Askari Polisi wafundisha sekondari

Mtoto wa Mkulima

JF-Expert Member
Apr 12, 2007
681
126
wakuu hii imekaaje? kwanini serikali isjipange vizuri? Bado tunaupungufu wa askari na upungufu wa waalimu sasa asikari ndio wamekuwa waalimu. Du hii sijui wazee nyie mnaiona je.

Askari Polisi wajitolea kufundisha sekondari Serengeti
Na Anthony Mayunga, Serengeti

ASKARI polisi wenye taaluma ya ualimu wamejitolea kufundisha shule ya Sekondari ya Mugumu ikiwa ni sehemu ya juhudi za kukabiliana na uhaba wa walimu wilayani Serengeti.


Akitoa taarifa wakati wa uzinduzi wa mradi wa vyumba vitatu vya madarasa vilivyoibuliwa na kamati ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf), Mkuu wa shule hiyo, Amon Majura, alisema kuwa askari hao wawili wameziba upungufu wa walimu ulioko katika shule hiyo.


Alisema kuwa shule hiyo ina wanafunzi 850 kwa kidato cha kwanza hadi cha nne lakini ina walimu watano tu wa kuajiriwa wa kujitolea wakiwa saba, miongoni mwao wakiwemo askari polisi ambao pia wana taaluma ya ualimu.


Alisema kwamba uwepo wao umekuwa ni msaada mkubwa kwa masomo ya Jiografia, Historia na Hisabati kwa kidato na cha nne ambayo pia hayakuwa na walimu.


Majura alikiri shule hiyo ina wanafunzi wengi kwa mwaka huu ambapo wamepelekwa 320 kwa mikondo minane lakini wana upungufu mkubwa wa walimu na kuomba juhudi za makusudi zifanywe na serikali kurekebisha hali hiyo.


Hata hivyo alisema kwamba walimu waliopo wamejitahidi kwa kiwango kikubwa ambapo mwaka jana wanafunzi wa Kidato cha Pili 178,kati ya 179 waliofanya mtihani walifaulu, huku mmoja pekee akiwa ameshindwa mtihani wa kuingia kidato cha tatu.


Kwa upande wa madarasa alikiri kuwepo upungufu wa vyumba vya madarasa ya kusomea ambapo kwa sasa vipo vyumba 13 kwamba kutokana na ikama ya watoto vinatakiwa vyumba 21 ambapo kila chumba kitakuwa na watoto 40.


Akizindua mradi huo Diwani wa Kata ya Mugumu mjini, Ryoba Charles alisema utekelezaji wake unatakiwa kufanyika kwa haraka ili kuepuka kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali ambao unaweza kuathiri utekelezaji wa mradi huo
 
Hii nchi inaendeshwa na wanasiasa ambao hawana shule na matokeo yake ni kutoa maamuzi ambayo huligharimu taifa. Hii inatokana na maamuzi ya kukurupuka ya ujenzi wa shule za sekondari za kata,ukimsikia lowassa hili uwa anajisifia sana kwasababu uwezo wake naye wa kufikiri ni mdogo. Majengo tunayo, walimu hatuna,unataka mwanakijiji aache kukaa town akafundishe Nyangao sekondari, kakuambia nani atakubali,wakati kila kukicha majengo marefu ya serikali yajengwa mjini?
 
wakuu hii imekaaje? kwanini serikali isjipange vizuri? Bado tunaupungufu wa askari na upungufu wa waalimu sasa asikari ndio wamekuwa waalimu. Du hii sijui wazee nyie mnaiona je.
Mimi nawaunga mkono askari polisi waliojitolea kufundisha, nnadhani watatumia muda wao mapumziko kufanikisha hilo. Naomba na wengine wajitokeze kwa hilo, elimu ndio mkombozi wetu wa kweli.
 
Hili linahitaji kupongezwa! Kwanza Polisi hawa watasaidia kunyanyua elimu huko Serengeti na pili kujenga mahusiano memam na jamii. Kudos wale waliojitolea!
 
Haingii akilini kusema kwamba hao ni askari wenye taaluma ya ualimu kwani ualimu siku hizi ni highly marketable hapa bongo na I am sure (kihalali) unalipa zaidi ya upolisi. Kwa hiyo mimi nna doubt na hata huo uwezo wa hao polisi. I guess jamaa alikuwa anataka kupunguza maswali. Ok na ni kwa vp shule ikafunguliwa bila walimu, huu usanii wa JK na EL mpaka lini. Maana ukiwasikia kuhusu mafanikio waliyopata alwayz wanataja shule hizo!
 
Si vibaya polisi kufundisha sekondari lakini kumbuka kuwa kazi zapolisi wanakimbilia failures na wengi vyeti vyao ni vya kugushi. Tatizo ni product itakayotoka kwenye hizo sekondary kwani bora mwnanafunzi ajitafutia mwenyewe materials kuliko kupotoshwa.
 
Nichukue nafasi hii kuwapongeza polisi hao kwa moyo waliouonyesha katika kulijenga taifa.
Ni wachache miongoni mwetu ambao tungechukua hatua hiyo!
 
