kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Nimekutana na Askari mmoja tulisoma wote primary miaka 1995, katika mazungumzo akanidokeza kwamba alifanikiwa kujiendeleza na Sasa Ni graduate kwa miaka minne Sasa ila analipwa nakutambulika kama sejini. Kumuuliza kwanini akasema wamewabania kuwapandisha na hata kutambua elimu zao. Anatamani uchaguzi huu ukamlete mtu anayeweza kuwatetea wasikae Tena miaka mitano bila elimu zao kutambulika wala kulipwa.
Jambo la pili akasema, anatamani Askari waache kujinunulia na kushona uniform kwa gharama zao wenyewe. Kipindi Cha nyuma walikuwa wanashonewa uniform ila Sasa hivi wameachwa wajitaftie wenyewe. Ana kiu yakuona thamani yao nakuwapa stahiki zao.
Jambo la tatu, nyumba hazitoshi na wanaokaa uraiani awalipiwi Kodi ya nyumba. Umeme maeneo mengine wanajinunulia tofauti na huko tulikotoka...akitokea wakuwasemea atampa kura.
Nilipomuuliza kwanini Wana changamoto lukuki lakini azitamkwi popote akasema wanatii bila shuruti. Lakini pia malipo mengi yanajadiliwa Bungeni ila ukweli hawalipwi.
Wanasiasa wasaidieni walinzi wenu, tungependa muwe mnasikiliza waache kulalamika mtaani na kwenye vijiwe, waache kutusimamisha na magari nakuchukua elfu mojamoja... graduate kuchukua rushwa ya elfu moja Tena mlinzi wa Mali zetu nadhani nikutaka apate pesa yakulisha familia na kushona uniform
Siku zilizobaki waelezeni mtawasaidiaje?
Jambo la pili akasema, anatamani Askari waache kujinunulia na kushona uniform kwa gharama zao wenyewe. Kipindi Cha nyuma walikuwa wanashonewa uniform ila Sasa hivi wameachwa wajitaftie wenyewe. Ana kiu yakuona thamani yao nakuwapa stahiki zao.
Jambo la tatu, nyumba hazitoshi na wanaokaa uraiani awalipiwi Kodi ya nyumba. Umeme maeneo mengine wanajinunulia tofauti na huko tulikotoka...akitokea wakuwasemea atampa kura.
Nilipomuuliza kwanini Wana changamoto lukuki lakini azitamkwi popote akasema wanatii bila shuruti. Lakini pia malipo mengi yanajadiliwa Bungeni ila ukweli hawalipwi.
Wanasiasa wasaidieni walinzi wenu, tungependa muwe mnasikiliza waache kulalamika mtaani na kwenye vijiwe, waache kutusimamisha na magari nakuchukua elfu mojamoja... graduate kuchukua rushwa ya elfu moja Tena mlinzi wa Mali zetu nadhani nikutaka apate pesa yakulisha familia na kushona uniform
Siku zilizobaki waelezeni mtawasaidiaje?