Askari wa JWTZ na POLISI wachapana Kavukavu Mwanza

GHOST RYDER

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
1,025
475
Katika kile kinachoonekana kama kuhitimisha kwa mbwembwe Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Hussein Mwinyi, chanzo chetu cha uhakika kutoka jijini mwanza kinaarifu askari ya jeshi la Polisi na na wale wa Jeshi la wananchi Tanzania kuchapana kavukavu katika eneo la Kituo cha polisi kilichopo eneo la kiwanda cha nguo Mwatex jijini humo.

Chanzo cha mkasa huu inadaiwa kuwa ni askari wa jeshi la polisi kumkamata mwananchi aliyekuwa amevalia sare za kiraia na kofia ya kombati za jeshio kichwani.

Bila kutambua kuwa raia huyo hakuwa raia wa kawaida bali askari wa jeshi la Polisi, walimtia nguvuni. Katika zoezi la mahojiano alionekana kukaidi maswali ya polisi na kutojitambulisha yeye ni nani ndipo Polisi wakachukua uamuzi wa kumsweka lupango huku wakijisahau kumfanyia upekuzi.

Kosa hilo lilimpa mwanya kutumia simu yake ya kiganjani aliyoswekwa nayo lockup kuwasiliana na wanaJWTZ wenzake ambao bila kupoteza muda walifika katika eneo la tukio na kutifua vumbi la kipekee huku wakifanikiwa kumnasaua mtuhumiwa kutoka lupango.

Katika kujibu mapigo Polisi nao walimimina Defender mbili za FFU na kufungua mapigano makali kati ya Askari wa Polisi na JWTZ huku umati wa wananchi ukiungana na wanaJWTZ wachache kuwakabili Polisi.

Hata hivyo kadhia hiyo ilitulizwa baada ya kuwasili kwa maofisa wawili kutoka pande mbili husika na kuwatawanya vijana wao kwa amri za kiafande.

Ni bahati mbaya jana media zilifunikwa na Taarifa za Rostam kuvua gamba na hata wadau wetu kutoka huko walifunikwa na wingu hilo.

Tunaendelea kusaka picha za majeruhi na bila shaka kudadidi kama Polisi leo huko Mwanza watatoa tamko lolote kufuatia tukio hulo ambalo kwa namna ya kipekee lilihitimisha Hotuba ya Bajeti ya Hussein Mwinyi hapo jana.

More updates to follow

ADIOS
 
Kama kawaida ya leo Alhamis ni Mwaswali ya Papo kwa papo kwa Waziri Mkuu.

Bibi Kiroboto ndani ya Nyumba...

G.R. Live from Mjengoni Today...NO Power failurer, May internet connection failurer
 
Picha mkuu...pia hawa JWTZ wamezoea kupiga wenzao,FFU wameonesha ukomavu wa mafunzo,lakin kwakua ni wenzao hajafa mtu,wangekua wamachinga wapigwa risasi za moto,police wetu ni wasanii!
 
Huwa najisikia raha sana wanapokong'otwa askari wa JWTZ.

Hawa jamaa wanajionaga miungu watu wakati wanakula mishahara ya bure.
 
Huwa najisikia raha sana wanapokong'otwa askari wa JWTZ.

Hawa jamaa wanajionaga miungu watu wakati wanakula mishahara ya bure.

Basi nasikia jana raia waliamua kuwaunga Mkono. Sijui ndo woga na kuendela kuwaabudia, ila mshikemshike ulikuwa si wa kawaida. Vijana bado wanasaka picha kama walau zilipatikana hata katika simu ya mkononi
 
Huu ni moto wa kesho ambao utakuja kuwaka baada ya wanajeshi na wananchi kuungana pamoja kuiondoa serikali iliyoko madarakani kwa kushirikiana kama ilivyokuwa misri hawa vibaka wanaitwa polisi tutakuja kuwasahau siku moja
 
Huu ni moto wa kesho ambao utakuja kuwaka baada ya wanajeshi na wananchi kuungana pamoja kuiondoa serikali iliyoko madarakani kwa kushirikiana kama ilivyokuwa misri hawa vibaka wanaitwa polisi tutakuja kuwasahau siku moja

ahsante kwa kunisaidia kusema, i cant wait for this to happen hii ni dalili elekezi na nzuri naamini serikali itajifunza kitu japo kidogo.
 
Hii inaonyesha ni jinsi gani jeshi letu la polisi lisivyofuata sheria wakati wa kumuarrest mtu. Kama wangemuhoji vizuri kabla hawajamuarrest, huenda angewapa kitambulisho na haya yote yasingetokea. Bila shaka walianza na zile zao za kuomba chochote na mjeshi akatia ngumu.

Yote kwa yote, kwa kuwa waziri alitaka uthibitisho wa vitendo vya kihuni vinavyofanywa na baadhi ya wanajeshi wetu basi sidhani kama atakuwa na swali tena
 
Hii inaonyesha ni jinsi gani jeshi letu la polisi lisivyofuata sheria wakati wa kumuarrest mtu. Kama wangemuhoji vizuri kabla hawajamuarrest, huenda angewapa kitambulisho na haya yote yasingetokea. Bila shaka walianza na zile zao za kuomba chochote na mjeshi akatia ngumu.

Yote kwa yote, kwa kuwa waziri alitaka uthibitisho wa vitendo vya kihuni vinavyofanywa na baadhi ya wanajeshi wetu basi sidhani kama atakuwa na swali tena

Tukio liliangukia wakati muafaka baada ya mbwembwe nyingi za asubuhi na wakati huo anahitimisha Hotuba yake Nd. Mwinyi haya yanajiri Mwanza. Nashangaa wanahabari na Media zilizopo Mwz kukosa tukio hili lilodumu zaidi ya saa 1 na nusu kama tunavyoarifiwa
 
Huu ni moto wa kesho ambao utakuja kuwaka baada ya wanajeshi na wananchi kuungana pamoja kuiondoa serikali iliyoko madarakani kwa kushirikiana kama ilivyokuwa misri hawa vibaka wanaitwa polisi tutakuja kuwasahau siku moja

What a distant Focus???
 
Hii ni nzuri sana, jeshi karibuni kwenye chama chetu tusaidiane kuikomboa nchi, tunaibiwa sana ati.
 
Huwa najisikia raha sana wanapokong'otwa askari wa JWTZ.

Hawa jamaa wanajionaga miungu watu wakati wanakula mishahara ya bure.

Ungejiuliza ni kwa nini wananchi waliamua kuungana na JWTZ kuwashughulikia Polisi. Kuna sababu.
 
Mbona hapa ni jeshi linatetewa tu!??

Well mimi ninaamini,
"Jambo usilolijua, ni kama usiku wa giza." -Wahenga
 
Vurugu zalipuka tena Mwanza
Na Cosmas Mlekani
14th July 2011
Kwa mara nyingine, Jiji la Mwanza jana lilishuhudia vurugu, baada ya askari wa Jeshi la Polisi waliokuwa katika operesheni ya kukamata pikipiki zenye makosa ya usalama wa barabarani, kumshambulia kwa kipigo askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Askari huyo wa JWTZ, ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, alikumbwa na mkasa huo, baada ya askari polisi kukamata pikipiki yake kwa lengo la kukagua uhalali wa kuendeshwa barabarani.
Hata hivyo, wakati askari polisi wakimhoji, askari huyo wa JWTZ alimgeukia mmoja wao na kumuamuru kuvua kofia aliyokuwa amevaa kwa madai kwamba, ni mali ya JWTZ.
Amri ya askari huyo wa JWTZ ilipingwa na askari polisi, ambao walianza kumpa kipigo.
Kitendo hicho kiliwaudhi wananchi waliokuwa wakifuatilia tukio hilo, ambao waliingilia kati na kuanza kuwashambulia askari hao kwa mawe, ikiwa ni pamoja na kuchoma moto matairi ya gari barabarani.
Askari hao walipoona wamezidiwa, walikimbilia katika kituo cha polisi cha Market na wananchi hao waliendelea kuwashambulia kwa mawe.
Vurugu hizo zilizotokea katika eneo la Nyakato, zilisababisha Barabara ya Musoma kufungwa kwa muda.
Kutokana na vurugu hizo, askari polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) walifika na kuanza kuwatawanya wananchi hao kwa mabomu ya machozi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro, alifika katika eneo la tukio, lakini hakuwa tayari kuzungumzia tukio hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro, alithibitisha kuwapo operesheni ya kukamata pikipiki na kusisitiza kuwa itaendelea.

IPP MEDIA
 
Tukio liliangukia wakati muafaka baada ya mbwembwe nyingi za asubuhi na wakati huo anahitimisha Hotuba yake Nd. Mwinyi haya yanajiri Mwanza. Nashangaa wanahabari na Media zilizopo Mwz kukosa tukio hili lilodumu zaidi ya saa 1 na nusu kama tunavyoarifiwa

Huwa nafurahi sana hawa jamaa wa JW wakitoa kichapo kwa hao jamaa wanaojiona magari yote ya barabarani ni yao...
 
Back
Top Bottom