Kamgomoli
JF-Expert Member
- May 3, 2018
- 1,865
- 3,802
Ukisikiliza au kutazama vyombo vya habari vya Tanzania utagundua "serious stories" ni chache sana licha ya kuwa na utitiri wa vyombo vya habari kuanzia "main stream media hadi TV za mtandaoni.
Kuna mambo mazito yanayoendelea nchini na yanahitaji mijadala mizito. Mfano:
1. Katiba mpya
2. Udhaifu wa mihimili ya mahakama na Bunge.
3. Mgogoro wa Loliondo
4. Kuongezeka kwa kasi kwa Deni la Taifa na
5. Kuongezeka kwa gharama za maisha.
6. Mjadala kuhusu Bajeti ya 2022/2023.
7. "Updates" ya Miradi mikubwa ya kimkakati km SGR na Bwawa la Mwl. Nyelele.
8. Miradi ya gesi n.k
Haya ni mambo ambayo ni vema Watanzania wakawa wanayasikia kila mara kujua kinachoendelea na kujadili nini kifanyike.
Kwa wenzetu Kenya kwa mfano, ukifungulia TV asubuhi unakutana na jopo la wachambuzi wabobezi( Panelists) wakijadili current issues very serious and deeply about their Nation.
Sisi kwetu kutwa nzima story ni Simba vs Yanga, Music na habari za umbea. TV za mitandaoni ndo kabisaa! Ujinga wote umejaa huko. Mijadala ni Kufumaniana, mapenzi ya Konde na kajala na upuuzi mwingine. Ni Tanzania pekee ambako machawa wanahusudiwa na kupewa udhamini (endorsement) kwa sababu ya uchawa wao.
What a shameful country! kwamba Baba Levo na Mwijaku ni "ma-rolemodel" wa watoto wetu,tunajenga taifa gani baadae?
Miaka ya nyuma wakati magezeti yana nguvu kipindi km hiki cha Bunge la bajeti ilikuwa moto sana. Ni kupitia mijadala mikali na uandishi wa kiuchunguzi ndipo kuliibuliwa kashifa kubwa kubwa km Richmond, Dowans n.k. Ndio maana sasa hivi akina Mwigulu wametuandalia bajeti mbovu kuwahi kutokea lakini hakuna " criticism" zozote. Sisi vyovyote sawa tu muhimu ni Yanga na Simba yetu.
Hata bungeni pia kumekuwa na utoto na mzaha mwingi kuhusu Yanga na Simba. Utazani tuliwatuma wakazodoane kuhusu mpira. Taifa limefanywa kuwa la mizaha mizaha kwa mgongo wa Simba na Yanga. Wanasiasa wanafurahia kwani ni rahisi sana kuongoza watu wasiojali mijadala na hoja nzito.
TV au Radio wanaofanya mijadala, wanafanya kwa namna ya komedi. Wachambuzi wenyewe ndo akina Mwijaku, Baba Levo, Zembwela na Mpoki. Kipindi kizima ni makelele na kucheka cheka tu. Nchi hii ukisha kuwa maarufu no matter ni umaarufu wa nini basi wewe tayari ni zaidi ya Profesa. Mtu yupo tayari ajidhalilishe ili apate umaarufu.Watu wamefunga hadi ndoa feki just for the kiki and trending. Very disgusting!
Taifa limekuwa la machawa,watengeneza kiki na wambea.Ili kijana a-make maisha kirahisi lazima eti afuate huo mkondo.
Tunaenda kujenga Taifa la ajabu ajabu sana kama tusipobadirika.
Nawasilisha.
Kuna mambo mazito yanayoendelea nchini na yanahitaji mijadala mizito. Mfano:
1. Katiba mpya
2. Udhaifu wa mihimili ya mahakama na Bunge.
3. Mgogoro wa Loliondo
4. Kuongezeka kwa kasi kwa Deni la Taifa na
5. Kuongezeka kwa gharama za maisha.
6. Mjadala kuhusu Bajeti ya 2022/2023.
7. "Updates" ya Miradi mikubwa ya kimkakati km SGR na Bwawa la Mwl. Nyelele.
8. Miradi ya gesi n.k
Haya ni mambo ambayo ni vema Watanzania wakawa wanayasikia kila mara kujua kinachoendelea na kujadili nini kifanyike.
Kwa wenzetu Kenya kwa mfano, ukifungulia TV asubuhi unakutana na jopo la wachambuzi wabobezi( Panelists) wakijadili current issues very serious and deeply about their Nation.
Sisi kwetu kutwa nzima story ni Simba vs Yanga, Music na habari za umbea. TV za mitandaoni ndo kabisaa! Ujinga wote umejaa huko. Mijadala ni Kufumaniana, mapenzi ya Konde na kajala na upuuzi mwingine. Ni Tanzania pekee ambako machawa wanahusudiwa na kupewa udhamini (endorsement) kwa sababu ya uchawa wao.
What a shameful country! kwamba Baba Levo na Mwijaku ni "ma-rolemodel" wa watoto wetu,tunajenga taifa gani baadae?
Miaka ya nyuma wakati magezeti yana nguvu kipindi km hiki cha Bunge la bajeti ilikuwa moto sana. Ni kupitia mijadala mikali na uandishi wa kiuchunguzi ndipo kuliibuliwa kashifa kubwa kubwa km Richmond, Dowans n.k. Ndio maana sasa hivi akina Mwigulu wametuandalia bajeti mbovu kuwahi kutokea lakini hakuna " criticism" zozote. Sisi vyovyote sawa tu muhimu ni Yanga na Simba yetu.
Hata bungeni pia kumekuwa na utoto na mzaha mwingi kuhusu Yanga na Simba. Utazani tuliwatuma wakazodoane kuhusu mpira. Taifa limefanywa kuwa la mizaha mizaha kwa mgongo wa Simba na Yanga. Wanasiasa wanafurahia kwani ni rahisi sana kuongoza watu wasiojali mijadala na hoja nzito.
TV au Radio wanaofanya mijadala, wanafanya kwa namna ya komedi. Wachambuzi wenyewe ndo akina Mwijaku, Baba Levo, Zembwela na Mpoki. Kipindi kizima ni makelele na kucheka cheka tu. Nchi hii ukisha kuwa maarufu no matter ni umaarufu wa nini basi wewe tayari ni zaidi ya Profesa. Mtu yupo tayari ajidhalilishe ili apate umaarufu.Watu wamefunga hadi ndoa feki just for the kiki and trending. Very disgusting!
Taifa limekuwa la machawa,watengeneza kiki na wambea.Ili kijana a-make maisha kirahisi lazima eti afuate huo mkondo.
Tunaenda kujenga Taifa la ajabu ajabu sana kama tusipobadirika.
Nawasilisha.