Askari kuua watu 'wanaodhaniwa ni majambazi' na kutoa taarifa wakijisifia ni sawa?

Paul Alex

JF-Expert Member
Jul 14, 2012
4,240
9,527
Kumekuwa na utaratibu ambao umezoeleka wa askari wetu kutoka kwenye vyombo vya habari na kujisifia kua wameua majambazi!

Binafsi sifurahii hii picha askari wanayoitoa, sijui wewe!

Tunajuaje kama hawa ni majambazi kweli?
Au ukishaitwa jambazi na askari tayari unakua jambazi!

Mahakama ni ya nini kama askari wanatoa hukumu wenyewe?
Utaratibu huu ukiachwa uendelee, yeyote kati yetu na siku yoyote anaweza kuitwa jambazi na kupigwa risasi za kutosha!

Askari anaposema ameua jambazi ni nani mwingine anayeenda kuchunguza kuhakiki kama aliyeuawa ni jambazi?
Hizi roadside justice zinazotumika kupandisha watu vyeo, sikumoja zitatupoteza.

Kama askari amepata taarifa kuwa kuna uhalifu unataka kutokea, kwanini asimkamate mshukiwa na kuepusha uhalifu kabla haujatokea?
Kwanini ajipange tu kuua?

Kuna tabia katikati yetu hazipaswi kupewa nafasi!
Ukatili na kuhalalisha mauaji katija awamu hii ni moja ya vitu vinavyoshusha heshima yetu kama taifa!
 
Hili ni kweli, kwa kigezo cha ujambazi kuna haja ya kufanyia uchunguzi kabisa, kwani pamoja na jitihada za Jeshi la Polisi ila kuna kitu hapa hakipo sawasawa, na hapa ukija kuuliza kama watu hawa waliouawa wote wamechukuliwa Sample za DNA na kuhifadhiwa kwa ajili ya matumizi hata ya uchunguzi hapo baadae utaambiwa hakuna.
 
Mkuu ulichozungumza ni hakika.
Kinachofanywa na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ni kule "kumpa mbwa jina baya ili upate uhalali wa kumuua". Na hili lilishatokea kuna kijana alipata kuuwawa hali alikuwa ni mpita njia tu maskini kijana yule na kanzu na kiremba chake akaambiwa kuwa ni jambazi. Ndugu tafuta haki yake huku na kule mpaka Leo kizungumkuti.
Hili lisipotazamwa vyema kwa kweli litaumiza watu wengi wasio na hatia.
 
Kumekuwa na utaratibu ambao umezoeleka wa askari wetu kutoka kwenye vyombo vya habari na kujisifia kua wameua majambazi!

Binafsi sifurahii hii picha askari wanayoitoa, sijui wewe!

Tunajuaje kama hawa ni majambazi kweli?
Au ukishaitwa jambazi na askari tayari unakua jambazi!

Mahakama ni ya nini kama askari wanatoa hukumu wenyewe?
Utaratibu huu ukiachwa uendelee, yeyote kati yetu na siku yoyote anaweza kuitwa jambazi na kupigwa risasi za kutosha!

Askari anaposema ameua jambazi ni nani mwingine anayeenda kuchunguza kuhakiki kama aliyeuawa ni jambazi?
Hizi roadside justice zinazotumika kupandisha watu vyeo, sikumoja zitatupoteza.

Kama askari amepata taarifa kuwa kuna uhalifu unataka kutokea, kwanini asimkamate mshukiwa na kuepusha uhalifu kabla haujatokea?
Kwanini ajipange tu kuua?

Kuna tabia katikati yetu hazipaswi kupewa nafasi!
Ukatili na kuhalalisha mauaji katija awamu hii ni moja ya vitu vinavyoshusha heshima yetu kama taifa!
Kuua sio sifa na ni dhambi mbele za Mungu katika mazingira yeyote yale,ni kutojitambua.
 
Kumekuwa na utaratibu ambao umezoeleka wa askari wetu kutoka kwenye vyombo vya habari na kujisifia kua wameua majambazi!

Binafsi sifurahii hii picha askari wanayoitoa, sijui wewe!

Tunajuaje kama hawa ni majambazi kweli?
Au ukishaitwa jambazi na askari tayari unakua jambazi!

