Greatest Of All Time
JF-Expert Member
- Jan 1, 2017
- 20,501
- 44,611
Afande Rashid wa kituo cha polisi Mpwapwa, amepoteza maisha baada ya timu yake ya Yanga kuifunga Simba jana kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii.
Afande alishikwa na furaha iliyopitiliza hali iliyosababisha kukutwa na mauti huko Mpwapwa, Dodoma!
Poleni sana wafiwa, kwa kupoteza mpendwa wenu, hizi timu inabidi tuzipende kwa kiasi!
====
Askari Polisi wa Kituo cha Polisi Mpwapwa, Rashid Mohamed Juma ambaye ni Shabiki wa Yanga amefariki Dunia jana wakati akitazama mchezo wa Simba na Yanga kwenye TV, Shuhuda aliyekuwa akitazama nae mpira amesema alifika pale dakika ya pili ya mchezo na hakuchukua zaidi ya dakika tano alianza kuishiwa nguvu
"Alianza kuguna akiwa amesimama na nikamdaka baada ya kumlaza chini ndio akaendelea kuguna kama ng'ombe na kurusha mikono baadaye akaguna mara ya mwisho na kunyoosha miguu na mikono baadaye walikuja Askari kumchukua baadaye wakasema ameshafariki sio kwamba amefariki baada ya goli hapana, wakati anaendelea kurusha mikono goli ndio lilikuwa linaingia" ——— Joseph Ndani Mutalima, Mkazi wa Mpwapwa
Mwili wa Rashid umesafirishwa kuelekea Rukwa kwa ajili ya mazishi, Marehemu ameacha mjane na Watoto wawili na mazishi yanatarajiwa kufanyika keshokutwa.
Afande alishikwa na furaha iliyopitiliza hali iliyosababisha kukutwa na mauti huko Mpwapwa, Dodoma!
Poleni sana wafiwa, kwa kupoteza mpendwa wenu, hizi timu inabidi tuzipende kwa kiasi!
====
Askari Polisi wa Kituo cha Polisi Mpwapwa, Rashid Mohamed Juma ambaye ni Shabiki wa Yanga amefariki Dunia jana wakati akitazama mchezo wa Simba na Yanga kwenye TV, Shuhuda aliyekuwa akitazama nae mpira amesema alifika pale dakika ya pili ya mchezo na hakuchukua zaidi ya dakika tano alianza kuishiwa nguvu
"Alianza kuguna akiwa amesimama na nikamdaka baada ya kumlaza chini ndio akaendelea kuguna kama ng'ombe na kurusha mikono baadaye akaguna mara ya mwisho na kunyoosha miguu na mikono baadaye walikuja Askari kumchukua baadaye wakasema ameshafariki sio kwamba amefariki baada ya goli hapana, wakati anaendelea kurusha mikono goli ndio lilikuwa linaingia" ——— Joseph Ndani Mutalima, Mkazi wa Mpwapwa
Mwili wa Rashid umesafirishwa kuelekea Rukwa kwa ajili ya mazishi, Marehemu ameacha mjane na Watoto wawili na mazishi yanatarajiwa kufanyika keshokutwa.