Askari wa Usalama Barabarani wanaichafua Serikali kwa uonevu wanaofanya kwa wamiliki wa magari

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Trafiki wamekuwa kero hasa kipindi hiki cha Uchaguzi ambacho viongozi wote wa serikali wamekimbilia kwenye majukwaa ya siasa. Wamefanya mradi kwa daladala, kila ukipita umwachie 1000 au 2000 bila hivyo anakuandikia elfu 30000.

Zipo video na picha zinazoonyesha namna wanavyokusanya mapato binafsi. Makusanyo haya yanafanywa kwa wajasiriamali na walala hoi lakini uoni wenye mashangingi na magari ya hadhi wakisumbuliwa.

Bodaboda kila kona wanakamatwa, bajaji na vigari vidogo vya mzigo ndo usiseme. Je, viongozi wa wizara ya mambo ya ndani amwoni? Viongozi wa polisi hiki kinachotokea amkioni? Mnadhani uchungu walionao bodaboda, madalala drivers, makondakta na waendesha vigari vidogo utaicha CCM salama?

Jifunze kutenda haki, simamieni haki, kuweni sehemu ya kuboresha maisha ya wajasiriamali wa nchi hii,punguzeni wahalifu kwa kulinda kundi la vijana lililojitolea kujiajiri.
 
Mara nyingi watoto huiga tabia ya Baba. Baba anabambikia kesi watu, wanalipishwa mabilioni. Wadogo wanawakamua wadogo wenzao elfu mbilimbili.
 
Nilishasema, nasema tena, madereva watamkumbuka Lugora, nahili jambo kamanda musilim amelibariki siku kiongozi wa madereva kule mbeya alivyo lalamikia swala la dereva kupigwa faini igunga na kukamatiwa misigiri!

Muslim alijibu tutakukamata popote, sasa km umeweza kupiga picha unashindwaje kumkamata, hii inafanya traffic police kupiga picha ovyo ovyo naukifika mbali ukamatwe na ukihoji unaambiwa kosa umelifanya 100km! Km hutoi pesa utakaa hapo, au unakula cheti.
 
Back
Top Bottom