Asili ya watu wa Dodoma kuwa ombaomba

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,049
12,418
Hii ishu ya watu wa Dodoma kuwa ombaomba ni ya kihistoria. Ilianza zamani enzi za misafara ya biashara kutoka Bagamoyo hadi Ujiji. H. M. Stanley ameliandika vema hili katika kitabu chache How i Found Livingstone(1871).

Zamani kila misafara inakopita ilitakiwa kuacha kodi(Hongo)kwa chifu. Mara nyingi kodi hii ilikuwa vipande vya nguo(doti) Na hakuna watu waliokuwa wanategemea Na kutoza hongo kubwa kama Wagogo. Pia wakazi wa Ugogo walikuwa wanasumbua sana kambi za wasafiri. Wakiomba na kujaribu kuiba. Kabla hajaanza safari, Stanley alitaarifiwa jambo hilo. Hivyo alinunua rasmi mbwa kwaajili ya kufukuza wagogo kambini mwake. Bahati mbaya alikufa kabla hajafika Ugogo.

Kuna kipindi wagogo wengi sana walijaa kambini kwake wakitaka chochote. Ikabidi achukue mjeledi kuanza kuwafukuza. Mara wakamind kuwa mzungu anatupigaje kwenye nchi yetu. Hadi mjumbe wa chifu alipokuja kuwafukuza akiwatishia kuwa atakayeonekana kambini kwa mzungu atatozwa faini ndipo alipopata ahueni.

Machifu wa kigogo walikuwa wanatoza kodi kubwa kuliko machifu wote. Karibu na kumaliza kupita Ugogo, Stanley alilazimika kupita njia za porini ili kumuepuka chifu aliyesifika kwa kutoza kodi kubwa kupita kiasi.
Hii habari ya watu wa Dodoma kuombaomba imeanza mbali sana.
 
Hii ishu ya watu wa Dodoma kuwa ombaomba ni ya kihistoria. Ilianza zamani enzi za misafara ya biashara kutoka Bagamoyo hadi Ujiji. H. M. Stanley ameliandika vema hili katika kitabu chache How i Found Livingstone(1871).

Zamani kila misafara inakopita ilitakiwa kuacha kodi(Hongo)kwa chifu. Mara nyingi kodi hii ilikuwa vipande vya nguo(doti) Na hakuna watu waliokuwa wanategemea Na kutoza hongo kubwa kama Wagogo. Pia wakazi wa Ugogo walikuwa wanasumbua sana kambi za wasafiri. Wakiomba na kujaribu kuiba. Kabla hajaanza safari Stanley alitaarifiwa jambo hilo. Hivyo alinunua rasmi mbwa kwaajili ya kufukuza wagogo kambini mwake. Bahati mbaya alikufa kabla hajafika Ugogo.

Kuna kipindi wagogo wengi sana walijaa kambini kwake wakitaka chochote. Ikabidi achukue mjeledi kuanza kuwafukuza. Mara wakamind kuwa mzungu anatupigaje kwenye nchi yetu. Hadi mjumbe wa chifu alipokuja kuwafukuza akiwatishia kuwa atakayeonekana kambini kwa mzungu atatozwa faini ndipo alipopata aueni.

Machifu wa kigogo walikuwa wanatoka kodi kubwa kuliko machifu wote. Karibu na kumaliza kupita Ugogo, Stanley alilazimika kupita njia za porini ili kumuepuka chifu aliyesifika kwa kutoza kodi kubwa kupita kiasi.
Hii habari ya watu wa Dodoma kuombaomba imeanza mbali sana.

Wewe unabifu na the Spika???
 
Dodoma hali ngumu sana. Nikiwa mafunzo ya JKT makutupora mwaka 2001, nilikuwa nikiona wakiokota chakula jalalani nilifikiri wanaenda kupikia nguruwe... Kumbe kile ndo kilikuwa chakula chao. Mwaka ule mvua ilianza kunyesha katikati ya Dec 2001 na ikakata Februari 2002, haikunyesha tena.
Mazao yalinyauka kabisa... Sasa inahitajika akili kubwa sana ku transform maisha ya dodoma, mvua ya asili hakuna kabisa kule
 
Hii ishu ya watu wa Dodoma kuwa ombaomba ni ya kihistoria. Ilianza zamani enzi za misafara ya biashara kutoka Bagamoyo hadi Ujiji. H. M. Stanley ameliandika vema hili katika kitabu chache How i Found Livingstone(1871).

Zamani kila misafara inakopita ilitakiwa kuacha kodi(Hongo)kwa chifu. Mara nyingi kodi hii ilikuwa vipande vya nguo(doti) Na hakuna watu waliokuwa wanategemea Na kutoza hongo kubwa kama Wagogo. Pia wakazi wa Ugogo walikuwa wanasumbua sana kambi za wasafiri. Wakiomba na kujaribu kuiba. Kabla hajaanza safari Stanley alitaarifiwa jambo hilo. Hivyo alinunua rasmi mbwa kwaajili ya kufukuza wagogo kambini mwake. Bahati mbaya alikufa kabla hajafika Ugogo.

Kuna kipindi wagogo wengi sana walijaa kambini kwake wakitaka chochote. Ikabidi achukue mjeledi kuanza kuwafukuza. Mara wakamind kuwa mzungu anatupigaje kwenye nchi yetu. Hadi mjumbe wa chifu alipokuja kuwafukuza akiwatishia kuwa atakayeonekana kambini kwa mzungu atatozwa faini ndipo alipopata aueni.

