ntagunga
JF-Expert Member
- Aug 13, 2011
- 654
- 256
15.09.2012 Akiwa na askari mwenzake na mgambo wawili, walikuwa kazini wakifanya msako maeneo ya KASOMERI SENGEREMA, waliibukia kwenye kundi la watu walikuwa wakiandaa na kunywa pombe ya moshi au GONGO. Waliwakamata walioweza kuwakamata na vitendea kazi vyao tayari kuwapeleka kituo cha polisi.
Wakati wakienda kituo cha polisi, walizingirwa na wanakijiji, pamoja na kujitambulisha lakini bado hawakusikilizwa. Ndipo walipoamua kujulisha kwa uongozi wao, wakaambiwa wawaachie wapika/wanywa gongo hao.
Ndipo askari hao bila hiyana, wakawaachia na kutaka kuendelea na safari ya kurudi kituoni. Mara wananchi wakaanza kuwashambulia kwa mawe, fimbo, mapanga na silaha nyingine nyingi za kijadi hali iliyopelekea askari mmoja aliyeajulikana kwa jina moja tu la HAMISI kujeruhiwa vibaya sana maeneo ya kichwani na kukimbizwa hospitalini sengerema walioamua kumwandikia rufaa hadi bungando alipo kwa sasa.
Bado hali yake si nzuri, na watu 14 wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
maswali/changamoto
1. Je, kama askari huyo angekuwa na bunduki, angeshindwa kuitumia ili kujilinda?
2. Askari akiiumizwa/akiuwawa katika kazi yake, mbona wanaharakati hatuwasikii wakitoa matamko?
3. Je hii haina maana kuwa wako biassed na kazi zao? wanaegamia upande mmoja wa shilingi? Kimaadili inafaa?
5. Kwa nini watanzania hatupendi kuwajibika kwa makosa ambayo tumyatenda? Tunafanya uhalifu wenyewe, lakini tukikamatwa tunagoma kukamatwa? Huu uwajibikaji tunaodai kwa viongozi wetu sisi tunao?
NAWASILISHA.
Wakati wakienda kituo cha polisi, walizingirwa na wanakijiji, pamoja na kujitambulisha lakini bado hawakusikilizwa. Ndipo walipoamua kujulisha kwa uongozi wao, wakaambiwa wawaachie wapika/wanywa gongo hao.
Ndipo askari hao bila hiyana, wakawaachia na kutaka kuendelea na safari ya kurudi kituoni. Mara wananchi wakaanza kuwashambulia kwa mawe, fimbo, mapanga na silaha nyingine nyingi za kijadi hali iliyopelekea askari mmoja aliyeajulikana kwa jina moja tu la HAMISI kujeruhiwa vibaya sana maeneo ya kichwani na kukimbizwa hospitalini sengerema walioamua kumwandikia rufaa hadi bungando alipo kwa sasa.
Bado hali yake si nzuri, na watu 14 wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
maswali/changamoto
1. Je, kama askari huyo angekuwa na bunduki, angeshindwa kuitumia ili kujilinda?
2. Askari akiiumizwa/akiuwawa katika kazi yake, mbona wanaharakati hatuwasikii wakitoa matamko?
3. Je hii haina maana kuwa wako biassed na kazi zao? wanaegamia upande mmoja wa shilingi? Kimaadili inafaa?
5. Kwa nini watanzania hatupendi kuwajibika kwa makosa ambayo tumyatenda? Tunafanya uhalifu wenyewe, lakini tukikamatwa tunagoma kukamatwa? Huu uwajibikaji tunaodai kwa viongozi wetu sisi tunao?
NAWASILISHA.