Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Watu wengi wasichoelewa ni kwamba vurugu na mkanganyiko inaoukabili Chadema kwa sasa ilikuwa ni programu maalum iliyopangwa ili kuimaliza Chadema baada ya kuona nguvu za Chadema na kukubalika kwake kwa wananchi kulizidi kuongezeka. Mkakati uliopangwa ilikuwa kutumia kila mbinu ili ikiwezekana kuiondoa kabisa Cahdema katika wigo wa siasa nchini.
Mkakati huu pia ulihusu propaganda dhidi yao, kutia ndani kununua viongozi ambao walitakiwa kuihujumu Chadema wakiwa ndani ya Chadema, mashitaka na kufungwa kwa viongozi, kunyamazishwa Bungeni kwa kila namna, kuzuiwa kufanya mikutano ili wasiongeze ushawishi kwa wananchi, kununuliwa kwa viongozi wake nk. Kuna kila dalili kwamba mbinu mojawapo ilihusu hata kuuwawa kwa viongozi wake!
Katika suala la propaganda, timu za watu ziliandaliwa ili kukosoa na kukashifu kila walichofanya, kutia ndani katika vyombo vya habari na hata mitandao ya jamii. Kuna watu walilipwa kwa kufanya hili. Mkakati ulihusu pia viongozi wa ngazi za wilaya na mkoa kuhusishwa katika kampeni hii. Vyombo vya dola vilitumiwa na watauele wa juu waliambiwa hili wazi.
Kwa mkakati uliopangwa kuimaliza Chadema haingekuwa rahisi kwa chama chochote kupona. Na hili lilifanya iwe rahisi kutokana na udhaifuwa mbalimbali wa kiuongozi ndani ya Chadema. Ksingizio kimojawapo kilichotumiwa ni kwamba Chadema wakichukua nchi wataiuza kwa wageni au kusababisha vurugu nchini kwa kulipiza visasi kwa viongozi waliopita hata maraisi, hivyo lazima wapigwe vita kwa kila namna! Na ilisemwa pia watavunja muungano. Na pia watu waliaminishwa kwamba ni chama cha kijimbo, kitu ambacho toka zamani hata Nyerere alijaribu ku-supress ujimbo huo.
Mbinu nyingine iliyopangwa ilikuwa kuwafanya waonekane hawafai ukilinganishwa na vyama vingine vya siasa, na hususa chama kidogo kilichoonekana hakina nguvu, NCCR, kilitumiwa kufanikisha hili. Na ndio maana nasema wazi kwamba urafiki wa NCCR kwa CCM ni wa kimkakati sana dhidi ya Chadema, na utakuwapo ili mradi NCCR haifikii kuwa tishio kwa chama tawala. NCCR wasidhani kwamba wakianza kuwa na nguvu kama Chadema watabaki kuonwa rafiki wa CCM. James Mbatia anatumiwa bila kujitambua - kama hajatambua hilo.
Nimeamua kuyasema haya kwa kuwa binafsi nachukizwa na mbinu hizi chafu katika siasa za Tanzania. Kama Mtanzania, sina tatizo kuona CCM au Chadema au NCCR nk wakiwa chama tawala, lakini ningependa kuwepo chama cha upinzani nchini chenye kutoa changamoto kwa chama tawala kwa ajili ya kuchochea maendeleo nchini. Kupanga mkakati wa kukimaliza chama kikubwa cha upinzani ni uroho wa madaraka, umasikini mkubwa wa uwezo wa kufikiri, na ukosefu wa uzalendo wa kiwango cha juu kabisa.
Inasikitisha sana kuona kwamba uchanga wa upeo wa kuelewa mambo wa Watanzania wengi unafanya wasione mchezo mchafu unaofanyika dhidi ya Chadema. Huu mkakati mchafu haukuwa dhidi ya Chadema tu, ulikuwa dhidi ya Watanzania wote. Matumaini yangu ni kwamba kuna siku Watanzania wataamka na kuelewa jinsi gani katika nchi yetu kuna watu wanacheza siasa chafu sana kwa faida yao binafsi na si kwa maslahi ya Tanzania
Mkakati huu pia ulihusu propaganda dhidi yao, kutia ndani kununua viongozi ambao walitakiwa kuihujumu Chadema wakiwa ndani ya Chadema, mashitaka na kufungwa kwa viongozi, kunyamazishwa Bungeni kwa kila namna, kuzuiwa kufanya mikutano ili wasiongeze ushawishi kwa wananchi, kununuliwa kwa viongozi wake nk. Kuna kila dalili kwamba mbinu mojawapo ilihusu hata kuuwawa kwa viongozi wake!
Katika suala la propaganda, timu za watu ziliandaliwa ili kukosoa na kukashifu kila walichofanya, kutia ndani katika vyombo vya habari na hata mitandao ya jamii. Kuna watu walilipwa kwa kufanya hili. Mkakati ulihusu pia viongozi wa ngazi za wilaya na mkoa kuhusishwa katika kampeni hii. Vyombo vya dola vilitumiwa na watauele wa juu waliambiwa hili wazi.
Kwa mkakati uliopangwa kuimaliza Chadema haingekuwa rahisi kwa chama chochote kupona. Na hili lilifanya iwe rahisi kutokana na udhaifuwa mbalimbali wa kiuongozi ndani ya Chadema. Ksingizio kimojawapo kilichotumiwa ni kwamba Chadema wakichukua nchi wataiuza kwa wageni au kusababisha vurugu nchini kwa kulipiza visasi kwa viongozi waliopita hata maraisi, hivyo lazima wapigwe vita kwa kila namna! Na ilisemwa pia watavunja muungano. Na pia watu waliaminishwa kwamba ni chama cha kijimbo, kitu ambacho toka zamani hata Nyerere alijaribu ku-supress ujimbo huo.
Mbinu nyingine iliyopangwa ilikuwa kuwafanya waonekane hawafai ukilinganishwa na vyama vingine vya siasa, na hususa chama kidogo kilichoonekana hakina nguvu, NCCR, kilitumiwa kufanikisha hili. Na ndio maana nasema wazi kwamba urafiki wa NCCR kwa CCM ni wa kimkakati sana dhidi ya Chadema, na utakuwapo ili mradi NCCR haifikii kuwa tishio kwa chama tawala. NCCR wasidhani kwamba wakianza kuwa na nguvu kama Chadema watabaki kuonwa rafiki wa CCM. James Mbatia anatumiwa bila kujitambua - kama hajatambua hilo.
Nimeamua kuyasema haya kwa kuwa binafsi nachukizwa na mbinu hizi chafu katika siasa za Tanzania. Kama Mtanzania, sina tatizo kuona CCM au Chadema au NCCR nk wakiwa chama tawala, lakini ningependa kuwepo chama cha upinzani nchini chenye kutoa changamoto kwa chama tawala kwa ajili ya kuchochea maendeleo nchini. Kupanga mkakati wa kukimaliza chama kikubwa cha upinzani ni uroho wa madaraka, umasikini mkubwa wa uwezo wa kufikiri, na ukosefu wa uzalendo wa kiwango cha juu kabisa.
Inasikitisha sana kuona kwamba uchanga wa upeo wa kuelewa mambo wa Watanzania wengi unafanya wasione mchezo mchafu unaofanyika dhidi ya Chadema. Huu mkakati mchafu haukuwa dhidi ya Chadema tu, ulikuwa dhidi ya Watanzania wote. Matumaini yangu ni kwamba kuna siku Watanzania wataamka na kuelewa jinsi gani katika nchi yetu kuna watu wanacheza siasa chafu sana kwa faida yao binafsi na si kwa maslahi ya Tanzania