Baada ya askari anayesemekana kutukunwa na mke wa waziri wa mambo ya Nje kupost audio aliyeirekodi mitandaoni katika mazungumzo yaliyojumuisha bosi wake pamoja na mke wa waziri (Mama Mahiga), licha ya kitendo hicho kimemsadia kumpandisha cheo lakini kwa upande wa pili wa maadili/taratibu na kanuni za Jeshi la polisi lipo swali la kujiuliza kama kitendo cha kurekodi mazungumzo kati yake na bosi wake pamoja mke wa Mahiga akiwa kazini na kupost katika mitandao ya kijamii kama kitendo hichoo kilifuata maadili/kanuni na Taratibu za Jeshi la polisi ?
Ili kulijibu swali hili inatupasa kufahamu kuwa Jeshi la polisi linaongozwa kwa taratibu,kanuni na sheria ambazo zinatakiwa kufutwa kwa asilimia mia moja kinyume cha hapo askari ambaye amekiuka ni lazima akabiliwe na kosa la kinidhamu na hatua dhidi yake huchukuliwa pasipo kuchelewa.
Ili kubaini kama askari huyu alifanya makosa ya kimaadili kupost mitaandaoni, mwanasheria yeyote atapaswa kuzisoma kanuni za polisi yaani THE POLICE FORCE SERVICE REGULATIONSI G.N. No. 162 of 1998, napia anapswa kusoma P.G.O yaani Police General Orders, ambapo katika sheria zote mbili zinakifungu kinachosema without due authority discloses or conveys any information concerning any investigation or other police or departmental kwa hiyo sheria zote mbili zimeanisha ni kosa kwa askari kutoa taarifa zinahusu upelelezi, ama taarifa za askari wengine ama taarifa zinahusu idara yoyote ya polisi bila ya kuwa na mamlaka.
Kwa kuangalia kanuni,taratibu, na sheria zinazotawala Jeshi la Polisi na hata majeshi mengine yanayoamini katika nidhamu kitendo alichokifanya askari huyo cha kupost mitandaonii mazungumzo akiwa kazini kama askari,yamekiuka kabisa kanuni,taratibu na sheria za jeshi ambapo hatua za kinidhamu zilipaswa kuchukuliwa dhidi yake.ikizingatiwa kwa cheo chake hakuwa na mamlaka ya kutoa habari.
NA PIA ieleweke sio polisi tuu na askari waliowekewa mipaka ya kutoa taarifa za taasisi, pia hata watumishi wengine wa umma nao hawaruhusiwi kutoa taarifa zozote zinahusu taasisi bila ya kibali au bila ya kuwa na mamlaka kufanya hivyo, hivyo bado nasisitiza askari huyo alivunja maadili ya jeshi na pia hata angekuwa mtumishi wa umma katika taasisi nyingine za serikali na hata za binafsi pia angekuwa amekiuka maadili, licha ya ujasiri aliouonesha katika kazi yake anapaswa kupongezwa na kupandishwa cheo lakini kwa upande mwingine anapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa kukiuka taratibu na kanuni za Jeshi la polisi ili uwe mfano kwa askari wengine hali hii isipozibitiwa na ikaendelea kushabikiwa itaruhusu uvunjwaji wa kanuni na misingi ya nidhamu ya Jeshi la Polisi.
Ili kulijibu swali hili inatupasa kufahamu kuwa Jeshi la polisi linaongozwa kwa taratibu,kanuni na sheria ambazo zinatakiwa kufutwa kwa asilimia mia moja kinyume cha hapo askari ambaye amekiuka ni lazima akabiliwe na kosa la kinidhamu na hatua dhidi yake huchukuliwa pasipo kuchelewa.
Ili kubaini kama askari huyu alifanya makosa ya kimaadili kupost mitaandaoni, mwanasheria yeyote atapaswa kuzisoma kanuni za polisi yaani THE POLICE FORCE SERVICE REGULATIONSI G.N. No. 162 of 1998, napia anapswa kusoma P.G.O yaani Police General Orders, ambapo katika sheria zote mbili zinakifungu kinachosema without due authority discloses or conveys any information concerning any investigation or other police or departmental kwa hiyo sheria zote mbili zimeanisha ni kosa kwa askari kutoa taarifa zinahusu upelelezi, ama taarifa za askari wengine ama taarifa zinahusu idara yoyote ya polisi bila ya kuwa na mamlaka.
Kwa kuangalia kanuni,taratibu, na sheria zinazotawala Jeshi la Polisi na hata majeshi mengine yanayoamini katika nidhamu kitendo alichokifanya askari huyo cha kupost mitandaonii mazungumzo akiwa kazini kama askari,yamekiuka kabisa kanuni,taratibu na sheria za jeshi ambapo hatua za kinidhamu zilipaswa kuchukuliwa dhidi yake.ikizingatiwa kwa cheo chake hakuwa na mamlaka ya kutoa habari.
NA PIA ieleweke sio polisi tuu na askari waliowekewa mipaka ya kutoa taarifa za taasisi, pia hata watumishi wengine wa umma nao hawaruhusiwi kutoa taarifa zozote zinahusu taasisi bila ya kibali au bila ya kuwa na mamlaka kufanya hivyo, hivyo bado nasisitiza askari huyo alivunja maadili ya jeshi na pia hata angekuwa mtumishi wa umma katika taasisi nyingine za serikali na hata za binafsi pia angekuwa amekiuka maadili, licha ya ujasiri aliouonesha katika kazi yake anapaswa kupongezwa na kupandishwa cheo lakini kwa upande mwingine anapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa kukiuka taratibu na kanuni za Jeshi la polisi ili uwe mfano kwa askari wengine hali hii isipozibitiwa na ikaendelea kushabikiwa itaruhusu uvunjwaji wa kanuni na misingi ya nidhamu ya Jeshi la Polisi.