Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,049
- 12,418
Hii ishu ya watu wa Dodoma kuwa ombaomba ni ya kihistoria. Ilianza zamani enzi za misafara ya biashara kutoka Bagamoyo hadi Ujiji. H. M. Stanley ameliandika vema hili katika kitabu chache How i Found Livingstone(1871).
Zamani kila misafara inakopita ilitakiwa kuacha kodi(Hongo)kwa chifu. Mara nyingi kodi hii ilikuwa vipande vya nguo(doti) Na hakuna watu waliokuwa wanategemea Na kutoza hongo kubwa kama Wagogo. Pia wakazi wa Ugogo walikuwa wanasumbua sana kambi za wasafiri. Wakiomba na kujaribu kuiba. Kabla hajaanza safari, Stanley alitaarifiwa jambo hilo. Hivyo alinunua rasmi mbwa kwaajili ya kufukuza wagogo kambini mwake. Bahati mbaya alikufa kabla hajafika Ugogo.
Kuna kipindi wagogo wengi sana walijaa kambini kwake wakitaka chochote. Ikabidi achukue mjeledi kuanza kuwafukuza. Mara wakamind kuwa mzungu anatupigaje kwenye nchi yetu. Hadi mjumbe wa chifu alipokuja kuwafukuza akiwatishia kuwa atakayeonekana kambini kwa mzungu atatozwa faini ndipo alipopata ahueni.
Machifu wa kigogo walikuwa wanatoza kodi kubwa kuliko machifu wote. Karibu na kumaliza kupita Ugogo, Stanley alilazimika kupita njia za porini ili kumuepuka chifu aliyesifika kwa kutoza kodi kubwa kupita kiasi.
Hii habari ya watu wa Dodoma kuombaomba imeanza mbali sana.
Zamani kila misafara inakopita ilitakiwa kuacha kodi(Hongo)kwa chifu. Mara nyingi kodi hii ilikuwa vipande vya nguo(doti) Na hakuna watu waliokuwa wanategemea Na kutoza hongo kubwa kama Wagogo. Pia wakazi wa Ugogo walikuwa wanasumbua sana kambi za wasafiri. Wakiomba na kujaribu kuiba. Kabla hajaanza safari, Stanley alitaarifiwa jambo hilo. Hivyo alinunua rasmi mbwa kwaajili ya kufukuza wagogo kambini mwake. Bahati mbaya alikufa kabla hajafika Ugogo.
Kuna kipindi wagogo wengi sana walijaa kambini kwake wakitaka chochote. Ikabidi achukue mjeledi kuanza kuwafukuza. Mara wakamind kuwa mzungu anatupigaje kwenye nchi yetu. Hadi mjumbe wa chifu alipokuja kuwafukuza akiwatishia kuwa atakayeonekana kambini kwa mzungu atatozwa faini ndipo alipopata ahueni.
Machifu wa kigogo walikuwa wanatoza kodi kubwa kuliko machifu wote. Karibu na kumaliza kupita Ugogo, Stanley alilazimika kupita njia za porini ili kumuepuka chifu aliyesifika kwa kutoza kodi kubwa kupita kiasi.
Hii habari ya watu wa Dodoma kuombaomba imeanza mbali sana.