Askari Labda Hao Wa Enzi Zenu Ndo Walikuwa Hawajaenda Shule Kwa Taarifa Yako Tafuta Data Za Polisi Walio Higher Learning Kwa Kila Mwaka Hawapungui 100 Achilia Mbali Hivyo Vi Diploma Vya Ualimu Ili Ufundishe Secondary.na Kama Ni Issue Ya Kwenda Kazi Fulani Baada Ya Kufeli Sielewi Kufeli Kwa Mujibu Wa Mchangiaji Ni Kitu Gani? Kwa Sababu Hata Mwenye Div 4 Huandikiwa Amepass Vile Vile Ualimu Watu Huenda Baada Ya Kufell Form 6 Kwa Maana Yako Ya Kufell Otherwise Mambo Sikuhizi Yamebadilika Japokuwa Zamani Mapolisi Wengi Shule Yao Ilikuwa Ndogo Sikuhizi Waliokwenda Shule Wengi Na Wasioenda Wapo Vile Vile!! Tena Formsix Waliopass Ndo Wamejaa Na Wala As Long As Polisi Is Concerned Kuwa Form 6 Wala Siyo Issue Ndo Maana Wengi Wanasaka Madigrii Vyuoni.
 
Askari Labda Hao Wa Enzi Zenu Ndo Walikuwa Hawajaenda Shule Kwa Taarifa Yako Tafuta Data Za Polisi Walio Higher Learning Kwa Kila Mwaka Hawapungui 100 Achilia Mbali Hivyo Vi Diploma Vya Ualimu Ili Ufundishe Secondary.na Kama Ni Issue Ya Kwenda Kazi Fulani Baada Ya Kufeli Sielewi Kufeli Kwa Mujibu Wa Mchangiaji Ni Kitu Gani? Kwa Sababu Hata Mwenye Div 4 Huandikiwa Amepass Vile Vile Ualimu Watu Huenda Baada Ya Kufell Form 6 Kwa Maana Yako Ya Kufell Otherwise Mambo Sikuhizi Yamebadilika Japokuwa Zamani Mapolisi Wengi Shule Yao Ilikuwa Ndogo Sikuhizi Waliokwenda Shule Wengi Na Wasioenda Wapo Vile Vile!! Tena Formsix Waliopass Ndo Wamejaa Na Wala As Long As Polisi Is Concerned Kuwa Form 6 Wala Siyo Issue Ndo Maana Wengi Wanasaka Madigrii Vyuoni.

Nakuunga mkono ndugu Manyiri.
Maafande wengi sana siku hizi wameenda shule, na wapo wa kila taaluma, kuanzia ualimu, sheria, uhasibu, uhandisi, urubani, uanamaji, sayansi za jamii na kadhalika. Kumbuka kwamba wengine wanaenda katika jeshi kwa sababu ya kupenda kazi hiyo ya kwata na ulinzi wa usalama na nchi kwa ujumla, ingawa wanakuwa na taaluma nyingine pia, kwa hiyo kama maafande wenye taaluma ya elimu wanaamua kufundisha watoto wetu mi sioni shida yoyote ile, maadam kama wana vyeti vinavyowaruhusu kufanya kazi hiyo! Ndio maana hapo juu nimewapongeza maafande hao kwa kujitolea kuliendeleza taifa!
Nakumbuka nikiwa nasoma mlimani, nilisoma na maafande kibao sana waliokuwa wametoka kazini kuj kujiendeleza. Kwa hiyo sitashangaa sana iwapo nitasikia walimu hao mapolisi wanafundisha mahali!
 
I have read both sides kwa wale wanaounga mkono kwa polisi kufundisha na kwa wale wanaooona si vema. pande zote mbili zina mantiki sahihi ingawa reasons za kitaaluma ndiyo hazichambiliwa kisawasawa.

Kwanza Ninailaumu serikali kwa kufungua shule bila walimu. Shule si majengo mazuri. Shule ni pamoja na walimu wazuri wenye taaluma ya kuwawezesha wanafunzi kusoma na kufaulu masomo ambayo yatawasaidia katika maisha yao. kwa hiyo usanii wa kukurukupuka kufungua SHULE Hiyo ni PWAGU na PWAGUZI.

Pili kama hao Polisi wamhetimu Ualimu wa sekondari si mbaya kufundisha lakini Tatizo ni kuwa taaluma ya kufundisha kama zilivyo taaluma zingine zinahitaji kuendelea kujionoa kila wakati. Sasa hao polisi baada ya kuqualify kama Polisi moja kwa moja kuna vitu wamevikosa kipindi walipoacha kufundisha na kuingia Upolisi. They have the skills yes lakini I am not sure kama they are compentent enough kufundisha sylabus ambayo inabadilika. Unless wame atend course fupi tu ya kuwanoa./ Otherwise wanawasaidia wanafunzi kusolve past papers basi wanaonekana vipanga. Elimu sio kusolve past papers!

Tatu serengeti naijua vema vipi hali ya usalama wa raia, je ujambazi na wizi wa ng'ombe umeisha? vipi madhila mengine ya yanayowakera wanamchi yanayohusiana na crime, unless kumekuwa Vatican ndogo. I dont think so.

Nnne kipsycholojia hao Polisi they are stretched to the limit, kwani muda wa kuwa mapumziko then inabidi waandae notice kwani sidhani kama shule haina walimu iwe na vitabu vya kiada vya kutosha, kwa hiyo hao majamaa lazima wanatumia MADESA!!!! hata yaliyopitwa na wakati. Unless Kuna maktaba mpya yenye Nondo za kileo kwa ajili ya rejea.

Mwisho msimamo wangu ni kuwa Hao polisi wameonesha moyo wa kupenda kufundisha, hivyo inabidi waamue iwe part time na walipwe mshahara wa masaa wanayofundisha. NA KWA KUSEMA hivyo nina maana wapelekwe kujinoa tena hata mwezi katika vyuo pale TARIME au BUTIMBA. na wawe na Immunity ya kuhamishwahamiswa, Kwani ikitokea Saidi mwema akawatunuku labda kwenda kozi ya cheo watagoma ili wafundishe?? HII NI PWAGU NA PWAGUZI.
 
Back
Top Bottom