingine inahusu "the assignment of status functions," na kanuni ya tatu inahusu "constitutive rules." Ninataka kuongelea hii kanuni ya tatu, ambayo ni kanuni ya kubuni na kutumia alama.


Kanuni hii inasema hivi: watu wanaweza kukaa wakakubaliana kwamba katika mazingira haya (X), kitu hiki (Y) kitakuwa alama inayowakilisha kitu kile (Z), na mapatano haya yatakoma pale watakapokaa tena na kukubaliana kuyabadilisha. (John R. Searle, Speech acts: An essay in the philosophy of language (Cambridge University Press; 1969, p. 34))

Mfano wake muhimu ni jumuiya ya wanampira waliokubaliana kuwa, katika mazigira ya uwanja wa mpira wa miguu (X), mchezaji akipokea mpira wakati anaelekea kufunga kwenye goli la mpizani wake wakati mbele yake hakuna mchezaji wa timu pinzani (Y), basi hilo ni kosa linaitwa offside (Z).

Kanuni hii inafaa kwenye mpira wa miguu pekee, na sio kwenye mpira wa mikono wala kwenye mpira wa kikapu.

Kwa hiyo, ikitokea siku wachezaji wa michezo yote hii wakajikuta wako pamoja kwa ajili ya mchezo mmoja, itabidi waunde kanuni mpya zinazokubalika kwa wote na kuwafaa wote. Ni vivyo hivyo kwenye maisha ya jamii mseto.

Yaani, kanuni zenye kutokana na mchakato wa mapatano ya kijamii (social constructionism) zinaweza kutumika kwenye jamii ya watu wenye imani moja, lakini sio kwenye jamii za leo ambako kuna utitiri wa kifikra (plural society).

Mfano, wakati wa Papa Yohanne Paulo II, baadhi ya viongozi wa Kanisa Katoliki waliweka msimamo kwamba mahunta sio binadamu.

Mfano wa mwathirika ni Padre Selwyn Gross (jina la zamani la kiume) na baadaye Padre Sally Gross (jina jipya la kike), baada ya kubadilisha jinsia yake.

Hivyo, "Padre Sally Gross" aliyekuwa hunta (intersexual), alivuliwa upadre, kwa kuwa wanawake hawana haki ya kuwa mapadre.

Pia alifutiwa ubatizo kwa hoja kwamba mahunta sio binadamu, na hivyo hawana haki ya kubatizwa.

Lakini, sayansi mamboleo inathibitisha mahunta wana kromozomu 46 kama watu baki walioko kwenye ukoo wa homosapiensia.

Yaani kumwondoa Padre Sally kwenye tabaka la binadamu ulikuwa ni uamuzi wenye sura ya "category mistake."

Hivyo, Kanisa Katoliki sasa limejisahihishana halibebi tena mawazo yale potofu kuhusu hulka ya mahunta. Kanuni za maumbile ziliwaleta karibu na ukweli.

Kwa sasa bado Kanisa Katoliki linapambana na fundisho lake tata kwamba "a copulating pair is a biological organism"

Fundisho hili ni zao la mradi wa social constructionism wa miaka ya 1968, na ni fundisho linalopingana na kanuni za kibayolojia na kifalsafa.

Kifalsafa, neno "organism" lina maana tatu. Yaani "biological organism" kama vile binadamu na kondoo; "social organism" kama vile familia na timu a mpira; na "mechanical organism" kama vile gari au saa ya kuhesabu majira.

Ufanano wake ni kwamba, aina zote tatu ni mifumo yenye sehemu nyingi zinazofanya kazi kwa kushirikiana bila kupingana kwa ajili ya kufanikisha lengo la pamoja.

Tofauti kati ya "biological organism" kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine, "social organism" na "mechanical organism" ni kwamba, wakati "kanuni ya uratibu" iko ndani ya "biological organism," kauni hiyo iko nje ya "social organism" na "mechanical organism"

Tofauti kati ya "biological organism" na "social organism" ni kwamba, kiungo cha mwili wa "biological organism" kikikatwa kinakufa, lakini kiungo cha mwili wa "social organism" kikikatwa hakifi.

Mfano, mchezaji wa mpira wa miguu akipewa kadi nyekundi anaondoka uwanjani na anabaki hai. Lakini, mkono wako ukikatawa unaoza haraka.

Kwa upande mwingine uhai wa "social organism" unaanzia na kukomea kwenye mapatano ya kijamii kati ya wanachama husika. Lakini uhai wa "biological organism" hauko hivyo.

Na "mechanical organism" inaendeshwa na dereva ambaye sio sehemu yake. Mfano kujaza ufunguo kwenye saa ya kamani, kuendesha gari.