Mahakama ni ya nini kama askari wanatoa hukumu wenyewe?
Utaratibu huu ukiachwa uendelee, yeyote kati yetu na siku yoyote anaweza kuitwa jambazi na kupigwa risasi za kutosha!

Askari anaposema ameua jambazi ni nani mwingine anayeenda kuchunguza kuhakiki kama aliyeuawa ni jambazi?
Hizi roadside justice zinazotumika kupandisha watu vyeo, sikumoja zitatupoteza.

Kama askari amepata taarifa kuwa kuna uhalifu unataka kutokea, kwanini asimkamate mshukiwa na kuepusha uhalifu kabla haujatokea?
Kwanini ajipange tu kuua?

Kuna tabia katikati yetu hazipaswi kupewa nafasi!
Ukatili na kuhalalisha mauaji katija awamu hii ni moja ya vitu vinavyoshusha heshima yetu kama taifa!
Mara nyingi kama siyo mara zote wanaodhaniwa kuwa majambazi huuawa na polisi katika majibizano ya risasi. Sijawahi sikia polisi wamemkuta mtu anayedhaniwa jambazi wakampiga risasi bila yeye kutumia nguvu kukimbia. Kama wewe ungekuwa polisi kuna mtu hujui kama ni jambazi au la anarusha risasi ungeenda kumkamata kwa mikono? Nadhani usingekuwepo duniani. Mtu yeyote akirusha risasi lazima ajibiwe na risasi za polisi na ikiwezekana auawe tu maana akikimbia na hiyo silaha madhara yake ni makubwa.
Safi sana polisi yeyote akiwarushia risasi lazima ajibiwe kwa risasi akipona bahati yake.
 
Kwa kasi ya ajabu tumeshakuwa ni police state,na kwa ukondoo wetu,ujinga wetu,sisi middle class tumesharidhika na maisha tunakokwenda ni giza zaidi,kisheria polisi HUWEZI tumia silaha za moto unless kuna tishio la maisha ya raia au polisi means kama watuhumiwa wameamua kujibizana kwa silaha na polisi ,hapo polisi wana uwezo wa nao kujihami dhidi yao (to use deadly force)ila kama mtuhumiwa au watuhumiwa wanakimbia kutoka kwenye crime scene polisi HAWARUHUSIWI kutumia silaha dhidi yao ndio maana wamepewa nyenzo nyingi zitakazowasaidia kuwakamata watuhumiwa na pia kuwatangaza suspects in press kabla ya kufikishwa mahakamani pia ni kosa mno.na mwisho bila ya kuwa na polisi wa kuwa polisi ,polisi tuna safari ndefu kwa waliopitia jeshini wanaelewa why tuna Military police ndani ya majeshi?hivyo hivyo tulitakiwa tuwe nao ndani ya jeshi la polisi(ukiona haujatendewa haki na polisi ,huku ndiko kwenda kulalamika but now umepigwa na polisi halafu unaenda kulalamika polisi!!!!
 
wezi nadhani baadhi wanajulikana kama polisi wanapewa taarifa ya wizi wao wanajibu hawana usafiri je hili litaisha kweli la kutuhumiana na kuuana. Nchi isiwe dampo la kutuhumiana na kumiminiana risasi
 
Kumekuwa na utaratibu ambao umezoeleka wa askari wetu kutoka kwenye vyombo vya habari na kujisifia kua wameua majambazi!

Binafsi sifurahii hii picha askari wanayoitoa, sijui wewe!

Tunajuaje kama hawa ni majambazi kweli?
Au ukishaitwa jambazi na askari tayari unakua jambazi!

Mahakama ni ya nini kama askari wanatoa hukumu wenyewe?
Utaratibu huu ukiachwa uendelee, yeyote kati yetu na siku yoyote anaweza kuitwa jambazi na kupigwa risasi za kutosha!

Askari anaposema ameua jambazi ni nani mwingine anayeenda kuchunguza kuhakiki kama aliyeuawa ni jambazi?
Hizi roadside justice zinazotumika kupandisha watu vyeo, sikumoja zitatupoteza.

Kama askari amepata taarifa kuwa kuna uhalifu unataka kutokea, kwanini asimkamate mshukiwa na kuepusha uhalifu kabla haujatokea?
Kwanini ajipange tu kuua?

