Askari polis sengerema, apigwa kipigo cha mwizi, Hali yake ni mbaya.

15.09.2012 Akiwa na askari mwenzake na mgambo wawili, walikuwa kazini wakifanya msako maeneo ya KASOMERI SENGEREMA, waliibukia kwenye kundi la watu walikuwa wakiandaa na kunywa pombe ya moshi au GONGO. Waliwakamata walioweza kuwakamata na vitendea kazi vyao tayari kuwapeleka kituo cha polisi.

Wakati wakienda kituo cha polisi, walizingirwa na wanakijiji, pamoja na kujitambulisha lakini bado hawakusikilizwa. Ndipo walipoamua kujulisha kwa uongozi wao, wakaambiwa wawaachie wapika/wanywa gongo hao.

Ndipo askari hao bila hiyana, wakawaachia na kutaka kuendelea na safari ya kurudi kituoni. Mara wananchi wakaanza kuwashambulia kwa mawe, fimbo, mapanga na silaha nyingine nyingi za kijadi hali iliyopelekea askari mmoja aliyeajulikana kwa jina moja tu la HAMISI kujeruhiwa vibaya sana maeneo ya kichwani na kukimbizwa hospitalini sengerema walioamua kumwandikia rufaa hadi bungando alipo kwa sasa.

Bado hali yake si nzuri, na watu 14 wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

maswali/changamoto
1. Je, kama askari huyo angekuwa na bunduki, angeshindwa kuitumia ili kujilinda?
2. Askari akiiumizwa/akiuwawa katika kazi yake, mbona wanaharakati hatuwasikii wakitoa matamko?
3. Je hii haina maana kuwa wako biassed na kazi zao? wanaegamia upande mmoja wa shilingi? Kimaadili inafaa?
5. Kwa nini watanzania hatupendi kuwajibika kwa makosa ambayo tumyatenda? Tunafanya uhalifu wenyewe, lakini tukikamatwa tunagoma kukamatwa? Huu uwajibikaji tunaodai kwa viongozi wetu sisi tunao?

NAWASILISHA.
wamekwenda kufanya kazi ambayo hakutumwa na wakubwa wao.
 
Hii ni stori ya upande wako wewe uliyejitanabaisha waziwazi kwamba ni mshabiki wa CCM au mmoja wa mapolisi wa ovyo ovyo tulio nao; bado hatujasikia simulizi za upande mwingine. Sasa unataka tuwahukumu wananchi kwa hadithi yako ya kutungatunga tena ya upande mmoja?
Hakuna Mtanzania asiyejua kwamba Gongo, bangi na madawa ya kulevya na makosa ya trafiki vimekuwa vyanzo vikubwa vya mapato kwa polisi wanaolipwa chini ya viwango kwa kujipatia fedha kutokana na rushwa. Ni mara ngapi vidhibiti kama gongo, bangi na madawa ya kulevya vimeyeyuka vilipofikishwa mahakamani? Pia hakuna Mtanzania asiyefahamu wahalifu wanaokamatwa na kupelekwa rumande na mahakamani ni wale tu waliokosa uwezo wa kuwahonga polisi wala rushwa waliosheheni katika Jeshi hili, tena wengi wa 'wahalifu' hao wakiwa wamebambikiziwa kesi za kupatikana na hizo bange, madawa ya kulevya ? Laiti tungekuwa na polisi wanaowajibika kikamilifu vijana wetu wangenusurika na janga la madawa ya kulevya yanayosambazwa nchi nzima kwa msaada wa hao hao polisi. Wanaharakati wanafanyia kazi facts - proven beyond reasonable doubts na siyo hizi hadithi zenu za Kalumekenge. Shame on you police officers.

mkuu nimekusoma, umezungumzia uwajibikaji. Ni ukweli kabisa, kuna baadhi ya uhalifu unaendelea ni kwa kuwa tu POLISI nao hawataki kuwajibika kwa nafasi zao. Hilo halina ubishi.

sasa turudi kwenye mada. askari kapigwa akiwa anatekeleza wajibu wake, na amepigwa nusra ya kufa, je hana haki kwa sababu baadhi ya askari wanaendekeza rushwa katika utumishi wao? Je ni kweli anastahili kipigo hicho alichopewa kwa kisingizio polisi wenzake wanakula rushwa?