Kwa sababu hizi, sasa ulimwengu wa wanasayansi unakubaliana kwamba "a copulating pair is a social organism," na sio "biological organism," kama inavyodaiwa na baadhi ya makuwadi wa "teolojia ya mwili mmoja," yaani, "theology of one bodily union"

Lakini bado mijadala inaendelea na wataalam wa falsafa ya kibayolojia (philosophical biology) hapa wamesaidia sana kuleta mapinduzi ya kifikra yanayotakiwa kuhusiana na swali hili hapa: "what is biological individuality?"

Msingi wa kimetafizikia wa kanuni za maadili asilia, sio nadharia ya ukweli uliofinyangwa na watu na utakaokufa pale watu watakapokubaliana kuukataa (social constructionism), bali nadharia ya ukweli unaogunduliwa na watu na utakaoendelea kuwepo hata kama watu wataukataa (social realism).

Hitimisho na mapendekezo

Kwa hiyo, njia pekee ya kujenga imani ya jamii inayokubalika kwa watu wote katika jamii yenye mapokeo mseto sio kutumia kanuni za social constructionism zinazoanzia kwenye "kanuni za taharuki ya kijamii isiyo na uhalali" (unwarranted moral panic)

Badala yake, tunapaswa kuanzia kwenye kanuni za maadili asilia yanayoweza, na yanayopaswa, kuthibitika kwa njia ya urazini huru miongoni mwa umma mpana (public reason).

Bila kukubaliana na ukweli huu, kazi ya ujenzi wa imani ya jamii yenye imani mseto itakwama, maana mwafaka wa kijamii ni ajenda ya mpito tu.

Mwisho, niseme tu kuwa, katika mradi huu wa kujenga imani ya jamii, kila mdau, yaani wanateolojia, wanasayansi asilia, wanasayansi ya jamii, wanafalsafa, wanasasiolojia, wanahistoria, na wanazuoni baki wanayo nafasi.

Lakini, mchango wa kila mmoja una mipaka inayokamilishwa na michango ya wenzake.

Mfano, kwenye Safina ya Nuhu tunaambiwa kuwa Nuhu aliagizwa kuweka kila kiumbe kwa kuzingatia kanuni ya ME na KE.

Lakini, leo hii sayansi inatwambia kuwa kuna viumbe havina mgawanyo huo wa ME na KE. Mfano ni minyoo. Kwa hiyo, mwandishi wa Agano la Kale hakuwa na habari ya ukweli huu wa viumbe wasio na mgawanyo wa jinsia ya ME na KE.

Na hii maana yeke ni kwamba, wanateolojia wanaofanya udadavuzi kwa kuanzia kwenye Biblia wanahitaji kuelimishwa na wanabayolojia katika suala ya asexual reporoduction. Biblia haina mamlaka katika jambo hili.

Sote tunakamilishana kimaarifa, na hivyo kuna haja ya kuunganisha nguvu katika kufanikisha mradi wa kujenga imani ya jamii yenye utulivu, haki na amani.

Tujenge hoja bila mihemuko wala taharuki.
Sioni kosa la Askofu Bagonza...

Yeye kaongelea ushoga kwa maana ya ushoga kwa ujumla wake...

Honestly, shoga ni shoga tu. Na tabia ya ushoga haikubaliki ktk jamii yetu kwa sababu ni kunyume cha maadili na utamaduni wetu. Aidha ni kinyume na imani zote za kiroho...

Kwa hiyo, narudia tena kusema, sijaona kosa la Askofu Bagonza. Na naamini kuwa kila mtu wa kawaida aliyemsikiliza kwa kiasi kikubwa amemwelewa askofu kuwa alikuwa anazungumzia ushoga (wanaume) na usagaji (wanawake) yaani ngono ya watu wa jinsi moja...

Wanaotafuta kasoro za ndani na za kimantiki ni sisi wasomi kama wewe Mama Amon na wengine. Otherwise, watu wa kawaida wamemwelewa vyema sana Askofu Bagonza...

Na kwa ndugu yangu Bams ni kweli kabisa wapo watu wenye matatizo haya ambayo ni ya kuzaliwa na hivyo kujikuta tu wana sura na maumbile ya kiume au kike lakini hormones zao zinavutia kwenye opposite sex...

Lakini hii haiondoi maana ya kuwa huo ni ushoga tu. Hawa nakubaliana na wewe kuwa, wanahitaji msaada...

Lakini kwa ujumla wake, ushoga haukubaliki ktk jamii yetu na Mungu hapendi kabisa tabia hizi...
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom