Asili ya maneno 'Shikamoo' na 'Marahaba' ni utumwa, kwanini tunaendelea kuyatumia?

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
834
Kwa nilivyosikia mimi neno shikamoo maana yake ni "niko chini ya miguu yako.

Pia nimesikia hilo neno ni la kitumwa na lilikuwa linatumiwa na watumwa kuwaonyesha heshima wakuu wao.

Kuna baadhi ya watu nawajua hawapendi kupewa shikamoo na hata wakipewa hawajibu marahaba.

Je kama hili neno ni la kitumwa, kwanini sisi tuendelee kulitumia kama neno linaloashiria heshima?

Kama lilitumika kuwakandamiza mababu zetu kwanini na sisi tulipe nafasi? Au tunalitumia kama wenzetu Wamarekani weusi wanavyo tumia neno "nigga" ambalo lilitumika kudharau mababu zao na kulifanya la kwetu sasa?


Nianze na kuuliza , nini maana ya neno "shikamoo"?

Kuna sehemu nimeona na kusikia kuwa maana yake ni "nipo chini ya miguu yako". Salamu ambayo watumwa walikuwa wanawasalimia mabwana zao (kama maana niliyotoa si sahihi naomba msaada wenu kurekebisha hapo).

Asa swali langu ni dogo tu, Je mpaka sasa bado kuna utumwa hapa Tanzania?!

Ni kutuko maana mpaka mtu mzima mwenye akili zake bila hata aibu anallilia "shikamoo" alaf baada ya hapo anajisifu kuwa eti 'Tanzania hakuna utumwa'

Hivi hili baraza la Kiswahili wanafanya kazi gani sasa?

Nimejaribu kuchunguza kidogo na kubaini kuwa salamu ni kujuliana hali au kutakiana heri! mfano, kwa Kingereza wanasalimia "Good morning" wakimmaniasha asubuhi njema "Good evening" wakimaanisha jiono njema n.k, kwa Kihaya kuna "Ma' Olailoota" mama umalalaje/umeamkaje (kama sijakosea) najua kuwa kuna salamu za makabila mangine mengi tu wakijuliana hali na kutakiana heri. Lakini Kiswahili chetu kinashangaza, eti shikamoo!

Kwa mimi napendelea zaidi "habari za saa hizi", "za saa hizi" au hata "mambo" inatosha sana kulliko hata shikamoo. Ila kutana na kibabu fulani kiambie "za saa hizi" utasikia "mtoto anajifanya amekua huyu eenh!!"
mimi naishia hapo kwa leo.

Nawasilisha Hoja!!

Wadau, labda ni vyema kushare nanyi suryey ambayo tuliifanya muda kidogo, nayo ni kuhusu salam ya 'Shikamoo'.

Katika suryey yetu tukagundua kuwa;

1. Watu wengi hawajui maana ya neno 'Shikamoo' zaidi ya kusema kuwa ni heshima, wengine wakasema ina maana ya 'nipo chini ya miguu yako'

2. Asili yake ni ya kitumwa,yaani walioinzisha hawaitumii kama salamu yao ya kawaida ila walioipokea ndio wanaitumia katika matumizi yao ya kila siku.

3. Ime simama katika kuangalia umri, kitu ambacho muda mwingine ni ngumu kujua au kukisia umri wa mtu sababu waweza muamkia mtu kumbe ni mdogo wako

4. Imejengwa katika nidhamu ya uoga, ndio maana ni rahisi kumkuta mtu mkubwa kiumri ana msalimu mtu mdogo kiumri sababu tu anayeamkiwa ana nguvu kubwa kifedha au kimadaraka.

5. Imepitwa na wakati, yaani wengine hawataki kabisa kuisikia ama wanajishusha umri, ndio maana mtu anaamkiwa anasema poa, au salama.

6.Imesababisha ugomvi au wengine kutosalimiana kwa sababu tu hakuna anayependa kuwa mdogo.

Wadau toeni mapendekezo yenu juu ya kile mliona na mnavyodhani juu ya suala hili...

Wachangiaji mbalimbali waliandika
"Ni kweli shikamoo lina asili ya utumwa..".

Je kuna mtu mwenye uhakika?

Kuna utafiti wa kihistoria?
Jibu "marahaba" ni umbo la salamu ya kawaida ya Kiarabu huko wanasalimiana "marhaba" na jibu ni "marhabteen" (=marhaba mara mbili).

Jinsi ilivyo "Shikamoo" ni moja kati ya salamu katika tamaduni mbalimbali zinazotambua tofauti ya cheo.

* Zamani watu wa Ulaya walipiga magoti mbele mkubwa wakimsalimu;

* watu wa Uajemi walijulikana kwa desturi ya kujitupa chini kabisa ardhini mbele ya mkubwa;

* katika sehemu ya Asia ya kusini watu husalimiana kwa kufunga mikono yote miwili (karibu kama wakatoliki wakisali) na kama ni mkubwa wanashika mikono juu ya kichwa kama ni cheo sawa mbele ya uso na kama ni mdogo chini ya kichwa kifuani.