Kuna tabia katikati yetu hazipaswi kupewa nafasi!
Ukatili na kuhalalisha mauaji katija awamu hii ni moja ya vitu vinavyoshusha heshima yetu kama taifa!
tuanzie hapa wanatufunza nakutupatia hizo silaha, la sivyo turudi enzi za mababu zetu
About 19,100,000 results (0.37 seconds)








Search Results
Web results
Video shows police firing 76 shots at suspect. The officers won't be ...

https://edition.cnn.com/2019/05/09/us/anaheim-police-shooting-video/index.html

May 9, 2019 - The two police officers who were involved in a fatal shooting last summer in Anaheim, California, will not face any criminal charges, the police chief said Wednesday. Sean Staymates and Kevin Pedersen fired more than 70 times at 50-year-old Eliuth Penaloza Nava, who they'd been ...
Police shot at the vehicle of a robbery suspect — and hit 3 children ...

https://www.washingtonpost.com/.../police-shot-vehicle-robbery-suspect-hit-children-ins...

Apr 27, 2019 - Law enforcement officials have released little information about a police shooting Friday afternoon in a southeastern Oklahoma town, declining to provide answers to what led officers to shootat a robbery suspect in a pickup truck — injuring him and three of the four children ...
 
Kumekuwa na utaratibu ambao umezoeleka wa askari wetu kutoka kwenye vyombo vya habari na kujisifia kua wameua majambazi!

Binafsi sifurahii hii picha askari wanayoitoa, sijui wewe!

Tunajuaje kama hawa ni majambazi kweli?
Au ukishaitwa jambazi na askari tayari unakua jambazi!

Mahakama ni ya nini kama askari wanatoa hukumu wenyewe?
Utaratibu huu ukiachwa uendelee, yeyote kati yetu na siku yoyote anaweza kuitwa jambazi na kupigwa risasi za kutosha!

Askari anaposema ameua jambazi ni nani mwingine anayeenda kuchunguza kuhakiki kama aliyeuawa ni jambazi?
Hizi roadside justice zinazotumika kupandisha watu vyeo, sikumoja zitatupoteza.

Kama askari amepata taarifa kuwa kuna uhalifu unataka kutokea, kwanini asimkamate mshukiwa na kuepusha uhalifu kabla haujatokea?
Kwanini ajipange tu kuua?

Kuna tabia katikati yetu hazipaswi kupewa nafasi!
Ukatili na kuhalalisha mauaji katija awamu hii ni moja ya vitu vinavyoshusha heshima yetu kama taifa!
Kama na wewe ni jambazi kaa chonjo !
Kwa taarifa yako rate ya ujambazi nchini imeshuka sana ,wewe jipendekeze,tutakupitia na tutajigamba pia
 
Mara nyingi kama siyo mara zote wanaodhaniwa kuwa majambazi huuawa na polisi katika majibizano ya risasi. Sijawahi sikia polisi wamemkuta mtu anayedhaniwa jambazi wakampiga risasi bila yeye kutumia nguvu kukimbia. Kama wewe ungekuwa polisi kuna mtu hujui kama ni jambazi au la anarusha risasi ungeenda kumkamata kwa mikono? Nadhani usingekuwepo duniani. Mtu yeyote akirusha risasi lazima ajibiwe na risasi za polisi na ikiwezekana auawe tu maana akikimbia na hiyo silaha madhara yake ni makubwa.
Safi sana polisi yeyote akiwarushia risasi lazima ajibiwe kwa risasi akipona bahati yake.
Maelezo haya, kuwa kulikuwa na majibizano ya risasi anayatoa nani? Si ni polisi wenyewe? Unayaamini vipi? Au tumesahau yale ya kina Zombe?
 
Askari wamegeuka Mahakama kitaambo sana na hii ilichochewa na Kauli za Baadhi ya Watawala hasa zile zilizowahi kutolewa kutoka kwa Mhimili ulio jichimbia,Wananchi nao wamekuwa wapole sana kiasi ime zoeleka sasa ni mwendo wa kuuwana na kutafutiana jina baya ili kuhalalisha mauaji.Tukumbuke Maiti haina usemi tena so inaweza kusingiziwa chochote na ikakubalika.
 
Kumekuwa na utaratibu ambao umezoeleka wa askari wetu kutoka kwenye vyombo vya habari na kujisifia kua wameua majambazi!

Binafsi sifurahii hii picha askari wanayoitoa, sijui wewe!

