Jana nilikuwa nasafiri kwa gari kutoka Posta kwenda Sinza. Nilipofika opposite na Mahakama ya Ndizi (baada ya Barabara inayoenda Mabibo) kushoto niliona watu wengi sana wamekusanyika.
Kila mtu alifikiri kuna ajali imetokea. Baada ya kuuliza waliokuwepo walisema askari wawili wa JWTZ walikuwa wakimwamuru mpiga debe mmoja kuogelea kwenye maji machafu ya Mtaro. Nilipofika Sinza nilisikia mtu mmoja akisema alikuwepo kwenye hilo tukio la kikatili na huyo mpiga debe alikuwa akiambiwa kuogelea kutoka upande mmoja aliopo askari mmoja kwenda upande mwingine alioko pia askari na kurudi.
Huyo shuhuda alisema kisa ni kwamba askari mmojawapo aliibiwa simu yake ya mkononi wiki iliyopita na hivyo walichokuwa wakifanya ilikuwa ni kutokana na huo wizi. Nilisikitika sana. Ni wazi kuwa hao askari hawakuwa wametumwa na mkuu wao wa kazi kufanya ukatili kama huo kwa mtu ambaye pengine hakuhusika kabisa na wizi uliotokea.
Huwa nasikia askari akifanyiwa kosa eneo fulani basi huenda kuwakusanya wenzake na kwenda kwenye hilo eneo na kuanza kupiga raia yeyote watakayemkuta. Je, hii ndiyo nidhamu ya jeshi letu. Na kama mambo kama haya yanafanyika wakati tuna amani, kukitokea machafuko askari wetu wata'behave' namna gani? Kwa kweli inasikitisha na hii si utawala bora au wa sheria./COLOR]
Kila mtu alifikiri kuna ajali imetokea. Baada ya kuuliza waliokuwepo walisema askari wawili wa JWTZ walikuwa wakimwamuru mpiga debe mmoja kuogelea kwenye maji machafu ya Mtaro. Nilipofika Sinza nilisikia mtu mmoja akisema alikuwepo kwenye hilo tukio la kikatili na huyo mpiga debe alikuwa akiambiwa kuogelea kutoka upande mmoja aliopo askari mmoja kwenda upande mwingine alioko pia askari na kurudi.
Huyo shuhuda alisema kisa ni kwamba askari mmojawapo aliibiwa simu yake ya mkononi wiki iliyopita na hivyo walichokuwa wakifanya ilikuwa ni kutokana na huo wizi. Nilisikitika sana. Ni wazi kuwa hao askari hawakuwa wametumwa na mkuu wao wa kazi kufanya ukatili kama huo kwa mtu ambaye pengine hakuhusika kabisa na wizi uliotokea.
Huwa nasikia askari akifanyiwa kosa eneo fulani basi huenda kuwakusanya wenzake na kwenda kwenye hilo eneo na kuanza kupiga raia yeyote watakayemkuta. Je, hii ndiyo nidhamu ya jeshi letu. Na kama mambo kama haya yanafanyika wakati tuna amani, kukitokea machafuko askari wetu wata'behave' namna gani? Kwa kweli inasikitisha na hii si utawala bora au wa sheria./COLOR]