Na je nini nafasi ya wanaharakati, wanatetea haki za kundi fulani la watu huku makundi mengine wakiyaacha kwa sababu tu watu wa ofisini kwao wananuka kwa utumishi mbovu?
 
kama naelewa vizuri ni kuwa inaonekana hii gongo si hatari saaaaana kama wanavyoivumisha, bali ni miongoni mwa vinywaji ambovyo kisheria, narudia kisheria tunakatazwa kukitumia, lakini kijamii kinapingana na katazo la kisheria, nina maana sheria ilitungwa kuwafukarisha wagema wazawa, manake nimeshangaa kijiji kizima kimemlia denge polisi ili kumzuia asiibughudhi "village breweries" na kwa maelezo ya thread ni kuwa polisi mkamataji aliambiwa na afande wake, awaachie!!!!

Sijui kama kuna muunganiko mzuri hapo, uwaachie wahalifu halafu waanze kukupiga, mimi nadhani kipigo ndio kilisitisha ukamataji.

Story ni kwamba, walikuwa askari wawili na mgambo wawili kwa jishi nilivyoelezwa. Wqalipokamata ili kuwapeleka kituoni, wananchi wakawazingira kwa minajili ya kuzuia zoezi hilo. Kwa kuwa nguvu yao ilikuwa ndogo, wakaomba msaada kwa kiongozi wao ndipo alipowashauri waachane nao, na kama ni ukamataji utafanyika kivingine siku nyingine. baada ya kuwaachia likaibuka kundi lingine sasa likaanza kutoa kipondo, mmoja ndiye aliyeathirika zaidi.

Inawezekana hakuwa mwepesi, na inawezekana kuna tafrani ilitokea hata mimi sijui.

Lakini tuchukue taarifa ya awali kuwa polisi apigwa kichapo cha mwizi nusra ya kuuwawa. Je wanaharakati nini nafasi yao katika suala kama hili? vyombo vya habari isipokuwa JF, kwani ndiyo inatuwezesha kujadili jambo hili mbona hata haikusika? au haki zinawahusu kundi la watu baadhi tu? hili ndilo swala langu
 
Hapa tayari umeshawahukumu wanakijiji!!Unaweza kuta jamaa kazidi kuchukua kitu kidogo kwa hao wapika gongo,ikawa mazoea kiasi kwamba hata wananchi wamewachoka!
Issue ni kuwa ukimkamata polisi unamshtaki wapi?ukienda huko kwao hawakawii kukugeuzia kibao!

ha ha ha ha, kwa hiyo polisi kisheria hakuna sehemu ya kumshtaki? yuko juu ya sheria? mi nadhani uko utaratibu wa kuwashtaki ingawa sijui vizuri. Kuna mwaka hapa mwanza polisi alipigwa na wanazengo, alipodai ni polisi wakambeba wakampeleka kwa kamanda wake, wanamwuliza, huyu ni askari wako? sijui ilimalizika vipi
 
kosa moja halisahihishi kosa jingine, wanaharakati hawajaunga mkono askari kuumizwa, lakini askari kuua au kupiga raia ni mbaya sana kwa vile askari ana mafunzo maalumu na raia hawana na askari analipwa na kodi za raia hivyo askari alitakiwa atumie mbinu alizofundishwa kuwatoroka maadui kama wanavyoonyesha mbele ya mheshimiwa wakati wakihitimu mafunzo.
 
kosa moja halisahihishi kosa jingine, wanaharakati hawajaunga mkono askari kuumizwa, lakini askari kuua au kupiga raia ni mbaya sana kwa vile askari ana mafunzo maalumu na raia hawana na askari analipwa na kodi za raia hivyo askari alitakiwa atumie mbinu alizofundishwa kuwatoroka maadui kama wanavyoonyesha mbele ya mheshimiwa wakati wakihitimu mafunzo.