Tunajuaje kama hawa ni majambazi kweli?
Au ukishaitwa jambazi na askari tayari unakua jambazi!

Mahakama ni ya nini kama askari wanatoa hukumu wenyewe?
Utaratibu huu ukiachwa uendelee, yeyote kati yetu na siku yoyote anaweza kuitwa jambazi na kupigwa risasi za kutosha!

Askari anaposema ameua jambazi ni nani mwingine anayeenda kuchunguza kuhakiki kama aliyeuawa ni jambazi?
Hizi roadside justice zinazotumika kupandisha watu vyeo, sikumoja zitatupoteza.

Kama askari amepata taarifa kuwa kuna uhalifu unataka kutokea, kwanini asimkamate mshukiwa na kuepusha uhalifu kabla haujatokea?
Kwanini ajipange tu kuua?

Kuna tabia katikati yetu hazipaswi kupewa nafasi!
Ukatili na kuhalalisha mauaji katija awamu hii ni moja ya vitu vinavyoshusha heshima yetu kama taifa!
Hizo ni porojo tuu jf. Ulishakuwa kwenye medani wewe? Tujibizane risasi nimkwangue nisijisifu! Nieleze ni wapi jambazi kauwawa bila majibizano ya risasi? Usilete siasa kwenye mapambano wewe!
 
Kama na wewe ni jambazi kaa chonjo !
Kwa taarifa yako rate ya ujambazi nchini imeshuka sana ,wewe jipendekeze,tutakupitia na tutajigamba pia

Umeelewa kinacho zungumziwa Mkuu ,hebu soma tena sababu Mauaji yapo na Wezi bado wapo.
 
Maelezo haya, kuwa kulikuwa na majibizano ya risasi anayatoa nani? Si ni polisi wenyewe? Unayaamini vipi? Au tumesahau yale ya kina Zombe?
Usichukulie senario moja tuu uka justify kwa kila tukio. Mara ngapi askari wanauwawa na kujeruhiwa na majambazi?
 
Hizo ni porojo tuu jf. Ulishakuwa kwenye medani wewe? Tujibizane risasi nimkwangue nisijisifu! Nieleze ni wapi jambazi kauwawa bila majibizano ya risasi? Usilete siasa kwenye mapambano wewe!

Unao uhakika kuwa walio uwawa wote kwenye Majibizano walikuwa ni Wezi !?..

Unaikumbuka Kesi ya Zombe na Askari wenzie !?

Unakumbuka walicho tuaminisha katika Taarifa zao na Ukweli halisi ulio semwa Mahakamani !?
 
Mara nyingi kama siyo mara zote wanaodhaniwa kuwa majambazi huuawa na polisi katika majibizano ya risasi. Sijawahi sikia polisi wamemkuta mtu anayedhaniwa jambazi wakampiga risasi bila yeye kutumia nguvu kukimbia. Kama wewe ungekuwa polisi kuna mtu hujui kama ni jambazi au la anarusha risasi ungeenda kumkamata kwa mikono? Nadhani usingekuwepo duniani. Mtu yeyote akirusha risasi lazima ajibiwe na risasi za polisi na ikiwezekana auawe tu maana akikimbia na hiyo silaha madhara yake ni makubwa.
Safi sana polisi yeyote akiwarushia risasi lazima ajibiwe kwa risasi akipona bahati yake.
Si mara zote, jaribu kufuatilia, wakati mwingine Polisi wanasema kuwa walikuwa na Mtuhumiwa ama watuhumiwa kwenda kuwaonyesha mazingira waliokuwa wameficha siraha na mara mtuhumiwa ama watuhumiwa wakaanza kukimbia na ndiyo wakaanza kuwarushia ili wasimame. Je inaingia akilini kweli Umeshamshika Mtuhumiwa na wakati anaenda kuonyesha huko anakimbia, hii kwa kweli haiingii kichwani. Na pia kama ingekuwa ni kwa kesi moja naweza kukubali lakini sasa sababu inakuwa ileile kila mara eti alikuwa anakimbia inawezekana vipi? Labda waseme hawana vifaa ama zana za kutosha, ila kwa maoni yangu vifaa vya kazi wanavyo, na wanaweza kuwafunga pingu mikononi na miguuni kama tunavyoona kule kwa mabeberu wakati wanawashikilia watu hatari
 
Back
Top Bottom