Machifu wa kigogo walikuwa wanatoka kodi kubwa kuliko machifu wote. Karibu na kumaliza kupita Ugogo, Stanley alilazimika kupita njia za porini ili kumuepuka chifu aliyesifika kwa kutoza kodi kubwa kupita kiasi.
Hii habari ya watu wa Dodoma kuombaomba imeanza mbali sana.
Ila mazingira ya Dodoma sii rafiki sana kuishi hasa kwa watu wasioweza kujiongeza(kutawala mazingira yao) ili kupata chakula cha kutosha. Kwa asili nafikiri ni wafugaji ila sii wakulima wazuri, kwa Waafrica wengi hula nafaka nyama kwa wafugaji sio walaji wazuri pamoja na kuwa na mifugo mingi. Sasa maeneo ya Dodoma sii rafiki sana kwa kilimo. Hapo ndipo issue ya kuomba ilipoanza kujengeka. Mwisho ukitaka kujua hili nisemalo hata kwenye salam zao lazima umuulize mwenzio umekula nini na jibu ni mimekula mlenda na .... Hii inaashiria mlo ni shida au ni jambo la kuuliza kwa jirani au rafiki.
 
Ni mazingira. Hali ya hewa ngumu na fursa ya wasafiri.
kwa kiasi nakubaliana na wewe na hali hii ya kuomba kwa wenyeji imepungua kwa kiasi kikubwa hasa baada ya wageni kuja mji huu na kuongeza fursa za kipato na pia elimu mbalimbali na fursa zingingine zilizotolewa na NGO zimepunguza kiasi kikubwa sana.
changamoto iliyopo ni kuwa kwa sasa Dodoma imevamiwa na waombaji maarufu wa vibiskeli ambao wengi wao sio Wagogo na kwa kuwa wageni hawaelewi na mjini una watu wachache na wao walishakuwa waanzilishi ndivyo wanavyo baki kuhukumiwa.
vinginevyo wakazi wa mji huu hawataacha kumshukuru MWENYEZI MUNGU kwa Magufuli ambaye serikali yake iliwezesha kubadilisha sura ya Dodoma na uchumi wake kwa sasa.
 
Dodoma hali ngumu sana. Nikiwa mafunzo ya JKT makutupora mwaka 2001, nilikuwa nikiona wakiokota chakula jalalani nilifikiri wanaenda kupikia nguruwe... Kumbe kile ndo kilikuwa chakula chao. Mwaka ule mvua ilianza kunyesha katikati ya Dec 2001 na ikakata Februari 2002, haikunyesha tena.
Mazao yalinyauka kabisa... Sasa inahitajika akili kubwa sana ku transform maisha ya dodoma, mvua ya asili hakuna kabisa kule


Makao makuu yatatransform maisha ya Dodoma.
 
Chanzo cha ukame kule dodoma ni nini??

Je kuna miaka ambayo kulikua na mvua za kutosha ama ni hivyo tangu kufahamika kwake??
 
Hapana Kuna dhambi haikutubiwa ndio maana hili tatizo linaendelea hapo
Angalia Singida ilivyobarikiwa Sasa ni kwa sababu Kuna watu wamefanyia kazi tatizo
Sasa hivi They are very blessed.
Cheki maboga yalivyo mengi , mwaka huu pamoja na ukame lakini jamaa ndio wenye mahindi nilikuwa juzi tu mwezi wa nne ziarani
 
Nimeona wachangiaji wengi wamejikita na michango hasi tu mara genetics mara dhambi upuuzi tu,

Nchi ya Wagogo ilipigwa na ukame mkubwa mwaka 1917-1920

Wenyeji waliuita ukame huo "Mtunya" yani "Scramble" ikimbukwe ukame huu ulitokea baada tu ya kumalizika kwa vita ya kwanza ya dunia 1914-1918

Tuende kwenye athari ambazo vita ya kwanza ya dunia ililetea afrika.

Over exploitation of afrika resources to rescue Europe economy after the war

Baada ya vita kumalizika kulitokea upungufu mkubwa chakula hivyo wakoloni walichukua kila kilichowafaa na kupelekwa kwao (mazao, mifugo etc) na hiyo haikutokea ugogoni tu bali tanganyika na hata afrika nzima

Turudi kwenye Ukame mkali "mtunya" ambao uliu wagogo 150k ambayo ilikuwa ni karibu asilimia 90% ya population yote ya wagogo, ikumbukwe kipindi wagogo wanapigwa na ukame na njaa kali serekal8 ya wakoloni inaendelea kupunguza mifugo yao na kuwazuia wagogo kuendelea kuendea kuzalisha chakula kwa kuchukua nguvu kazi kama Labour kwenye plantation zao

Walichofanyiwa wagogo na ukoloni kilipaswa kuitwa genocide kama ilivyokuwa kwa Wanama na Waheroro wa Namibian

Kupoteza asilimia 90% ya population yenu kwa miaka minne sio kitu kidogo hata ikipita miaka mia mbili

**************

"The Gogo, in their own interpretation of the famine, stress the ways in which this famine made them dependent on the colonial economy. For them, this famine represented a terrible loss of autonomy, a loss of the ability to control the reproduction of their own society"
-John Iliffe, The Journal of African History
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom