BigBaba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2017
- 1,909
- 9,038
Asili ya neno "salary" (mshahara) linatokana na neno la Kilatini "sal' ama 'salarium' lililomaanisha "salt" (chumvi), zamani wakati wa Milki ya Warumi (Roman Empire) wanajeshi wa Kirumi walikuwa wakipewa pesa ndogo kwa ajili ya kununulia chumvi. Enzi hizo, chumvi ilikuwa bidhaa adimu na ya anasa, miaka ilivyozidi kwenda neno Salarium lilibadilika na kuwa Salary huku likitumiwa kumaanisha mshahara/ ujira wa kazi.