hacena sasa kama angekuwa na risasi hapo kungetokea nini mkuu. Na kwa kuwa yeye amepewa mafunzo ndo akipigwa asitetewe!!
 
nini tena mkuu? kimsingi hakuna aliyejuu ya sheria, wote tunatakiwa kuitii sheria. Kwa ninavyo jua mimi, watu hao lazima wafunguliwe mashataka stahili na sidhani kama kuna atakayepewa dhamana kwa sasa. watakaa rumande hadi afya ya huyo mpiginaji irejee katika hali yake ya awali. maana unaweza kuwaachia watu halafu mtu akafa, wale jamaa wanaweza kusepa.

Kuhu wanaharaka, nchi yetu imejaa unafki mkubwa sana. tuliowengi ni wanafiki, tunachokikataa, tunakitetea kwa mgongo mwingine. Wanaharakati hadi sasa hawajalaani kitendo cha wananchi kuzuia afisa wa serikali kuwajibika kwa nafasi yake, lakini ingekuwa ni polisi kwafanyia raia kitu hiyo, akina nkya wangekuwa wamesha peleka mashataka ICC. HUU ni unafiki mkubwa.

kawaida na sheria inavyoelekeza ingetakiwa waambatane na viongozi wa mtaa ambao wangewathibitishia watuhumiwa kuwa hao ni polisi vilevile wananch wasingefanya fujo mbele ya viongoz wao ila hawa askari ambao wanajifanya wapo juu ya sheria wamevuna walichopanda, kwan raia walijua watakuwa ni majambazi ndo mana wakawashushia kipigo, polisi jifunzen kufuata sheria bila shuruti, pia nawapongeza wananchi wa sengerema kwa kujirinda dhid ya majambaz yanayojiita polis ni iman yangu hawa mambaz hawatarud tena na wakirud nagemea kuta taarifa ya polis waliokuwa wanafanya uharif wameuwawa na wananch wenye hasira kali
 
kosa moja halisahihishi kosa jingine, wanaharakati hawajaunga mkono askari kuumizwa, lakini askari kuua au kupiga raia ni mbaya sana kwa vile askari ana mafunzo maalumu na raia hawana na askari analipwa na kodi za raia hivyo askari alitakiwa atumie mbinu alizofundishwa kuwatoroka maadui kama wanavyoonyesha mbele ya mheshimiwa wakati wakihitimu mafunzo.

hahahaa! Hawa polis wetu hawa lolote yale huwa ni maigizo tu,ht wewe kwa mbinu ulizo nazo unawaacha polis mbali sn. Hawa polis wetu mbinu walizo nazo ni za kuomba rushwa nas kunyanyasa raia
 
Gongo inayotengenezwa na wazalendo inaonekana haram ila baa zetu zimejaa gongo tupu mfano ni gongo za viroba mbona zenyewe hawazikamati
 
kawaida na sheria inavyoelekeza ingetakiwa waambatane na viongozi wa mtaa ambao wangewathibitishia watuhumiwa kuwa hao ni polisi vilevile wananch wasingefanya fujo mbele ya viongoz wao ila hawa askari ambao wanajifanya wapo juu ya sheria wamevuna walichopanda, kwan raia walijua watakuwa ni majambazi ndo mana wakawashushia kipigo, polisi jifunzen kufuata sheria bila shuruti, pia nawapongeza wananchi wa sengerema kwa kujirinda dhid ya majambaz yanayojiita polis ni iman yangu hawa mambaz hawatarud tena na wakirud nagemea kuta taarifa ya polis waliokuwa wanafanya uharif wameuwawa na wananch wenye hasira kali

hilo nalo neno, mtu anaweza kwenda kukamata lakini mamlaka za eneo hataki kuwahusiha, hii inaweza kujenga mzingira ya rushwa pia, na wanaogopa kuwahusisha mamlaka za mtaa kwa kuwa rushwa haitachukulika
 