Tamaduni zilizobadilika sana watu waliacha mara nyingi aina hizi za kusalimia angalia Marekani ambako watu hupeana tu sauti kama "hai" (Hi!) isiyo na maana ndani yake.

Ni juu ya watu kuamua. Binafsi sioni ubaya kumpa mzee maskini heshima ya kifalme kwa kumsalimia kwa "shikamoo".

Nakumbuka watoto wangu walipofika Kenya mara ya kwanza waliwasalimu watu wazima kwa "shikamoo" kote tulikoenda madukani n.k. Walilalamika saaana ya kwamba hawa Wakenya hawakujibu! Ni kweli- nje ya Mombasa hawajui kabisa.

Maana ya shikamoo ni hii ambayo inatumika sasa na Waswahili, hiyo uliyoitoa haipo katika kamusi tunazotumia. Inawezekana ilikuwa inatumika zamani wakati wa utumwa, lakini lugha hubadilika, maneno hubadilika na halikadhalika maana za maneno nazo sio tuli.

Tanzania hakuna utumwa, huu ni mfumo wa maisha na hauwezi kuamuliwa na uwepo wa neno moja tu katika lugha nzima. Kung'amua uwepo wa utumwa ni lazima tuchunguze mifumo ya maisha ya Watanzania na sio kutazama neno moja kisha kuhitimisha.

Watu wazima huwa 'wanalilia' hiyo shikamoo kwa kuwa ndio utaratibu wa jamii kuwa salamu hii itatoka kwa mdogo kwenda kwa mkubwa. Kama ambavyo tu mtu huyu huyu mzima anavyolilia kupishwa siti kwenye daladala wakati haijaandikwa popote.

Baraza la Kiswahili la Taifa hutunga sera ya Lugha pamoja na kuishauri Serikali masuala mbalimbali yanayohusu lugha. Kiswahili hakishangazi, bali kina namna yake ya pekee ya kutazama salamu (Salamu kama kujuliana hali, na salamu kama ishara ya heshima). Wanaofahamu lugha ya kibantu yenye dhana hii pia wanaweza kuja kutufahamisha. Ukishangaa ya Kiswahili inabidi ushangae pia na Kifaransa ambapo majina yake huwa na jinsia (eti kuna gari la kike na la kiume... Inachekesha eeh?)

Kupendelea kutumia aina fulani ya salamu ni haki yako, lakini isije kukugharimu ukweni siku moja (natania tu).

Hoja yako umeiwasilisha vema, karibu sana.
 
Hapo umechukua uhalisia wa neno, lakini katika kiswahili neno hili linatumika kama salamu, tazama mfano mwingine:

mambo: haina maana ya salamu lakini watu wanatumia kama salamu.

upo hapo?
 
MwanaFalsafa1,

Kwa asili neno hilo kweli lilimaanisha hicho ulichosema. Lakini ujue lugha inazaliwa, inakua na kubadilika kadiri jamii inavyobadilika kufuatana na wakati. Kumbe katika lugha nyingi - si Kiswahili tu - misamiati imenyumbuka, kubadilika na hata kuwa na maana tofauti na ile ya mwanzo. Ndiyo maana kuna kitu kinaitwa etymology ya neno au msamiati.

Kwa hiyo neno "shikamoo" lenye asili ya Kiarabu lilimaanisha kujidunisha chini ya bwana. Lakini kadiri muda ulivopita, na hasa neno lilivoingia katika lugha ya Kiswahili, lilibadilika maana yake badala ya ile kitumwa likamaanisha Heshima ya mdogo kwa mkubwa wake. Kumbe likawa na maana chanya badala ya ile hasi.

Kumbe wanaokataa kupokea "shikamoo" hawajui tu. Waelimishwe wajue kwamba kwa leo tena kwa Kiswahili lina maana nzuri tu japo kiasili likuwa na maana hasi ya kudhalilisha.
 
Last edited by a moderator:
Ndio maana linatumika kumsalimia mtu aliyekuzidi umri, kwa ajili ya heshima uliyonayo kwake.......
 
Ndio maana mtoto hawezi kumsalimia mtoto mwenzake "Shikamoo" au watu wenye umri unaolingana hawasalimiani shikamoo.....
SALAMU YA SHIKAMOO NI KWA AJILI YA KUMSALIMIA MTU ALIYEKUZIDI UMRI TUU.............
 
Nafikiri matumizi yake kwa sasa ni tofauti na zamani. Kama ndiyo hivyo hata maana yake pia itakuwa imebadirika na kuchukuliwa kama linavyotumika kwa sasa yaani salamu za mdogo kwenda kwa mkubwa.
 
MwanaFalsafa1,

Kila kitu ulichoandika hapo juu umepatia. Ni neno la kitumwa kweli lakini ndio hivyo mababu zetu kwa kupenda umwinyi wakaliendeleza tu. Mara nyingi mimi huwa nalikuwepa neno hilo kwa kutumia "asalam aleykum".
 
Last edited by a moderator:
Sawa ni salamu ya mdogo kwa mkubwa lakini inakuwaje pale inapotokea unashindwa kukadiria kwa haraka umri wa unayemsalimia na umri wako? Unapompa mtu shikamoo kumbe ulitakiwa wewe kupewa hiyo shikamoo, hapa huwa haileti picha nzuri kwakweli
 
Sawa ni salamu ya mdogo kwa mkubwa lakini inakuwaje pale inapotokea unashindwa kukadiria kwa haraka umri wa unayemsalimia na umri wako? Unapompa mtu shikamoo kumbe ulitakiwa wewe kupewa hiyo shikamoo, hapa huwa haileti picha nzuri kwakweli
Nawapa shikamoo walionizidi miaka mitano au zaidi. Sio rahisi nikaenda fyongo
 
kila kitu ulichoandika hapo juu umepatia.ni neno la kitumwa kweli lakini ndio hivyo mababu zetu kwa kupenda umwinyi wakaliendeleza tu.mara nyingi mimi huwa nalikuwepa neno hilo kwa kutumia "asalam aleykum" .

Mzee Wenger vipi bwana? hata hiyo pia siyo asilia tumekopi mahali!
Labda ungekuwa unasema "habari za saa hizi, za leo, za siku nk"

Au uwe unasalimia kilugha, huwa hakina ukubwa au udogo;
Solowenyo.......inajibiwa solowenyo
Mihanyenye ....... Misaha
Wabonaki........Nabonakantu
Ulmphola...........
Nazinginezo... zinasidia sana kuikwepa shikamoo, upo?
 
Ndio maana linatumika kumsalimia mtu aliyekuzidi umri, kwa ajili ya heshima uliyonayo kwake.......

Hili neno hata mimi huwa linanipa maswali nikifikiria historia. Kwani TUK (Taasis ya Uchunguzi wa Kiswahili) katika tafiti zao mbalimbali hawajaweza kupata neno lingine kutoka makabila yaliyopo Tanzania kama mbadala wake?

Kwenye kabila langu kwa mfano, hakuna neno linalofanana na shikamoo! Zipo salamu za kila wakati zenye kuonyesha heshima kwa waliokuzidi umri. Naamini hata makabila mengine wanayo.

Ila inavyoonekana SHIKAMOO IS HERE TO STAY!
 
Mimi huwa inanikera kumsalimia shiakamoo mtu ninayemzidi umri at. kwa sababu ni shemeji yako Mkubwa yaani dada mkubwa wa mke au mama mdogo wa mke amabye labda unamzidi miaka 10. mambo ya uswahilini utakuta wanaidai kabisa. Kwangu shikamoo siyo salaam mbaya kwa anayekuzidi umri zaidi ya miaka 5
 
Bado ukweli uko palepale kwamba hili neno lilikuwepo kukandamizwa watumwa(haswa sisi weusi), iweje tulichukue na kulifanya letu?

Kama WoS alivyo sema kwani hamna neno mbadala? Iweje kumuambia mtu nipo chini ya miguu yako iwe heshima? Kwani lazima tuige kila kitu? Au sasa ni sisi tunaendeleza utumwa wa kimawazo bila pingu na kengele?

Nawashukuru wachangiaji wote hata wale ambao tuna mawazo tofauti.
 
Last edited:
Ni kweli shikamoo lina asili ya utumwa, lakini kama walivyotanabaisha wachangiaji wengine lugha hukua na sehemu moja wapo ya ukuaji wa lugha ni kama haya mabadiliko tunayoyaona kwenye neno shikamoo.

Na sio neno hili pekee ambalo limekuwa "adopted" katika kiswahili kwa maana nzuri tu japo mwanzo yalikuwa na asili fulani ya uduni hivi, mfano neno 'rabeka' ni neno ambalo lilitumika na mwanamke kumuitikia mume wake, na lina asili ya kiarabu pia, na kwa jinsi ilivyokuwa wanawake kwa waarabu walikuwa hawathamini sana, lakini sasa linatumika kama heshima ya mwanamke kumuitikia mumewe hasa katika ukanda wa pwani, neno jingine ni ' naam' ni neno lilikuwa linatumika kukubali kitu au jambo, lakini kwa sasa kwenye kiswahili linatumika kama kiitikio cha heshima kwa mtoto wa kiume aitwapo.

Yapo maneno mengi tu kama mem sahib, sasa linatumika kama mamsapu nk
 
Ok inajulikana kuwa shikamoo ni salaam unayompa mtu aliyekujizi umri (sifahamu kama kuna age limit) Ila Kuna wababa wengine especially binti wa kike akimwambia shikamoo humjibu "salama tuu binti hujambo".And why is that?.
 
Ok inajulikana kuwa shikamoo ni salaam unayompa mtu aliyekujizi umri (sifahamu kama kuna age limit) Ila Kuna wababa wengine especially binti wa kike akimwambia shikamoo humjibu "salama tuu binti hujambo".And why is that?.

SF,
Hii inatokana na kwamba - unapotanguliza shikamoo ni kama umeweka kizuizi cha heshima.Anapokataa kuitika inavyotakiwa ni kwamba alikuwa ana mpango mwingine na wewe na anashangaa barrier ya nini tena?
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom