Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Leo asubuhi nimeona kituko cha ajabu sana kuhusiana na askari mmoja wa kampuni binafsi ya ulinzi akiwa lindoni kwenye duka la kubadilishia fedha Snow Crest mtaaa India street akiwa amesimama mlangoni akiwa ameshika bunduki huku amelewa chakari huku anaikok bunduki yake na kuwatishia watu waliokua wanapita, mtaa mzima watu akawa amechanganyikiwa wasijue la kufanya, lakini muda si mrefu wahusika wa pale dukani wakapiga simu kwenye kampuni iliyo muajiri pamoja na polisi wakafika hapo na kumyang'anya ile silaha nakuondoka naye. Pamoja na kunyang'anya silaha hiyo ilikua ni mbinde mpaka jamaa alipozidiwa nguvu. Hayo ndio mambo mseto asubuhi hii jijini Arusha.