Story ni kwamba, walikuwa askari wawili na mgambo wawili kwa jishi nilivyoelezwa. Wqalipokamata ili kuwapeleka kituoni, wananchi wakawazingira kwa minajili ya kuzuia zoezi hilo. Kwa kuwa nguvu yao ilikuwa ndogo, wakaomba msaada kwa kiongozi wao ndipo alipowashauri waachane nao, na kama ni ukamataji utafanyika kivingine siku nyingine. baada ya kuwaachia likaibuka kundi lingine sasa likaanza kutoa kipondo, mmoja ndiye aliyeathirika zaidi.

Inawezekana hakuwa mwepesi, na inawezekana kuna tafrani ilitokea hata mimi sijui.

Lakini tuchukue taarifa ya awali kuwa polisi apigwa kichapo cha mwizi nusra ya kuuwawa. Je wanaharakati nini nafasi yao katika suala kama hili? vyombo vya habari isipokuwa JF, kwani ndiyo inatuwezesha kujadili jambo hili mbona hata haikusika? au haki zinawahusu kundi la watu baadhi tu? hili ndilo swala langu
ntagunga nimekuelewa, naku-regard kama miongoni mwa wahabarishaji wazuri!

Sikuchangia chochote kuhusu wanaharakati kwenye kadhia hii ya polisi kupigwa, lakini nikwambie sasa kuwa tukio hilo linalingana kwa maudhui kama si taathira, na maji kupanda mlima.

Tuwe na uelewa wa pamoja, Askari anapatiwa mafunzo mahsusi ya jinsi ya kutekeleza majukumu yake, kwa maneno mengine askari ni mtaalam wa saikolojia ya jamii angalau kwa mafunzo ya miezi 9.

Utaona wazi hapa polisi hakuwa mweledi vya kutosha ama alipuuza kwa maksudi au kwa msukumo wa kipato cha ziada, tahadhari ya "mob justice" ukijumlisha na maelezo yangu ya awali kuihusu gongo, utapata jawabu la hii "mob" ninayoi-refer kupambana na wanayemdhania kuwa mtunzi na mtia mkazo sheria wanayoiona kuwa kandamizi dhidi yao kwenye nyanja ya kiburudisho cha kilevi rahisi.

Ni kutokujitendea haki ikiwa tutadhani hili ni tukio la kupigiwa kelele na wanaharakati ambao wanauelewa wa kutosha kuhusu mamlaka, nguvu na wajibu walionao kisheria polisi wetu juu ya raia na mali zao.

Sisemi kuwa polisi wapigwe, la hasha, nasisitiza polisi kutumia taaluma yao preciously and positively.sheria na kanuni za kazi zizingatiwe, Kwa mfano ikitokea rabsha kwa wapenzi wa simba na yanga uwanja wa taifa, wakati simba inaongoza 4-0!!!!!!!!!! labda kamuhanda pekee ndiyo anaweza, lakini itakuwa ni kosa la mauaji kujaribu kutuliza rabsha hizo kwa mabomu ya mchozi kwenye uwanja uliofurika watazamaji zaidi ya 65,000. Likewise askari watatu kufanya jaribio la kukiarest kijiji kizima (hapa ni kwa mtizamo mpana) tegemea kuamsha jazba na munkari wa jamii husika.

Hapa uelewe hawa wananchi walikuwa wanafanya kama JWTZ ilivyofanya kwa idd amini alipovamia tanzania, ilikuwa kumpiga na kumtokomeza asionekane tena ili tishio lake litokomee pamoja naye,
walitaka huyu polisi asirudi tena au akome "kuwaonea" nimeutafsiri mtazamo wao.
 
Last edited by a moderator:
Unataka wanaharakati waseme nini? wanaharakati husemea wale wanyonge na pale haki inaposhindwa kupatikana lakini sasa hapa tayari watu waliotenda kosa washakamatwa na ninaamini hao Polisi watawashughulikia ipasavavyo................
 
ntagunga nimekuelewa, naku-regard kama miongoni mwa wahabarishaji wazuri!

Sikuchangia chochote kuhusu wanaharakati kwenye kadhia hii ya polisi kupigwa, lakini nikwambie sasa kuwa tukio hilo linalingana kwa maudhui kama si taathira, na maji kupanda mlima.

Tuwe na uelewa wa pamoja, Askari anapatiwa mafunzo mahsusi ya jinsi ya kutekeleza majukumu yake, kwa maneno mengine askari ni mtaalam wa saikolojia ya jamii angalau kwa mafunzo ya miezi 9.

Utaona wazi hapa polisi hakuwa mweledi vya kutosha ama alipuuza kwa maksudi au kwa msukumo wa kipato cha ziada, tahadhari ya "mob justice" ukijumlisha na maelezo yangu ya awali kuihusu gongo, utapata jawabu la hii "mob" ninayoi-refer kupambana na wanayemdhania kuwa mtunzi na mtia mkazo sheria wanayoiona kuwa kandamizi dhidi yao kwenye nyanja ya kiburudisho cha kilevi rahisi.

Ni kutokujitendea haki ikiwa tutadhani hili ni tukio la kupigiwa kelele na wanaharakati ambao wanauelewa wa kutosha kuhusu mamlaka, nguvu na wajibu walionao kisheria polisi wetu juu ya raia na mali zao.

Sisemi kuwa polisi wapigwe, la hasha, nasisitiza polisi kutumia taaluma yao preciously and positively.sheria na kanuni za kazi zizingatiwe, Kwa mfano ikitokea rabsha kwa wapenzi wa simba na yanga uwanja wa taifa, wakati simba inaongoza 4-0!!!!!!!!!! labda kamuhanda pekee ndiyo anaweza, lakini itakuwa ni kosa la mauaji kujaribu kutuliza rabsha hizo kwa mabomu ya mchozi kwenye uwanja uliofurika watazamaji zaidi ya 65,000. Likewise askari watatu kufanya jaribio la kukiarest kijiji kizima (hapa ni kwa mtizamo mpana) tegemea kuamsha jazba na munkari wa jamii husika.

Hapa uelewe hawa wananchi walikuwa wanafanya kama JWTZ ilivyofanya kwa idd amini alipovamia tanzania, ilikuwa kumpiga na kumtokomeza asionekane tena ili tishio lake litokomee pamoja naye,
walitaka huyu polisi asirudi tena au akome "kuwaonea" nimeutafsiri mtazamo wao.

jogi NAKUSHUKURU JOG KWA UCHAMBUZI WAKO NA NAMNA ULIVYOTAFSIRI MAAMUZI YA WANANCHI NA UKIMYA WA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU SUALA HILI. THANK YOU JOG
 
Unataka wanaharakati waseme nini? wanaharakati husemea wale wanyonge na pale haki inaposhindwa kupatikana lakini sasa hapa tayari watu waliotenda kosa washakamatwa na ninaamini hao Polisi watawashughulikia ipasavavyo................

HA HA HA......KWAMBA WATALIPIZA KISASI? NTAFUATILIA NIONE NINI KITAWAFIKA, NITAWAJUZA WADAU. LAKINI MIMI SIJAFURAHISHWA NA KUMPIGA MTU NUSRA YA KUFA. SIO FUNZO JEMA DA Elizabeth Dominic
 
imani na nyie polisi imepotea nawalaumu sana raia kwa kumuacha na uhai wangeua tu ,tulipie ile ya mwangosi,potelea mbali kila nikimuna polisi nashikwa na hasira yani kitendo chakugundua mleta mada ni polisi umeniharibia siku yangu,nikiwaona tu njiani natema mate chini laana kweli kweli hamwezi mkawa mnatumwa kama majini mnakwenda tu kama roboto,ninyamaze nsijekula ban bure mie
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom